Machapisho

TANZIA

Picha
  SPIKA WA BUNGE LA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE. MUSSA AZZAN ZUNGU (MB) ANASIKITIKA KUTANGAZA KIFO CHA MBUNGE WA PERAMIHO MHE. JENISTA JOAKIM MHAGAMA KILICHOTOKEA LEO 11,DESEMBA,2025 JIJINI DODOMA.

AMNESTY INTERNATIONAL YALISHUTUMU KUNDI LA HAMAS

Picha
SHIRIKA la Amnesty International limeishtumu Hamas na makundi mengine ya wapiganaji wa Kipalestina kwa mara ya kwanza kwa uhalifu dhidi ya ubinadamu, ikiwemo mauwaji, wakati na baada ya shambulio la Oktoba 7, 2023 lililochochea vita vya Gaza. #HamasIsISIS ##palestine #AmnestyInternational

UJUMBE WA LEO KUTOKA RSA TANZANIA

Picha
   NDANI ya Jiji la Dar es Salaam au kwengineko ukiendesha kwa mwendo wa wastani wa kati ya 50-60Kph kwenye Zebra yoyote utaweza kusimama na kuwapisha wavukaji wavuke, ila spidi ikizidi hapo sio rahisi kusimama hasa mwenda kwa miguu anapotokea ghafla.  Hata hivyo, Jizoeshe Kusimama kwenye kila zebra kupisha watu wavuke, maana hata wewe ni mwenda kwa miguu ukitoka kwenye usukani.  Usiposimama kuwapisha, hawatakuwa na mahala pengine salama pa kuvuka zaidi ya kuhatarisha maisha yao.  Hivyo jambo la kwanza ondoa ile kasumba au mtazamo kuwa *Aagh wasumbufu hawa*, kwakuwa hata wao hao unaowaona kero wana haki ya kutumia barabara. Ni tofauti ya kipato tu au mazingira ya wakati huo ndio yamewafanya kwenda kwa miguu.  Na jinsi miji inavyozidi kukua ndivyo idadi ya watu inavyoongezeka huku kukiwa na miundo mbinu michache sana ya waenda kwa miguu, tegemea idadi kubwa ya waenda kwa miguu kila kwenye zebra. Hivyo kuwa mwenda kwa miguu sio dhambi.  Hii ndio sababu k...

AMUUA MWANAYE KWA KIPIGO

Picha
Na Mwandishi Wetu, Mbeya. MWANAMKE Mmoja  aitwaye ,Marry Timotheo mkazi wa kijiji cha Garijembe kata ya Tembela Wilaya ya Mbeya anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kumuua kwa kumpiga na kitu kizito kichwani mtoto wake, Scola Mwaba(10)kwa madai ya kuzidi utukutu kisha mwili wake kutupa shamba lilo karibu na nyumbani anakoishi . Akizungumzia tukio hilo Desemba 10,2025 Kamanda wa Polisi Mkoani Mbeya, Benjamin Kuzaga amesema marehemu Scola alikuwa Mwanafunzi wa Darasa la Nne shule ya Msingi Ngonde wilaya ya Mbeya.  Kuzaga amesema kuwa tukio hilo limetokea Desemba 9,2025 ,majira ya saa 6.30 mchana katika Kijiji cha Garijembe ,Kata na Tarafa ya Tembela  Wilaya ya Mbeya. "Mama wa marehemu alimshambulia kwa kitu kizito kichwani  mtoto wake kwa madai ya kuzidi utukutu kisha mwili wake kutupa jirani na shamba la nyumba anakoishi "amesema Kamanda Kuzaga.  Aidha Kuzaga ameeleza kuwa pia licha ya  kumshikilia mama wa marehemu ,pia  jirani yake ,Sharifa Nz...

