Machapisho

MICHEZO

Picha
RATIBA ya Michuano ya Kagame Cup 2025.   

DKT. LADISLAUS CHANG’A ASHIRIKI KATIKA MKUTANO WA 6 WA MAWAZIRI NA MAMLAKA ZA MAZINGIRA WA ASIA NA PASIFIKI

Picha
Nadi, Fiji.  KAIMU Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC), Dkt. Ladislaus Chang’a, kwa mwaliko wa Programu ya Umoja wa Mataifa uratibu wa Mazingira (UNEP) ameshiriki kikamilifu katika Mkutano wa 6 wa Mawaziri na Mamlaka za Mazingira wa Asia na Pasifiki (6th AP Forum) uliofanyika kuanzia tarehe 26–29 Agosti 2025 Jijini Nadi, Fiji. Mkutano huo uliandaliwa kwa pamoja na Serikali ya Fiji na UNEP ukiwa na kaulimbiu “Kutafuta Suluhisho Endelevu katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi Duniani”. Sambamba na mkutano huo, Dkt. Chang’a alikuwa na vikao mbalimbali na waheshimiwa na taasisi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kikao na Mhe. Rupa B. K., Waziri wa Serikali ya Nepal, Wizara ya Misitu na Mazingira, ambapo alimpatia taarifa kuhusu mpango kazi wa IPCC unaotekelezwa hadi mwaka 2029.  Mazungumzo hayo yalijikita katika kuimarisha ushirikiano wa kikan...

REA YAENDELEA KUTEKELEZA KWA VITENDO MKAKATI WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

Picha
 *Majiko banifu 4,836 kusambazwa na kuuzwa kwa bei ya ruzuku mkoa wa Njombe.  Jiko moja kuuzwa kwa bei ya ruzuku ya TZS 8,850 tu.  📌 *Kila walaya kupata majiko 1,209*  Na Mwandishi Wetu, Njombe.  KATIBU Tawala wa Mkoa wa Njombe Bi. Judica Omari amekutana na Timu ya Wataalam kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA) leo Septemba 1, 2025 na kupata taarifa ya mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku ambao unatarajia kuanzia mapema mwezi wa 9, 2025. Akiwasilisha taarifa ya mradi kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe, Mhandisi wa miradi Kutoka wakala wa Nishati Vijijini, Raya Majallah, amesema, Wakati Taifa likiwa kwenye mkakati wa kuhakikisha Watanzania wanatumia nishati safi na salama ya kupikia, Wakala wa Nishati Vijijini umekuja na mpango wa usambazaji na uuzaji wa  majiko banifu 200,000 kwa bei ya ruzuku yanayotumia kuni na mkaa mchache sana na yenye ufanisi mkubwa katika matumizi yake. Mradi huu umekuja kwa lengo la kuimarisha na kubor...

WANANCHI WAHIMIZWA KUACHA MATUMIZI YA MKAA NA KUNI, WATAKIWA KUTUMIA MAJIKO YA NISHATI SAFI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  ILI kupunguza madhara ya kiafya na kimazingira yanayosababishwa na matumizi ya kuni na mkaa, wananchi wametakiwa kuachana na nishati hizo na kuhamia kwenye matumizi ya majiko yanayotumia umeme na sola kupitia kampeni ya kitaifa ya Pika Smart. Kampeni hii imefika mkoa wa tano kwa Dodoma huku lengo likiwa ni kuelimisha jamii kuhusu faida za kutumia nishati safi kwa gharama nafuu ambayo inalenga kupunguza utegemezi wa nishati zisizo salama na zisizo endelevu. Akizungumza wakati wa kampeni hiyo Septemba Mosi jijini Dodoma, Rightness Felix Balozi wa Pika Smart, amesema kuwa matumizi ya kuni na mkaa yana gharama kubwa kwa familia na yana madhara kwa afya na mazingira.  “Kwa kutumia majiko ya umeme, mtu anaweza kupika kwa gharama ndogo sana. Kwa mfano, unaweza kutumia shilingi 1,000 tu na ukapika mlo wako bila moshi wala madhara ya kiafya tuna vifaa salama kabisa, tofauti na mitazamo iliyokuwepo awali kuwa majiko ya umeme yanapiga shoti,” amesema Felix. Am...

MICHEZO

Picha
NAIBU katibu Mkuu wa Wizara  ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Felister Mdemu amewaaga wanamichezo wa wizara hiyo watakaoshiriki katika michezo ya Shirikisho la Michezo kwa wizara na Idara za serikali leo Septemba 1, 2025 kuelekea Jijini Mwanza. Felister ametoa rai kwa washiriki hao kuwa makini na kujali afya zao pindi wanapokuwa katika mashidano hayo ili waweze kurejea salama na kuendelea na majukumu yao.

