Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni 7, 2026

TANZANIA NA UTURUKI KUIMARISHA BIASHARA NA MAENDELEO YA VIWANDA

Picha
  Na Lubango Mleka.  WAZIRI wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga, akiwa katika ziara ya kikazi nchini Uturuki Juni 06, 2026, Jijini Istanbul amefanya mazungumzo na Waziri wa Viwanda na Teknolojia wa Uturuki, Mehmet Fatih Kacır pamoja na Waziri wa Biashara wa Uturuki, Ömer Bolat, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na viwanda kati ya nchi hizi mbili. Mazungumzo na Waziri Kacır yamejikita katika kukuza maendeleo ya viwanda vya kimkakati, kuimarisha matumizi ya teknolojia, pamoja na kuhamasisha uwekezaji katika viwanda rafiki kwa mazingira. Mhe. Kapinga ameeleza dhamira ya serikali ya kutumia ushirikiano huo kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya mwaka 2050 ya kuwa nchi ya kipato cha kati cha juu kupitia mageuzi ya sekta ya viwanda, huku Uturuki ikiahidi kuendeleza ushirikiano wa kiufundi, kiteknolojia na ubunifu kwenye sekta hiyo. Kwa upande wa biashara, mazungumzo na Waziri Bolat yamejikita katika kuimarisha mazingira wezeshi ya uwekezaji na kuongeza kiwango cha ...

CSP na VI AGROFORESTRY WAADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA KWA KUPANDA MITI 1,200

Picha
  Na Mwandishi wetu, Babati  SHIRIKA lisilo la kiserikali la Civic Social Protection Foundation (CSP) na Vi Agroforestry wameadhimisha siku ya mazingira duniani kwa kupanda miti 1,200 na kufanya shughuli mbalimbali za uhifadhi wa mazingira Mjini Babati, Mkoani Manyara. Mwanasheria wa CSP Eliakim Paul, akizungumza kwenye maadhimisho hayo ameeleza kuwa shirika hilo hiyo limeendelea kushirikiana na jamii katika juhudi za kulinda mazingira kupitia upandaji miti, elimu ya mazingira na shughuli za usafi. Eliakim amesema katika maadhimisho ya mwaka huu wa 2026 wamepanda miti 1,200 ya matunda, mbao na kivuli kwenye maeneo mbalimbali yakiwemo shule ya msingi Malangi, zahanati ya Malangi, shule za sekondari FT Sumaye na Himiti na ofisi ya kijiji cha Himiti.  Amesema pia wamegawa miti hiyo kwa mtu mmoja mmoja ili kuhamasisha utunzaji wa mazingira katika ngazi ya familia na jamii kwa ujumla. "Sambamba na zoezi la upandaji miti, shughuli za usafi wa mazingira zimefanyika katika shule ...

WAKAZI USUNGA WAMPONGEZA RAIS SAMIA

Picha
Na Allan Kitwe, Tabora.  WAKAZI wa Kijiji Cha Usunga, Kata ya Usunga Wilayani Sikonge Mkoani Tabora wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwapelekea mradi wa maji safi na salama ya kunywa. Wametoa pongezi hizo jana kwenye shamra shamra za kilele cha Maadhimisho ya Miaka 58 tangu kuanzishwa kwa Kijiji hicho ambacho kimekuwa mfano wa kuigwa kwa kudumisha mila, utamaduni, mshikamano na ulinzi wa jadi. Akizungumza na wananchi kwenye shamrashamra hizo zilizopambwa na ngoma, burudani, chakula cha asili na vinywaji, Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji hicho James Mgulu ameishukuru serikali kwa kumaliza kero ya maji katika Kata hiyo. Amefafanua kuwa tangu kuanzishwa kwake wakazi wa Kijiji hicho wameendeelea kunufaika na mambo mengi mazuri yanayofanywa na serikali yao ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ikiwemo kudumisha umoja, amani na mshikamano.   Akielezea kiini cha sherehe hiyo, Diwani wa Kata hiyo Jackson Mbasha amesema kuwa utaratibu...