Machapisho

TCAA YAWEZESHA MAFANIKIO YA REKODI YA DUNIA NDANI YA HIFADHI YA TARANGIRE.

Picha
Na Lubango Mleka, Tarangire. MAMLAKA ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imeratibu na kusimamia kwa mafanikio safari ya kihistoria ya puto la hewa moto (hot air balloon) iliyoifanya Tanzania kuorodheshwa rasmi kama nchi ya 123 katika jaribio la rekodi ya dunia la kurusha balloon na rubani akiwa pekee yake, lililoendeshwa na Dkt. Rubani Allie Dunnington. Safari hiyo maalum imefanyika katika Hifadhi ya Taifa ya Tarangire ikiwa ni mara ya kwanza kwa safari ya aina hii kufanyika na mtu mmoja ndani ya eneo la hifadhi. Uamuzi huu wa kipekee ulifikiwa na TCAA baada ya kufanya tathmini ya kina ya kiusalama, utaratibu wa kiufundi na uhalali wa operesheni ndani ya eneo hilo nyeti. Kwa mujibu wa TCAA, safari hiyo imefuata kikamilifu kanuni, taratibu na viwango vya usalama vya kitaifa na kimataifa. TCAA imeshirikiana kwa karibu na wadau wa uhifadhi pamoja na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kuhakikisha zoezi linafanyika kwa usalama, ufanisi na kulinda uadilifu wa mazingira ya hifadhi. Dkt. Ruba...

RACHEL NJAU AMSHUKURU RAIS SAMIA KUWAPATIA WANAWAKE LESENI

Picha
  Na Mwandishi wetu, Mirerani  MAKAMU Mwenyekiti wa chama cha wachimbaji madini wanawake Tanzania (TAWOMA) Rachel Joseph Njau amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kwa kuwapatia wanawak leseni za uchimbaji na ununuzi wa madini bila malipo. Hivi karibuni Waziri wa Madini Anthony Mavunde aliwapatia leseni ya uchimbaji madini na leseni ya ununuzi wa madini wanawake na vijana 423 waliopo katika vikundi 21 wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara. Rachel ambaye pia ni Katibu wa chama cha wachimbaji madini Mkoa wa Manyara (MAREMA) Tawi la Mirerani ametoa shukrani hizo kwenye uchaguzi wa TAWOMA Tawi la Mirerani ambapo Magreth Nelson alichaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa TAWOMA kwa wanawake wafanyabiashara wa magonga ndani ya ukuta unaozunguka migodi ya madini ya Tanzanite. Ameeleza kwamba kitendo cha Rais Samia Suluhu Hassan kuwasaidia wanawake kwenye mpango huo kinaongeza idadi ya wanawake wanaonufaika na sekta ya madini. "Tunampongeza Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kumtuma Waziri Ant...

MAGE NELSON MWENYEKITI MPYA TAWOMA MIRERANI

Picha
  Na Mwandishi wetu, Mirerani  MFANYABIASHARA maarufu wa kuongeza thamani madini ya Tanzanite wa mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, Magreth Nelson amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama cha wanawake wanaojihusisha na shughuli za madini Tanzania (TAWOMA) Tawi la Mirerani. Mage atatumikia kwa muda wa miaka mitano nafasi hiyo ya Mwenyekiti wa wanawake wafanyabiashara wa magonga ndani ya ukuta unaozunguka migodi ya madini ya Tanzanite mji mdogo wa Mirerani. Katika uchaguzi huo uliofanyika chini ya Makamu Mwenyekiti wa TAWOMA, Rachel Joseph Njau na Katibu Mkuu wa TAWOMA, Salma Ernest Kundi na kusimamiwa na Mwenyekiti wa MAREMA Tawi la Komolo Swalehe Abdalah na mjumbe wa MAREMA Tawi la Mirerani Jafar Matimbwa na kushuhudiwa na Afisa maendeleo ya jamii mamlaka ya mji mdogo wa Mirerani Floriana Mcharo. Mwenyekiti wa MAREMA Tawi la Komolo, Swalehe Abdalah akitangaza matokeo hayo amesema Magreth Nelson ambaye hakuwa na mpinzani alishinda nafasi hiyo kwa kupata kura ...

