Machapisho

ASKARI WA TFS WAPONGEZWA KULINDA SHAMBA LA MITI SILAYO.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Chato WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb),amewapongeza askari wa uhifadhi kutoka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) wanaofanya kazi katika Shamba la Miti Silayo, wilayani Chato, kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kulinda na kuhifadhi shamba hilo kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo. Dkt. Kijaji ametoa pongezi hizo leo, Aprili 16, 2026, alipokuwa katika ziara ya kukagua shamba hilo, akibainisha kuwa mafanikio yaliyopatikana yametokana na ari ya kujituma, mshikamano na umoja wa askari hao katika kuhakikisha shamba linabaki katika hali bora na ya kuridhisha. “Niwapongeze sana askari wetu mnaofanya kazi nzuri sana huku uwandani. Kazi yenu ni njema mno, tunawapongeza sana. Na pongezi hizi hazitoki kwangu tu, bali zinatoka moja kwa moja kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye amenituma kuwafikishia pongezi hizi,” amesema Dkt. Kijaji. Aidha, ameongeza kuwa kazi wanayoifanya askari hao ni muhimu sana ...

CCM YATAKA WATENDAJI, WATAALAMU KUWAJIBIKA IPASAVYO

Picha
  Na Gilbert Dioniz na Allan Kitwe, Ngara CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Wilayani Ngara Mkoani  Kagera kimewataka Watendaji na Wataalamu waliopewa dhamana kusimamia miradi ya maendeleo kuwajibika ipasavyo katika nafasi zao ili kuharakisha maendeleo ya wananchi. Kauli hiyo imetolewa jana na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ngara Vitalice Ndairagije kwenye ziara ya Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya kukagua miradi ya maendeleo. Amesema kuwa kiu ya wananchi ni kuona miradi inayotekelezwa na serikali yao inakamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa, na hili haliwezi kufanikiwa kama Watendaji na Wataalamu waliopewa dhamana hawatafanya kazi kwa weledi. ‘Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuleta mamilioni ya fedha hapa Ngara kwa ajili ya miradi ya maendeleo, fedha hizi tunataka zifanye kazi iliyokusudiwa na zisimamiwe ipasavyo’, amesema. Mwenyekiti alidokeza kuwa miradi ikisimamiwa ipasavyo itakamilika kwa wakati na thamani ya fedha zilizotumika ...

HATUA MPYA PANGANI! USAMBAZAJI WA MITUNGI YA GESI YA RUZUKU WAANZA RASMI

Picha
  Na Mwandishi Wetu Pangani.  WILAYA ya Pangani mkoani Tanga imepiga hatua muhimu katika kuboresha maisha ya wananchi wake kupitia utambulisho wa mradi wa uuzaji na usambazaji wa mitungi ya gesi ya kilo sita kwa bei ya ruzuku. Mradi huo unalenga kuongeza upatikanaji wa nishati safi na salama ya kupikia, hususan kwa kaya zenye kipato cha chini. Akizungumza wakati wa hafla ya kutambulisha mradi huo mbele ya katibu tawala wa Wilaya ya Pangani, Bi. Ester Gama, msimamizi wa mradi  kutoka REA, Ndugu Abdulrazack Mkomi ameeleza kuwa lengo kuu la mradi huo ni kupunguza matumizi ya kuni na mkaa, ambayo yamekuwa yakichangia uharibifu wa mazingira pamoja na athari za kiafya kwa wananchi, hasa wanawake na watoto. Alifafanua kuwa kupitia mradi huo, mitungi ya gesi ya kilo sita itapatikana kwa bei nafuu ya shilingi 17,500 tu kutokana na ruzuku iliyotolewa, hali itakayowezesha wananchi wengi zaidi kuimudu na kuanza kutumia nishati mbadala iliyo rafiki kwa mazingira.  Aidha, mfumo mz...

