Machapisho

DIAMOND AMJIBU BABA LEVO NA MBOSSO.

Picha
STARA wa Bongo Fleva, @diamondplatnumz , ameweka wazi msimamo wake kupitia ujumbe aliouandika kwenye ukurasa wake wa Instagram akieleza kutofurahishwa na mwenendo wa rapa Baba Levo juu ya Msanii @mbosso_ Diamond amesema anamuheshimu Baba Levo kama kijana mwenzake, lakini vitendo vyake vinamfanya ahisi kuna agenda asiyoijua, jambo linalomlazimisha kukaa mbali naye. #Diamondplatinumz #WCB #Babalevo #Mwijaku #Mbosso 

AJALI YA BASI.

Picha
BASI LA KAMPUNI YA MBEYA CITY EXPRESS LIMEPATA AJALI LEO 17.08.2025 ENEO LA CHIMALA.

MWENGE WA UHURU WAZINDUA DARAJA LA KINYANG'ERERE MARA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Mara.  JUMLA ya shilingi Milioni 148.5 zimetumika Kujenga Daraja la kinyang'erere lililopo katika kijiji cha kinyang'erere halmashauri ya Musoma Mkoani Mara. Akisoma Taarifa ya ujenzi wa Mradi huo Kaimu Meneja wa TARURA Wilaya ya Musoma, Mhandisi Mohmed Etanga amesema daraja hilo limekamilika ujenzi wake kwa asilimia mia moja na kutoa huduma kwa Wananchi kama ilivyo kusudiwa. Mhandisi Etanga ameongeza kuwa daraja hilo ni kiungo muhimu kwa wakazi wa kijiji hicho kwaajili ya usafirishaji wa Mazao na kwenda kupata huduma za kijamii katika vijiji vingine ambapo kuna kituo cha Afya pamoja na wanafunzi kuvuka kwenda shule. Ameongeza kuwa kipindi cha Masika wakazi hao walikuwa wakipitia kadhia ya kushindwa kuvuka mto ambao unakuwa umejaa maji jambo lilikuwa likisababisha baadhi ya wajawazito kujifungulia njiani na kushindwa kuuza mazao yao kutokana na ubovu wa barabara . Naye Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa, Ndugu Ismail Ali Ussi ameipongeza TARURA kwa kufanya...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO TANZANIA.

Picha
TMA: Utabiri wa hali ya hewa Tanzania saa 24. 

DKT.MWINYI AONGOZA KIKAO CHA KAMATI MAALUM ZANZIBAR

Picha
MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar,  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali Mwinyi akiongoza Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa NEC,  kilichofanyika Afisi Kuu CCM Kisiwandui Zanzibar tarehe 17, Agosti 2025.

IDADI YA MAFUNDI WALIOOKOLEWA CHINI YA ARDHI MGODINI YAFIKIA SABA.

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Shinyanga.  Idadi ya mafundi waliookolewa baada ya kufunikwa na kifusi mgodini imefikia saba, baada ya Marko Ngelela (26), mkazi wa Sengerema na Machia Shabani (43) mkazi wa Ishokela mkoani Mwanza kuokolewa wakiwa tayari wamefariki dunia. Ajali hiyo ilitokea Agosti 11, 2025 katika mgodi wa Nyandolwa, wakati mafundi 25 walipokuwa wakifanya kazi ya ukarabati katika maduara matatu tofauti ambayo ni Na. 20, 103 na 106. Kwa mujibu wa taarifa za awali, ardhi ilititia ghafla na kusababisha kifusi kuporomoka, hali iliyowafunika baadhi ya mafundi waliokuwa kazini chini ya ardhi. Tangu tukio hilo kutokea, juhudi kubwa zimekuwa zikiendelea kutoka kwa timu ya uokoaji ya mgodi huo kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama, pamoja na wataalamu wa usalama wa migodini.  Hadi sasa, mafundi saba wamefanikiwa kutolewa chini ya kifusi, ambapo wanne kati yao waliokolewa wakiwa hai ambapo mmoja kati yao alifariki wakati akipatiwa matibabu katika Kituo cha Af...

