Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba 19, 2025

TAARIFA KWA UMMA

Picha
 

FAHAMU KUHUSU GAZETI LA SERIKALI

Picha
 

WAASI WA M23 WAANZA KUTOZA ADA KWA SHULE MJI WA GOMA.

Picha
  SHULE ambazo hapo awali zilikuwa zinatoa elimu bila malipo katika mji wa Goma ,nchini DRC sasa zimeanza kutoza ada chini ya udhibiti wa waasi wa M23, huku walimu wakikosa mishahara kutoka serikali kuu , jambo linalozua wasiwasi mkubwa miongoni mwa wazazi na walimu kuhusu upatikanaji wa elimu, wakati huu juhudi za upatanishi zinazoongozwa na Qatar zikilenga kushughulikia mzozo mpana wa eneo hilo. #M23 #drceducation #goma #drcgoma #Elimu

TBS YAONDOA TANI 42 ZA BIDHAA ZA CHAKULA ZA WATOTO ZENYE MIDOLI NDANI YAKE MAARUFU KWA JINA LA CHAMA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.  SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limeondoa sokoni tani 42 za bidhaa za chakula za watoto maarufu chama zenye ‘mido li’ ndani yake.  Pia, limesema baada ya kufanya uchunguzi na kubaini uwepo wa viwanda vinavyozalisha bidhaa hizo, ilipiga marufuku na kusitisha uzalishaji na uingizwaji wa bidhaa hizo sokoni.  Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji wa Sheria wa TBS, Kandida Shirima alitoa ufafanuzi huo wakati wa mkutano wa wahariri na waandishi wa habari uliofanyika jana kuelezea mafanikio ya TBS katika miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita.  Aidha, shirika lilibaini uwepo wa baadhi ya wazalishaji wanaofunga vyakula na vitu vingine kama midoli hasa kwenye bidhaa za chakula za watoto kwa lengo la kuvutia watumiaji.  Amesema kuwa, baadaye walichukua hatua ya kutoa taarifa kwa umma na kuvifikia vi wanda vinavyozalisha bidhaa hizo na kusitisha uzalishaji wake.  “Tumefanya ukaguzi kupitia ofisi zetu za kanda nchi nzima na tum...

TANZANIA YAANDAA WATAALUMU WA SAYANSI NA TEKNOLOJIA YA NYUKLIA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Austria  TANZANIA imeanza kuandaa wataalamu wa Sayansi na Teknolojia ya Nyuklia kupitia vyuo vya ndani na nje ya nchi kwa lengo la kujenga uwezo wa kitaifa na kupunguza utegemezi wa wataalamu kutoka nje. Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, amesema hayo hivi karibuni jijini Vienna, Austria wakati wa kikao maalum na Mkurugenzi wa Divisheni ya Afrika wa Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki (IAEA), Dkt. Gashaw Gebeyehu Wolde, kando ya Mkutano Mkuu wa 69 wa IAEA. Katika mazungumzo yake na Theresa Wutz, Afisa Mkuu Muidhinishaji wa Miradi wa kampuni ya eee Austria, Prof. Nombo alipongeza hatua ya Austria kupitia UniCredit – Bank of Austria kuendelea kufadhili Mradi wa Elimu Kidigitali Zanzibari, akieleza kuwa msaada huo utafungua fursa za kupanua matumizi ya TEHAMA hadi shule na vyuo vya Tanzania Bara. Kukamilika kwa awamu za mradi huo kutaiwezesha Tanzania kuwa na mifumo madhubuti ya kidigitali, miundombinu imara na rasilima...