Machapisho

MMOJA AFARIKI, WAWILI WAJERUHIWA WAKIBISHANIA SIMBA NA YANGA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mwanza.  MTU mmoja amefariki dunia na wengine wawili kujeruhiwa baada ya kutokea ugomvi uliozuka kutokana na ushabiki wa mpira kati ya mashabiki wa timu za Simba na Yanga Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza. Kwa mujibu taarifa iliyotolewa leo na Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, DCP Wilbrod Mutafungwa amesema tayari wameanzisha msako wa kumtafuta kijana mmoja (jina limehifadhiwa) kwa tuhuma za kumuua Abel Mganga Mazuri (25) mkazi wa Nyamahengo, na kuwajeruhi watu wawili kufuatia ugomvi uliotokana na ushabiki wa mpira. Taarifa hiyo imesema tukio hilo limetokea Machi 24, 2026 majira ya saa 5:30 usiku katika kitongoji cha Nyamahengo, kijiji na kata ya Sumve, wilayani Kwimba, mkoani Mwanza. "Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limeanza msako wa kumtafuta kijana mmoja (jina limehifadhiwa kwa sasa) kwa tuhuma za mauaji ya Abel Mganga Mazuri, miaka25, mkazi wa Nyamahengo aliyeuawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali kifuani kisha kuwajeruhi watu wawili kwa kutumia kitu c...

FDC URAMBO WAJIVUNIA MAFANIKIO MAKUBWA

Picha
  Na Allan Kitwe, Urambo.  CHUO Cha Maendeleo ya Wananchi (FDC) Urambo kimeishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha miundombinu na kukipatia vifaa vya mafunzo ambavyo vimekiongezea mapato. Hayo yamebainishwa jana na Mkuu wa Chuo hicho Elias Niima alipokuwa akiongea na waandishi wa habari Ofisini kwake ambapo alieleza kufurahishwa na uamuzi wa serikali ya Awamu ya Sita kukifanyia maboresho makubwa chuo hicho.   Amesema kuwa kipindi cha miaka 4 ya Uongozi wa Rais Samia na siku 100 za awamu yake ya pili tangu aingie madarakani, chuo kimepata mafanikio makubwa ikiwemo kuzalisha samani za taasisi mbalimbali na kuingiza mapato. Ametaja baadhi ya samani zilizotengenezwa kuwa ni madawati, viti na meza zaidi ya 7,000 kwa shule za msingi na sekondari za halmashauri za Wilaya ya Urambo na 2,500 za halmashauri ya Wilaya ya Kaliua. ‘Miradi hii imetekelezwa na Chuo kwa kutumia nguvu kazi ya wanafunzi na walimu wao, ikiwa ni sehe...

TAKUKURU, TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA YASAINI MIKATABA YA KUDHIBITI RUSHWA.

Picha
  Na Hamida Ramadhan,  Dodoma.  TAASISI  ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa kushirikiana na Tume ya Maendeleo ya Ushirika zimesaini makubaliano ya ushirikiano yatakayolenga kuzuia na kupambana na vitendo vya rushwa katika vyama vya ushirika nchini.  Hatua hiyo inalenga kuimarisha uwajibikaji, uwazi na kurejesha imani ya wanachama wa ushirika. Akizungumza katika hafla ya utiaji saini wa makubaliano hayo, Msajili na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika, Dkt. Benson Ndiege, alisema sekta ya ushirika imekuwa ikikabiliwa na changamoto za usimamizi wa rasilimali, ambazo kwa kiasi kikubwa zimechangiwa na vitendo vya rushwa. Alieleza kuwa wanachama wengi wamekuwa wakiweka fedha, mazao na rasilimali zao katika vyama vya ushirika kwa matarajio ya kunufaika, lakini vitendo vya rushwa vimekuwa vikikwamisha malengo hayo na kupunguza imani yao. “Ushirikiano huu unalenga kukomesha vitendo vya rushwa na kurejesha matumaini ya wanachama tumejipanga kuhakik...

REA YAENDELEZA MAPINDUZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KOROGWE.

Picha
  Wananchi Wanufaika na usambazaji na uuzaji wa Mitungi ya Gesi kwa bei ya ruzuku.  Na Mwandishi Wetu, Korogwe - Tanga.  WANANCHI wa wilaya ya Korogwe mkoani Tanga  wameanza kuona mwanga mpya wa maisha kufuatia kuendelea kwa mpango wa usambazaji na uuzaji wa mitungi ya gesi ya kilo sita kwa bei ya ruzuku unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).  Mpango huo unaolenga kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, umeleta matumaini mapya kwa kaya nyingi zilizokuwa zikitegemea kuni na mkaa. Katika muendelezo wa zoezi hilo, REA imeendelea kusambaza mitungi ya gesi kwa gharama nafuu, hatua inayolenga kuhakikisha hata wananchi wa kipato cha chini wanapata fursa ya kutumia nishati salama na rafiki kwa mazingira.  Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Msimamizi wa mradi kutoka REA, Ndugu Abdulrazack Mkomi ameeleza kuwa jitihada hizo ni sehemu ya mkakati mpana wa serikali wa kupunguza utegemezi wa nishati za jadi ambazo zimekuwa zikichangia uharibifu wa mazi...

