Machapisho

WAZIRI SHARIFF AZINDUA JENGO LA MRI HOSPITALI YA ABDULAA MZEE

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Pemba. WAZIRI wa Kazi na Uwekezaji Shariff Ali Shariff amesema Uwepo wa huduma ya MRI katika Hospitali ya Abdulaa Mzee Mkoani, Pemba ni hatua kubwa katika kuimarisha uwezo wa mfumo wetu wa afya na utawezesha wagonjwa kupata uchunguzi wa haraka, sahihi na wa uhakika.  Hayo ameyaeleza katika Hospitali ya Abdulla Mzee Mkoani wakati wa alipofungua jengo la huduma za MRI ikiwa ni sehemu ya shamra shamra za Miaka 62 ya Mapinduzi Zanzibar.  Waziri Shariff amesema huduma ya MRI itaongeza uwezo wa madaktari kufanya maamuzi ya kitabibu kwa ufanisi zaidi, sambamba na matumizi ya teknolojia ya kisasa katika sekta ya afya na itasaidia kupunguza kuchelewa kwa matibabu, kuokoa maisha na kupunguza gharama kwa familia na Serikali kwa ujumla.  Aidha amesema kuwa uwamuzi wa kuanzisha huduma ya MRI kisiwani Pemba unaonesha wazi dhamira ya dhati ya Serikali ya Awamu ya Nane ya kusogeza huduma muhimu karibu kwa wananchi na kupunguza rufaa zisizo za lazima, kuimarisha ...

BANK YA AMANA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA TRA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam. KAMISHNA Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Yusuph Juma Mwenda, leo tarehe 24.12.2025 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Bank ya Amana, Bw. Abubakar Athman Ali, katika ofisi za TRA jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi hizo mbili. Katika kikao hicho, viongozi hao wamejadili maeneo mbalimbali ya ushirikiano ikiwemo kuboresha mifumo ya ulipaji kodi kupitia taasisi za kifedha, pamoja na kuhamasisha walipakodi kulipa kodi kwa hiari kwa kutumia huduma za kibenki. Bw. Abubakar amesema Bank ya Amana ipo tayari kushirikiana kwa karibu na TRA katika kuhakikisha huduma bora zinapatikana kwa walipakodi, huku akiweka mkazo kwenye uboreshaji wa mifumo na elimu ya kodi kwa wateja wa benki hiyo. Kwa upande wake, Kamishna Mkuu Bw. Mwenda amepongeza ushirikiano huo na kusema kuwa hatua kama hizo zinaimarisha mazingira ya ulipaji kodi na kuchangia katika kukuza mapato ya Taifa.

DKT PIMA AAGIZA WAKUU WA SHULE KUSIMAMIA NIDHAMU

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora WALIMU Wakuu wa shule za msingi na sekondari katika Halmashauri ya Manispaa Tabora wameagizwa kusimamia ipasavyo nidhamu za walimu na wanafunzi katika shule zao ili kuinua juu taaluma.   Agizo hilo limetolewa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa hiyo Dkt John Pima alipokuwa akifunga semina maalumu ya Maafisa Elimu, Walimu wa Nidhamu, Waratibu na Wakuu wa shule zote mjini hapa. Amesema kuwa serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imefanya maboresho makubwa ya miundombinu katika shule zote za Manispaa hiyo hivyo kuboreshwa mazingira ya ufundishaji na kujifunza. ‘Mazingira bora yaliyopo katika shule zetu ni chachu muhimu ya kuwezesha watoto wetu kufanya vizuri zaidi katika mitihani yao ya kitaifa hivyo kuongeza ufaulu katika manispaa yetu, katika hili ni lazima tuimarishe nidhamu’, ameeleza. Dkt.Pima ameahidi kutoa motisha nzuri kwa kila mwalimu ambaye somo lake litapata alama A za ufaulu kwa idadi yoy...

