Machapisho

ZIMAMOTO YAWAKARIBISHA WANANCHI KUPATA ELIMU YA UOKOAJI KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Dodoma.  WANANCHI wametakiwa kutumia fursa ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kutembelea banda la Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ili kupata elimu ya kujikinga na majanga ya moto pamoja na mbinu za uokoaji wakati wa dharura. Akizungumza katika maadhimisho hayo yanayoendelea jijini Dodoma, Naibu Kamishna wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Puyo Nzalayaimisi, alisema banda la jeshi hilo limekuwa likitoa elimu kwa wananchi kuhusu namna ya kuokoa maisha na mali pindi majanga yanapotokea. Amesema wananchi wanaofika katika banda hilo wanapata mafunzo kuhusu hatua za kuchukua kabla, wakati na baada ya kutokea kwa majanga ya moto pamoja na maafa mengine yanayohitaji huduma za uokoaji. "Tunatumia maonesho haya kukutana moja kwa moja na wananchi na kuwapa elimu itakayowasaidia kujikinga na majanga pamoja na kuelewa namna ya kushirikiana na jeshi la zimamoto wakati wa dharura," amesema. Nzalayaimisi ameleza kuwa elimu hiyo ni sehemu ya mkakati wa jeshi hilo wa ku...

VETA YAONESHA BIDHAA ZINAZOTENGENEZWA NA WANAFUNZI WAKATI WA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

Picha
  Na Jasmine Shamwepu, Dodoma.  MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imetumia maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kuonesha bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na wanafunzi wake, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha jamii kutambua mchango wa mafunzo ya ufundi stadi katika maendeleo ya kiuchumi. Akizungumza katika maonesho hayo, Meneja wa Rasilimali Watu wa VETA, Eliaika Manyanga, akimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo, alisema bidhaa zinazooneshwa zimetengenezwa na wanafunzi kwa kushirikiana na walimu wao kupitia mafunzo ya vitendo yanayotolewa katika vyuo vya VETA. Alisema bidhaa hizo zinajumuisha vifaa mbalimbali vya matumizi ya nyumbani na ofisini vinavyotumiwa na makundi tofauti ya jamii, huku vikionesha kiwango cha ujuzi na ubunifu unaopatikana kwa wahitimu wa taasisi hiyo. Manyanga alisema VETA inaendelea kutoa mafunzo ya muda mfupi na muda mrefu yanayolenga kuwawezesha vijana kujiajiri na kuajirika, huku akibainisha kuwa udahili wa wanafunzi kwa muhula ...

ASMA MWINYI FOUNDATION YAADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA KWA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUMU

Picha
  Na Jasmine Shamwepu, Dodoma.  MWANZILISHI na Mkurugenzi wa Taasisi ya Asma Mwinyi Foundation, ambaye pia ni Mbunge wa Welezo, Unguja, Asma Ally Hassan Mwinyi, ameungana na watoto wenye usonji (Autism), ugonjwa wa Down Syndrome na mtindio wa ubongo (Cerebral Palsy), pamoja na wazazi wao, kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika kwa kuwapa fursa ya kusikika na kujadili changamoto zinazowakabili. Katika maadhimisho hayo ya Juni 16, Asma Mwinyi Foundation kwa kushirikiana na Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe iliandaa ziara maalumu ya watoto hao na wazazi wao katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Dodoma, ambapo walipata nafasi ya kuzungumza na viongozi na kueleza changamoto wanazokabiliana nazo katika maisha ya kila siku. Akizungumza wakati wa shughuli hiyo, Asma alisema lengo la kuwakutanisha watoto hao na wazazi wao ni kuendelea kutoa elimu kwa jamii, kuondoa unyanyapaa na kuhamasisha upatikanaji wa huduma bora za afya na matibabu kwa watoto wenye mahitaji...

WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA YAHIMIZA VIJANA KUTUMIA FURSA ZA KIUCHUMI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  WAZIRI ya Viwanda na Biashara imewahimiza wananchi, hususan vijana na wajasiriamali, kutumia kikamilifu fursa zinazotolewa na taasisi zake ili kukuza biashara, kuongeza kipato na kuchangia maendeleo ya uchumi wa taifa. Wito huo umetolewa leo Juni 17, 2026 na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Saidi Msabimana, wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma. Msabimana amesema wizara hiyo, ambayo ni miongoni mwa taasisi muhimu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, imeshiriki maonesho hayo pamoja na taasisi nane zilizo chini yake kwa lengo la kusogeza huduma karibu na wananchi pamoja na kutoa elimu kuhusu biashara, viwanda na uwekezaji. Amesema jukwaa hilo limetumika kuwafikia wananchi moja kwa moja kwa kuwapa taarifa za huduma zinazotolewa na kuwaelekeza namna ya kutumia fursa zilizopo kwa maendeleo yao binafsi na taifa kwa ujumla. “Tunatumia jukwaa hili ku...