RAIS SAMIA ALETA NEEMA KWA MABINTI WALIOKOSA ELIMU SIKONGE

Picha
Na Allan Kitwe, Sikonge MABINTI zaidi ya 34 waliokosa fursa ya kupata elimu ya sekondari Wilayani Sikonge Mkoani Tabora wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuwapa fursa ya kupata elimu hiyo kwa miaka miwili pasipo kulipa gharama yoyote. Mabinti hao ambao wengi wao walikatishwa masomo kwa sababu mbalimbali ikiwemo hali duni ya maisha ya wazazi wao, kupata ujauzito, kukatishwa masomo ili waozeshwe katika umri mdogo na mtizamo hasi wa wazazi wao kuhusu elimu. Wakizungumza na waandishi wa habari waliotembelea Chuo Cha Maendeleo ya Wananchi (FDC) Wilayani humo jana walimshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fursa kwa watoto wa kike waliokosa elimu kurudi shuleni. Watoto hao licha ya kupata fursa ya kusoma elimu ya sekondari bure kwa miaka 2 (QT) pia wanasoma masomo ya ufundi stadi ambapo kila mmoja anasoma fani anayopenda, hii inampa fursa ya kupata elimu ya sekondari na ujuzi wa ufundi pia. Miracle Mvungu (25) kutoka Kata ya Igigwa Wilayani humo ameeleza kuwa baada ya kumal...

BREAKING NEWS: - WAZIRI LUKUVI AFARIKI DUNIANI

Picha
 

SERIKALI YAIMARISHA UPATIKANAJI WA MAFUTA YA PETROLI NCHINI MALAWI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam SERIKALI kupitia Bandari ya Dar es Salaam imeendelea kuwa nguzo muhimu ya upatikanaji wa mafuta kwa nchi jirani ya Malawi, hatua inayochochea shughuli za kiuchumi na kuboresha maisha ya wananchi wa nchi hizo mbili. Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua miundombinu ya mafuta katika Kituo cha Kurasini Oil Jet (KOJ-1), kilichopo katika Bandari ya Dar es Salaam leo Machi 24, 2026, Waziri wa Nishati na Madini wa Malawi, Mhe. Dkt. Jean Mathanga, aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa mchango wake mkubwa katika kuwezesha mtiririko wa mafuta kwenda nchini Malawi. Alisema kuwa kutokana na Malawi kutokuwa na bandari, nchi hiyo inategemea kwa kiasi kikubwa miundombinu ya nchi jirani, hususan Tanzania, katika kuhakikisha upatikanaji wa mafuta unaendelea kuwa wa uhakika. Alibainisha kuwa ziara hiyo imelenga kujionea kwa vitendo namna mafuta yanavyopokelewa na kusimamiwa bandarini ili kuboresha mipango ya ununuzi na usambazaji wa mafuta nchini Malawi.  Kwa ...

TAFITI ZAENDELEA KUTUMIKA KATIKA MAAMUZI YA SERA KUPITIA PORTAL MPYA YA SERIKALI

Picha
  Na Jasmine Shamwepu,Dodoma HATUA ya Serikali kuanzisha mfumo wa kidijitali wa kukusanya na kusambaza tafiti mbalimbali nchini, inatarajiwa kuleta mapinduzi katika matumizi ya ushahidi wa kisayansi kwenye maamuzi ya sera na mipango ya maendeleo. Kupitia portal hiyo mpya, matokeo ya tafiti yaliyokuwa yakibaki kwenye makabrasha au kuhifadhiwa ndani ya taasisi, sasa yatapatikana kwa urahisi na kutumiwa moja kwa moja na watunga sera, wataalamu pamoja na wadau wa maendeleo. Akizungumza Machi 23, 2026 jijini Dodoma wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kitaifa wa taasisi za utafiti, Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi Kida, amesema mfumo huo ni sehemu ya mageuzi ya kimkakati ya kuifanya Tanzania kuwa taifa linaloongozwa na ushahidi katika kufanya maamuzi. Ameeleza kuwa portal hiyo itaongeza uwazi, kuimarisha ushirikishwaji wa wadau na kuhakikisha tafiti zinatumika kutatua changamoto halisi za wananchi. “Mfumo huu utasaidia kuungan...

HALMASHAURI YA JIJI LA DAR KURASIMISHA SHUGHULI ZA WACHAKATAJI TAKA KUJIINUA KIUCHUMI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam.  HALMASHAURI ya Jiji la Dar es Salaam kupitia Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji imeendelea kuchukua hatua za kuimarisha uchumi wa Wananchi kwa kurasimisha shughuli za wachakataji wa taka rejea. Kupitia kikao kilichofanyika tarehe 18 Machi 2026,  katika ukumbi mdogo wa meya Jijini Dar es salaam. wadau wamepewa mwongozo wa namna ya kufanya shughuli zao kwa kuzingatia sheria, ikiwemo usajili na upatikanaji wa leseni za biashara. Hatua hii inalenga kufungua fursa zaidi za ajira kwa vijana na wanawake, kulinda mazingira, na kuongeza kipato kwa wajasiriamali wadogo. Aidha, urasimishaji huu utawezesha upatikanaji wa elimu, teknolojia na masoko bora, hivyo kuchangia maendeleo endelevu ya jiji.