Machapisho

WAKALA WA NISHATI VIJIJINI (REA) YASHIRIKI TAMASHA LA KILIMO JIJINI MBEYA.

Picha
Wahamasisha Nishati Safi ya Kupikia.  Na Mwandishi Wetu, Iwambi- Mbeya.  WAKALA wa Nishati Vijijini (REA) unashiriki katika tamasha la kilimo linalofanyika katika  viwanja vya Iwambi jijini Mbeya kuanzia tarehe 25 mpaka 29 Aprili 2026, ambapo zaidi ya watu 100,000 wakiwemo vijana kutoka mikoa mbalimbali ya kanda ya nyanda za juu kusini wanatarajiwa kushiriki. Wakala unatumia jukwaa hilo kuelimisha na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wananchi pamoja na kueleza hali ya upatikanaji wa huduma ya umeme katika maeneo ya vijijini. Kupitia banda lake, REA imeonesha bidhaa mbalimbali za nishati safi ya kupikia, ambapo bidhaa kuu zinazohamasishwa ni pamoja na matumizi ya majiko ya umeme, majiko ya gesi pamoja na majiko banifu. Teknolojia hizo zimebainishwa kuwa suluhisho muhimu katika kupunguza matumizi ya nishati chafu kama kuni na mkaa, kulinda mazingira na kuboresha afya za watumiaji. Akifungua rasmi maonesho hayo, Kaimu mkuu wa wilaya ya Mbeya ambae pia ni Mk...

BUNGE LAPITISHA BIL. 174.9/- KWA WIZARA YA MADINI

Picha
  Yalenga kuchangia trilioni 1.4/- za maduhuli, Makusanyo yafikia Trilioni 1 na Milioni 156, Jumla ya tani 23.8 za dhahabu zakusaywa ndani ya miezi 18, Ni Juhudi za Rais.Dkt.Samia Suluhu Hassan.  Na Hamida Ramadhan, Dodoma.  Bunge la Jamhuru ya Muungano wa Tanzania, limeridhia na kupitisha bajeti ya Wizara ya Madini ya shilingi bilioni 174.9 kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 ili kuiwezesha Wizara ya Madini kufanikisha ukusanyaji wa maduhuli ya shilingi trilioni 1.4. Akiwasilisha Bungeni makadirio ya Mapato na Matumizi leo Aprili 27, 2026, Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde amesema fedha hizo zitawezesha kufanikisha utekelezaji wa majukumu ya Wizara pamoja na taasisi zilizo chini yake, huku zikilenga kuendeleza kasi ya ukuaji wa sekta ya madini kwa kufanya tafiti za jiosayansi nchini. Akifafanua mgawanyo wa Bajeti hiyo, Waziri Mavunde amesema kiasi cha  shilingi bilioni 71.5 sawa na asilimia 40.9 zimetengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo, wakati shilingi bilioni 103....

KAMATI YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI YASISITIZA UFANISI WA MIRADI YA MAENDELEO YA SEKTA YA MADINI

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Dodoma KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeitaka Serikali kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa miradi yote ya sekta ya madini ili kuhakikisha inaleta manufaa ya moja kwa moja kwa wananchi na kuimarisha mchango wake katika uchumi wa taifa. Akiwasilisha maoni ya Kamati hiyo bungeni Aprili 27, 2026, Makamu Mwenyekiti wa Kamati, Simon Lusengekile, alisema Serikali inapaswa kuhakikisha miradi ya maendeleo inapatiwa rasilimali za kutosha pamoja na usimamizi madhubuti ili ikamilike kwa wakati na kwa viwango vinavyotakiwa. Alibainisha kuwa usimamizi imara wa miradi hiyo utaongeza tija katika sekta ya madini na kuboresha huduma kwa wananchi kupitia miradi ya kimkakati inayolenga kuongeza thamani ya rasilimali za madini. Kamati imeishauri Wizara kuhakikisha miradi yote inatekelezwa kwa kuzingatia mipango ya taifa, viwango vya ubora na muda uliopangwa ili kuepuka ucheleweshaji na kupunguza changamoto za utekelezaji. Aidha, imeitaka Serikali kuimarisha usi...