NBS YAONA TAKWIMU NI NGUZO MUHIMU YA UTEKELEZAJI WA DIRA 2050

Picha
Na Hamida Ramadhan, Dodoma.  OFISI ya Taifa ya Takwimu (NBS) imesema takwimu rasmi zitakuwa nyenzo muhimu katika kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inayolenga kuifikisha Tanzania katika uchumi wa dola trilioni moja na kuongeza kipato cha wananchi. Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa NBS, Daniel Masolwa, alisema hayo wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea jijini Dodoma, ambapo taasisi hiyo inashiriki kutoa elimu kwa wananchi kuhusu huduma na majukumu yake. Masolwa amesema kaulimbiu ya mwaka huu inayosema “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu” imeipa NBS fursa ya kueleza umuhimu wa takwimu rasmi katika kupanga maendeleo, kufanya maamuzi sahihi na kufuatilia utekelezaji wa mipango mbalimbali ya taifa. Amesema kwa mujibu wa Sheria ya Takwimu, Sura ya 351, NBS imepewa mamlaka ya kukusanya, kuchakata na kusambaza takwimu rasmi zinazotumika katika sekta mbalimbali za maendeleo. “Takwimu rasmi ni msingi wa upangaji ...

WANANCHI WATAKIWA KUHESHIMU HAKI ZA WATOTO

Picha
Na. Wellu Mtaki, Dodoma.  Wazazi na walezi wamehimizwa kuwalea watoto katika maadili mema ili kuwaepusha na tabia za kuiga zisizofaa ambazo zinaweza kuwaletea madhara katika maisha yao.  Sambamba na hilo, wananchi wametakiwa kutambua na kuheshimu haki za watoto ili kuhakikisha wanakua katika mazingira salama na yenye upendo. Kauli hiyo imetolewa na Kamishna wa Ustawi wa Jamii, Faithmary Lukindo, alipokuwa akimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Eliakim Chacha Maswi, katika maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika Kituo cha Malezi ya Watoto Kikombo jijini Dodoma. Maadhimisho hayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo viongozi wa kijiji, viongozi wa dini, wastaafu pamoja na waimbaji wa Kwaya ya Gethsemane. Akizungumza katika hafla hiyo, Lukindo alisema mtoto anapopewa haki ya kusikilizwa na kutoa maoni yake, hujengewa hali ya kujiamini na kujiona mwenye thamani ndani ya familia na jamii inayomzungu...

CCM YASHITUKA KUHUSU MIKUTANO YA KUCHOCHEA MAAANDAMANO.

Picha
  Na Jasmine Shamwepu, Dodoma.  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kinazo taarifa zinazoashiria kuwepo kwa mikutano inayofanywa na baadhi ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambayo inadaiwa kuhusisha mipango ya kuhamasisha maandamano yenye uwezekano wa kuvuruga hali ya amani nchini. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) wa CCM anayeshughulikia Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani Kihongosi, alisema chama hicho kimeendelea kuwataka Watanzania kuzingatia umuhimu wa utulivu na mshikamano wa kitaifa. Kihongosi ameeleza kuwa CCM inaamini maendeleo endelevu hayawezi kupatikana iwapo kutakuwa na misukosuko ya kisiasa, akisisitiza kuwa tofauti za vyama zinapaswa kuishia kwenye majadiliano ya sera. Alisema chama hicho kinatoa tahadhari kwa wananchi kutoshawishika kushiriki katika matukio yanayoweza kusababisha machafuko, akibainisha kuwa amani ndiyo msingi wa maendeleo ya taifa. “Taarifa tulizonazo zinaonyesha k...