MHANDISI SANGA AONGEZA MWEZI MMOJA KLINIKI YA ARDHI KIVULE KUONGEZA KASI YA UTOAJI HATI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.  Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga ameongeza mwezi mmoja kwa watumishi wanaotoa huduma za ardhi kwenye Kliniki ya Ardhi inayofanyika Kata ya Kivule Ilala Dar e salaam kuanzia Agosti 18, 2025 ili kupunguza mzingo mkubwa kwa wananchi ambao hawana hati. Mhandisi Sanga ametoa maekelezo hayo Agosti 16, 2025 jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Kivule ambao wanaendelea kupata huduma kwenye Kliniki hiyo.  “Tunatamani zoezi hili limalize changamoto zenu zote, kwa sababu tukimaliza changamoto zenu hapa hamtakuja ofisini, nawaagiza wasaidizi wangu, zoezi hili liendelee kwa muda wa mwezi mzima baada ya tarehe 18 Agosti 2025 ambayo ilipangwa ili kumaliza changamoto zenu za ardhi katika maeneo yenu” amesema Mhandisi Sanga. Ili kuleta tija katika zoezi hilo, Mhandisi Sanga ameelekeza watumishi 10 waongezwe katika kliniki hiyo ambao watatoka maeneo mbalimbali nchini ili kuongeza kasi y...

ASKARI WANAFUNZI 15 WAJERUHIWA KATIKA AJALI YA GARI.

Picha
Na Lubango Mleka, Moshi.  ASKARI Wanafunzi 15 wamejeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori la mizigo aina ya Fuso katika eneo la Kwasadala, wilayani Hai, mkoani Kilimanjaro. Mkuu wa Mkoa huo, Nurdin Babu amesema askari hao walikuwa wakitokea eneo la mazoezi ya medani za kivita la Kilele Pori, lililoko wilayani Siha, wakiwa kwenye gari aina ya Land Cruiser lililogongana uso kwa uso na Fuso. Majeruhi wa ajali hiyo iliyotokea leo Agosti 12, saa sita mchana wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya KCMC na Hospitali ya Wilaya ya Hai. 

TCRA YAENDELEA KUTOA ELIMU YA MATUMIZI SAHII NA SALAMA YA HUDUMA YA MAWASILIANO.

Picha
MENEJA wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Ofisi ya Zanzibar, Bi. Esuvatie-Aisa akitoa dondoo muhimu kwa watumiaji wa huduma za mawasiliano katika kipindi maalumu cha Kituo cha Crown FM Zanzibar tarehe 12 Agosti, 2025 Unguja - Zanzibar.  TCRA inaendelea kutoa elimu kwa umma ikisisitiza matumizi sahihi na salama ya huduma za mawasiliano na kukumbusha wajibu wa watumiaji wa kusambaza taarifa za ukweli na uhakika na kufuta na kutosambaza ujumbe au taarifa zinazochochea upotoshaji, uzushi, chuki na uvunjifu wa amani. #tcratz #elimukwaumma #futadeletekabisa

WACHIMBAJI WADOGO 25 KATIKA MGODI WA NYANDOLWA WAMEFUKIWA NA KIFUSI.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Shinyanga.  JUMLA ya wachimbaji wadogo 25 katika mgodi mdogo wa Nyandolwa uliopo kijiji cha Mwongozo Halmashauri ya Shinyanga, wamefukiwa na kifusi baada ya mgodi kutitia. Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kushirikiana na wachimbaji katika eneo hilo wamefanya juhudi za kuwaokoa wachimbaji hao na tayari wachimbaji wawili wameokolewa. Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Julius Mtatiro amesema kuwa wachimbaji hao walikuwa katika mashimo matatu tofauti, ikiwemo shimo la duara namba 106 lenye watu 6, 103 lenye watu 11, na duara namba 20 lenye watu 8. Juhudi za uokoaji bado zinaendelea. Tukio la kutitia kwa mgodi huo limetokea Agosti 11, 2025 saa nne asubuhi, wakati shughuli za matengenezo ya maduara hayo zikiendelea. Mtatiro amewasihi wachimbaji kuwa watulivu wakati jitihada za kuokoa uhai wa walioko chini zikiendelea.

