Machapisho

FCC YANG’ARA KATIKA KONGAMANO LA 16 LA WATAALAMU WA MANUNUZI NA UGAVI

Picha
Na.Mwandishi, Wetu. TUME ya Ushindani (FCC) imetunukiwa tuzo maalum ya kutambua mchango wake katika maendeleo ya Sekta ya Manunuzi na Ugavi nchini. Tuzo hiyo imekabidhiwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mshamu Munde, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, na kupokelewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha FCC, Bi. Roberta Feruzi. Hafla ya utoaji wa tuzo hiyo ilifanyika katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi, lililofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), jijini Arusha lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB). FCC imeshiriki kongamano hilo kama mdau muhimu wa sekta ya manunuzi na ugavi, ambapo iliwasilisha mada kuhusu umuhimu wa ushindani wa haki katika masuala ya manunuzi na ugavi, hususan katika kulinda mnyororo wa thamani. Kupitia kongamano hilo, Tume pia ilitoa elimu kwa wadau mbalimbali kuhusu majukumu na kazi zake, ikisisitiza nafasi yake katika kuhakikisha mazingira ya ushindani yanayochochea uwazi, ufanisi na ...

ELIMU YA USHINDANI YAONGEZA UWAZI KWA WAFANYABIASHARA MBEYA

Picha
Na.Mwandishi Wetu. BARAZA la Ushindani (FCT) jana Desemba 18, 2025, limeendesha semina ya elimu kwa wadau mkoani Mbeya kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu majukumu na huduma zinazotolewa na Baraza hilo. Semina hiyo ilifanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya na kufunguliwa na Katibu Tawala Msaidizi – Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Mbeya, Bi Anna Mwambene, ambaye aliwahimiza wadau kutumia ipasavyo mifumo ya kisheria iliyopo na kuwa mabalozi wa kuitangaza huduma za Baraza la Ushindani. Bi Mwambene alisema uelewa wa sheria na taratibu za ushindani ni muhimu katika kukuza mazingira bora ya biashara na uwekezaji, akisisitiza umuhimu wa wadau kushiriki kikamilifu katika kulinda haki zao kwa kutumia mifumo rasmi iliyowekwa na Serikali. Katika semina hiyo, Baraza la Ushindani liliwapatia washiriki elimu kuhusu matumizi ya mfumo wa kidijitali wa kuwasilisha rufaa zinazotokana na maamuzi ya Tume ya Ushindani (FCC) pamoja na mamlaka mbalimbali za udhibiti, zikiwemo LATRA, E...

TAKA ZAWAKELA WAFANYABIASHARA SOKO LA SABASABA DODOMA

Picha
  Na Hamida Ramadhani, Dodoma. WAFANYABIASHARA  wa soko la matunda na mbogamboga Sabasaba jijini Dodoma wameliomba Jiji la Dodoma kuondoa takataka zilizojaa katika dampo lililopo ndani ya soko hilo, wakisema hali hiyo inahatarisha afya zao. Wakizungumza kwa nyakati tofauti, watanyabiashara hao wamesema dampo hilo limejaa kupita kiasi na takataka kushindwa kuondolewa kwa wakati, hali inayosababisha harufu kali na mazingira machafu, jambo linalodaiwa kuchangia baadhi yao kuugua maradhi mbalimbali yakiwemo ya mfumo wa hewa. Paulina, maarufu kama Mama Kibibi, ni mmoja wa wafanyabiashara sokoni hapo. Anasema hali ya taka kujaa kwa muda mrefu imemletea matatizo ya kiafya, hali inayomfanya ashindwe kufanya shughuli zake ipasavyo. Kwa upande wake, Agaudence Temba, mfanyabiashara wa matunda katika soko hilo, ameuomba uongozi wa Jiji la Dodoma kukaa meza moja na wafanyabiashara ili kutafuta suluhisho la kudumu. Anapendekeza kuwepo kwa mchango wa shilingi mia mbili kwa siku kutoka kwa wa...

