Machapisho

MZIZE ASHINDA TUZO YA MFUNGAJI BAO BORA LA MWAKA 2025 YA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU AFRIKA.

Picha
MSHAMBULIAJI  wa Yanga, Clement Mzize, ameshinda tuzo ya Mfungaji wa Bao Bora la Mwaka 2025 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF). Mzize ametangazwa mshindi wa kipengele hicho katika hafla ya utoaji wa tuzo hizo inayoendelea kufanyika Rabat, Morocco, leo Jumatano, Novemba 19, 2025. Bao lililompa tuzo hiyo ni lile alilofunga dhidi ya TP Mazembe katika mchezo wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu wa 2024/2025, uliochezwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Januari 4, 2025, ambapo Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 3-1. Mzize ameibuka mshindi mbele ya Ghizlane Chebbak, Abdellah Ouazane, Barbra Banda, Anas Roshdy, Asharaf Tapsoba, Calvin Fely, Ibrahim Adel, Jean Claude, Ndabayithethwa Ndlonolo, Refiloe Jane, Oussama Lamlioui na Soufiane Bayazid.

TIMU YA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAMTEMBELEA MDAU WA UTALII MZEE GEOFF FOX.

Picha
Na Lubango Mleka, Iringa. TIMU  ya Wataalamu kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii ikiongozwa na Mkurugenzi Msaidizi, Bi. Dainess Kunzugala leo Novemba 19,2025 imemtembelea mdau mkubwa  wa utalii na uhifadhi  kwa Kanda za Nyanda za juu Kusini Mzee Geoff Fox wilayani Mufindi mkoani Iringa lengo ikiwa ni kumhamasisha kuingia katika kuwania tuzo za uhifadhi na utalii za Serengeti 2025. Mzee Fox anamiliki kambi za kitalii (lodges) 7 ndani ya hifadhi na ndiye mwanzilishi wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani. Aidha, Mzee Fox ni mwekezaji wa kwanza wa kambi ya utalii katika Hifadhi ya Taifa Ruaha na ni kinara katika uhifadhi kwa kutunza na kulinda miti ya asili.

MRADI WA MAJIKO BANIFU WATAMBULISHWA HANANG

Picha
Majiko banifu 1,583 kusambazwa na kuuzwa kwa bei ya ruzuku, Jiko moja kuuzwa kwa bei ya ruzuku TZS 11,200. Na Mwandishi Wetu, Hanang. WAKAZI wa Hanang waaswa kuunga mkono jitihada za Serikali katika utunzaji wa mazingira kwa kutumia nishati safi na salama ya kupikia. Rai hiyo imetolewa  leo tarehe 19 Novemba, 2025 na Mkuu wa Wilaya ya Hanang Mheshimiwa Almishi Hazali wakati wa uzinduzi wa mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku. "Kinachofanyika leo ni kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia katika kutunza na kuhifadhi mazingira" alisema Mhe. Hazali. Mradi huu unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ni mwendelezo wa  juhudi za serikali  katika kutunza mazingira na kuboresha afya za  wananchi kwa kuhakikisha wananchi wanapata elimu ya kutosha ya umuhimu wa matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia. Aidha Serikali imeweke ruzuku ya asilimia 80 katika  kila j...

TUMEKUJA KUTIMIZA NDOTO YA RAIS SAMIA YA KULIJENGA TAIFA- MHE. CHANDE

Picha
Na Mwandishi wetu – Dodoma NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Hamad Chande (Mb) ameitaka menejimenti ya Wizara ya Maliasili na Utalii kutoa ushirikiano katika kutimiza ndoto za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kulijenga Taifa. Ameyasema hayo katika kikao na menejimenti ya Wizara hiyo kilichofanyika Mtumba jijini Dodoma Novemba 18,2025 mara baada ya kuripoti ofisini hapo. “Rais Samia amesema miradi tunayoihitaji kutekeleza ni mingi muda ni mchache na ndani ya siku 100 yako mambo anayotaka tuwe tumeyafikia hivyo sisi hatuwezi kuyafikia bila uwepo  wenu ninyi kwa taaluma zenu na mashirikiano yenu ya dhati kwetu” amesema Mhe. Chande. Pia ameitaka menejimenti hiyo kutekeleza falsafa ya  “Ishi vyema na watu ,Ufanye kazi kwa utu, Uwatambue watu ili na wewe uwe mtu mbele za watu."