VIWANGO VYA KUBADIRISHIA FEDHA ZA KIGENI HAPA NCHINI.

Picha

RAIS MWINYI:SERIKALI ITAENDELEA KUIMARISHA MASLAHI YA WALIMU.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar.  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewahakikishia walimu kuwa Serikali itaendelea kuimarisha maslahi na mazingira ya ufundishaji na kujifunza kwa dhamira ya kuboresha elimu zaidi.  Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 12 Agosti 2025, katika kongamano la kumpongeza lililoandaliwa na Shirikisho la Walimu Zanzibar kufuatia mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya elimu nchini katika kipindi cha uongozi wake. Hafla hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Dkt. Ali Mohamed Shein, Tunguu, Mkoa wa Kusini Unguja. Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amesema kuwa, katika kuongeza motisha kwa walimu, Serikali imeboresha maslahi yao kwa kuongeza mishahara, posho za likizo na ufiwa, pamoja na kulipa malimbikizo mengine. Halikadhalika, Rais Dkt.Mwinyi amesema Serikali  imeajiri walimu wapya 5,265 na kuwapatia mafunzo mbalimbali ili kuongeza ufanisi wao. Ameeleza kuwa kiasi cha shilingi bilioni 1.8 kimetumika katika mwaka wa ...

JESHI LA POLISI LATAKIWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA WADAU WA UCHAGUZI NCHINI.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Moshi.  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema ni muhimu Jeshi la Polisi kuimarisha ushirikiano wa karibu na wadau wote wa uchaguzi, hatua ambayo itasaidia kuhakikisha kila mdau anatendewa haki, na kuondoa tofauti zinazoweza kusababisha migongano.   Makamu wa Rais ametoa wito huo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi unaofanyika katika ukumbi wa Chuo Cha Polisi (CCP) Moshi Mkoani Kilimanjaro. Amesema Baadhi ya maeneo muhimu ya ushirikiano ni pamoja na kuhakikisha mikutano ya kampeni inafanyika kwenye maeneo yaliyoruhusiwa na ndani ya muda uliopangwa,  Kuzuia maandamano yasiyo na kibali, kuimarisha ulinzi wa wagombea na viongozi wa vyama vya kisiasa, bila kujali vyama vyao au itikadi zao pamoja na kudhibiti misongamano mikubwa ya watu ili kuhakikisha shughuli nyingine za kijamii na kiuchumi zinaendelea bila usumbufu.   Pia Makamu wa Rais amelitaka Jeshi la Polisi ku...

RAIS MWINYI ATEMBELEA ENEO LA OFISI ZA MJI WA SERIKALI NA LINALOJENGWA UWANJA MPYA WA AFCON

Picha
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar.  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameeleza kuwa Serikali inaendelea kusimamia utekelezaji wa mradi mkubwa wa uwanja wa AFCON pamoja na miundombinu mbalimbali inayojengwa Fumba, hivyo ni muhimu kubaini mapema maeneo yatakayotumika kwa mradi huo ili kuepusha mwingiliano wa matumizi ya ardhi katika eneo hilo kati ya taasisi husika. Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 11 Agosti 2025, katika kikao maalum na mawaziri mbalimbali akiwemo Mhe. Rahma Kassim Ali, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi, Mhe. Shariff Ali Shariff, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji, Mhe. Tabia Maulid Mwita, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mhe. Dkt. Khalid Salum Mohamed, Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, pamoja na Taasisi ya Ofisi ya Rais, Ufuatiliaji na Usimamizi wa Utendaji Serikalini (ZPDB), kwa lengo la kupata uelewa wa pamoja kuhusu matumizi sahihi ya ardhi katika maeneo ya uweke...