Machapisho

MISRI YAADHIMISHA KUMBUKUBU YA UHURU WA SINAI.

Picha
Na Hassan Ali Ghazaly, Misiri.  KILA mwaka  25 Aprili, Misri huadhimisha kumbukumbu ya uhuru wa Sinai, baada ya uondoaji wa majeshi ya Israel kutoka eneo hilo mwaka 1982. Siku hii huenzi tukio muhimu katika historia ya kisasa ya taifa la Misri. Pia inaakisi mafanikio ya juhudi za kisiasa katika kurejesha ardhi. Uhuru wa Sinai ulitokana na mazungumzo na makubaliano ya kimataifa, pamoja na mchango wa jeshi la Misri katika Vita vya Oktoba 1973. Pia, Serikali inaendelea kuadhimisha kumbukumbu hii kila mwaka kupitia shughuli rasmi na kuelimisha vizazi vipya. #NasserForum #nasseryouthmovement   #NLF #hassanghazaly #NasserNet #habarikamilitv #uzalendokwanza

DC MYINGA ATOA AGIZO ZITO KWA VIONGOZI SIKONGE JUU YA UPUNGUFU WA MADAWATI KWA SHULE ZA MSINGI.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Sikonge-Tabora.  UPUNGUFU wa madawati katika shule za msingi Wilayani Sikonge umechukua sura mpya baada ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Mheshimiwa Thomas Myinga, kutoa agizo kali kwa viongozi wa vijiji na kata kuhakikisha wanatumia rasilimali zilizopo kumaliza changamoto hiyo kwa haraka. Akizungumza katika kikao kazi kilichowakutanisha viongozi wa serikali za vijiji, kata pamoja na walimu, kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Mheshimiwa Myinga alisisitiza kuwa hakuna sababu ya wanafunzi kuendelea kukaa chini ilhali maeneo yao yana rasilimali za kutosha, ikiwemo misitu inayoweza kutumika kutengeneza madawati. Alielekeza viongozi hao kupanga na kutekeleza bajeti zao kwa kuzingatia kipaumbele cha elimu, akibainisha kuwa ushirikiano kati ya serikali, wananchi na wadau wa maendeleo ni muhimu katika kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira bora ya kujifunzia. Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Seif Salum...

SERIKALI YAJA NA MKAKATI MPYA WA KULINDA FEDHA ZA USHIRIKA

Picha
  Na Jasmine Shamwepu, Dodoma.  SERIKALI imezindua mkakati mpya wa kuimarisha usimamizi wa vyama vya ushirika nchini, ukiwa na lengo la kulinda fedha za wanachama na kuongeza uwajibikaji kwa viongozi. Akizungumza jijini Dodoma katika Mkutano wa Wadau wa Maendeleo ya Ushirika, Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo, amesema kuwa sekta ya ushirika ina mchango mkubwa katika uchumi wa taifa, ikizingatiwa kuwa inazungusha fedha zinazokadiriwa kufikia trilioni sita. Amesema kuwa ili kuhakikisha fedha hizo zinalindwa ipasavyo, serikali inapanga kuimarisha mifumo ya ukaguzi, usimamizi na uwazi, sambamba na kuanzisha miundombinu maalum ya kushughulikia makosa yanayohusiana na vyama vya ushirika. “Lengo letu ni kuona vyama vya ushirika vinakuwa salama, vinawanufaisha wanachama, na vinaendeshwa kwa uadilifu mkubwa,” amesema Chongolo. Katika hatua nyingine, serikali imeweka mkazo katika matumizi ya teknolojia ya kidijitali ili kurahisisha ufuatiliaji wa shughuli za kifedha, kuongeza uwazi...

MJIKO BANIFU KWA BEI YA RUZUKU YAWAFIKIA WANANCHI CHUNYA.

Picha
Majiko 1,555 kuuzwa kwa bei ya ruzuku, Serikali kutoa ruzuku ya asilimia 85 kwa kila jiko. Na Mwandishi Wetu, Chunya - Mbeya*  KAIMU Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa halmashauri hiyo, Wakili Athumani Bamba leo Aprili 24, 2026 amezindua rasmi mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku katika mji mdogo wa Makongolosi, wilayani Chunya mkoani Mbeya. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo, Kaimu Mkurugenzi huyo alisema mradi huo unalenga kuwapatia wananchi nishati mbadala iliyo nafuu, salama na rafiki kwa mazingira, huku ukichochea kupunguza matumizi makubwa ya kuni na mkaa ambao umeendelea kuwa chanzo cha uharibifu wa misitu. Ameeleza kuwa kupitia mpango huo wa ruzuku, wananchi wataweza kumudu kununua majiko banifu kwa gharama nafuu zaidi, jambo litakalosaidia kupunguza matumizi ya nishati zisizo rafiki pamoja na kuboresha afya za watumiaji kwa kupunguza athari za moshi majumbani. “Ni muhimu wananchi wakautumia vyem...

