Machapisho

RAIS MWINYI:SMZ ITAENDELEA KUIMARISHA MIUNDOMBINU YA USAJILI KIDIJITALI.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar.  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema kuwa Serikali itaendelea kuimarisha miundombinu ya usajili kidijitali wa matukio ya kijamii kutokana na umuhimu wake kwa maendeleo ya nchi. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 10 Agosti,  2025 katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Usajili Barani Afrika yaliyofanyika katika Ukumbi wa Idrissa Abdulwakil, Kikwajuni, Mkoa wa Mjini Magharibi. Ameeleza kuwa hatua hiyo itaongeza ufanisi na utoaji wa huduma bora kwa wananchi unaofanywa na Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar (ZCSRA) katika usajili wa vizazi, vifo, talaka, ndoa na vitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi. Rais Dkt. Mwinyi amesema hakuna maendeleo ya kweli bila usajili wa utambulisho wa wananchi katika mifumo imara inayotambulika kisheria na inayotumia teknolojia ya kisasa ya kidijitali. Aidha, Dkt. Mwinyi ametoa rai kwa ZCSRA kuanzisha kampeni maalum kwa kushirikiana na masheha kuha...

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.

Picha

MWILI WA SPIKA MSTAAFU WA BUNGE LA TANZANIA NA ALIYEKUWA MBUNGE WA KWONGWA UMEWASILI VIWANJA VYA BUNGE.

Picha
MWILI wa hayati Spika Mstaafu wa Bunge na aliyekuwa Mbunge wa Kongwa  Mhe. Job Justino Ndugai, umeshawasili katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma kwa ajili ya viongozi wa kitaifa, familia, wabunge na wananchi kutoa heshima zao za mwisho na baada ya hapo mwili wa hayati Job Yustino Ndugai utaelekea nyumbani kwake Kongwa Jijini Dodoma.

UJENZI WA JENGO LA UBIA KATI YA NHC NA TOSH LOGISTICS KARIAKOO.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Kariakoo- Dar es Salaam.  SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC) kwa ubia na Tosh Logistics Ltd linaendelea na ujenzi wa jengo la kisasa la biashara na makazi katika eneo la Tandamti, Kariakoo – Dar es Salaam. Mradi huu unaojengwa kwenye viwanja sita (3/16 hadi 14/16) unalenga kubadilisha sura ya Kariakoo kwa kujenga majengo ya kisasa yenye matumizi mchanganyiko. Jengo limegawanywa katika Block A na Block B ambapo kazi zinasonga mbele kwa kasi, block A ipo hatua ya ujenzi wa ghorofa ya pili, block B imefikia ghorofa ya sita. Mradi huu unatekelezwa kuanzia Oktoba 15, 2024 hadi Oktoba 15, 2026, ni sehemu ya jitihada za NHC kukuza miundombinu ya kisasa na kuchochea uwekezaji kwenye maeneo ya mijini kupitia ubia wa kimkakati na sekta binafsi. #NHCProjects #ToshLogistics #MajengoYaKisasa #KariakooMpya #UjenziEndelelevu #PublicPrivatePartnership #MaishaNiNyumba#CrownMedia #Ayotv

MATUKIO KATIKA PICHA.

Picha
MGOMBE wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya ACT Wazalendo Ndugu Luhaga Mpina, Mgombea Mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Fatma Ferej na Mgombea wa Urais wa Zanzibar Ndugu Othman Masoud Othman wamepokelewa na maelfu ya wanachama wa ACT Wazalendo na wananchi wa Zanzibar kwa ajili ya kujitambulisha upande wa Unguja leo tarehe 9 Agosti 2025. Oktoba #LindaKura #MuhuniHasusiwi @ACTwazalendo

RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA URAIS.

Picha
Dodoma. RAIS DKT. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 09.08.2025  akiwa na Mgombea Mwenza DKT. Balozi Emmanuel Nchimbi wamefika katika Ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya Urais na Makamu wa Rais kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu Octoba 2025.