MC PILIPILI AFARIKI DUNIA BAADA YA KUSHAMBULIWA, POLISI DODOMA WACHUNGUZA CHANZO

Picha
Na Jasmine Shamwepu, Dodoma. JESHI la Polisi Mkoa wa Dodoma limethibitisha kifo cha msanii maarufu wa vichekesho Emmanuel Mathias Matebe, maarufu kama MC Pilipili, kilichotokea Novemba 16, 2025 katika Kituo cha Afya Ilazo, jijini Dodoma, ambako alikuwa akipatiwa matibabu. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo, Novemba 19, 2025, Kamishna Msaidizi wa Polisi William Mwamafupa alisema kuwa MC Pilipili alifikishwa kituoni hapo akiwa katika hali mbaya na alifariki dunia majira ya saa 9:00 alasiri. Kwa mujibu wa taarifa za awali, kabla ya kifo chake, majira ya saa 8:00 mchana, msaidizi wake Hassan Ismail alipigiwa simu na mtu asiyefahamika na kuitwa mahali fulani kwa mazungumzo.  Baada ya muda, walitokea watu watatu ambao hawakufahamika wakimtumia MC Pilipili wakiwa ndani ya gari dogo jeupe na kumkabidhi kwa msaidizi wake kisha kuondoka kwa haraka. Wataalamu wa afya kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wamebaini kuwa marehemu alionyesha dalili za kushambuliwa sehemu mbalimba...

RAIS DKT.SAMIA AONGOZA KIKAO CHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI IKULU CHAMWINO

Picha
 RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza Kikao Kazi cha Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu kilichofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 19 Novemba, 2025.

CHAMA CHA MAPINDUZI KUWASHUGHULIKIA WATENDAJI WAZEMBE

Picha
Na Jasmine Shamwepu, Dodoma. CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimetangaza kuwa kitachukua hatua kali dhidi ya viongozi wote wazembe na wanaojihusisha na vitendo vya rushwa, kikisisitiza kwamba hakitavumilia kiongozi yeyote anayeshindwa kuwajibika kwa wananchi.  Akitoa kauli hiyo jijini Dodoma, Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenan Kihongosi, amesema chama kitaweka vipimo maalum vya kupima utendaji wa viongozi katika ngazi zote ili kuhakikisha uwajibikaji unazingatiwa kikamilifu. "Mawaziri na Manaibu Mawaziri walioteuliwa na Rais wanapaswa kwenda sambamba na kasi ya utendaji ya kiongozi wa nchi, akibainisha kuwa ingawa baadhi yao ni wapya na wanafurahia uteuzi, wanapaswa kufahamu kuwa Rais anataka kazi yenye matokeo kwa wananchi na hana mzaha katika masuala ya utumishi wa umma." Amesisitiza kuwa CCM haitasita kumchukulia hatua yoyote atakayekwenda kinyume na maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan. Aidha, Kihongosi amesema chama kipo bega kwa bega na ...

ADAKWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUJITEKA

Picha
Na Allan Kitwe, Tabora JESHI la Polisi Mkoani Tabora linamshikilia Hadija Jimmy Mrijo (39) mpare, kwa tuhuma za kutoa taarifa za uongo kuwa ametekwa na watu wasiojulikana ili ajipatie fedha isivyo halali kutoka kwa mume wake. Kamanda wa Polisi Mkoani hapa SACP Richard Abwao amethibitisha kushikiliwa mwanamke huyo ambaye ni mke wa Emanuel Peter Charles mkazi wa Tabora Mjini. Amesema kuwa mtuhumiwa alikamatwa baada ya kupata taarifa kutoka kwa mumewe kuwa alipigiwa simu na mtu asiyemfahamu akidai kuwa wamemteka hivyo awatumie fedha kiasi cha sh mil 2 ili wamwachie. Amedokeza kuwa mume wa mtuhumiwa baada ya kupokea taarifa hiyo na kusikia mlio wa kuteswa aliingiwa na hofu na kuanza kutafuta kiasi hicho cha fedha ambapo alifanikiwa kutuma kiasi cha sh 1,385,800/-. Kamanda Abwao amefafanua kuwa baada ya kufanya uchunguzi wa kina tumebaini kuwa mtuhumiwa hakuwa ametekwa ila alijiteka mwenyewe ili apate fedha hizo, akishirikiana na wenzake na wote wamekamatwa.  Ametaja watuhumiwa wengine ...