SALALI: AIPONGEZA SERIKALI KUANDA SERA INAYOZINGATIA MAKUNDI MAALUM

Picha
  Na Carlos Claudio, Dodoma. Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Foundation Disability Hope (FDH), Maiko Salali, ameipongeza serikali kwa kuandaa sera jumuishi inayozingatia makundi maalum, ikiwemo watu wenye ulemavu, hatua aliyoieleza kuwa ni muhimu katika kukuza usawa wa kijamii na kiuchumi nchini. Akizungumza leo Jumatano, 2026, katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma, wakati wa uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Mnyororo wa Ugavi ya Mwaka 2025, Salali alisema sera hiyo imezingatia kwa kiasi kikubwa dhana ya ujumuishwaji. Alieleza kuwa utekelezaji wa sheria ya ununuzi wa umma inayotenga asilimia 30 kwa makundi maalum umeendelea kufungua milango ya fursa kwa watu wenye ulemavu kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi. “Tumeridhishwa na namna sera hii ilivyozingatia ujumuishwaji. Hata watu wenye ulemavu wa kuona wamewezeshwa kuipata sera hii kupitia maandishi ya nukta nundu,” alisema Salali. Aidha, alibainisha kuwa uongozi wa Rais S...

WADAU WA KILIMO WAOMBA SERIKALI KUONDOA KODI YA ONGEZEKO (VAT)

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  WADAU wa Kilimo wameiomba serikali kuondoka kodi ya ongezeko la thamani (VAT) ya asilimia 18 kwenye mifuko ya tabaka ya kuhifadhia mazao ya nafaka na mbegu ili kuwesha wakulima kuongeza kipato na usalama wa chakula. Hayo yalielezwa Jijini Dodoma  na Afisa Mradi Jukwaa la Wadau wa Kilimo wasiokuwa wa Kiserikali (ANSAF)  Werner Hillary wakati akifungua warsha ya kujadili maboresho ya kisera ili kudhibiti changamoto za upotevu kwa wakulima wadogo kwa kushirikiana na Shirika la Helvetas. " Warsha hii ilitohusisha wadau mbalimbali wa Kilimo ikiwemo Serikali, wazalishaji wadogo na Asasi za Kiraia ni sehemu ya mradi unaotekelezwa kwa ushirikiani wa Helvetas Tanzania, SAT, Chuo cha Kilimo SUA na Chuo Kikuu cha Zurich. Afisa huyo amesema lengo la wadau kuiomba Serikali kuondoa kodi ya VAT ni kuwezesha wakulima wadogo kuwa na uwezo wa kununua na kutumia mifuko hiyo inayozuia wadudu waharibifu na upotevu wa nafaka. "Matumizi ya mifuko ya tabaka hus...

ENABEL YAWEZESHA MABINTI 200 KASULU KUPATA ELIMU

Picha
  Na Allan Kitwe, Kasulu.  SHIRIKA la Maendeleo la Ubelegiji (ENABEL) limeunga mkono juhudi za serikali kwa kuwezesha watoto wa kike zaidi ya 200 Wilayani Kasulu Mkoani Kigoma kupata mafunzo ya ujuzi katika Chuo Cha Maendeleo ya Wananchi Kasulu (FDC). Hayo yamebainishwa jana na Mkuu wa Chuo hicho Fridegarda Mukyanuzi alipokuwa akiongea na waandishi wa habari Ofisini kwake ambapo ameeleza kufurahishwa na ujio wa mradi huo ili kuwezesha wasichana wasio na uwezo. Amebainisha kuwa kupitia mradi huo Shirika limegharamia mahitaji yote ya Chuo kwa watoto hao na kuwawezesha kusoma fani mbalimbali za ufundi ikiwemo ushonaji nguo, ususi na urembo, umeme wa majumbani na ufundi bomba. Fani nyingine ni ufundi magari, uchomeleaji na uungaji vyuma, umeme wa magari na wa majumbani na kila wanapohitimu Shirika huwawezesha vifaa vya kuanzia shughuli zao. Amefafanua kuwa mradi huo wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 600 umekuwa mkombozi kwa Chuo na kwa watoto hao kwani umesaidia kuboresha...

AKAMATWA NA POLISI KWA KUTOA MIMBA YA MIEZI 6

Picha
Na Allan Kitwe, Tabora JESHI la Polisi Mkoani Tabora linamshikilia mwanamke mmoja (21) mkazi wa Mtaa wa Singo, Kata ya Gongoni katika halmashauri ya manispaa Tabora kwa tuhuma za kutoa ujauzito wake unaokadiriwa kuwa na umri wa miezi 6. Kamanda wa Polisi Mkoani hapa Richard Abwao amethibitisha kutokea tukio hilo Aprili 6 mwaka huu majira ya saa 12.45 za jioni katika Kata hiyo ambapo mwanamke huyo mpare, mkristo na mkulima aligundulika kufanya kitendo hicho. Amesema kuwa mtuhumiwa baada ya kumeza dawa ya kutoa ujauzito huo, uchafu aliuweka kwenye kopo na kuufunga kwenye mfuko ili akautupe kwenye shimo la takataka lililo jirani na eneo hilo. Kamanda ameongeza kuwa mbali na mtuhumiwa huyo pia wamemkamata mwanaume mmoja (25) msukuma, mkazi wa Kata ya Chemchem katika manispaa hiyo ambaye ni Mtaalaumu wa Maabara aliyempatia dawa za kutolea mimba hiyo. Ameeleza sababu ya kutoa ujauzito huo kuwa ni mwanaume aliyempa mimba hiyo kuikataa hivyo akaamua kwenda kwa Mtaalaumu binafsi wa Maabara ili ...