WAZIRI MAVUNDE AMPONGEZA RMO KASEZA

Picha
Na Mwandishi wetu, Mirerani  WAZIRI wa Madini Mhe Anthony Peter Mavunde, amempongeza Afisa madini mkazi (RMO) wa mkoa wa kimadini wa Mirerani, George Kaseza kwa namna anavyotekeleza wajibu wake ipasavyo, bila kulalamikiwa au kubagua wachimbaji. Waziri Mavunde ameeleza hayo wakati akizungumza na wadau wa madini ya Tanzanite mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, alipofanya ziara ya kutembelea machimbo ya madini ya Tomarini ya kijani eneo la Lemshuku na madini ya Tanzanite mji mdogo wa Mirerani. Amesema RMO Kaseza ni kiongozi mzoefu katika suala zima la eneo tengefu la Mirerani ndiyo sababu akateuliwa kuwa kiongozi wa hapo ambaye wadau wa madini pia wanamkubali kupitia utendaji kazi wake. "RMO Kaseza umekuwa mara nyingi ukiandika maandiko mengi ya eneo tengefu la Mirerani ndiyo sababu tukakuleta hapa sasa yake maandiko yako yafanye kuwa uhalisia ili yaonekane kwa vitendo," amesema Waziri Mavunde. Amewaasa wadau wa madini wa eneo hilo kumpa ushirikiano wa kutos...

URA – SACCOS YAPATA HATI SAFI MIAKA TISA MFULULIZO.

Picha
  Na. Lubango Mleka, Arusha.  KAMISHINA wa fedha na lojistiki (CP) Liberat Sabas amekipongeza Chama cha ushirika cha kuweka na kukopa cha Jeshi la Polisi (URA SACCOS LTD) kwa kuendelea kupata hati safi kwa miaka tisa (9) mfululizo kutoka kwa mkaguzi wa nje, jambo ambalo limewezesha  kuwa chama bora kitaifa kwa miaka mitano mfululizo na kuwa  chama kinachoongoza kwa mtaji mkubwa, mali na idadi kubwa ya wanachama. Kamishna Sabas yameyasema hayo leo Novemba 28, 2025 wakati akimwakilisha mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Camillius Wambura kufungua mkutano wa 17 wa chama hicho unaofanyika jijini Arusha.   “kupata hati hizo safi kwa mfululizo, zinaakisi uwazi na uadilifu wa uendeshaji makini wa chama chetu” alisema CP Sabas. Matokeo ya ufanisi huo kwa mwaka 2025 yametokana na uongozi bora, nidhamu ya kifedha na moyo wa umoja na  kujituma  kwa watendaji wa chama hicho. CP Sabas aliongeza kuwa uongozi bora na nidhamu ya kifedha imewezesha chama hicho kuwa na ak...

PET SCAN IANZE KUFANYA KAZI OCEAN ROAD- DKT SHEKALAGHE

Picha
Na. Lubango Mleka, Dar es Salaam. KATIBU Mkuu Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe, ameuagiza uongozi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road na mkandarasi anayesimika kifaa tiba cha PET Scan kuhakikisha wanakamilisha usimikaji wa kifaa hicho ndani ya muda waliokubaliana. Dkt. Shekalaghe ametoa agizo hilo Novemba 25, 2025, wakati wa ziara yake ya ukaguzi wa utoaji wa huduma katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, jijini Dar es Salaam. “Tumekubaliana kwamba hadi siku ya Ijumaa, mkandarasi anatakiwa kumpatia Mkurugenzi wa Ocean Road uhakiki wa benki (Bank Guarantee) ili Mkurugenzi aweze kumlipa asilimia 75 ya malipo yake. Hii itamwezesha mkandarasi kufanya maandalizi ya kuhakikisha PET Scan inaanza kufanya kazi. Wataalam wamenishauri kuwa baada ya hapo tutahitaji siku 30 kwa ajili ya maandalizi ya mashine hiyo kuzalisha mionzi tiba kwa ajili ya kugundua kansa,” amesema Dkt. Shekalaghe. Aidha, amewahakikishia wananchi wanaofika hospitalini hapo kupata huduma, kuwa Serikali imenunua galimu ...

