Machapisho

SIKU YA NYUKI DUNIANI’ YAADHIMISHWA KITAIFA TABORA

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora.  MAADHIMISHO ya Siku ya Nyuki Duniani yanayoyohusisha utundikaji mizinga, maonesho ya bidhaa na mazao ya nyuki yameanza leo katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Vita Mjini Tabora na kuvuta umati mkubwa wa wananchi. Wakizungumza kwenye maadhimisho hayo wakazi wa Tabora wameeleza kufurahishwa na tukio hilo kwa kuwa linawapa fursa wageni kutembelea Mkoa huo na kuonja utamu wa asali inayozalishwa katika misitu ya Mkoa huo. Daud Elisha, mjasiriamali mkazi wa Kata ya Kanyenye, Halmashauri ya manispaa ya Tabora ameeleza kuwa zao la asali ni miongoni mwa mazao ya kujivunia yanayozalishwa katika Mkoa huo na kuuzwa kwa bei kubwa ndani na nje ya nchi. ‘Haya maadhimisho ni fursa muhimu sana kwa wana Tabora kuuza asali yao na kupanua wigo wa uzalishaji zao hilo katika Wilaya zote za Mkoa huu, hivyo kuwaneemesha zaidi kiuchumi’, amesema. Amina Madereka, mjasiriamali anayejishughulisha na utundikaji mizinga na uuzaji asali katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi ame...

TANROADS YAENDELEA KULINDA BARABARA.

Picha
  Na Ahmed Ahmed - Dodoma.  WAKALA wa Barabara Tanzania (TANROADS) inaendelea kulinda miundombinu ya barabara ili iweze kudumu kwa muda mrefu na kuwa salama kwa watumiaji wakati wote. Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega ameyasema hayo Mei 20, 2025 wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka 2026/2027. "Kwa hakika haya ni mafanikio makubwa yaliyopatikana ndani ya muda mfupi kwa upande wa miundombinu ya barabara na madaraka," alisema. Ulega amesema barabara zinaendelea kuwa miundombinu muhimu ya usafiri nchini kutokana na kufika katika maeneo mengi ikilinganishwa na miundombinu mingine ya usafiri na usafirishaji. Amesema katika kipindi cha Julai 2025 hadi Aprili 2026, ukarabati wa kawaida ya barabara zenye urefu wa kilomita 16,782.58 umefanyika pamoja na marekebisho maalum ya kilomita 1,101.12.

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2026 AIPONGEZA REA UHAMASISHAJI WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Madaba, Ruvuma.  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2026 ,Ndugu Wazo Michael Mwang’onda ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa juhudi kubwa inazoendelea kuzifanya katika utekelezaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia nchini, akieleza kuwa miradi hiyo imekuwa na mchango mkubwa katika kuhamasisha wananchi kutumia nishati safi, salama na rafiki kwa mazingira. Pongezi hizo amezitoa wakati alipotembelea banda la REA katika maonesho yanayoendelea sambamba na Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri ya Wilaya ya Madaba mkoani Ruvuma, ambapo alipata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na wakala huo katika kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanapata huduma ya nishati safi ya kupikia kwa gharama nafuu. Akizungumza mara baada ya kutembelea banda hilo, kiongozi huyo amesema REA imeendelea kuwa chachu muhimu katika utekelezaji wa ajenda ya taifa ya matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi pamoja na...

MANISPAA TABORA YATOA MOTISHA KWA WALIMU

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora.  HALMASHAURI ya manispaa Tabora imetoa motisha kwa walimu na shule za sekondari zilizofanya vizuri zaidi katika masomo mbalimbali kwenye mitihani ya taifa ya kidato cha 4, 6na ule wa kujipima wa kidato cha 2 kwa mwaka 2025. Akitoa taarifa kwenye kikao cha baraza la madiwani, Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Dkt John Pima, ameeleza kuwa wametoa motisha hiyo ili kuwatia moyo walimu na shule zao ili waendelee kufanya vizuri zaidi. Amefafanua kuwa kwa mwaka wa masomo 2025 halmashauri ya manispaa hiyo ilishika nafasi ya kwanza Kimkoa kati ya halmashauri 8 katika mitihani ya taifa ya kidato cha 6, 4 na upimaji wa kidato cha 2. Pima ameongeza kuwa kwa ujumla shule zote katika manispaa hiyo zilifanya vizuri katika mitihani hiyo ikilinganishwa na mwaka uliopita sababu kuu ikitajwa kuwa ni juhudi na weledi wa walimu katika kufundisha watoto hao. Amedokeza kuwa katika mitihani ya kidato cha 4 walimu wa shule za sekondari za kata ambao masomo yao yalipata ...