IGUNGA YAIBUKA MSHINDI WA KWANZA NANENANE TABORA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Tabora.  HALMASHAURI ya Wilaya ya Igunga imeibuka mshindi wa kwanza katika kundi la Mamlaka za Serikali za Mitaa (Tabora na Kigoma) wakati wa Maonesho ya Nanenane mwaka 2025 ngazi ya kanda yaliyofanyika Uwanja wa Maonesho Ipuli - Tabora. Aidha, imeshika nafasi ya pili katika kundi la washindi wa jumla wa mikoa ya Tabora na Kigoma wakati wa Maonesho hayo. Akizungumza baada ya Halfa hiyo, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Ndug. Elizabeth Rwegasira amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Selwa Hamid kwa ushirikiano mzuri na Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Grace Nyamwanji kwa kufanikisha ushindi huo. Kwa upande wa Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Halamshauri hiyo, Grace Nyamwanji amewashukuru na kuwapongeza, Wakuu wa Idara na Vitengo, Watumishi na  Wadau wote waliyoshiriki maonesho hayo kwa sababu wao ndio chachu ya ushindi huo.

RATIBA YA UCHAGUZI MKUU 2025

Picha
 

KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAKULIMA NANE NANE

Picha
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Nzega (NZUWASA) inakutakia Heri ya Sikukuu ya Wakulima (Nane Nane). 

MUUGUZI BANDIA AKAMATWA BAADA YA KUHUDUMIA WAGONJWA ZAIDI YA 4,000 FLORIDA.

Picha
MWANAMKE mmoja amekamatwa nchini Marekani kwa tuhuma za kujifanya muuguzi aliyesajiliwa. Uchunguzi wa polisi ulianzishwa baada ya wakuu wa hospitali kukatisha kandarasi ya Autumn Bardisa kutokana na wasiwasi kuhusu sifa zake za kikazi. Wachunguzi waligundua kuwa mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 29 alikuwa ametoa huduma za matibabu kwa wagonjwa 4,486 kati ya Juni 2024 na Januari 2025. "Hii ni moja ya kesi za kutatanisha zaidi za udanganyifu wa kimatibabu ambazo tumewahi kuchunguza," Mkuu wa Kaunti ya Flagler Rick Staly alisema. Bardisa aliajiriwa na AdventHealth Palm Coast Parkway huko Palm Coast kuanzia Julai 2023 hadi Januari 2025. Anadaiwa kuwasilisha hati za uwongo na kutoa nambari ya leseni ya muuguzi aliye na jina moja la kwanza ambaye aliajiriwa na AdventHealth katika hospitali tofauti. Ofisi ya Kaunti ilisema alielezea tofauti hiyo kwa kudai kwamba alikuwa ameolewa hivi majuzi na amebadilisha jina lake la ukoo. Aliombwa kutoa leseni yake ya ndoa lakini hakufanya hivy...

TRUMP KUKUTANA NA PUTIN

Picha
RAIS Donald Trump wa Marekani amedokeza kuwa atakutana na na rais wa Urusi Vladimir Putin ana kwa ana hivi karibuni ili kujadili usitishwaji wa vita vinavyoendelea nchini Ukraine. Trump amesema mkutano wake na Putin ni matokeo ya mazungumzo yenye tija kubwa yaliyofanyika mjini Moscow kati ya mjumbe wake maalum Steve Witkoff na Rais Putin. Urusi tayari imethibitisha kuhusu mkutano huo huku Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky nae akitoa wito wa kukutana ana kwa ana na Putin ili kuzungumza namna ya kuvimaliza vita hivyo vilivyodumu kwa zaidi ya miaka mitatu.  #USA #Trump #Russia 

DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AKUTANA NA WANA MICHEZO ZANZIBAR.

Picha
KUMBUKUMBU KATIKA MICHEZO..  ZANZIBAR :- Kabla ya kuanza ujenzi wa viwanja vya michezo na maeneo rasmi ya mazoezi, Mgombea Urais wa CCM Zanzibar mwaka 2020, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, alikutana na wanamichezo katika maeneo mbalimbali ya Unguja na Pemba kwa lengo la kusikiliza changamoto sugu walizokuwa wakikabiliana nazo na kufahamu mazingira halisi ya michezo Zanzibar. Kipindi cha kampeni za Urais za mwaka 2020, Dkt. Hussein Ali Mwinyi hakutilia mkazo hotuba ndefu majukwaani, bali aliamua kushuka mitaani, kukutana na wanamichezo, makocha na mashabiki. Aliahidi si tu kuboresha mazingira ya michezo, bali pia kuwezesha ndoto za wanamichezo wa Zanzibar kutimia. Picha hii ni ushahidi wa Uongozi Unaoacha Alama. Kwa bashasha na ukaribu, Dkt. Hussein Ali Mwinyi alikutana na wadau mbalimbali wa michezo, akashiriki nao mchezo wa mpira wa mikono, na hatimaye kuwaahidi kuwa siku za matumaini kwa maendeleo ya sekta ya michezo Zanzibar zinakuja.