HABARI PICHA

Picha
Shirika lisilo la kiserikali la Marafiki wa Serengeti Uswiss, wametoa msaada wa vifaa vya doria vya aina mbalimbali ikiwemo mahema, tochi, sleeping bags na matairi kwaajili ya kusaidia shughuli za doria. #wildanimals #travelphoto #wizarayamaliasilinautalii

USINDI AMCOS WANUNUA TREKTA KWA KILIMO NA KUJIONGEZEA KIPATO

Picha
  Na Lubango Mleka, Kaliua. CHAMA Cha Msingi Usindi AMCOS Ltd cha Kaliua Mkoani Tabora kimenunua Trekta kwa ajili ya kufanyia shughuli za Kilimo na pia watakodishia kufanyia shughuli za Kiuchumi kujiongezea kipato. Uzinduzi wa Trekta umefanywa Desemba 23, 2025 na Katibu Tawala Wilaya ya Kaliua Sosthenes Chakupanyuka, katika Mkutano Mkuu wa kufunga mwaka wa Chama hicho. Sosthenes amewapongeza kwa hatua hiyo kubwa na kusema Usindi AMCOS ni chama cha mfano wa kuigwa kwa Kaliua kwa kutimiza vyema lengo lao la kununua Trekta yao ya pili.Ameahidi kuwa nao pamoja  penye changamoto ashirikishwe. Pia amefurahishwa sana na namna ambayo wamekuwa wakijali jamii kwani wameweza kutoa mifuko 100 ya Simenti kwa ajili ya kujenga shule, kuweka umeme kwenye shule za Msingi na kujenga barabara ya kuelekea Zahanati ya Usindi. Mrajis Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Tabora Venance Msafiri ameahidi kuwapeleka wakulima mafunzo kuongeza Elimu ya Kilimo na Madereva wa Matrekta kuongeza ujuzi....

SERIKALI YASHAURIWA KUVIPA RUZUKU VYOMBO VYA HABARI

Picha
Na Mwamdishi Wetu, WAHARIRI nchini, wameishauri serikali kuvipa ruzuku Vyombo vya Habari ili vifanye kazi kwa ufanisi zaidi. Akizungumza kwenye semina ya siku moja iliyoandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) leo, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile alitoa kauli hiyo iliyoungwa mkono na Wahariri wenzake. “Hatuwezi kufanya kazi vizuri bila kuwezeshwa, tuachane na kutoka mataifa ya nje kwamba, serikali ikiwezesha Vyombo vya Habari, havitakuwa huru. “Tunaonaje aibu kuviwezesha Vyombo vya Habari ili vijenge miundombinu ya fikra ili watu wasichome nchi yao? Mbona Vyama vya Upinzani vinapewa ruzuku na bado vinaisimamia serikali bila kuyumbishwa?” amesema Balile. Balile alitoa kauli hiyo baada ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Hamis Masauni kushauri Vyombo vya Habari kuelimisha wananchi hususani vijana kuhusu faida na fursa zilizopo ndani ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

CHUO CHA UHASIBU ARUSHA MABINGWA SHIMIVUTA

Picha
Na Allan Kitwe, Tabora CHUO cha Uhasibu Arusha (IAA) kimetwaa ubingwa wa jumla wa mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Vyuo Vikuu Tanzania (SHIMIVUTA) yaliyomalizika jana katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Wavulana Tabora. IAA imetwaa ubingwa huo baada ya kushika nafasi ya kwanza kati ya vyuo vikuu 16 vilivyoshiriki mashindano hayo mwaka huu kati ya Vyuo Vikuu 25 wanachama wa Shirikisho hilo. Chuo hicho kimekuwa mshindi wa kwanza katika mchezo wa riadha, draft, bao, mpira wa mikono, wavu na kushika nafasi ya pili katika michezo ya pool table, pete, kikapu na nafasi ya tatu kwenye karata. Rais wa Shirikisho hilo Juhudi Elirehema Sam ameeleza kufurahishwa na mashindao ya mwaka huu kutokana na ushindani mkubwa ulikuwepo na kuahidi kuwa mwakani maandalizi yatakuwa makubwa zaidi ya hapo. Amesistiza kuwa licha ya viwanja kujaa maji kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nchini timu zote zilicheza kwa ustadi mkubwa na kuonesha vipaji vya hali ya juu. Akihitimisha mashindano hayo jana...