TAARIFA KWA UMMA

Picha
 

TAARIFA KWA UMMA

Picha
Gaza  ABU Obeida, anayejulikana kwa kuonekana akiwa amejifunika uso kwenye ujumbe wa video, alikuwa msemaji wa kikosi cha kijeshi cha Qassam na sauti kuu ya propaganda ya Hamas. Tangu kuanza kwa vita vya Gaza, Israel imewaua viongozi kadhaa wa Hamas, akiwemo Yahya Sinwar, anaetajwa kuwa mpangaji mkuu wa mashambulizi ya Oktoba 7, 2023 kusini mwa Israel.  #Gaza #Israel #Hamas #AbuObeida #MiddleEastConflict Credit DW. 

JESHI LA ISRAEL LAFANYA MASHAMBULIZI USIKU KUCHA GAZA

Picha
JESHI la Israel limefanya mashambulizi ya usiku kucha kwenye maeneo yaliyoko Mjini Gaza kutokea angani na ardhini na kuharibu majumba na kuzilazimu familia zaidi kuondoka eneo hilo. #Gaza #Israel #evacuation

NISHATI SAFI YA KUPIKIA KUTUMIKA MAGEREZA YOTE NCHINI

Picha
Matukio mbalimbali katika picha yakimuonesha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa wakati wa hafla ya uzinduzi wa matumizi ya nishati safi ya kupikia magerezani, iliyofanyika Agosti 30, 2025, Gereza Karanga, Kilimanjaro.

ABIRI AKAMATWA BAADA YA KUMPIGA NGUMI MUHUDUMU WA KWENYE NDEGE

Picha
POLISI wamemkamata abiria kutoka kwenye ndege iliyowasili kutoka Saudia kwenye uwanja wa ndege huko Heathrow mapema Alhamisi ya wiki iliyopita.  Polisi na Maofisa wa  Wazima Moto waliizingira ndege ya Saudia Airlines katika uwanja wa ndege wa Heathrow na kumkamata abiria wa kiume mwenye umri wa miaka 33 ambaye inadaiwa alimpiga ngumi mfanyakazi na kujaribu kufungua mlango wa ndege hiyo. Huduma za dharura zilikimbilia kwenye Boeing 787 muda mfupi baada ya kutua kutoka Jeddah majira ya saa 7 mchana ya Alhamisi. Kwa mujibu wa gazeti la The Sun, ndege hiyo ilifunga breki kali kwenye barabara ya teksi kuelekea Terminal 4 baada ya tukio hilo, na kuwafanya marubani kuita usaidizi wa haraka. Ngazi ziliwekwa na maafisa walipanda ndege hiyo, iliyokuwa imebeba abiria kwenye Flight namba SV119. Picha zilizopatikana na gazeti la The Sun zinaonyesha angalau malori manne ya zima moto, magari sita ya polisi na ambulensi kadhaa kwenye eneo la tukio.

INEC YAKUTANA NA WAWAKILISHI WA VYAMA VYA SIASA KUPITIA NA KUFANYA MABADIRIKO MADOGO KWENYE MIKUTANO YA HADHARA YA RAIS NA MAKAMU RAIS.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  MKURUGENZI wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) Ndugu. Kailima Ramadhani leo tarehe 30 Agosti, 2025 ameongoza kikao cha wawakilishi wa vyama vya siasa kupitia na kufanya mabadiliko madogo kwenye ratiba ya mikutano ya hadhara ya kampeni za wagombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais. Mikutano hiyo iliyoanza tarehe 28 Agosti, 2025 inaendelea hadi tarehe 28 Oktoba, 2025 kwa Tanzania Bara na tarehe 27 Oktoba, 2025 kwa Tanzania Zanzibar. Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano na Madiwani kwa Tanzania Bara utafanyika tarehe 29 Oktoba, 2025.

DK.MWINYI:CCM ITAFANYA KAMPENI ZA KISTAARABU KWA SERA ZENYE TIJA KWA WANANCHI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar.  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ambaye pia ni Mgombea Mteule wa Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), amechukua fomu ya kugombea nafasi hiyo katika Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) na kuahidi kuwa CCM itafanya kampeni za kistaarabu zitakazozingatia Utamaduni, Silka na Desturi za Wazanzibari. Dkt. Mwinyi amechukua fomu hiyo katika Afisi za Tume ya Uchaguzi leo, tarehe 30 Agosti 2025, asubuhi, na hatimaye msafara wake ukaelekea Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui kupitia Barabara ya Miembeni, Kariakoo, Rahaleo na Michenzani, akisindikizwa na mamia ya wanachama wa chama hicho waliokuwa wamejipanga pembezoni mwa barabara. Aidha, Dkt. Mwinyi amezuru Kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Hayati Abeid Amani Karume, na kisha kuzungumza na Wazee wa Chama Cha Mapinduzi afisini hapo. Akizungumza na mamia ya wanachama wa CCM katika Uwanja wa Mao Tse Tung, Mgombea Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesisitiza kuwa...