Machapisho

MBUNGE MNZAVA AWAKABIDHI WAZEE 300 BIMA ZA AFYA KUPITIA MAKUYUNI FESTIVAL

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Korogwe. MBUNGE wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Mhe. Timotheo Mnzava, ameendelea kutekeleza mikakati ya kuboresha huduma za afya kwa wazee kwa kugawa Bima za Afya kwa zaidi ya wazee 300 waliohudhuria Makuyuni Festival, tamasha lililowakutanisha wakazi wa maeneo mbalimbali ya jimbo hilo. Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mhe. Mnzava amesema  hatua hiyo inalenga kuhakikisha wazee wanapata huduma bora za matibabu bila vikwazo vya kifedha, huku akisisitiza kuwa afya ya wazee ni sehemu muhimu ya ustawi wa jamii.  "Bima hizo zitawawezesha wazee kupata matibabu kwa wakati wowote na katika vituo vilivyosajiliwa, hatua inayotafsiriwa kama kupunguza mzigo wa gharama za afya kwa familia nyingi za kipato cha chini."amesema Mhe.Mnzava Katika tamasha hilo, Mbunge Mnzava pia alipata fursa ya kushiriki chakula cha pamoja na wazee, watu wenye ulemavu, vijana na wananchi wengine waliohudhuria, akisema kitendo hicho ni sehemu ya kuimarisha mshikamano na kuonyesha ushiriki...

WAZEE TABORA WANENA MAZITO KWA RAIS SAMIA

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora ZIKIWA zimebakia siku chache kumalizika mwaka 2025 na kuanza mwaka mpya wa 2026, wazee wa Mkoa wa Tabora wameeleza kuridhishwa na utendaji wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika awamu yake ya pili baada ya kuingia madarakani. Wameeleza kuwa weledi na ufanisi wa Kiongozi mzuri unapimwa kwa mambo makubwa matatu ambayo ni hali ya usalama wa nchi, kasi ya maendeleo na uchumi, mambo haya yamesimamiwa vizuri na nchi inapiga hatua kubwa. Mzee Elisha Daud Mponeja ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi wa Jadi katika halmashauri ya manispaa Tabora ameeleza kuwa Rais Samia amefanya kazi nzuri sana katika kipindi chake cha miaka minne na hata sasa anaendelea vizuri. Amefafanua kuwa baada ya kukabidhiwa nchi Machi 19, 2021 kutoka kwa mtangulizi wake aliyetangulia mbele za haki, Dkt John Pombe Magufuli, watanzania walishuhudia kasi kubwa ya utekekezaji miradi ya maendeleo katika sekta zote. ‘Katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wake mambo makubwa yamefanyika ikiw...

ASKOFU MEIVUKIE ATAKA UPENDO, HAKI NA AMANI VIDUMISHWE

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora ASKOFU wa Kanisa la TAG Jimbo la Tabora Kati na Kiongozi wa Kanisa la Kitete Christian Centre (KCC) la Mjini Tabora Rev. Paul Meivukie ameomba upendo, haki na amani viendelee kudumishwa nchini ili jamii iishi kwa utulivu. Ametoa rai hiyo leo kwenye ibada ya sikukuu ya krismas ambapo ameeleza kuwa krismasi ni tukio kubwa linalobeba ujumbe wa upendo, haki na amani kwa watu wote, hivyo mamlaka na jamii kwa ujumla hawana budi kuyadumisha. Amesisitiza kuwa tunapoadhimisha sikukuu hii ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo hatuna budi kumwomba Mungu ili taifa liendelee kuwa na amani na utulivu na upendo na haki viendelee kudumishwa wakati wote ili Mungu aliinue taifa lake. ‘Taifa liliingia kwenye wakati mgumu sana Oktoba 29, 2025 siku ya uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani, hili halipaswi kufumbiwa macho, kama taifa tunapaswa kusameheana na kupendana ili kudumishwa amani yetu', amesema. Askofu Meivukie ameasa waumini wa kanisa hilo na jamii kwa ujumla kuishi tabia na...

KONYAGI INATOA FURSA YA KIPEKEE MSIMU HUU WA SIKUU

Picha
Konyagi inatoa fursa ya kipekee mashabiki wake kujishinda Zawadi mbali mbali kupitia maswali mbali mbali.

TANGAZO

Picha
Kwa Matangazo wasiliana nasi kupitia namba 0789852956 na 0624489100. Tunatoa punguzo kwa kila Tangazo katika kipindi hiki cha Msimu wa Sikuu ya Krismas na Mwaka Mpya. Mteja wetu na mdau wetu wa habari wahi mapema......