NAIBU WAZIRI MAKAMBA AIPONGEZA PBPA KWA UTENDAJI KAZI MZURI

Picha
Na Mwandishi Wetu - Dar es Salaam  Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (Mb) ameipongeza Wakala ya Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) kwa utendaji kazi mzuri katika kuhakikisha nchi inakuwa na akiba ya mafuta ya kutosha. Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na Menejimenti ya PBPA leo jijini Dar es Salaam. "Nawapongeza kwa kazi nzuri mnayoifanya lakini hakikisheni mnatoa elimu kwa Watanzania kuhusu majukumu yenu na kazi zenu" amesema Mhe. Salome. Aidha, ametumia nafasi hiyo kuitaka PBPA kuwawezesha Watanzania wazawa kuingia kwenye biashara ya mafuta na kufanya kazi kwa ushirikiano. "Lazima tupate wawekezaji wa Tanzania, tuwawezeshe waingie kwenye hii biashara " amesisitiza Mhe. Salome. Naye, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala ya Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), Bw. Erasto Simon amesema wakala hiyo imefanikiwa kuhakikisha kunakuwa na akiba ya mafuta ya kutosha, uwepo wa takwimu sahihi za kiasi cha mafuta pamoja na kuiwezesha Serikali kupanga ukusanyaji wa mapato. ...

KALEYA MOLLEL ACHAGULIWA KUWA MWENYEKITI MPYA SIMANJIRO

Picha
  Na Mwandishi wetu, Simanjiro DIWANI wa Kata ya Msitu wa Tembo, Kaleya Melita Mollel amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara, kwa kura zote 24 za Madiwani waliohudhuria kikao. Mwakilishi wa Katibu Tawala wa wilaya ya Simanjiro, Edosi Evaristi Ndikwiki amesema Mollel ambaye ni Diwani wa Kata ya Msitu wa Tembo, amepata kura zote 24 zilizopigwa  Ndikwiki pia amesema, madiwani hao wamemchagua Diwani viti maalum wa Tarafa ya Terrat, Mwanjaa Jacob kuwa Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja kwa kura zote 24 za ndiyo. Amesema katika uchaguzi huo uliofanyika  mji mdogo wa Orkesumet ulihusisha madiwani wote wanaotokana na CCM wa kata zote 18 na viti maalumu sita. Ndikwiki amewaasa madiwani hao kutoa ushirikiano kwa wataalam wa halmashauri hiyo kwani wameshaapa kutumikia nafasi zao. "Tuzingatie mahusiano mazuri na watumishi, tuwape ushirikiano na tuwe watatuzi wa migogoro tusiibue migogoro ambayo itaturudisha nyu...

WANANCHI BABATI WAIPA KONGOLE REA

Picha
Mitungi ya gesi 3,255 kusambazwa  na kuuzwa kwa bei ya ruzuku, Mitungi mmoja kuuzwa kwa bei ya ruzuku TZS 17,500. Na Mwandishi Wetu, Babati. Kongole hizo zimetolewa leo, tarehe 04 Disemba, 2025 na wananchi wa kata ya Ayalagaya Wilaya ya Babati mkoani manyara wakati wa usambazaji na uuzaji wa mitungi ya gesi kwa bei ya ruzuku katani hapo. Uuzaji wa majiko hayo umeongozwa na  diwani wa kata ya Ayalagaya Mheshimiwa Sabil John , mwakilishi wa mkuu wa wilaya ya Babati, mtendaji kata ya Ayalagaya , Afisa kutoka REA na mwakilishi wa kampuni Manjis Logistics Limited.  "Kinachofanyika leo ni kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia  katika kutunza mazingira na afya za wananchi" amesema Mhe. Sabil. Mhe. Sabil amesema, Lengo la mradi huu unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ni kuendeleza juhudi za utunzaji wa mazingira na Afya za wananchi kwa kuhakikisha wananchi wanapata elimu  na hamasa ya ...

TCAA YAWEZESHA MAFANIKIO YA REKODI YA DUNIA NDANI YA HIFADHI YA TARANGIRE.

Picha
Na Lubango Mleka, Tarangire. MAMLAKA ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imeratibu na kusimamia kwa mafanikio safari ya kihistoria ya puto la hewa moto (hot air balloon) iliyoifanya Tanzania kuorodheshwa rasmi kama nchi ya 123 katika jaribio la rekodi ya dunia la kurusha balloon na rubani akiwa pekee yake, lililoendeshwa na Dkt. Rubani Allie Dunnington. Safari hiyo maalum imefanyika katika Hifadhi ya Taifa ya Tarangire ikiwa ni mara ya kwanza kwa safari ya aina hii kufanyika na mtu mmoja ndani ya eneo la hifadhi. Uamuzi huu wa kipekee ulifikiwa na TCAA baada ya kufanya tathmini ya kina ya kiusalama, utaratibu wa kiufundi na uhalali wa operesheni ndani ya eneo hilo nyeti. Kwa mujibu wa TCAA, safari hiyo imefuata kikamilifu kanuni, taratibu na viwango vya usalama vya kitaifa na kimataifa. TCAA imeshirikiana kwa karibu na wadau wa uhifadhi pamoja na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kuhakikisha zoezi linafanyika kwa usalama, ufanisi na kulinda uadilifu wa mazingira ya hifadhi. Dkt. Ruba...

