Machapisho

HALMASHAURI YA JIJI LA DAR KURASIMISHA SHUGHULI ZA WACHAKATAJI TAKA KUJIINUA KIUCHUMI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam.  HALMASHAURI ya Jiji la Dar es Salaam kupitia Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji imeendelea kuchukua hatua za kuimarisha uchumi wa Wananchi kwa kurasimisha shughuli za wachakataji wa taka rejea. Kupitia kikao kilichofanyika tarehe 18 Machi 2026,  katika ukumbi mdogo wa meya Jijini Dar es salaam. wadau wamepewa mwongozo wa namna ya kufanya shughuli zao kwa kuzingatia sheria, ikiwemo usajili na upatikanaji wa leseni za biashara. Hatua hii inalenga kufungua fursa zaidi za ajira kwa vijana na wanawake, kulinda mazingira, na kuongeza kipato kwa wajasiriamali wadogo. Aidha, urasimishaji huu utawezesha upatikanaji wa elimu, teknolojia na masoko bora, hivyo kuchangia maendeleo endelevu ya jiji.

CCM SIMANJIRO WAENDELEA NA ZIARA

Picha
  Na Mwandishi wetu, Simanjiro.  SEKTRETARIETI ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, imeendeleza na ziara ya kata mbalimbali ili kushukuru, kusikiliza kero na kukagua uhai. Katibu wa CCM Wilaya ya Simanjiro, Wambura Igembya ameongoza wajumbe wa sekretarieti hiyo katika ziara ya kutembelea kata hizo. Wambura ameongozana na wajumbe wa sekretarieti ya CCM ya Wilaya hiyo, akiwemo Katibu Mwenezi Mosses Makeseni, Katibu wa Wazazi Sasi Mirumbe na Katibu wa UWT Tichomo Sangija Amesema lengo la ziara hiyo ni kuwashukuru wana Simanjiro kwa kuichagua CCM kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2026, kusikiliza kero zao na kukagua uhai wa chama. "Tunawashukuru wana Simanjiro kwa kumpa kura nyingi za kishindo Rais Samia Suluhu Hassan, kumchagua mbunge kwa tiketi ya CCM James Ole Millya ambaye ameteuliwa na Rais kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na kuwachagua madiwani wa CCM," amesema Wambura. Amesema katika ziara hiyo wataanza kwa kuzite...

NKINGA HOSPITALI YAOKOA MAISHA YA MAMA ALIYEPATA TATIZO LA KUJIFUNGUA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Nkinga - Igunga.  IDARA ya Wanawake na Uzazi katika Hospitali ya Rufaa ya Nkinga imefanikiwa kuokoa maisha ya bi. Mbalu Jisinza (45), mkazi wa kijiji cha Mwanzugi wilayani Igunga, aliyepata tatizo hatari la kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua, hali iliyohatarisha maisha yake kabla ya kupatiwa matibabu ya haraka na ya kibingwa hospitalini hapo. Akizungumza wakati anapatiwa matibabu Hospitalini hapa Bi.Jisinza amesema, anachokumbuka mara ya mwisho alikuwa kwenye kituo cha afya kwaajili ya kujifungua, ambapo alijifungua mtoto mfu kisha akaanza kutokwa na damu nyingi, juhudi za madaktari kuzuia  tatizo la kutokwa na damu zilishindikana wakamfanyia upasuaji wa kuondoa kizazi, lakini bado damu zilikuwa zinatoka. Akiwa kituoni hapo alianza kushindwa kupumua wakamuwekea mpira wa Oxygen akiwa hajitambui, alipata fahamu akiwa chumba cha (ICU) hapa Nkinga Hospitali, Bi.Mbalu amewashukuru madaktari na Wauguzi wa Nkinga Hospitali kwa huduma nzuri waliyompat...