SERIKALI YAWEKA MKAZO SEKTA YA MADINI KUPITIA VIPAUMBELE NANE 2026/2027

Picha
  Na Hamida Ramadhan, DODOMA WIZARA ya Madini imeweka bayana mkakati wa vipaumbele nane kwa mwaka wa fedha 2026/2027, hatua inayolenga kuifanya sekta hiyo kuwa chachu ya ukuaji wa uchumi, kuongeza ajira na kuhakikisha rasilimali zinasimamiwa kwa ufanisi zaidi. Akiwasilisha mpango wa bajeti bungeni, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, alisema serikali imejipanga kuimarisha utafiti wa madini ili kubaini maeneo mapya yenye utajiri na kuongeza upatikanaji wa takwimu sahihi zitakazovutia wawekezaji zaidi. Alieleza kuwa mkazo pia utawekwa kwenye uongezaji thamani wa madini kwa kuyachakata ndani ya nchi, jambo litakaloongeza mapato ya taifa, kufungua ajira mpya na kuinua thamani ya mauzo ya nje. Katika kuhakikisha Watanzania wananufaika zaidi, wizara inalenga kuongeza ushiriki wao katika mnyororo mzima wa thamani wa madini, hususan kwa kuwawezesha wachimbaji wadogo na wa kati kupitia mafunzo na uwezeshaji wa kitaalamu. Aidha, serikali itaendelea kuwaendeleza wachimbaji wadogo kwa kuwapatia...

BAJETI YA WIZARA YA MADINI 2026/2027 YALENGA KUIMARISHA MAPATO NA USIMAMIZI WA RASILIMALI

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Dodoma WIZARA ya Madini imewasilisha ombi bungeni la kuidhinishiwa jumla ya shilingi bilioni 174.98 kwa ajili ya mwaka wa fedha 2026/2027, fedha zitakazotumika kutekeleza majukumu mbalimbali ya sekta hiyo. Akiwasilisha makadirio hayo Aprili 27, 2026, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, alieleza kuwa sehemu ya fedha hizo, takribani shilingi bilioni 71.51 sawa na asilimia 40.87, imepangwa kuelekezwa kwenye miradi ya maendeleo. Kwa upande mwingine, kiasi cha shilingi bilioni 103.47, sawa na asilimia 59.13 ya bajeti yote, kimetengwa kwa matumizi ya kawaida ya wizara pamoja na taasisi zilizo chini yake. Ndani ya fungu hilo, shilingi bilioni 27.36 zitatumika kulipa mishahara ya watumishi, huku shilingi bilioni 76.11 zikigharamia shughuli nyingine za kiutendaji. Waziri Mavunde alisisitiza kuwa utekelezaji wa bajeti hiyo utachangia kuimarika kwa ukusanyaji wa mapato ya serikali, yakilenga kufikia shilingi trilioni 1.4, sambamba na kuboresha usimamizi na uendelezaji wa ...

MISRI YAADHIMISHA KUMBUKUBU YA UHURU WA SINAI.

Picha
Na Hassan Ali Ghazaly, Misiri.  KILA mwaka  25 Aprili, Misri huadhimisha kumbukumbu ya uhuru wa Sinai, baada ya uondoaji wa majeshi ya Israel kutoka eneo hilo mwaka 1982. Siku hii huenzi tukio muhimu katika historia ya kisasa ya taifa la Misri. Pia inaakisi mafanikio ya juhudi za kisiasa katika kurejesha ardhi. Uhuru wa Sinai ulitokana na mazungumzo na makubaliano ya kimataifa, pamoja na mchango wa jeshi la Misri katika Vita vya Oktoba 1973. Pia, Serikali inaendelea kuadhimisha kumbukumbu hii kila mwaka kupitia shughuli rasmi na kuelimisha vizazi vipya. #NasserForum #nasseryouthmovement   #NLF #hassanghazaly #NasserNet #habarikamilitv #uzalendokwanza