RACHEL NJAU AMSHUKURU RAIS SAMIA KUWAPATIA WANAWAKE LESENI

Picha
  Na Mwandishi wetu, Mirerani  MAKAMU Mwenyekiti wa chama cha wachimbaji madini wanawake Tanzania (TAWOMA) Rachel Joseph Njau amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kwa kuwapatia wanawak leseni za uchimbaji na ununuzi wa madini bila malipo. Hivi karibuni Waziri wa Madini Anthony Mavunde aliwapatia leseni ya uchimbaji madini na leseni ya ununuzi wa madini wanawake na vijana 423 waliopo katika vikundi 21 wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara. Rachel ambaye pia ni Katibu wa chama cha wachimbaji madini Mkoa wa Manyara (MAREMA) Tawi la Mirerani ametoa shukrani hizo kwenye uchaguzi wa TAWOMA Tawi la Mirerani ambapo Magreth Nelson alichaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa TAWOMA kwa wanawake wafanyabiashara wa magonga ndani ya ukuta unaozunguka migodi ya madini ya Tanzanite. Ameeleza kwamba kitendo cha Rais Samia Suluhu Hassan kuwasaidia wanawake kwenye mpango huo kinaongeza idadi ya wanawake wanaonufaika na sekta ya madini. "Tunampongeza Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kumtuma Waziri Ant...

MAGE NELSON MWENYEKITI MPYA TAWOMA MIRERANI

Picha
  Na Mwandishi wetu, Mirerani  MFANYABIASHARA maarufu wa kuongeza thamani madini ya Tanzanite wa mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, Magreth Nelson amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama cha wanawake wanaojihusisha na shughuli za madini Tanzania (TAWOMA) Tawi la Mirerani. Mage atatumikia kwa muda wa miaka mitano nafasi hiyo ya Mwenyekiti wa wanawake wafanyabiashara wa magonga ndani ya ukuta unaozunguka migodi ya madini ya Tanzanite mji mdogo wa Mirerani. Katika uchaguzi huo uliofanyika chini ya Makamu Mwenyekiti wa TAWOMA, Rachel Joseph Njau na Katibu Mkuu wa TAWOMA, Salma Ernest Kundi na kusimamiwa na Mwenyekiti wa MAREMA Tawi la Komolo Swalehe Abdalah na mjumbe wa MAREMA Tawi la Mirerani Jafar Matimbwa na kushuhudiwa na Afisa maendeleo ya jamii mamlaka ya mji mdogo wa Mirerani Floriana Mcharo. Mwenyekiti wa MAREMA Tawi la Komolo, Swalehe Abdalah akitangaza matokeo hayo amesema Magreth Nelson ambaye hakuwa na mpinzani alishinda nafasi hiyo kwa kupata kura ...

WAZIRI MAVUNDE AMPONGEZA RMO KASEZA

Picha
Na Mwandishi wetu, Mirerani  WAZIRI wa Madini Mhe Anthony Peter Mavunde, amempongeza Afisa madini mkazi (RMO) wa mkoa wa kimadini wa Mirerani, George Kaseza kwa namna anavyotekeleza wajibu wake ipasavyo, bila kulalamikiwa au kubagua wachimbaji. Waziri Mavunde ameeleza hayo wakati akizungumza na wadau wa madini ya Tanzanite mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, alipofanya ziara ya kutembelea machimbo ya madini ya Tomarini ya kijani eneo la Lemshuku na madini ya Tanzanite mji mdogo wa Mirerani. Amesema RMO Kaseza ni kiongozi mzoefu katika suala zima la eneo tengefu la Mirerani ndiyo sababu akateuliwa kuwa kiongozi wa hapo ambaye wadau wa madini pia wanamkubali kupitia utendaji kazi wake. "RMO Kaseza umekuwa mara nyingi ukiandika maandiko mengi ya eneo tengefu la Mirerani ndiyo sababu tukakuleta hapa sasa yake maandiko yako yafanye kuwa uhalisia ili yaonekane kwa vitendo," amesema Waziri Mavunde. Amewaasa wadau wa madini wa eneo hilo kumpa ushirikiano wa kutos...