WAANDISHI WA HABARI NI WADAU MUHIMU KATIKA KUIMARISHA AMANI, USALAMA NA UTULIVU WA TAIFA

Picha
Na Lubango Mleka, Dodoma. NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Dennis Lazaro Londo, amewahakikishia waandishi wa habari nchini kuwa Serikali itaendelea kulinda uhuru wao wa kujieleza pamoja na kuhakikisha wanatimiza majukumu yao kwa usalama na weledi. Mhe. Londo amezungumza hayo leo Novemba 27, 2025 jijini Dodoma katika mafunzo ya waandishi wa habari yaliyowaleta pamoja Wanahabari 100 kutoka maeneo mbalimbali nchini, Mhe. Londo amesema Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi itaendelea kushirikiana na wadau wa habari katika maeneo yote yanayohusu usalama kwa waandishi wa habari. Aidha, amebainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka msukumo mkubwa katika kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi, sambamba na kulinda uhuru wa vyombo vya habari.  " Falsafa ya Mhe. Rais kupitia “4R” zinaipa tasnia ya habari nafasi muhimu katika kulinda amani, kuimarisha umoja wa kitaifa na kuendeleza mijadala yenye tija kwa jamii." Am...

MNADA WA KOROSHO MOROGORO

Picha
 

KANISA LA FPCT LAIPONGEZA SERIKALI KUSOGEZA HUDUMA ZA MOYO KWA WANANCHI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Nkinga - Igunga. KANISA la FPCT Jimbo la Nzega limeipongeza Serikali ya awamu 6 chini ya Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa ujio wa Madaktari Bingwa Bobezi wa Moyo walioweka Kambi ya matibabu ya Moyo Hospitali ya Rufaa ya Nkinga Igunga. Pongezi hizo zimetolewa leo na Askofu Ezekiel Silasi wa Jimbo la Nzega alipotembelea Hospitali ya Rufaa ya Nkinga ili kuona jinsi huduma za kambi zinavyotolewa kwa wananchi. "Ujio wao umeleta tija kubwa katika jamii yetu lakini kwa Kanisa la FPCT, tunasikia kuthaminiwa sana, binafsi kwaniaba ya Askofu Mkuu niwashukuru sana Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa kuja hapa Nkinga kutuletea huduma hii lakini pia kuwapa uzoefu Madaktari wetu." Ameongeza, "Ushirikiano huu uendelee kwa sababu Afya za watanzania zikiimarika hayo ndio maendeleo ya nchi yetu" amesema Askofu Silasi. Bw.Omary Kalonga mkazi wa kata ya Magengati wilayani Nzega ameipongeza Hospitali ya Rufaa ya Nkinga kuwaleta Madaktari hao kwani ingewagharimu fedha nying...

DKT. MWIGULU AWAONYA WAVUNJIFU WA SHERIA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es salaam. WAZIRI Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amevitaka vyombo vinavyosimamia usalama barabarani vitekeleze sheria hizo bila upendeleo kwani tabia ya kuogopana na kuoneana aibu imechangia baadhi ya watu kukwepa wajibu wakati wengine wakibebeshwa mzigo wa sheria.  “Yeyote atakayevunja sheria akamatwe na hatua zichukuliwe kwa usawa. Huyu mmoja anavunja sheria anakamatwa, analipa. Huyu mwingine anavunja mbele yake anaachwa. Kama una haraka, toka mapema zaidi si kufidia kwa kuvunja sheria.” Ametoa kauli hiyo leo (Jumatano, Novemba 26, 2025) wakati akifungua Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Usafiri Endelevu Ardhini katika ukumbi wa Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam. Amesema kuwa haitakuwa uungwana kuona baadhi ya watu wakilipa adhabu papo hapo wanapokosea ilhali wengine wakiachwa kupita bila kuchukuliwa hatua. Amewaonya baadhi ya viongozi na madereva wa Serikali ambao wanaelewa sheria vizuri lakini bado wanazikiuka kwa makusudi. “Ni muhimu kuwasaidia wa...

TFF YAUFUNGIA UWANJA WA MKWAKWANI TANGA

Picha

YANGA YAICHAPA AS FAR 1–0, YAENDELEA KUWIKA LIGI YA MABINGWA AFRIKA

Picha
  TIMU ya Yanga ambao ni Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, wameibuka na ushindi wa bao 1–0 dhidi ya AS FAR Rabat katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Barani Afrika uliopigwa leo, Novemba 22, 2025, katika Dimba la New Amaan Complex, Zanzibar. Yanga SC walipata bao pekee la mchezo huo kupitia kwa mshambuliaji wao Prince Dube dakika ya 58, akimalizia kwa ustadi pasi ya kutengeneza nafasi iliyotolewa na Mudathir Yahya. Kwa ushindi huo, Yanga SC wamefanikiwa kuvuna pointi tatu muhimu wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani, na hivyo kujiweka kwenye mazingira mazuri katika harakati zao za kusaka nafasi ya kusonga mbele kwenye michuano hiyo barani Afrika, na kuweka hisroria ya kuwa timu ya kwanza  kupata ushindi.

