CCM YASHITUKA KUHUSU MIKUTANO YA KUCHOCHEA MAAANDAMANO.
Na Jasmine Shamwepu, Dodoma. CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kinazo taarifa zinazoashiria kuwepo kwa mikutano inayofanywa na baadhi ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambayo inadaiwa kuhusisha mipango ya kuhamasisha maandamano yenye uwezekano wa kuvuruga hali ya amani nchini. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) wa CCM anayeshughulikia Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani Kihongosi, alisema chama hicho kimeendelea kuwataka Watanzania kuzingatia umuhimu wa utulivu na mshikamano wa kitaifa. Kihongosi ameeleza kuwa CCM inaamini maendeleo endelevu hayawezi kupatikana iwapo kutakuwa na misukosuko ya kisiasa, akisisitiza kuwa tofauti za vyama zinapaswa kuishia kwenye majadiliano ya sera. Alisema chama hicho kinatoa tahadhari kwa wananchi kutoshawishika kushiriki katika matukio yanayoweza kusababisha machafuko, akibainisha kuwa amani ndiyo msingi wa maendeleo ya taifa. “Taarifa tulizonazo zinaonyesha k...