WACHIMBAJI WATAKIWA KUJIUNGA WCF

Picha
  Na Mwandishi wetu, Mirerani.  WACHIMBAJI wa madini nchini wametakiwa kuwalipia wafanyakazi wao asilimia 0.5 ya mishahara yao ili kuwachangia kwenye mfuko wa fidia kwa wafanyakazi utakaowanufaisha pindi wakipata madhila kupitia mafao saba. Mwakilishi wa Meneja mkuu wa mfuko wa fidia kwa wafanyakazi (WCF) Naanjela Msangi ameeleza hayo akizungumza na viongozi wa wachimbaji madini ya Tanzanite mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara. Msangi ameeleza kuwa endapo wamiliki wa migodi wakiwalipia wafanyakazi wao asilimia 0.5 ya mishahara yao kila mwezi watanufaika na mambo mengi ikiwemo kujikinga na kuzuia vihatarishi vya ajali. Amesema endapo wafanyakazi wakichangiwa watanufaika kwa kulipwa fidia katika sekta rasmi wanaopata ajali, ugonjwa ama kufariki dunia. "Katika kuteketeza jukumu hili WCF inatoa jumla ya mafao saba ambayo ni huduma ya matibabu, malipo ya ulemavu wa muda na wa kudumu na malipo kwa anayemhudumia mgonjwa," amesema Msangi. Ametaja mafao mengine ni ...

ZFCT YARIDHISHWA NA MAFUNZO YA FCC KUHUSU USIMAMIZI WA MASHAURI YA USHINDANI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam.  BARAZA la Ushindani Halali Zanzibar (ZFCT) limefanya ziara ya mafunzo katika Tume ya Ushindani ya Haki (FCC) kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu katika masuala ya ushindani wa biashara, udhibiti wa bidhaa bandia pamoja na usimamizi wa mashauri yanayohusiana na ushindani. Ziara hiyo iliyofanyika katika ofisi za FCC Juni 10, 2026 Jijini Dar es Salaam, imeelezwa kuwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi hizo mbili ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao na kuhakikisha mazingira ya biashara yanakuwa ya haki kwa wadau wote. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa alisema kuwa kubadilishana uzoefu na taasisi za ndani ya nchi ni muhimu katika kuimarisha mifumo ya usimamizi wa ushindani na kulinda maslahi ya watumiaji dhidi ya vitendo vinavyokiuka sheria za ushindani na biashara. Alisema ujumbe wa ZFCT unapata fursa ya kujifunza namna FCC inavyotekelez...

TCDC YATOA ELIMU YA MALIPO KWA NJIA YA BENKI NA SIMU WILAYA YA MEATU

Picha
Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC) imetoa mafunzo ya elimu kuhusu mfumo wa malipo ya zao la pamba kwa njia ya benki na simu katika Wilaya ya Meatu, mafunzo hayo yamehusisha Makatibu Mameneja, Wenyeviti na Makarani wa AMCOS 71 kutoka wilaya hiyo.

BAROZI MATINYI AKABIDHI HATI KWA RAIS WA ALGERIA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Algeria.  BAROZI wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare  Matinyi, amekabidhi hati za utambulisho wa kibalozi kwa Mhe. Rais Abdelmadjid Tebboune wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria katika hafla iliyofanyika kwenye Ikulu ya jijini Algiers, tarehe 10 Juni, 2026, ikiwa ni ishara ya kuanza rasmi utekelezaji wa majukumu ya kibalozi. Katika mazungumzo yao mafupi yaliyofuatia baada ya hafla hiyo, Mhe. Balozi Matinyi alimshukuru Mhe. Rais Tebboune, serikali na watu wa Algeria kwa niaba ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kudumisha ushirikiano wa kindugu wa nchi hizi mbili ambao umedumu kwa zaidi ya miongo sita. Akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya mazungumzo yake na Mhe. Rais Tebboune, Balozi Matinyi alisema kwamba walijadiliana namna ya kusonga mbele baada ya kufikia mafanikio mazuri katika sekta za ulinzi na elimu ya juu ili kuhakikisha watu wa nchi hizi wananufaika pia katika sekta zingine muhimu. Mh...

UNYONYAJI WA WAFANYAKAZI WA MAJUMBANI BADO WATAJWA KUWA CHANGAMOTO

Picha
Na Jasmine Shamwepu, Habari Kamili Blog-Dodoma.  MATUKIO ya unyonyaji, mishahara duni na ukosefu wa mikataba ya ajira yameendelea kutajwa kuwa miongoni mwa changamoto zinazoathiri ustawi wa wafanyakazi wa majumbani nchini, hali inayochochea wito wa kuwepo kwa hatua zaidi za kuwalinda. Hayo yameelezwa na wadau wa sekta ya ajira wakati wa mkutano wa kujadili utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Kazi za Majumbani wa mwaka 2025/26 hadi 2029/30 uliofanyika jijini Dodoma. Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Majumbani nchini, Zanini Athumani, amesema pamoja na umuhimu wa kazi za majumbani katika jamii, bado baadhi ya wafanyakazi wanakabiliwa na mazingira yasiyozingatia haki zao za msingi. Amesema changamoto hizo zinajumuisha kucheleweshwa kwa mishahara, kutokuwepo kwa mikataba ya kazi na kukosekana kwa mifumo madhubuti ya kushughulikia malalamiko wanayokumbana nayo. “Wafanyakazi wengi wa majumbani bado wanahitaji ulinzi zaidi ili waweze kufanya kazi zao kwa usalama na kupata stahiki zao ...

