Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba 29, 2025

DIWANI AGUSWA NA KERO ZA AKINAMAMA WAJAWAZITO

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Tabora. DIWANI wa Kata ya Chemchem katika halmashauri ya manispaa Tabora kupitia CCM, Bandola Salum Milambo ameanza mikakati ya kutatua kero wanazopata akinamama wajawazito na wagonjwa wengine katika kata yake.  Akizungumza na wanahabari jana ameeleza kuwa baada ya kuapishwa sasa ana kazi moja tu ya kuhakikisha kero zote zinazowakabili wapiga kura wake zinashughulikiwa ipasavyo na mamlaka husika. Amedokeza kuwa kwa kuanzia anaanza na kero ya wajawazito ambao wamekuwa wakilalamikia kutozwa gharama kubwa wanapoenda kuanza kliniki kwenye Kituo cha kutolea huduma za afya cha Town Kliniki, kilichoko hapa Chemchem. ‘Nimepanga kutembelea Kituo hiki (Zahanati ya Town Kliniki) ili kujionea hali ya utoaji huduma lakini pia kufuatilia malalamiko ambayo yametolewa na akinamama wajawazito ya kutozwa gharama kubwa ili wapate huduma za kliniki’, ameeleza. Amesema kuwa utaratibu wa wananchi kuchangia huduma za afya unajulikana, lakini inapobainika kuwa wanatozwa gharama k...

KUONGEZWA KWA SAFARI ZA TRENI ZA SGR ILI KUKIDHI USUMBUFU WALIOUPATA ABIRIA DESEMBA 28, 2025.

Picha

HALI YA MVUA KUBWA NCHINI

Picha
MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inapenda kutoa taarifa ya mwenendo wa Mvua Kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali hapa nchini.  Mnamo tarehe 26 hadi 27 Desemba, 2025 Mamlaka iliendelea kutoa Tahadhari ya vipindi vya Mvua Kubwa katika maeneo mengi nchini kuanzia tarehe 26 hadi 29 Desemba, 2025. Kwa mujibu wa Tahadhari hiyo maeneo yaliyotarajiwa kuathirika na vipindi hivi vya mvua kubwa ni pamoja na Mikoa ya Kigoma, Tabora, Katavi, Rukwa, Mbeya, Songwe, Iringa, Njombe, Dodoma, Singida, Songea, Morogoro, Lindi, Mtwara, Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tanga, Dar es Salaam, Pwani (ikijumisha Kisiwa cha Mafia) pamoja na Visiwa vya Unguja na Pemba.  Kuanzia usiku wa kuamkia leo hadi hivi sasa maeneo mengi nchini yameendelea kupata vipindi vya Mvua Kubwa zikiambatana na upepo mkali na hivyo kusababisha uharibifu wa mali na miundombinu katika baadhi ya maeneo hapa nchini. Hadi kufikia saa 3:00 kamili asubuhi ya leo viwango vya mvua kubwa vinavyozidi milimita 50 ndan...