MRADI WA ESP KUNUFAISHA WASICHANA ZAIDI YA 60 NZEGA.

Picha
Na Allan Kitwe, Tabora.  WASICHANA zaidi ya 60 wanaotoka katika familia zisizo na uwezo Wilayani Nzega Mkoani Tabora wanatarajiwa kunufaika na mradi wa uwezeshaji mtoto wa kike kupata ujuzi (Empowerment Through Skills Program in Tanzania-ESP). Mradi huo unaofadhiliwa na nchi ya Canada (Canada Fund) kwa lengo la kuwezesha watoto wa kike wanaoishi katika mazingira magumu kupata fursa za ujuzi, unatekelezwa katika Vyuo 12 viivyopo katika Mikoa zaidi ya 8 hapa nchini. Chuo cha Maendeleo ya Wananchi (FDC) Mwanhala, Nzega ni miongoni mwa vyuo 12 vilivyoingizwa katika program ya ufadhili ili kutoa mafunzo hayo ya muda mfupi (short course) kwa watoto wa kike.   Akizungumza juzi na waandishi wa habari kwa niaba ya Mkuu wa Chuo hicho Enock Lalida, Afisa Utumishi Hekima Amri Lupembe ameeleza kuwa mradi huo ni muhimu sana kwa kuwa unawapa fursa watoto wa kike kupata ujuzi. ‘Wasichana 30 wanaotoka katika kaya zinazoishi katika mazingira magumu Wilayani hapa tayari wamesajiliwa na kuan...

RUWASA KIGOMA WAMWAGA PONGEZI KWA RAIS SAMIA

Picha
  Na Allan Kitwe, Kigoma.  WAKALA wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mkoani Kigoma wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 79 za miradi ya maji. Pongezi hizo zimetolewa na Meneja wa Wakala huo Mkoani hapa Mhandisi Mathius Mwenda alipokuwa akiongea kwenye mahojiano maalumu na waandishi wa habari Ofisini kwake. Amesema kuwa RUWASA Kigoma ina kila sababu ya kuishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kufanikisha utekelezaji miradi mbalimbali ya maji katika Wilaya zote 7 za Mkoa huo hivyo kupunguza kwa kiasi kikubwa kero ya maji. Mhandisi Mwenda amebainisha kuwa kuanzia Machi 2021 hadi Februari 2026, Rais Dkt Samia Suluhu Hassan alitenga zaidi ya shilingi bilioni 79 kwa ajili ya kutekeleza miradi 113 ya maji katika maeneo mbalimbali ya Mkoa huo. Amedokeza kuwa kati ya kiasi hicho cha fedha, serikali ilitoa jumla ya shilingi bilioni 55.9 na wadau wakaiunga mkono kwa kutoa kiasi cha shiling...

ASKOFU MEIVUKIE AASA JAMII KUCHUKUA TAHADHARI

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora WAKRISTO na jamii kwa ujumla wameaswa kuchukua tahadhari na kumwomba Mungu ainue wapatanishi dhidi ya mataifa ya Marekani, Israel na Iran ili vita inayoendelea sasa baina yao imalizike kwa amani ili kuepusha athari kwa jamii. Wito huo umetolewa jana na Askofu Paul Meivukie wa Kanisa la TAG-Jimbo la Tabora Kati ambaye pia ni Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Kitete Christian Centre (KCC) alipokuwa akitoa salamu za pasaka kwenye ibada kanisani hapo. Amesema kuwa athari za vita vinavyoendelea sasa katika mataifa hayo ni kubwa mno, na Tanzania sio kisiwa, haiwezi kujitegemea kwa kila kitu, hivyo ni muhimu sana kumwomba Mungu na kutumia vizuri chakula tulicho nacho. Huu sio wakati wa kulaumu viongozi bali kuwaombea ili Mwenyezi Mungu awaongoze na kuwapa hekima ya kutoa maamuzi sahihi ili kuepusha bei za bidhaa kupanda zaidi hali inayoweza kuleta shida kwa wananchi. ‘Sote tunafahamu vita inayoendelea baina ya Marekani, Israel na Iran, naomba tuendelee kuchukua taha...