URA – SACCOS YAPATA HATI SAFI MIAKA TISA MFULULIZO.

Picha
  Na. Lubango Mleka, Arusha.  KAMISHINA wa fedha na lojistiki (CP) Liberat Sabas amekipongeza Chama cha ushirika cha kuweka na kukopa cha Jeshi la Polisi (URA SACCOS LTD) kwa kuendelea kupata hati safi kwa miaka tisa (9) mfululizo kutoka kwa mkaguzi wa nje, jambo ambalo limewezesha  kuwa chama bora kitaifa kwa miaka mitano mfululizo na kuwa  chama kinachoongoza kwa mtaji mkubwa, mali na idadi kubwa ya wanachama. Kamishna Sabas yameyasema hayo leo Novemba 28, 2025 wakati akimwakilisha mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Camillius Wambura kufungua mkutano wa 17 wa chama hicho unaofanyika jijini Arusha.   “kupata hati hizo safi kwa mfululizo, zinaakisi uwazi na uadilifu wa uendeshaji makini wa chama chetu” alisema CP Sabas. Matokeo ya ufanisi huo kwa mwaka 2025 yametokana na uongozi bora, nidhamu ya kifedha na moyo wa umoja na  kujituma  kwa watendaji wa chama hicho. CP Sabas aliongeza kuwa uongozi bora na nidhamu ya kifedha imewezesha chama hicho kuwa na ak...

PET SCAN IANZE KUFANYA KAZI OCEAN ROAD- DKT SHEKALAGHE

Picha
Na. Lubango Mleka, Dar es Salaam. KATIBU Mkuu Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe, ameuagiza uongozi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road na mkandarasi anayesimika kifaa tiba cha PET Scan kuhakikisha wanakamilisha usimikaji wa kifaa hicho ndani ya muda waliokubaliana. Dkt. Shekalaghe ametoa agizo hilo Novemba 25, 2025, wakati wa ziara yake ya ukaguzi wa utoaji wa huduma katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, jijini Dar es Salaam. “Tumekubaliana kwamba hadi siku ya Ijumaa, mkandarasi anatakiwa kumpatia Mkurugenzi wa Ocean Road uhakiki wa benki (Bank Guarantee) ili Mkurugenzi aweze kumlipa asilimia 75 ya malipo yake. Hii itamwezesha mkandarasi kufanya maandalizi ya kuhakikisha PET Scan inaanza kufanya kazi. Wataalam wamenishauri kuwa baada ya hapo tutahitaji siku 30 kwa ajili ya maandalizi ya mashine hiyo kuzalisha mionzi tiba kwa ajili ya kugundua kansa,” amesema Dkt. Shekalaghe. Aidha, amewahakikishia wananchi wanaofika hospitalini hapo kupata huduma, kuwa Serikali imenunua galimu ...

WAANDISHI WA HABARI NI WADAU MUHIMU KATIKA KUIMARISHA AMANI, USALAMA NA UTULIVU WA TAIFA

Picha
Na Lubango Mleka, Dodoma. NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Dennis Lazaro Londo, amewahakikishia waandishi wa habari nchini kuwa Serikali itaendelea kulinda uhuru wao wa kujieleza pamoja na kuhakikisha wanatimiza majukumu yao kwa usalama na weledi. Mhe. Londo amezungumza hayo leo Novemba 27, 2025 jijini Dodoma katika mafunzo ya waandishi wa habari yaliyowaleta pamoja Wanahabari 100 kutoka maeneo mbalimbali nchini, Mhe. Londo amesema Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi itaendelea kushirikiana na wadau wa habari katika maeneo yote yanayohusu usalama kwa waandishi wa habari. Aidha, amebainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka msukumo mkubwa katika kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi, sambamba na kulinda uhuru wa vyombo vya habari.  " Falsafa ya Mhe. Rais kupitia “4R” zinaipa tasnia ya habari nafasi muhimu katika kulinda amani, kuimarisha umoja wa kitaifa na kuendeleza mijadala yenye tija kwa jamii." Am...