MATUKIO KATIKA PICHA

Picha
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji leo Novemba 18,2025 Ikulu jijini Dodoma.

WADAU WA UTALII NA UHIFADHI NYANDA ZA JUU KUSINI WAHAMASISHWA KUWANIA TUZO ZA SERENGETI

Picha
  Na Mwandishi Wetu - Iringa  WADAU wa uhifadhi na utalii  katika mikoa ya nyanda za juu kusini wamehamasishwa kushiriki katika tuzo za uhifadhi na utalii za Serengeti (Serengeti Awards 2025) zinazotarajiwa kufanyika mwezi Desemba 2025. Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Utalii, Bi. Dainess Kunzugala amesema hayo leo katika kikao na wadau hao wakiwemo makampuni na waendeshaji wa shughuli za utalii , waongoza watalii , watoa huduma za malazi , wahifadhi na mashirika au taasisi zenye mchango katika uhifadhi  kilichofanyika Novemba 17, 2025 Mkoani Iringa. "Natoa hamasa kwa wadau wetu wa utalii kutumia fursa hii muhimu kutuma maombi yao kuwania tuzo hizi muhimu ambapo kuna kategoria zipatazo saba ambazo zimeainisha makundi mbalimbali" amesema Bi. Kunzugala. Amesema lengo ni kutambua mchango wa wadau hao pamoja na kuifanya sekta ya utalii iwe na mwamko katika kuleta maendeleo nchini. Naye, Mwongoza Watalii kutoka kampuni ya Mukuta Travel and Tours, Bw.Fadhili Laizer ameishukur...

ZAIDI YA LESENI 700 ZATOLEWA KWA KIPINDI CHA MIAKA MITATU

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mahenge - Morogoro. KATIKA kipindi cha miaka mitatu kuanzia Mwaka 2022 hadi 2025 zimetolewa  leseni  714 katika Ofisi ya Afisa Madini Mkazi Mahenge zikijumuhisha leseni za  utafiti, uchimbaji na biashara ya madini kwa wadau mbalimbali wanajishughulisha na uwekezaji katika Sekta ya Madini. Hayo yalielezwa Novemba 12, 2025 na Afisa Madini Mkazi , Mkoa wa Kimadini Mahenge Jonas Mwano wakati akielezea kuhusu mafanikio yaliyopo. Mwano alisema kuwa, mafanikio hayo miaka mitatu yamepelekea kufikia lengo la ukusanyaji wa  maduhuli kwa asilimia 78.7 katika wilaya ya Ulanga, Malinyi na Kilombero. Aidha katika kipindi cha mwezi Julai mpaka Oktoba 2025 Ofisi imekusanya asilimia 61 ya lengo katika kipindi  husika. Akielezea kuhusu aina ya leseni zilitolewa Mwano alifafanua kuwa, katika kipindi husika kulitolewa aina mbalimbali za  leseni  kama leseni za utafiti 15, leseni kubwa ya uchimbaji 2, leseni ndogo ya uchimbaji 277, leseni kubwa ya...

JUKWAA LA NASSER LA KIMATAIFA LA SHEREHEKEA KISWAHILI KUTABULIWA RASMI NA UNESCO.

Picha
  Na Mwandishi Wetu. JUKWAA la Nasser la Kimataifa lisherehekea Kutambulishwa kwa Kiswahili Kama Lugha Rasmi ya UNESCO na Kuimarisha Umaarufu Wake Ulimwenguni. Jukwaa la Nasser limekumbushwa kwa sherehe katika taarifa yake kufuatia tangazo la Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) la kutambulisha Kiswahili rasmi kama mojawapo ya lugha za kazi katika mikutano mikubwa ya shirika hilo, wakati wa Kikao cha 43 cha Bunge Kuu kilichofanyika Samarkand – Uzbekistan kuanzia Oktoba 30 hadi Novemba 13, 2025. Uamuzi huu wa kihistoria ulitokana na ombi lililotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa ushirikiano na Baraza la Kiswahili BAKITA na BAKIZA, ambapo Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa na Mwakilishi wa Kudumu kwa UNESCO, Ali Jaberi Madini, alitoa hotuba ya nchi baada ya uamuzi huo kutambulishwa rasmi. Aidha, Jukwaa hilo limebainisha katika taarifa yake kwamba kwa mafanikio haya, Kiswahili ki...