JAFO ARIDHISHWA NA UJENZI WA MABWENI NA MADARASA SHULE YA SEKONDARI DK. SELEMANI JAFO

Picha
Na.Mwandishi Wetu-KISARAWE. MBUNGE wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, ameridhishwa na hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa mabweni mawili na madarasa katika Shule ya Sekondari Dkt.Selemani Jafo, na kuhimiza Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe kuhakikisha mradi huo unakamilika mapema ili ifikapo Januari 2026 shule hiyo iweze kupokea wanafunzi wa bweni. Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo wilayani Kisarawe, Dkt. Jafo amesema ziara hiyo ni sehemu ya kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), hususan katika sekta ya elimu. “Tumeendelea na ziara yetu ya kuhakikisha tunasukuma utekelezaji wa ilani wilayani Kisarawe, na eneo kubwa tulilolipa kipaumbele ni uimarishaji wa sekta ya elimu. Hapa Shule ya Sekondari Selemani Jafo kuna kazi kubwa inaendelea, ikiwemo ujenzi wa mabweni mawili na madarasa ili kuboresha mazingira ya utoaji wa elimu,” amesema. Dkt. Jafo amepongeza usimamizi wa mradi huo, akieleza kuwa ujenzi umefikia zaidi ya asil...

WATAALAM WA MAABARA WATAKIWA KUSIMAMIA WELEDI NA MATUMIZI SAHIHI YA RASILIMALI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam. Wataalam wa maabara wametakiwa kusimamia weledi katika utekelezaji wa majukumu yao pamoja na kuhakikisha matumizi sahihi ya rasilimali ili kuboresha utoaji wa huduma bora za afya kwa jamii. Wito huo umetolewa leo, Desemba 19, 2025, na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu kutoka Wizara ya Afya Bw. Issa Ng’imba wakati wa mahafali ya mafunzo ya Global Laboratory Leadership Program (GLLP) yaliyofanyika jijini Dar es Salaam. Bw. Ng’imba amesema mafunzo hayo yalilenga kuwajengea uwezo viongozi chipukizi wa maabara katika masuala ya uongozi na kuwapa mbinu za kukabiliana na changamoto zinazowakabili katika maeneo yao ya kazi.  Ameongeza kuwa mafunzo hayo yamekuja kwa wakati muafaka, hasa katika kipindi ambacho kuna hitaji la kuimarisha mifumo ya maabara, hususan katika masuala ya utawala, utatuzi wa kero za wagonjwa, upimaji pamoja na ushiriki katika ufuatiliaji wa magonjwa. “Niishukuru Serikali pamoja na mdau wetu, Global Fund, kwa kutambua umuhimu wa ku...

MABORESHO SEKTA YA AFYA YAGUSA WANANCHI TABORA

Picha
  Na Allan Kitwe, TABORA. VIONGOZI na Wadau mbalimbali Mkoani Tabora wamepongeza juhudi kubwa zilizofanywa na zinazoendelea kufanywa na serikali ya awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuboresha huduma za afya. Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti wameeleza kuwa maboresho makubwa ya miundombinu ya huduma za afya yaliyofanywa na serikali ya Awamu ya Sita yameleta na mageuzi makubwa katika sekta  hiyo. Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Mkoani hapa, Idd Moshi ameeleza kuwa ndoto ya Watanzania kupata huduma bora na za uhakika za afya imeanza kutimia baada ya maboresho makubwa ya miundombinu na ujenzi wa hospitali mpya za Wilaya, Vituo vya afya na zahanati katika Wilaya, Kata na Vijiji vyote.. Ameongeza kuwa hata kwenye mikutano ya kampeni za uchaguzi mkuu mwaka huu Rais Samia aliahidi kutekeleza mpango wa Huduma ya Bima ya Afya kwa wote ndani ya siku 100 tuu akiingia madarakani... 'Hii ni habari njema kwa Watanzania wote na inaonesha jinsi Rais ...

MWENYEKITI SIKONGE AHIMIZA KASI YA MAENDELEO

Picha
  Na Allan Kitwe, Sikonge. MWENYEKITI wa Halmasahauri ya Wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora Andrea Gasto amewataka Madiwani na Watendaji wa halmashauri hiyo kwenda na kasi ya serikali ya awamu ya sita katika kukusanya mapato ili kuharakisha maendeleo. Ametoa rai hiyo jana alipokuwa akiongea na watumishi na madiwani wa halmashauri hiyo baada ya kuchaguliwa kwa kishindo kuongoza halmashauri hiyo kwa kipindi cha miaka mitano ijayo, yaani 2025-2030. Amesema kuwa wakazi wa Halmashauri hiyo wana imani na matumaini makubwa na madiwani na watumishi wa halmashauri hiyo na wako tayari kuwapa ushirikiano ili kuchocheo kasi ya maendeleo yao. Mwenyekiti amedokeza kuwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan alishatoa mwelekeo wa yale atakayowafanyia wana Sikonge ndani ya siku 100 na mengineyo mengi kama yalivyobainishwa kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2025-2030. ‘Wakazi wa Sikonge wana imani kubwa na serikali yao ya Chama Cha Mapinduzi, naomba kila mmoja aliyepewa dhamana ya kusimamia maendeleo yao ...