WAFUGAJI WA JAMII YA KIMASAI HANDENI WAMETAKIWA KUEPUKA MIGOGORO NA KUSHIRIKIANA NA POLISI

Picha
  Na Mwandidhi Wetu, Tanga. WAFUGAJI kutoka vijiji vya Msomela na Kwamantuku, Wilaya ya Handeni Mkoa wa Tanga, wametakiwa kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kudhibiti matukio ya uhalifu na kudumisha amani katika jamii zao. Wito huo umetolewa leo tarehe 22 Novemba 2025 na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Tanga, ACP Wambura, alipokutana na wawakilishi hao katika kikao cha majadiliano. ACP Wambura amewaasa wananchi kushirikiana na Jeshi la Polisi, kutoa taarifa za viashiria vya uhalifu na kuchochea amani katika maeneo yao. Aidha, Wafugaji hao wametoa pongezi kwa juhudi za Polisi Mkoa wa Tanga, na kuahidi kuendeleza mahusiano mema na wakulima, kuepuka migogoro, na kuwa mabalozi wa amani kwa kutoa taarifa za uchochezi au vurugu mara wanapozibaini.

HAMZA ALLY MNGIA AJITOSA UENYEKITI KITETO

Picha
  Na Mwandishi wetu, Kiteto  DIWANI wa Kata ya Dosidosi Wilayani Kiteto Mkoani Manyara, Hamza Ally Mngia amejitosa kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Mngia ambaye ni mara yake ya kwanza kushinda nafasi ya udiwani akizungumza wakati akirejesha fomu ya kugombea amesema yeye bado ni kijana anayeamini uwezo, bidii na ufanisi wa kutumikia nafasi hiyo ya Mwenyekiti pindi akichaguliwa. "Wakati huu Mwenyekiti wa CCM na Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan ameonesha wazi kutuamini vijana na kutupa nafasi kubwa mbalimbali za kimaanuzi nchini na hiyo ndiyo sababu iliyonipa nguvu ya kuiomba nafasi hii ya Mwenyekiti wa  Halmashauri ya Wilaya ya kiteto," amesema. Amesema kwa sasa ni kusubiri mchakato na utaratibu wa vikao vya chama na hana hofu na CCM kwani anayo imani kubwa ukilinganisha na sifa zake za kiuongozi alizonazo. "Nikifanikiwa kuteuliwa nikianza kampeni nitaeleza sababu zangu kwanini nim...

WAKUU WA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA WASHIRIKI SHEREHE ZA KUTUNUKIWA KAMISHENI KWA MAAFISA WANAFUNZI WA JWTZ.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Arusha. WAKUU wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama wakiwa ni miongoni mwa viongozi mbalimbali waliohudhuria sherehe za kutunuku Kamisheni kwa Maafisa Wanafunzi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika sherehe zilizofanyika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA) Monduli mkoani Arusha tarehe 22 Novemba, 2025 ambapo Amiri Jeshi Mkuu, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametunuku Kamisheni.

IGP CAMILLUS WAMBURA- TUSIKUBALI KUGAWANYWA KWA SABABU YOYOTE

Picha
Na Mwandishi Wetu, Moshi. MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Camillus Wambura amewataka Watanzania kutokubali kugawanyika kwa sababu yoyote ile, iwe ya kidini, kisiasa au rasilimali na badala yake waendeleze upendo na amani ya taifa. IGP Wambura aliyasema hayo Novemba 21, 2025 wakati akifunga rasmi Mafunzo ya Awali ya Askari Polisi Kozi Namba 1/2024/2025 katika Shule ya Polisi Tanzania - Moshi, Kilimanjaro. IGP Wambura amesema amani ya nchi ni jambo la muhimu hivyo kila mmoja anawajibu wa kuendeleza amani na usalama wa nchi ambayo imedumu kwa muda mrefu tangu tumepata uhuru. Pia, amewataka watanzania kuendeleza ushirikiano, umoja na mshikamano na Jeshi la Polisi kwa maslahi ya taifa letu. Aidha, IGP Wambura amewataka askari wahitimu kwenda kutekeleza kwa vitendo yale waliyojifunza kwa kuhakikisha kuwa wanaimarisha usalama wa raia na mali zao kwa kudhibiti vitendo vya kihalifu. Vilevile, amemshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi M...