MHUBIRI WA KIMATAIFA DKT DANA MOREY AWASHA MOTO WA INJILI TABORA

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora.  WAKAZI wa Manispaa ya Tabora na Mikoa jirani wamemiminika kwenye mkutano mkubwa wa injili unaohubiriwa na Mwinjilisti wa Kimataifa kutoka nchini Marekani Dkt Dana Morey ulioanza jana Mjini Tabora na kupokea baraka na uponyaji. Wakizungumza baada ya kuombewa na Mwinjilisti huyo wameeleza kufurahishwa na uamuzi wa Serikali ya Mkoa kuruhusu mkutano huo uendelee baada ya awali kuuzuia kwa kile kilichoelezwa kuwa wanagwa vitu visivyo na maadili kwa jamii. Mkazi wa kata ya Tambuka-Reli katika Manispaa hiyo Magreth Lutaha (60) amweleza kuwa alikuwa na tatizo la uoni hafifu kwa zaidi ya miaka 10 lakini baada ya kuombewa na Mwinjili huyo amepokea uponyaji na sasa anaona vizuri. ‘Namshukuru Mungu nilikuwa sioni vitu vya mbali na kichwa kilikuwa kinaniuma kwa muda mrefu sana ila baada ya maombi kichwa hakiumi tena na sasa naona hata vitu vya mbali’, amesema. Mariam Mayani (40) mkazi wa Nzega na Furaha Jungu (30) mkazi wa Kiloleni katika manispaa ya Tabora wamee...

BODI YA MAJI BONDE LA ZIWA TANGANYIKA YABORESHA VYANZO VYA MAJI

Picha
  Na Allan Kitwe, Kigoma.  BODI ya Maji ya Bonde laZiwa Tanganyika imefanikiwa kuboresha uhifadhi na utunzaji wa vyanzo vya maji vilivyopo katika Mikoa 8 na Halmashauri 28 za Miji, Manispaa na Wilaya zilizopo katika Ukanda wa Magharibi mwa Tanzania. Hayo yamebainishwa juzi na Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Tanganyika Bona Mremi alipokuwa akiongea na wanahabari Ofisini kwake Mkoani Kigoma. Amefafanua shughuli zilizofanywa na Bodi hiyo katika Kanda hiyo kuwa ni kulinda, kuhifadhi na kutunza vyanzo vya maji ikiwemo mabwawa, mito, chemichemi, maziwa, maeneo oevu na fukwe za bahari. Shughuli nyingine ni kufuatilia mwenendo wa maji katika vyanzo vyote na kugawa maji kwa matumizi mbalimbali, kuongeza idadi ya Jumuiya za Watumiaji Maji kutoka 8 hadi 12 na kupanda miti zaidi ya milioni 2 katika vyanzo vya maji. ‘Tunaishukuru sana Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zilizotuwezesha kutekeleza majukumu yetu ya kusimamia, ...

KATIBU CCM SIMANJIRO ALETA FARAJA LOIBORSIRET

Picha
  Na Mwandishi wetu, Simanjiro.  KATIBU wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, Wambura Igembya ameagiza bibi kizee mwenye umri wa miaka 105, Maria Nongululu mkazi wa kijiji cha Loiborsiret, kurerejeshewa ekari nne za shamba lake alilonyang'anywa na uongozi wa kijiji hicho. Katibu Wambura ametoa agizo hilo akiwa na sekretarieti ya CCM Wilaya hiyo, Katibu Mwenezi Mosses Makeseni, Katibu wa Wazazi Sasi Mirumbe na Katibu wa UWT Tichomo Sangija, katika ziara ya kuwashukuru kwa kuichagua CCM, kusikiliza kero na kukagua uhai wa chama. Katibu Wambura akizungumza Kwenye mkutano wa kijiji cha Loiborsiret ametoa agizo la bibi kizee huyo arejeshwe eneo lake kwani ni haki yake. ""Natoa maelekezo nikiwa katibu wa chama, udhibitisho wa eneo lake unajionyesha dhahiri, mama akarudishiwe eneo lake, kuwatumikia wananchi tuache kuwanyanyasa watu, tumechaguliwa ili tuwatumikie," amesema Igembya. Amesema CCM Wilaya ya Simanjiro, walipokea malalamiko na kero juu y...