MIRERANI WAWAPATIA TABASAMU LA SIKUKUU WATOTO YATIMA

Picha
  Na Mwandishi wetu, Mirerani MAMLAKA ya Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, imewapatia zawadi ya vyakula, mbuzi na fedha taslimu, watoto yatima na waliokuwa wanaishi katika mazingira hatarishi wa kituo cha Light In Africa kwenye kusherehekea sikukuu ya Christmas na mwaka mpya wa 2026 kwa tabasamu. Afisa mtendaji mkuu wa mamlaka ya mji mdogo wa Mirerani, (TEO) Isack Mgaya akizungumza wakati akikabidhi vyakula hivyo ameeleza kwamba gharama walizotumia kuwapatia tabasamu watoto hao ni shilingi 1,847,000. Mgaya amesema lengo lao ni kuwapa tabasamu  kwenye sikukuu ya Christmas na mwaka mpya wa 2026 watoto hao wa kituo cha Light In Africa ambao ni yatima na waliokuwa wanaoishi katika mazingira hatarishi washerehekee kwa furaha. Amesema pamoja na kuwapa fedha taslimu shilingi 220,000 wametumia shilingi 1,627,000 katika kununua mahitaji mbalimbali ikiwemo mbuzi mmoja, nyama kilo 10  na vyakula kwa ajili ya kusherehekea sikukuu hizo za mwisho wa mwaka. Ameele...

WAZIRI SHARIFF AZINDUA JENGO LA MRI HOSPITALI YA ABDULAA MZEE

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Pemba. WAZIRI wa Kazi na Uwekezaji Shariff Ali Shariff amesema Uwepo wa huduma ya MRI katika Hospitali ya Abdulaa Mzee Mkoani, Pemba ni hatua kubwa katika kuimarisha uwezo wa mfumo wetu wa afya na utawezesha wagonjwa kupata uchunguzi wa haraka, sahihi na wa uhakika.  Hayo ameyaeleza katika Hospitali ya Abdulla Mzee Mkoani wakati wa alipofungua jengo la huduma za MRI ikiwa ni sehemu ya shamra shamra za Miaka 62 ya Mapinduzi Zanzibar.  Waziri Shariff amesema huduma ya MRI itaongeza uwezo wa madaktari kufanya maamuzi ya kitabibu kwa ufanisi zaidi, sambamba na matumizi ya teknolojia ya kisasa katika sekta ya afya na itasaidia kupunguza kuchelewa kwa matibabu, kuokoa maisha na kupunguza gharama kwa familia na Serikali kwa ujumla.  Aidha amesema kuwa uwamuzi wa kuanzisha huduma ya MRI kisiwani Pemba unaonesha wazi dhamira ya dhati ya Serikali ya Awamu ya Nane ya kusogeza huduma muhimu karibu kwa wananchi na kupunguza rufaa zisizo za lazima, kuimarisha ...

BANK YA AMANA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA TRA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam. KAMISHNA Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Yusuph Juma Mwenda, leo tarehe 24.12.2025 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Bank ya Amana, Bw. Abubakar Athman Ali, katika ofisi za TRA jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi hizo mbili. Katika kikao hicho, viongozi hao wamejadili maeneo mbalimbali ya ushirikiano ikiwemo kuboresha mifumo ya ulipaji kodi kupitia taasisi za kifedha, pamoja na kuhamasisha walipakodi kulipa kodi kwa hiari kwa kutumia huduma za kibenki. Bw. Abubakar amesema Bank ya Amana ipo tayari kushirikiana kwa karibu na TRA katika kuhakikisha huduma bora zinapatikana kwa walipakodi, huku akiweka mkazo kwenye uboreshaji wa mifumo na elimu ya kodi kwa wateja wa benki hiyo. Kwa upande wake, Kamishna Mkuu Bw. Mwenda amepongeza ushirikiano huo na kusema kuwa hatua kama hizo zinaimarisha mazingira ya ulipaji kodi na kuchangia katika kukuza mapato ya Taifa.

DKT PIMA AAGIZA WAKUU WA SHULE KUSIMAMIA NIDHAMU

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora WALIMU Wakuu wa shule za msingi na sekondari katika Halmashauri ya Manispaa Tabora wameagizwa kusimamia ipasavyo nidhamu za walimu na wanafunzi katika shule zao ili kuinua juu taaluma.   Agizo hilo limetolewa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa hiyo Dkt John Pima alipokuwa akifunga semina maalumu ya Maafisa Elimu, Walimu wa Nidhamu, Waratibu na Wakuu wa shule zote mjini hapa. Amesema kuwa serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imefanya maboresho makubwa ya miundombinu katika shule zote za Manispaa hiyo hivyo kuboreshwa mazingira ya ufundishaji na kujifunza. ‘Mazingira bora yaliyopo katika shule zetu ni chachu muhimu ya kuwezesha watoto wetu kufanya vizuri zaidi katika mitihani yao ya kitaifa hivyo kuongeza ufaulu katika manispaa yetu, katika hili ni lazima tuimarishe nidhamu’, ameeleza. Dkt.Pima ameahidi kutoa motisha nzuri kwa kila mwalimu ambaye somo lake litapata alama A za ufaulu kwa idadi yoy...

