Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni 22, 2026

SANGA AIPONGEZA CRDB KWA KUDHAMINI BUNGE BONANZA MIAKA MITANO MFULULIZO

Picha
Na Jasmine Shamwepu, Dodoma.  MWENYEKITI wa Bunge Bonanza, Festo Sanga, ameipongeza CRDB Bank kwa kuendelea kuwa mdhamini mkuu wa Bunge Bonanza kwa miaka mitano mfululizo, akisema mchango wa benki hiyo umekuwa nguzo muhimu katika mafanikio na ukuaji wa tukio hilo kila mwaka. Akizungumza katika Bunge Grand Bonanza lililofanyika katika Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma, Sanga amesema ushirikiano wa CRDB umechangia kuifanya shughuli hiyo kuwa zaidi ya tukio la michezo, kwa kuwa imekuwa jukwaa la kuimarisha afya, mshikamano na mahusiano mema miongoni mwa wabunge, watumishi wa Bunge na wadau mbalimbali. Amesema udhamini wa benki hiyo umewezesha bonanza hilo kuendelea kukua na kuvutia ushiriki mkubwa zaidi mwaka hadi mwaka, hali inayodhihirisha umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za umma na sekta binafsi katika maendeleo ya jamii. “Kwa mwaka wa tano mfululizo CRDB imeendelea kusimama nasi katika kufanikisha Bunge Bonanza. "  Tunatoa shukrani za dhati kwa Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB...

TANZANIA IPO TAYARI KUPOKEA AFCON 2027

Picha
  Na Jasmine Shamwepu, Dodoma.  NAIBU Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Daniel Sillo, amesema maandalizi ya kuelekea Mashindano ya Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 yanaendelea vizuri, huku akibainisha kuwa Tanzania ipo katika nafasi nzuri ya kupokea na kuandaa mashindano hayo kwa mafanikio. Sillo ametoa kauli hiyo wakati wa Bonanza la Bunge (Bunge Grand Bonanza) lililofanyika jijini Dodoma, ambapo amesema kaulimbiu ya bonanza hilo inayohusiana na AFCON 2027 ni ishara ya namna Watanzania wanavyoendelea kuhamasika na kujiandaa kwa tukio hilo kubwa la kimichezo. Amesema maandalizi yanayoendelea kufanywa na Serikali, ikiwemo uboreshaji wa miundombinu ya michezo na huduma nyingine muhimu, yanaonyesha dhamira ya dhati ya kuhakikisha Tanzania inakuwa mwenyeji bora wa mashindano hayo ya kihistoria. “AFCON 2027 ni fursa kubwa kwa Tanzania kujitangaza kimataifa kupitia sekta ya michezo. Sisi kama Bunge tutaendelea kutoa ushirikiano unaohitajika ili kuhakikisha maandalizi ...

WENYEVITI WA VIJIJI WA MONDULI WAMLIPUA MBUNGE WAO ISACK JOSEPH KWA KAULI YA KUNYANG'ANYWA MIHURI

Picha
Na Hamida Ramadhan, Monduli.   Mvutano mkubwa umeibuka katika Jimbo la Monduli baada ya Mbunge wa Jimbo hilo, Mheshimiwa Isack Joseph Copriano maarufu kama Kadogoo, kutoa kauli bungeni akiunga mkono hatua ya wenyeviti wa vijiji kunyang'anywa mihuri ya Serikali, kauli ambayo imezua hasira na malalamiko kutoka kwa viongozi wa Serikali za Mitaa katika wilaya hiyo. Wenyeviti hao wanasema kauli ya Mbunge wao imewadhalilisha, imewashushia hadhi mbele ya wananchi na imeondoa imani ya wananchi kwa viongozi waliowachagua kwa kura. Sintofahamu hiyo ilianza baada ya Mbunge Copriano kuchangia bungeni kuhusu migogoro ya ardhi na matumizi ya mihuri ya Serikali, ambapo alisema wazi kuwa anaunga mkono hatua ya kunyang'anywa kwa wenyeviti wa vijiji mihuri hiyo. Akizungumza bungeni, Mbunge huyo alisema: "Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro, na mimi nimefurahi sana na wenyeviti wa vijiji watanisamehe niwapongeze sana TAMISEMI kwa kunyang'anya wenyeviti wa vijiji mihuri. Wanyang'anyeni wa...