TAARIFA KWA UMMA

Picha
 

ZAIDI YA WANANCHI 1,500 KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJIKO BANIFU WILAYANI BABATI

Picha
  Majiko banifu 1,582 kusambazwa na kuuzwa kwa bei ya ruzuku, Jiko moja kuuzwa kwa bei ya ruzuku ya TZS 11,200. Na Lubango Mleka, Babati. MKUU wa Wilaya ya wa Babati, Mheshimiwa Emmanuela Kaganda, leo Novemba 12, 2025 kwa niaba ya wakazi wa wilaya ya babati amezindua mradi wa uuzaji na usambazaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku.   Uzinduzi huu ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya mkuu wa mkoa wa Manyara, Mheshimiwa Queen Sendiga akiwataka wakuu wa wilaya wote wa mkoa wa manyara kuzindua na kusimamia kikamilifu utekelezaji wa mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku katika wilaya zao. Uzinduzi umefanyika katika kata ya Magugu wilayani babati, ambapo jumla ya majiko banifu  1,582 yatauzwa na kusambazwa kwa bei ya ruzuku ya TZS 11,200 ambayo ni sawa na aslimia 80 ya ruzuku ya TZS 56,000 ambayo ni bei ya awali ya jiko. Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mheshimiwa Kaganda amesema mpango huo umelenga kuhakikisha wananchi wote, hususani wa kipat...

BALOZI PINDI CHANA AKIPA KATIKA KATIKA KIKAO CHA PILI CHA BUNGE LA TANZANIA

Picha
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Njombe,Mhe. Balozi Dkt.Pindi Chana akiapa rasmi kuwa mbunge katika Mkutano wa Kwanza, Kikao cha Pili cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Novemba 12,2025.

MTINDO BORA WA MAISHA _ LISHE ASILIA.

Picha
  Maelezo ya Kikundi (Group Description): MTINDO BORA WA MAISHA LISHE ASILIA ni jukwaa la kidigitali lililoanzishwa na Mtaala Mr Roghat Falme Robert kwa ushirikiano na wataalamu wa Lishe, afya na kilimo na kwa sasa tunao mabalozi tunaowaandaa.  Kauli Mbiu “Nourish to Flourish Lisha Mwili, Kuza Maisha.” Lengo kuu ni kuhamasisha ulaji wa chakula bora, kuboresha usalama wa chakula majumbani, na kukuza tabia njema za lishe kwa watu binafsi na jamii. Tunalenga kuwawezesha watu kupata maarifa na zana zinazowawezesha kufanya maamuzi sahihi ya lishe ili kuishi maisha yenye afya na ustawi. Malengo (Objectives) Kuelimisha na kuhamasisha kuhusu ulaji bora wa chakula. Kuboresha usalama wa chakula majumbani kwa kutoa rasilimali na msaada. Kukuza tabia njema za lishe kwa watu binafsi na jamii. Kutoa jukwaa la fursa halisi za ajira katika sekta ya kilimo na afya. Kutoa nafasi za matangazo kwa biashara zinazohusiana. Dira (Vision) Dunia ambayo watu na jamii wanapata chakula chenye lishe, elim...

SENDIGA AZINDUA MRADI WA USAMBAZAJI NA UUZAJI WA MAJIKO BANIFU KWA BEI YA RUZUKU MANYARA.

Picha
 *Majiko banifu 7,914 kusambazwa na kuuzwa kwa bei ya ruzuku, Jiko moja kuuzwa kwa bei ya ruzuku ya TZS 11,200.  Na Mwandishi Wetu, Manyara. MKUU wa Mkoa wa Manyara, Mheshimiwa Queen Sendiga, leo Novemba 10, 2025 amezindua rasmi mradi wa uuzaji na usambazaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku mkoani Manyara. Uzinduzi huu ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa upatikanaji na uhamasisha wa matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia. Aidha,uzinduzi huu umefanyika katika Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Manyara iliyopo wilaya ya Babati, ambapo jumla ya majiko banifu  7,914 yatauzwa na kusambazwa kwa bei ya ruzuku ya kiasi cha  TZS 11,200 ambayo ni sawa na aslimia 80 ya ruzuku ya TZS 56,000 ambayo ni bei ya awali ya jiko. Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mheshimiwa Sendiga amesema mpango huo umelenga kuhakikisha wananchi wote, hususani wa kipato cha chini, wanapata fursa ya kutumia nishati safi na salama ya kupikia kwa gharama nafuu. Aidha, amewaagiza Wakuu wa Wilaya...