ZAIDI YA WATOTO 173,255 IGUNGA KUPATIWA CHANJO YA POLIO BAADA YA KIRUSI KUGUNDULIKA JIJINI MWANZA

Picha
  Na Lubango Mleka, Igunga.  Zaidi ya watoto 173,255 wenye umri chini ya miaka kumi wanatarajiwa kupatiwa chanjo ya ugonjwa wa polio wilayani Igunga mkoani Tabora, kufuatia kugundulika kwa kirusi cha ugonjwa huo mkoani Mwanza. Hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za serikali kuzuia kusambaa kwa ugonjwa huo hatari, hasa kwa watoto wadogo ambao wako kwenye hatari kubwa ya maambukizi. Katika kujiandaa na zoezi hilo, Hospitali ya Wilaya ya Igunga imetoa elimu kwa wadau wa afya kwa lengo la kuwajengea uelewa pamoja na kuongeza nguvu ya uhamasishaji kwa jamii ili kuhakikisha mwitikio unakuwa mkubwa wakati wa utekelezaji wa chanjo hiyo. Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Mratibu wa Chanjo wilayani Igunga, Novat Bijana, pamoja na wataalam wengine wa afya, walisisitiza umuhimu wa jamii kujitokeza kwa wingi kuwapeleka watoto kupata chanjo ili kujikinga na madhara ya ugonjwa wa polio. Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Wilaya ya Igunga, Bi. Elizabeth Rwegasila, aliwataka wadau hao kufikisha ...

TANROADS YAPELEKA TABASAMU MWAMGONGO

Picha
Na Allan Kitwe, Kigoma.  WAKAZI wa Kitongoji cha Mgazo, Mtaa wa Lubona katika Kijiji cha Mwamgongo Kata ya Mwamgongo Wilaya ya Kigoma wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuanza kufungua barabara inayoingia kijijini kwao. Wakizungumza mbele ya waandishi wa habari jana wameeleza kuwa tangu nchi ipate uhuru mwaka 1961 Kijiji hicho hakijui usafiri wa barabara kwa sababu kiko kwenye milima na usafiri pekee wanaotegemea ni wa mitumbwi na boti. Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Lubona, Elias Lutaha ameeleza kufurahishwa na hatua ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuipatia TANROADS Kigoma shilingi bilioni 3 kwa ajili ya kuchonga milima na kuanza kufungua barabara hiyo. ‘Tangu tumepata uhuru barabara hii indo imeanza kufunguliwa, kwa sasa ukitoka Kigoma Mjini kupitia Mkongoro unafika katika Kitongoji hiki kwa usafiri wa barabara lakini haifiki Mwamgongo Kijijini’, ameeleza. ‘Barabara yetu imefunguliwa kutoka Chankere hadi hapa Mganzo lakini haifiki Mwamgongo, chonde chonde, Mheshimiwa R...

SERIKALI YAENDELEA KUTENGA MAENEO NA KUTOA LESENI KWA WACHIMBAJI WADOGO WA MADINI

Picha
Na Hamida Ramadhan,  Dodoma MKURUGENZI wa Ukaguzi wa Migodi na Mazingira kutoka Tume ya Madini, Hamisi Kamando, amesema serikali inaendelea kutenga maeneo maalum kwa ajili ya wachimbaji wadogo wa madini, kuwapatia leseni na kuwaendeleza ili waweze kunufaika na rasilimali za madini. Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dodoma, Mhandisi Kamando amesema kuwa kupitia Wizara ya Madini, serikali imeendelea kutenga maeneo ya uchimbaji wa madini kwa wachimbaji wadogo nchini, ambapo hadi sasa jumla ya maeneo 65 yamependekezwa kutengwa kwa ajili ya kugawiwa kwa wananchi. Amesema maeneo hayo yapo katika mikoa mbalimbali ya kimadini ikiwemo Mtwara, Manyara, Lindi, Morogoro, Dodoma, Tabora, Pwani, Tanga, Geita, Shinyanga, Mwanza, Mara, Mbeya na Ruvuma. Aidha amesema katika kipindi cha Julai hadi Desemba 2025, serikali ilitoa jumla ya leseni 5,983 za uchimbaji mdogo wa madini, sawa na asilimia 71 ya leseni zote zilizotolewa katika kipindi hicho, ambapo leseni hizo hutolewa kwa Watanzani...