Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba 26, 2025

MBUNGE MNZAVA AWAKABIDHI WAZEE 300 BIMA ZA AFYA KUPITIA MAKUYUNI FESTIVAL

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Korogwe. MBUNGE wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Mhe. Timotheo Mnzava, ameendelea kutekeleza mikakati ya kuboresha huduma za afya kwa wazee kwa kugawa Bima za Afya kwa zaidi ya wazee 300 waliohudhuria Makuyuni Festival, tamasha lililowakutanisha wakazi wa maeneo mbalimbali ya jimbo hilo. Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mhe. Mnzava amesema  hatua hiyo inalenga kuhakikisha wazee wanapata huduma bora za matibabu bila vikwazo vya kifedha, huku akisisitiza kuwa afya ya wazee ni sehemu muhimu ya ustawi wa jamii.  "Bima hizo zitawawezesha wazee kupata matibabu kwa wakati wowote na katika vituo vilivyosajiliwa, hatua inayotafsiriwa kama kupunguza mzigo wa gharama za afya kwa familia nyingi za kipato cha chini."amesema Mhe.Mnzava Katika tamasha hilo, Mbunge Mnzava pia alipata fursa ya kushiriki chakula cha pamoja na wazee, watu wenye ulemavu, vijana na wananchi wengine waliohudhuria, akisema kitendo hicho ni sehemu ya kuimarisha mshikamano na kuonyesha ushiriki...

WAZEE TABORA WANENA MAZITO KWA RAIS SAMIA

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora ZIKIWA zimebakia siku chache kumalizika mwaka 2025 na kuanza mwaka mpya wa 2026, wazee wa Mkoa wa Tabora wameeleza kuridhishwa na utendaji wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika awamu yake ya pili baada ya kuingia madarakani. Wameeleza kuwa weledi na ufanisi wa Kiongozi mzuri unapimwa kwa mambo makubwa matatu ambayo ni hali ya usalama wa nchi, kasi ya maendeleo na uchumi, mambo haya yamesimamiwa vizuri na nchi inapiga hatua kubwa. Mzee Elisha Daud Mponeja ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi wa Jadi katika halmashauri ya manispaa Tabora ameeleza kuwa Rais Samia amefanya kazi nzuri sana katika kipindi chake cha miaka minne na hata sasa anaendelea vizuri. Amefafanua kuwa baada ya kukabidhiwa nchi Machi 19, 2021 kutoka kwa mtangulizi wake aliyetangulia mbele za haki, Dkt John Pombe Magufuli, watanzania walishuhudia kasi kubwa ya utekekezaji miradi ya maendeleo katika sekta zote. ‘Katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wake mambo makubwa yamefanyika ikiw...

ASKOFU MEIVUKIE ATAKA UPENDO, HAKI NA AMANI VIDUMISHWE

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora ASKOFU wa Kanisa la TAG Jimbo la Tabora Kati na Kiongozi wa Kanisa la Kitete Christian Centre (KCC) la Mjini Tabora Rev. Paul Meivukie ameomba upendo, haki na amani viendelee kudumishwa nchini ili jamii iishi kwa utulivu. Ametoa rai hiyo leo kwenye ibada ya sikukuu ya krismas ambapo ameeleza kuwa krismasi ni tukio kubwa linalobeba ujumbe wa upendo, haki na amani kwa watu wote, hivyo mamlaka na jamii kwa ujumla hawana budi kuyadumisha. Amesisitiza kuwa tunapoadhimisha sikukuu hii ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo hatuna budi kumwomba Mungu ili taifa liendelee kuwa na amani na utulivu na upendo na haki viendelee kudumishwa wakati wote ili Mungu aliinue taifa lake. ‘Taifa liliingia kwenye wakati mgumu sana Oktoba 29, 2025 siku ya uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani, hili halipaswi kufumbiwa macho, kama taifa tunapaswa kusameheana na kupendana ili kudumishwa amani yetu', amesema. Askofu Meivukie ameasa waumini wa kanisa hilo na jamii kwa ujumla kuishi tabia na...