SERIKALI YATOA MWELEKEO MPYA KATIKA UWEKEZAJI VIWANDA VYA BIDHAA ZA AFYA NCHINI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam SERIKALI imetangaza rasmi mwelekeo mpya wa kimkakati wa kuharakisha uwekezaji wa viwanda vya bidhaa za afya nchini ikiwa ni lengo la kuimarisha usalama wa afya wa nchi, kupunguza utegemezi wa dawa, na kuliweka taifa kwenye ramani ya uzalishaji wa dawa barani Afrika na Duniani. Hayo yamebainishwa na Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa leo Desemba 23, 2025 katika kikao cha wazalishaji wa dawa na bidhaa za afya pamoja na uzinduzi wa kikosi kazi cha uharakishaji mchakato wa uwekezaji wa viwanda vya dawa nchini kilichofanyika Ofisi ndogo za Wizara ya Afya Jijini Dar es Salaam. “Ujenzi wa viwanda vya dawa si mpango wa majaribio bali ni uamuzi wa kimkakati uliokwisha amuliwa na Serikali, usalama wa afya wa Taifa hauwezi kujengwa kwa kutegemea uagizaji wa dawa pekee, bali unahitaji uzalishaji wa ndani unaokidhi viwango vya kimataifa” amesema Waziri Mchengerwa. Amebainisha kuwa Serikali imeanzisha mfumo maalum wa uharakishaji wa uwekezaji nchini kupitia...

EWURA, TRA KUIMARISHA USHIRIKIANO

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma. WATENDAJI wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) na wenzao wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), leo 23 Desemba 2025, wamekutana na  kujadili namna ya kuimarisha ushirikiano wa utendaji hususani katika usimamizi wa masuala ya kikodi yanayotokana na huduma zinazodhibitiwa na EWURA.  Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Bwana Gerald Maganga, amesema EWURA ni mshirika mzuri katika kuisaidia TRA kutekeleza wajibu wake wa usimamizi wa kodi nchini.  “Ushirikiano uliopo kati ya taasisi hizi mbili, utatupeleka mbele, tuudumishe na tusimamie utekelezaji wa makubaliano yetu,” alisema.  Meneja wa TRA mkoa wa Dodoma, Bwana Pendolake Elinisafi, ameishukuru EWURA kwa kuipatia TRA ushirikiano mzuri, na kuahidi kuuendeleza ili kuweka msingi imara wa mafanikio ya taasisi hizo mbili na taifa kwa ujumla.

UONGOZI WA APRM WAKUTANA NA VIONGOZI WA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam. KATIBU Mtendaji wa Mpango wa Hiari wa Nchi za Umoja wa Afrika wa Kujitathmini kwa Vigezo vya Utawala Bora (APRM) Tanzania, Bw. Lamau Mpolo, amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa wanafunzi kutoka vyuo vikuu mbalimbali nchini. Lengo la kikao hicho lilikuwa kujadili nafasi ya vijana katika kukuza dhana ya Utawala Bora kama nguzo muhimu ya kuimarisha amani na usalama nchini Tanzania. Katika kikao hicho, Bw. Mpolo alisisitiza umuhimu wa ushiriki wa vijana katika masuala ya utawala, akieleza kuwa vijana ni rasilimali muhimu katika kujenga jamii yenye uwajibikaji, uwazi na maamuzi jumuishi. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika Desemba 22, 2025, katika Ofisi za APRM zilizopo katika jengo la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, jijini Dar es Salaam.

KATAMBI AAGIZA KULINDWA USHINDANI WA HAKI, AKEMEA UKIRITIMBA WA BEI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas Katambi (Mb), ameliagiza Baraza la Ushindani (FCT) kuendelea kusimamia na kulinda ushindani wa haki ili kuondoa vitendo vya ukiritimba, hususan katika suala la kupandisha bei za bidhaa na huduma. Ameyasema hayo wakati wa ziara yake katika Baraza la Ushindani Desemba 22, 2025 Jijini Dar es Salaam akisisitiza kuwa ushindani wa haki ni msingi muhimu wa ukuaji wa biashara, kwani vitendo vya ukiritimba vimekuwa vikiathiri biashara nyingi na walaji. Ameeleza kuwa biashara zinapaswa kufanyika kwa kuzingatia ulinzi wa walaji, ambapo bei za bidhaa na huduma ziwe za haki, bidhaa ziwe na ubora, na uchunguzi wowote ufanyike kwa haki na kwa kuzingatia misingi ya kisheria. Mhe. Katambi amebainisha kuwa Serikali inaendelea kuhamasisha uwekezaji kwa kuboresha sera rafiki, kufanya marekebisho ya sheria na kuendelea na maboresho ya mazingira ya biashara ili kuhakikisha Tanzania inakuwa mahali salama na rafiki kwa kufanya...