AFISA USAFIRISHAJI SIMANJIRO KORTINI KWA WIZI

Picha
  Na Mwandishi wetu, Simanjiro.  Afisa usafirishaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, Ismail Khalifan amefikishwa mahakamani kwa kosa la jinai la wizi wa shilingi 500,000 akiwa mtumishi wa umma. Afisa usafirishaji huyo Ismail amefikishwa kwenye mahakama ya wilaya ya Simanjiro na kusomewa shitaka hilo la wizi wa shilingi 500,000 fedha ambazo ni mali ya Halmashauri hiyo. Mwendesha mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na rushwa (TAKUKURU) Faustin Mushi amesoma shataka hilo Aprili mosi, 2026 mbele ya hakimu mkazi mkuu mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Simanjiro Charles Uisso. Mushi amesema Ismail anashtakiwa kwa kosa la wizi akiwa mtumishi wa umma kinyume na kifungu cha 258 (1), 265 na 270 vya sheria ya kanuni ya adhabu sura ya  16 R:E 2023. Amesema Ismail anashitakiwa kwa kosa la wizi wa shilingi 500,000 alizopewa na mwajiri wake kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya magari ya halmashauri ya wilaya hiyo. Amesema katika kesi hiyo ya jinai namba 7118/2026...

MWENYEKITI MAREMA AWASIHI WACHIMBAJI KUSAIDIA WAATHIRIKA WA MAFURIKO

Picha
  Na mwandishi wetu, Mirerani.  MWENYEKITI wa chama cha wachimbaji madini Mkoa wa Manyara (MAREMA) Elisha Nelson Mnyawi amewaomba wadau wa madini kujitolea na kuwasaidia waathirika wa mafuriko katika Tarafa ya Moipo. Mwenyekiti huyo wa MAREMA Mnyawi ameyasema hayo mji mdogo wa Mirerani, leo jumapili Machi 29,2026 wakati akikabidhi kwa Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mwalimu Fakii Raphael Lulandana vyakula na vifaa vya thamani ya shilingi milioni 22 vilivyotolewa na kampuni ya Permanent Mining LTD kwa ajili ya waathirika wa mafuriko katika Tarafa ya Moipo. Ameeleza kuwa japokuwa wachimbaji madini wamekuwa wakijitoa mara kwa mara kupitia hisani kwa jamii (CSR) wasiliache hilo likapita bila kuchangia chochote. Amesema wachimbaji mbalimbali ikiwemo Franone Mining, God Mwanga, Chusa Mining, California Camp, Bilionea Saniniu Laizer, Sunda Mining wamekuwa wakisaidia jamii wasaidie pia waathirika hao waliokumbwa na mafuriko. "Kupitia hadhara hii nampongeza Mkurugenzi wetu God Charity amba...

MTI MMOJA, ENEO AMBALO SIMBA HULITUMIA KWA HONEYMOON KRETA YA NGORONGORO.

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Ngorongoro.  UNAWEZA kustaajabu lakini ukweli upo hivyo, ukitaka kuwaona simba wakiwa katika harakati za kuongeza familia fika katika  Kasoko ya Ngorongoro eneo la mti mmoja ambalo limezungukwa na vichaka, miti na nyasi za wastani. Eneo hili ni maarufu sana kwa waongoza utalii kutokana na makundi ya simba waliopo katika hifadhi hiyo kupenda kupumzika  na hasa wanapokuwa katika msimu wao wa kujamiina ama kutafuta watoto na kuongeza familia. Simba hupenda kujamiiana mara baada ya kushiba ambapo zoezi hilo linafanyika mda wowote mchana au usiku. Tofauti na Binadamu ambapo Kazi Ngumu hufanywa na wanaume, kwa Simba ni tofauti, kazi ya kutafuta chakula ama Mawindo kwa ajili ya msosi wa familia huongozwa na simba jike ambapo mara baada ya kuhisi njaa na tamaa ya kujamiina huamua kutafuta chakula ili kwanza kushiba halafu kuingia kwenye harakati ya kuongeza familia. Wakati wa mawindo simba huchagua chakula cha kushiba na hapa ina maana simba hahangaiki s...