WAKAZI USUNGA WAFURAHIA MRADI WA MAJI

Picha
  Na Allan Kitwe, Sikonge.  WAKAZI wa Kijiji Cha Usunga, Kata ya Usunga Wilayani Sikonge Mkoani Tabora wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwapelekea mradi wa maji safi na salama ya kunywa. Wametoa shukrani hizo kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 58 tangu kuanzishwa kwa Kijiji hicho zilizofanyika jana kwenye uwanja wa CCM (Centre) na kueleza bayana kuwa serikali imemaliza kilio chao cha muda mrefu. Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji hicho James Mgulu ameeleza kuwa mradi wa maji katika Kijiji hicho umeleta neema, furaha na shangwe kwa wananchi kwa sababu familia zao zilikuwa zinapata shida sana kwa kukosa maji safi na salama. ‘Tuna kila sababu ya kuishukuru serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutuletea mradi huu wa maji na miradi mingine ya maendeleo, wananchi sasa wana amani tele, na maisha yao yamekuwa bora zaidi’, ameeleza.  Ameongeza kuwa wanapoadhimisha sherehe hiyo kila mwaka wanalenga kudumisha mila, utamad...

MIUNDOMBINU CHUO CHA NYUKI TABORA YABORESHWA

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora.  CHUO Cha Ufugaji Nyuki (BTI) Tabora kimeendelea kuboresha miundombinu yake kwa kujenga jengo jipya la kisasa la mihadhara linalogharimu zaidi ya shilingi milioni 500, utekelezaji mradi huu umefikia zaidi ya asilimia 48. Hayo yameelezwa jana na Mkuu wa Chuo hicho Semu Daud alipokuwa akiongea na mwandishi wa gazeti hili ofisini kwake, ambapo ameeleza kuwa jengo hilo litaboresha ufundishaji wa wakufunzi na kutatua changamoto ya uhaba wa vyumba vya madarasa chuoni hapo. Amefafanua kuwa ujenzi wa jengo hilo unafadhiliwa na Mfuko wa Misitu Tanzania (TAFF) ambao wametoa kiasi cha shilingi milioni 500 sawa na asilimia 82 huku shilingi milioni 92 sawa na asilimia 20 zikitoka kwenye mfuko wa chuo. Ukumbi huo utakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 400 kwa wakati mmoja hivyo kukamilika kwake kutatoa fursa kwa wanafunzi wengi zaidi kujiunga na fani ya ufugaji nyuki. Mkuu amedokeza kuwa kupitia mradi huo mbali na wanafunzi kuongezeka chuoni hapo pia utasaidia kufa...

WILAYA YA LUSHOTO YAPOKEA MRADI WQ USAMBAZAJI NA UUZAJI WA MITUNGI YA GESI KWA BEI YA RUZUKU.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Lushoto - Tanga.  WANANCHI wa Wilaya ya Lushoto wamepata fursa mpya ya kunufaika na nishati safi ya kupikia baada ya wilaya hiyo kupokea rasmi mradi wa usambazaji na uuzaji wa mitungi ya gesi ya kilo sita kwa bei ya ruzuku unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).  Mradi huo umepokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Mheshimiwa Zephania Sumaye, kwa niaba ya wananchi wa wilaya hiyo, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuhakikisha nishati safi ya kupikia inawafikia Watanzania wengi zaidi. Hafla ya mapokezi ya mradi huo imefanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Lushoto na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, maafisa kutoka REA pamoja na wawakilishi wa kampuni ya Manjis Logistics Limited, ambayo imepewa jukumu la kutekeleza mradi huo kwa kushirikiana na REA. Mradi huo ni miongoni mwa miradi ya kimkakati inayotekelezwa na REA nchini kwa lengo la kuharakisha upatikanaji wa nishati safi na salama kwa wananchi, kupunguza utegemezi wa kuni ...