MWENYEKITI NAMALULU AWEKWA PEMBENI KUPISHA UCHUNGUZI

Picha
  Na Mwandishi wetu, Simanjiro MWENYEKITI wa kijiji cha Namalulu Wilayani Simanjiro, Mkoani Manyara, Marumai Kirikai amepumzishwa kazi kwa muda wa siku 28 ili kupisha uchunguzi wa matumizi mabaya ya madaraka katika kijiji hicho. Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, Fakii Raphael Lulandala ameunda kamati ya watu saba itakayofanya uchunguzi kwa muda wa siku 24 na baada ya siku 28 endapo  Mwenyekiti huyo atabainika hausiki na tuhuma hizo atarejea kwenye nafasi yake. Lulandala ameyasema hayo wakati akizungumza na wakazi wa kijiji cha Namalulu, baada ya kusikiliza kero, malalamiko na changamoto zao. Ameeleza kwamba hamsimamishi kazi Mwenyekiti huyo ila anapisha uchunguzi kwa muda wa siku 28 na endapo hatakuwa na makosa atarejea tena kwenye nafasi hiyo. "Hausimamishwi kaz ila unakaa pembeni kwa muda wa siku 28 ili kupisha uchunguzi na ofisa mtendaji wa kijiji cha Namalulu Sarafina Olotu ataongoza kijiji kwa kipindi hiki," amesema DC Lulandala. DC Lulandala amewataja wajumbe saba wa kamati ...

MAREMA WANUNUA UWANJA WA MILIONI 30

Picha
  Na Mwandishi wetu, Mirerani  CHAMA cha wachimbaji madini Mkoa wa Manyara (MAREMA) kimenunua kiwanja cha thamani ya Sh30 milioni kwa ajili ya ujenzi wa matumizi ya ofisi na ukumbi wa mikutano. Chama hicho cha wachimbaji madini Mkoa wa Manyara hakina ofisi ambayo ni mali yao hivyo kupitia kiwanja hicho watajenga ofisi zao na ukumbi wa mikutano. Mwenyekiti wa Marema, Elisha Nelson Mnyawi ameyasema hayo kwenye mkutano mkuu wa mwaka 2025 wa wanachama wa MAREMA, Tawi la Mirerani ambao wanachimba madini ya Tanzanite na kinywe. Mnyawi amesema kwa sababu makao makuu ya MAREMA yapo Mirerani, wamenunua kiwanja hicho kwa ajili ya kujenga ofisi zao na ukumbi. "Ninawashukuru Makamu Mwenyekiti Money Yusuf, kampuni ya California, Joseph Manga na mimi mwenyewe kwa kutoa Sh5 milioni kila mmoja kwa ajili ya kununua kiwanja hicho," amesema Mnyawi. Amesema lengo ni kuhakikisha MAREMA inakuwa na ofisi yake na kila tawi linakuwa na ofisi zake kwa lengo la kuwatumikia wachimbaji madini wa Manyara....

JAFO: MAONO YA RAIS SAMIA NI NGUZO YA MAENDELEO YA TAIFA

Picha
  Na Alex Sona, Kisarawe. MBUNGE wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, amewaomba wananchi wa Kisarawe na watanzania kwa ujumla kumuombea Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa ana maono makubwa ya kuwatumikia Watanzania na kulisukuma Taifa mbele kimaendeleo. Dkt. Jafo ametoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza katika kikao maalum cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe, kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo. “Niwaombe wajumbe wa Halmashauri Kuu kuhakikisha tunamuombea Rais Dkt. Samia kwa kuwa ana kazi kubwa ya kuwaletea maendeleo Watanzania na kuhakikisha Taifa letu linaendelea kusonga mbele,” amesema Dkt.Jafo. Ameongeza kuwa amani na usalama ni nguzo muhimu za maendeleo ya kiuchumi, hivyo ni wajibu wa kila Mtanzania kumuombea Rais na Taifa kwa ujumla. “Bila amani na usalama, nchi yetu haiwezi kupata...

HABARI PICHA

Picha
Wajumbe wa Mkutano wakifuatilia mada juu ya Haki za Binadamu na Misingi ya Utawala Bora zinazotolewa wakati wa mafunzo ya Sekretarieti ya Kusimamia Maadili na Kushughulikia Mrejesho ya Makao Makuu ya Polisi yanayofanyika katika Chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es salaam (DPA) Disemba 17, 2025.