WATAALAMU WA AFYA, SANYANSI ONGEZENI JUHUDI MATUMIZI YA TEKNOLOJIA

Picha
  Na Jasmine Shamwepu, Dodoma.  SELIKALI  imewataka wataalamu wa afya na sayansi nchini kuongeza juhudi katika kuimarisha matumizi ya teknolojia ya vinasaba, ili kuboresha huduma za afya na kusaidia utoaji wa haki jinai kwa ufanisi zaidi. Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Florence Samizi, wakati akifungua mkutano wa kisayansi wa teknolojia ya vinasaba uliofanyika jijini Dodoma, uliowakutanisha wataalamu wapatao 400 kutoka sekta mbalimbali. Amesema teknolojia ya vinasaba imekuwa mhimili muhimu katika huduma za kisasa za afya, ikisaidia katika upandikizaji wa viungo kama figo na uroto wa mifupa, pamoja na kuboresha utambuzi wa magonjwa na utoaji wa tiba za kisasa zikiwemo tiba jeni na chanjo. Mbali na sekta ya afya, amesema teknolojia hiyo imeleta mapinduzi katika mfumo wa haki jinai kwa kuwezesha upatikanaji wa ushahidi wa kisayansi unaosaidia uchunguzi na utoaji wa haki kwa usahihi zaidi. Dkt. Samizi ameeleza kuwa serikali imeendelea kuwekeza katika kuimari...

MKENDA:URASIMISHAJI UJUZI KUINUA HADHI YA VIJANA

Picha
  Na Jasmine Shamwepu, Dodoma WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema programu ya utambuzi na urasimishaji ujuzi inalenga kumpa kijana hadhi, sauti na fursa pana za ajira ndani na nje ya nchi. Amesema hayo Aprili 22, 2026 jijini Dodoma wakati wa uzinduzi wa Programu ya Mama Samia ya Utambuzi na Urasimishaji Ujuzi, inayolenga kuwasaidia vijana wenye ujuzi walioupata nje ya mfumo rasmi kutambuliwa kitaaluma. “Ujuzi ni mali, mtaji na nguvu ya taifa, hivyo vijana wanapaswa kujitokeza ili kutathminiwa na kurasimishwa,” amesema. Ameeleza kuwa utoaji wa vyeti kupitia programu hiyo siyo tu utoaji wa nyaraka, bali ni njia ya kumpa kijana nafasi ya kushindana katika soko la ajira kwa kuaminika zaidi. Aidha, amesema serikali imepanga kusogeza huduma karibu na wananchi ili mafundi wasilazimike kusafiri umbali mrefu, huku akisisitiza kuwa mchakato huo unatekelezwa bila gharama kwa wanufaika.  Ameongeza kuwa si kila mwenye ujuzi atapewa cheti moja kwa moja, bali ...

SERIKALI YAKIRI UHABA WA WATAALAMU, MALIPO YALALAMIKIWA

Picha
  Na Jasmine Shamwepu, Dodoma.  NAIBU Waziri wa Afya, Dkt. Florence Samizi, amesema serikali inatambua changamoto ya uhaba wa wataalamu wa usingizi na ganzi nchini, akibainisha kuwa kwa sasa kuna takribani wataalamu 2,950 wanaohudumia hospitali zaidi ya 800. Amesema serikali imeanza kuchukua hatua za kukabiliana na upungufu huo kwa kuongeza nafasi za mafunzo, hususan katika ngazi ya stashahada, ili kuongeza idadi ya wataalamu na kuboresha utoaji wa huduma za afya. “Lengo la serikali ni kuhakikisha tunakuwa na wataalamu wa kutosha watakaoweza kutoa huduma salama na kupunguza vifo vinavyotokana na upasuaji, hasa kwa mama na mtoto,” amesema. Hata hivyo, wataalamu wa huduma ya usingizi na ganzi wameiomba serikali kuhakikisha wanalipwa kwa wakati malipo ya saa za ziada wanazofanya, wakisema kucheleweshewa stahiki hizo kunapunguza ari ya kazi na kuhatarisha ubora wa huduma kwa wagonjwa. Akizungumza katika kongamano la nne la Chama cha Wataalamu wa Dawa za Usingizi, Ganzi na Upasuaji...