Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei 27, 2026

AHSANTE FOUNDATION WACHINJA NG'OMBE KONDOO NA MBUZI EID AL- ADHA MIRERANI

Picha
  Na Mwandishi wetu, Mirerani.  TAASISI ya Ahsante Foundation Tanzania imechinja ng'ombe 723, mbuzi na kondoo 2,500 na kutoa sadaka kwa watoto yatima, wajane, wahitaji na taasisi za serikali na binafsi, katika kusheherekea sikukuu ya Eid Al-Adha mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara. Meneja mipango wa taarifa ya Ahsante Foundation Tanzania, Omary Gyunda amesema lengo ni kuhakikisha jamii yenye mahitaji inanufaika na sadaka ya sikukuu hiyo ya Idd. Gyunda amesema taarifa ya Ahsante Foundation Tanzania wamechinja ng'ombe 723, mbuzi na kondoo 2,500 kwa ajili ya jamii kushiriki sherehe hiyo bila ubaguzi wa madhehebu katika mji mdogo na maeneo ya jirani. Amesema sadaka hiyo ya nyama ya kuchinja imetolewa kwa watoto yatima, wajane, wahitaji mbalimbali na taasisi za serikali na binafsi za mji mdogo wa Mirerani na majirani zao. "Tumetoa sadaka hiyo ya kuchinja kwa wahitaji hao na taasisi mbalimbali ikiwemo shule za msingi, sekondari, polisi, uhamiaji, zimamoto na ...

WANAMICHEZO 60 KUWAKILISHA SIMANJIRO UMITASHUMTA

Picha
  Na Mwandishi wetu, Simanjiro  WANAFUNZI wanamichezo 60 wa shule ya msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro wamechaguliwa kuiwakilisha Wilaya hiyo kwenye michuano ya michezo mbalimbali katika ngazi ya Mkoa wa Manyara. Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro, Gracian Max Makota akizungumza wakati akizindua rasmi michuano hiyo katika viwanja vya Mnyalu Complex Mji mdogo wa Mirerani amewaasa wanamichezo hao wanawawakilishe vyema na kuwa washindi katika ngazi ya Mkoa. "Mrudi na vikombe vya ushindi, mkashindane kwa akili, nguvu maarifa na nidhamu, kwani mchezaji mzuri ni yule ambaye anawasikiliza walimu na kutekeleza yale anavyoelezwa ili kufanikisha ushindi," amesema DED Makota. Afisa Elimu Msingi na Awali wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Darous Daudi Limandola amesema wanamichezo 60 wataiwakilisha Halmashauri hiyo kwenye ngazi ya Mkoa wa Manyara. Limandola amesema wanamichezo hao ni timu iliyosheheni hivyo wanatarajia watarudi na ushindi katika miche...