TANZANIA YASHINDA TUZO YA KIMATAIFA YA UFADHILI WA MIUNDOMBINU.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Afrika Kusini.  SERIKALI kupitia Wizara ya Fedha imeendelea kung’ara kimataifa baada ya kushinda tuzo ya “Infrastructure Finance Deal of the Year 2026” zinazotolewa na Global Banking & Markets, kufuatia mafanikio ya upatikanaji wa mkopo wenye masharti nafuu wa dola za Marekani bilioni 1.78 kwa ajili kugharamia ujenzi wa reli ya kisasa ya umeme (SGR) kwa kipande cha tatu na cha nne. Tuzo hiyo imepokelewa na Kaimu Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Rished Bade, kwa niaba ya Wizara ya Fedha katika hafla ya utoaji Tuzo za Global Banking & Markets iliyofanyika jijini Cape Town, Afrika Kusini. Ushindi huo unatokana na mpango mahiri wa utafutaji ufadhili wa mradi huo mkubwa wa kimkakati, unaotarajiwa kuchochea ukuaji wa uchumi na kurahisisha usafirishaji nchini na Ukanda wa Maziwa Makuu, mkopouliopatikana kupitia ushirikiano kati ya taasisi za bima kutoka nchi za Sweden, Poland na Italy pamoja na Benki za Maendeleo za Kikanda, chini ya uratibu wa Benki ya St...

DAKTARI HATIANI KUUZA SARUJI NA MATOFALI ZAHANATI SUKURO

Picha
  Na Mwandishi wetu, Simanjiro.  MGANGA mfawidhi wa zahanati ya kijiji cha Sukuro kata ya Komolo wilayani Simanjiro mkoani Manyara, Dk Daud Ndagala ametiwa hatiani kwa ubadhirifu wa mifuko ya saruji na matofali ya kukarabati zahanati hiyo. Mahakama ya wilaya ya Simanjiro imemtia hatiani Dk Ndagala kupitia shauri la jinai namba 4344/2026 kwa makosa mawili ya uhujumu uchumi. Hakimu mkazi mkuu mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Simanjiro Charles Uisso amesoma hukumu hiyo Machi 26,2026 na mwendesha mashtaka wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (Takukuru) kituo maalum cha Mirerani Gervas Sarakikiya. Hakimu Uisso ameieleza mahakama hiyo kuwa Dk Ndagala ametiwa hatiani kwa kufuja Sh1 milioni za mauzo ya mifuko 57 ya saruji ya kukarabati zahanati hiyo. Amesema pia, Dk Ndagala alichepusha tofali 220 zilizoandaliwa kwa ajili ya ukarabati huo kisha akaziuza Sh605,000 kwa mtu binafsi. Amesema mshtakiwa huyo amefanya makosa hayo akitumia nafasi yake ya mganga mfawidhi wa zahanati ya ...

MAMBO YALIYOJIFICHA KUHUSU HIFADHI YA TAIFA YA MILIMA UDZUNGWA

Picha
  1. Hifadhi ina njia mbalimbali za matembezi ya miguu na jumla ya Maporomoko ya maji 6 (Sanje, Sonjo, Njokamoni, Prince Benhard, Ichonde na Mwaya). 2. Vilele vikubwa vya  Milima (Luhomero mita 2,576  na Mwanihana mita 2,500 kutoka usawa wa bahari). 3. Kitovu cha Viumbe Adimu. Udzungwa ina viumbe wengi adimu ambao huwezi kuwapata mahala popote duniani. Spishi hizo ni pamoja na jamii mbili za primata (Ngolaga wa Sanje na Mbega wekundu wa Iringa), Spishi 2 za ndege (Kware wa Milima ya Udzungwa na “Rufous-winged Sunbird), Spishi 4 adimu za mimea ambapo moja wapo ni “Vernonia luhomeroensis”, Spishi 3 za vipepeo ambazo ni pamoja na “Charaxes lucyae mwanihanae”, Spishi ya Nyoka aitwaye “Red Snouted Wolf Snake na viumbe wengine wengi. 4. Baadhi ya Spishi nyingine adimu zinapatikana katika Milima ya Tao la Mashariki (Eastern Arc Mountains) baadhi ya spishi hizo  ni pamoja na Kinyonga Mfupi (Pygmy Chameleon).  #UdzungwaNountainsNationalPark #HikingParadise #tanzaniaparks...