HABARI PICHA

Picha
Shirika lisilo la kiserikali la Marafiki wa Serengeti Uswiss, wametoa msaada wa vifaa vya doria vya aina mbalimbali ikiwemo mahema, tochi, sleeping bags na matairi kwaajili ya kusaidia shughuli za doria. #wildanimals #travelphoto #wizarayamaliasilinautalii

USINDI AMCOS WANUNUA TREKTA KWA KILIMO NA KUJIONGEZEA KIPATO

Picha
  Na Lubango Mleka, Kaliua. CHAMA Cha Msingi Usindi AMCOS Ltd cha Kaliua Mkoani Tabora kimenunua Trekta kwa ajili ya kufanyia shughuli za Kilimo na pia watakodishia kufanyia shughuli za Kiuchumi kujiongezea kipato. Uzinduzi wa Trekta umefanywa Desemba 23, 2025 na Katibu Tawala Wilaya ya Kaliua Sosthenes Chakupanyuka, katika Mkutano Mkuu wa kufunga mwaka wa Chama hicho. Sosthenes amewapongeza kwa hatua hiyo kubwa na kusema Usindi AMCOS ni chama cha mfano wa kuigwa kwa Kaliua kwa kutimiza vyema lengo lao la kununua Trekta yao ya pili.Ameahidi kuwa nao pamoja  penye changamoto ashirikishwe. Pia amefurahishwa sana na namna ambayo wamekuwa wakijali jamii kwani wameweza kutoa mifuko 100 ya Simenti kwa ajili ya kujenga shule, kuweka umeme kwenye shule za Msingi na kujenga barabara ya kuelekea Zahanati ya Usindi. Mrajis Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Tabora Venance Msafiri ameahidi kuwapeleka wakulima mafunzo kuongeza Elimu ya Kilimo na Madereva wa Matrekta kuongeza ujuzi....

SERIKALI YASHAURIWA KUVIPA RUZUKU VYOMBO VYA HABARI

Picha
Na Mwamdishi Wetu, WAHARIRI nchini, wameishauri serikali kuvipa ruzuku Vyombo vya Habari ili vifanye kazi kwa ufanisi zaidi. Akizungumza kwenye semina ya siku moja iliyoandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) leo, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile alitoa kauli hiyo iliyoungwa mkono na Wahariri wenzake. “Hatuwezi kufanya kazi vizuri bila kuwezeshwa, tuachane na kutoka mataifa ya nje kwamba, serikali ikiwezesha Vyombo vya Habari, havitakuwa huru. “Tunaonaje aibu kuviwezesha Vyombo vya Habari ili vijenge miundombinu ya fikra ili watu wasichome nchi yao? Mbona Vyama vya Upinzani vinapewa ruzuku na bado vinaisimamia serikali bila kuyumbishwa?” amesema Balile. Balile alitoa kauli hiyo baada ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Hamis Masauni kushauri Vyombo vya Habari kuelimisha wananchi hususani vijana kuhusu faida na fursa zilizopo ndani ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

CHUO CHA UHASIBU ARUSHA MABINGWA SHIMIVUTA

Picha
Na Allan Kitwe, Tabora CHUO cha Uhasibu Arusha (IAA) kimetwaa ubingwa wa jumla wa mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Vyuo Vikuu Tanzania (SHIMIVUTA) yaliyomalizika jana katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Wavulana Tabora. IAA imetwaa ubingwa huo baada ya kushika nafasi ya kwanza kati ya vyuo vikuu 16 vilivyoshiriki mashindano hayo mwaka huu kati ya Vyuo Vikuu 25 wanachama wa Shirikisho hilo. Chuo hicho kimekuwa mshindi wa kwanza katika mchezo wa riadha, draft, bao, mpira wa mikono, wavu na kushika nafasi ya pili katika michezo ya pool table, pete, kikapu na nafasi ya tatu kwenye karata. Rais wa Shirikisho hilo Juhudi Elirehema Sam ameeleza kufurahishwa na mashindao ya mwaka huu kutokana na ushindani mkubwa ulikuwepo na kuahidi kuwa mwakani maandalizi yatakuwa makubwa zaidi ya hapo. Amesistiza kuwa licha ya viwanja kujaa maji kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nchini timu zote zilicheza kwa ustadi mkubwa na kuonesha vipaji vya hali ya juu. Akihitimisha mashindano hayo jana...