DC MYINGA ATOA AGIZO ZITO KWA VIONGOZI SIKONGE JUU YA UPUNGUFU WA MADAWATI KWA SHULE ZA MSINGI.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Sikonge-Tabora.  UPUNGUFU wa madawati katika shule za msingi Wilayani Sikonge umechukua sura mpya baada ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Mheshimiwa Thomas Myinga, kutoa agizo kali kwa viongozi wa vijiji na kata kuhakikisha wanatumia rasilimali zilizopo kumaliza changamoto hiyo kwa haraka. Akizungumza katika kikao kazi kilichowakutanisha viongozi wa serikali za vijiji, kata pamoja na walimu, kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Mheshimiwa Myinga alisisitiza kuwa hakuna sababu ya wanafunzi kuendelea kukaa chini ilhali maeneo yao yana rasilimali za kutosha, ikiwemo misitu inayoweza kutumika kutengeneza madawati. Alielekeza viongozi hao kupanga na kutekeleza bajeti zao kwa kuzingatia kipaumbele cha elimu, akibainisha kuwa ushirikiano kati ya serikali, wananchi na wadau wa maendeleo ni muhimu katika kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira bora ya kujifunzia. Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Seif Salum...

SERIKALI YAJA NA MKAKATI MPYA WA KULINDA FEDHA ZA USHIRIKA

Picha
  Na Jasmine Shamwepu, Dodoma.  SERIKALI imezindua mkakati mpya wa kuimarisha usimamizi wa vyama vya ushirika nchini, ukiwa na lengo la kulinda fedha za wanachama na kuongeza uwajibikaji kwa viongozi. Akizungumza jijini Dodoma katika Mkutano wa Wadau wa Maendeleo ya Ushirika, Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo, amesema kuwa sekta ya ushirika ina mchango mkubwa katika uchumi wa taifa, ikizingatiwa kuwa inazungusha fedha zinazokadiriwa kufikia trilioni sita. Amesema kuwa ili kuhakikisha fedha hizo zinalindwa ipasavyo, serikali inapanga kuimarisha mifumo ya ukaguzi, usimamizi na uwazi, sambamba na kuanzisha miundombinu maalum ya kushughulikia makosa yanayohusiana na vyama vya ushirika. “Lengo letu ni kuona vyama vya ushirika vinakuwa salama, vinawanufaisha wanachama, na vinaendeshwa kwa uadilifu mkubwa,” amesema Chongolo. Katika hatua nyingine, serikali imeweka mkazo katika matumizi ya teknolojia ya kidijitali ili kurahisisha ufuatiliaji wa shughuli za kifedha, kuongeza uwazi...

MJIKO BANIFU KWA BEI YA RUZUKU YAWAFIKIA WANANCHI CHUNYA.

Picha
Majiko 1,555 kuuzwa kwa bei ya ruzuku, Serikali kutoa ruzuku ya asilimia 85 kwa kila jiko. Na Mwandishi Wetu, Chunya - Mbeya*  KAIMU Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa halmashauri hiyo, Wakili Athumani Bamba leo Aprili 24, 2026 amezindua rasmi mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku katika mji mdogo wa Makongolosi, wilayani Chunya mkoani Mbeya. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo, Kaimu Mkurugenzi huyo alisema mradi huo unalenga kuwapatia wananchi nishati mbadala iliyo nafuu, salama na rafiki kwa mazingira, huku ukichochea kupunguza matumizi makubwa ya kuni na mkaa ambao umeendelea kuwa chanzo cha uharibifu wa misitu. Ameeleza kuwa kupitia mpango huo wa ruzuku, wananchi wataweza kumudu kununua majiko banifu kwa gharama nafuu zaidi, jambo litakalosaidia kupunguza matumizi ya nishati zisizo rafiki pamoja na kuboresha afya za watumiaji kwa kupunguza athari za moshi majumbani. “Ni muhimu wananchi wakautumia vyem...