MICHEZO

Picha
 

SALAMU ZA POLE

Picha
#HabarikamiliTvupdate #SMZ 

BREAKING NEWS

Picha
ALIYEWAHI kuwa Spika wa Bunge la Tanzania na Mbunge wa Kongwa, Job Yustino Ndugai amefariki Dunia leo August 06,2025 akiwa anaendelea kupatiwa matibabu Hospitalini baada ya kuugua ghafla. Ndugai amekuwa Spika wa Bunge tangu November 17,  2015 hadi Januari 06, 2022 alipojiuzulu na kuendelea kuwa Mbunge wa Kongwa  nafasi ambayo ameendelea kuitetea kwa kuchukua fomu tena mwaka huu ambapo ameshinda kwenye kura za maoni. Ndugai ambaye amezaliwa January 22,1960 alishinda kura za maoni za Ubunge wa Jimbo la Kongwa kwa kupata kura 5690.

NAIBU WAZIRI SANGU AONGOZA KURA ZA MAONI JIMBO LA KWELA

Picha
  Na. Mwandishi Wetu- Sumbawanga ALIYEKUWA Mbunge wa Kwela mkoani Rukwa, Mhe.Deus Sangu ambaye pia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na  Utawala Bora ameongoza kura za maoni jimboni humo na kuwaacha mbali wapinzani wake wanne  katika mchakato huo. Matokeo yaliyotangazwa mapema leo  Jumanne  Agosti 6, 2025 Mhe.Sangu  amepata kura 9,957,  dhidi ya Justin Hiari aliyepata kura 2,973,  Derick Sikale kapata 507,  Walter Simsokwe kapata 112  na Yuster Bahati  kaambulia kura  102 Taarifa za matokeo hayo zinaeleza kuwa jumla ya Wajumbe 13,496 walipiga  kura   ambapo kura halali zilikuwa 13,278 na kura 218  ziliharibika.

NDIYO MATOKEO MAJIMBO YA IGUNGA

Picha
 

MHE. DOTTO BITEKO ASHINDA KWA ASILIMIA 99.8

Picha
IDADI YA WAPIGA KURA JIMBO LA BUKOMBE - GEITA NI 7,845.  = Wajumbe waliohudhuria 7456.  = Wajumbe wasiohudhuria 389.  Idadi ya kura zilizopigwa 7456.  = Idadi ya kura zilizoharibika 15.  = Idadi ya kura halali 7441.  ✅ KURA ZA NDIO 7441.  = KURA ZA HAPANA 00.  *WASTANI WA WAPIGA KURA WALIOJITOKEZA NI ASILIMIA 95.04.  *WASTANI WA USHINDI NI ASILIMIA 99.8. @BUKOMBE @BITEKO @CCMTAIFA

WASIMAMIZI WASAIDIZI NGAZI YA KATA JIMBO LA MANONGA NA IGUNGA WATAKIWA KUENDELEZA UTENDAJI WAO KIUADILIFU. MSIMAMIZI wa

Picha
Na Mwandishi Wetu, Igunga.  MSIMAMIZI wa Uchaguzi Jimbo la Igunga na Manonga wilayani Igunga mkoani Tabora, Hamisi Hamisi amewaasa Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya kata kuendeleza utendaji wao wa kiuadilifu, uaminifu, uzalendo, uchapakazi na uaminifu. Hamisi ametoa rai hiyo wakati wa mafunzo kwa Wasimamizi hao yaliyofanyika katika ukumbi wa Maxweli mjini Igunga. “Nyinyi mliopo hapa mmeteuliwa kwa mujibu wa sheria, hivyo mnaowajibu wa kikatiba na sheria kusimamia na kuratibu uendeshaji wa uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani katika maeneo yenu’’ amesisitiza. Aidha, amewakumbusha wamebeba dhamana kubwa, nyeti na muhimu kwa mustakabali wa Tanzania Bara, hivyo wanategemewa kuzingatia utendaji wao na kuwajibika ipasavyo kipindi chote cha utumishi wao katika Tume Huru ya Uchaguzi.