REA KUIMARISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KUPITIA MAJIKO BANIFU MKOANI MWANZA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mwanza. WAKALA wa Nishati Vijijini (REA) umemtambulisha rasmi mtoa huduma, kampuni ya Envotec Services Limited, kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mheshimiwa Said Mtanda, kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku kwa wananchi wa mkoa huo. Utambulisho huo ni sehemu ya juhudi za Serikali kupitia REA za kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini, kwa lengo la kuboresha afya za wananchi, kupunguza matumizi ya nishati zisizo rafiki kwa mazingira pamoja na kuhifadhi mazingira. Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Mtanda, ameipongeza REA kwa kuendelea kutekeleza na kusimamia miradi mbalimbali ya nishati yenye manufaa kwa wananchi, ikiwemo mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku. Amesema mradi huo ni muhimu kwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza kwani utasaidia kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia, kupunguza matumizi makubwa ya kuni na mkaa pamoja na kusaid...

KONGAMANO LA UPANDIKIZAJI VIUNGO VYA BINADAMU KUFANYIKA DODOMA.

Picha
Na Ahmed Ahmed - Dodoma.  KONGAMANO la Kimataifa la Kisayansi la Wataalamu wa Upandikizaji Viungo linatarajiwa kufanyika jijini Dodoma. Akizungumza hivi karibuni jijini Dodoma, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Prof. Abel Makubi amesema madaktari bingwa wa upandikizaji wa viungo vya binadamu zaidi ya 150 kutoka nchi mbalimbali duniani wanatarajiwa kushiriki. "Madaktari hao watatoka katika nchi za Italia, Uingereza, Japani, Afrika Kusini, na Tanzania, lengo la kongamano hilo litakalofanyika kwenye ukumbi wa Domiya ni kuiimarisha Tanzania kwenye ramani ya upandikizaji viungo," alisema. Upandikizaji viungo ni moja ya mafanikio makubwa ya tiba ya kisasa ndani ya taaluma ya Upasuaji wa Kisasa na Immunolojia.  Hata hivyo, utekelezaji wake hutofautiana sana kati ya nchi kutokana na sheria, tamaduni, miundombinu ya afya, na uelewa wa jamii.

RC TABORA APEWA TUZO MAALUMU

Picha
Na Allan Kitwe, Tabora CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoani Tabora kimetoa tuzo maalumu kwa Mkuu wa Mkoa huo Paul Matiko Chacha kama ishara ya kutambua na kuthamini mchango wake katika suala zima la kusimamia maendeleo ya Mkoa huo. Tuzo hiyo imetolewa juzi kwenye Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM ngazi ya  Mkoa baada ya Wajumbe wa mkutano huo kuridhishwa na kazi nzuri inayofanywa na Kiongozi huyo hivyo kupendekeza apewa tuzo katika kikao hicho. Awali, akielezea tuzo hiyo, Katibu wa CCM Mkoa Wilson Nkambaku amesema kuwa pendekezo la kutoa tuzo hiyo lilitolewa na Wajumbe katika Kikao kilichopita, hivyo chama kimelifanyia kazi na sasa wapo tayari kumkabidhi. Ameongeza kuwa chama pia kitatoa tuzo kwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa Mheshimiwa Said Juma Nkumba kama ishara ya kutambua kazi yake njema ya kuimarisha, kudumisha na kujenga mshikamano thabiti ndani ya chama. Akikabidhi tuzo kwa Mkuu wa Mkoa, Mwenyekiti wa CCM Mkoa, Said Juma Nkumba amesema kuwa Chama kimeridhishwa na kazi yake, anatekeleza...

REA YAMTAMBULISHA MTOA HUDUMA WA MAJIKO BANIFU KAGERA.

Picha
Wananchi Kunufaika na Ruzuku ya Asilimia 80. Na Mwandishi Wetu, Bukoba-Kagera WAKALA wa Nishati Vijijini (REA) umemtambulisha rasmi mtoa huduma, kampuni ya Burn Manufacturing Company Limited, kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali Yahaya Ramadhani Kido, ikiwa ni hatua muhimu katika utekelezaji wa mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku kwa wananchi wa mkoa huo. Utambulisho huo umefanyika katika kikao kilichowakutanisha viongozi wa mkoa pamoja na wataalamu kutoka REA, ambapo ilielezwa kuwa kampuni hiyo itahusika moja kwa moja na usambazaji wa majiko hayo pamoja na kuhakikisha yanawafikia wananchi kwa bei nafuu kupitia utaratibu wa ruzuku uliowekwa na Serikali.  Mradi huo unalenga kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia na kupunguza utegemezi wa kuni na mkaa, ambavyo vimekuwa na athari kubwa kwa afya za wananchi na mazingira. Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali Yahaya Ramadhani Kido, ameipongeza REA kwa kuendelea kuibua na kusimamia...