URA – SACCOS YAPATA HATI SAFI MIAKA TISA MFULULIZO.
Na. Lubango Mleka, Arusha. KAMISHINA wa fedha na lojistiki (CP) Liberat Sabas amekipongeza Chama cha ushirika cha kuweka na kukopa cha Jeshi la Polisi (URA SACCOS LTD) kwa kuendelea kupata hati safi kwa miaka tisa (9) mfululizo kutoka kwa mkaguzi wa nje, jambo ambalo limewezesha kuwa chama bora kitaifa kwa miaka mitano mfululizo na kuwa chama kinachoongoza kwa mtaji mkubwa, mali na idadi kubwa ya wanachama. Kamishna Sabas yameyasema hayo leo Novemba 28, 2025 wakati akimwakilisha mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Camillius Wambura kufungua mkutano wa 17 wa chama hicho unaofanyika jijini Arusha. “kupata hati hizo safi kwa mfululizo, zinaakisi uwazi na uadilifu wa uendeshaji makini wa chama chetu” alisema CP Sabas. Matokeo ya ufanisi huo kwa mwaka 2025 yametokana na uongozi bora, nidhamu ya kifedha na moyo wa umoja na kujituma kwa watendaji wa chama hicho. CP Sabas aliongeza kuwa uongozi bora na nidhamu ya kifedha imewezesha chama hicho kuwa na ak...