Machapisho

MANISPAA TABORA YATOA MOTISHA KWA WALIMU

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora.  HALMASHAURI ya manispaa Tabora imetoa motisha kwa walimu na shule za sekondari zilizofanya vizuri zaidi katika masomo mbalimbali kwenye mitihani ya taifa ya kidato cha 4, 6na ule wa kujipima wa kidato cha 2 kwa mwaka 2025. Akitoa taarifa kwenye kikao cha baraza la madiwani, Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Dkt John Pima, ameeleza kuwa wametoa motisha hiyo ili kuwatia moyo walimu na shule zao ili waendelee kufanya vizuri zaidi. Amefafanua kuwa kwa mwaka wa masomo 2025 halmashauri ya manispaa hiyo ilishika nafasi ya kwanza Kimkoa kati ya halmashauri 8 katika mitihani ya taifa ya kidato cha 6, 4 na upimaji wa kidato cha 2. Pima ameongeza kuwa kwa ujumla shule zote katika manispaa hiyo zilifanya vizuri katika mitihani hiyo ikilinganishwa na mwaka uliopita sababu kuu ikitajwa kuwa ni juhudi na weledi wa walimu katika kufundisha watoto hao. Amedokeza kuwa katika mitihani ya kidato cha 4 walimu wa shule za sekondari za kata ambao masomo yao yalipata ...

REA KUIMARISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KUPITIA MAJIKO BANIFU MKOANI MWANZA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mwanza. WAKALA wa Nishati Vijijini (REA) umemtambulisha rasmi mtoa huduma, kampuni ya Envotec Services Limited, kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mheshimiwa Said Mtanda, kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku kwa wananchi wa mkoa huo. Utambulisho huo ni sehemu ya juhudi za Serikali kupitia REA za kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini, kwa lengo la kuboresha afya za wananchi, kupunguza matumizi ya nishati zisizo rafiki kwa mazingira pamoja na kuhifadhi mazingira. Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Mtanda, ameipongeza REA kwa kuendelea kutekeleza na kusimamia miradi mbalimbali ya nishati yenye manufaa kwa wananchi, ikiwemo mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku. Amesema mradi huo ni muhimu kwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza kwani utasaidia kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia, kupunguza matumizi makubwa ya kuni na mkaa pamoja na kusaid...

KONGAMANO LA UPANDIKIZAJI VIUNGO VYA BINADAMU KUFANYIKA DODOMA.

Picha
Na Ahmed Ahmed - Dodoma.  KONGAMANO la Kimataifa la Kisayansi la Wataalamu wa Upandikizaji Viungo linatarajiwa kufanyika jijini Dodoma. Akizungumza hivi karibuni jijini Dodoma, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Prof. Abel Makubi amesema madaktari bingwa wa upandikizaji wa viungo vya binadamu zaidi ya 150 kutoka nchi mbalimbali duniani wanatarajiwa kushiriki. "Madaktari hao watatoka katika nchi za Italia, Uingereza, Japani, Afrika Kusini, na Tanzania, lengo la kongamano hilo litakalofanyika kwenye ukumbi wa Domiya ni kuiimarisha Tanzania kwenye ramani ya upandikizaji viungo," alisema. Upandikizaji viungo ni moja ya mafanikio makubwa ya tiba ya kisasa ndani ya taaluma ya Upasuaji wa Kisasa na Immunolojia.  Hata hivyo, utekelezaji wake hutofautiana sana kati ya nchi kutokana na sheria, tamaduni, miundombinu ya afya, na uelewa wa jamii.

RC TABORA APEWA TUZO MAALUMU

Picha
Na Allan Kitwe, Tabora CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoani Tabora kimetoa tuzo maalumu kwa Mkuu wa Mkoa huo Paul Matiko Chacha kama ishara ya kutambua na kuthamini mchango wake katika suala zima la kusimamia maendeleo ya Mkoa huo. Tuzo hiyo imetolewa juzi kwenye Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM ngazi ya  Mkoa baada ya Wajumbe wa mkutano huo kuridhishwa na kazi nzuri inayofanywa na Kiongozi huyo hivyo kupendekeza apewa tuzo katika kikao hicho. Awali, akielezea tuzo hiyo, Katibu wa CCM Mkoa Wilson Nkambaku amesema kuwa pendekezo la kutoa tuzo hiyo lilitolewa na Wajumbe katika Kikao kilichopita, hivyo chama kimelifanyia kazi na sasa wapo tayari kumkabidhi. Ameongeza kuwa chama pia kitatoa tuzo kwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa Mheshimiwa Said Juma Nkumba kama ishara ya kutambua kazi yake njema ya kuimarisha, kudumisha na kujenga mshikamano thabiti ndani ya chama. Akikabidhi tuzo kwa Mkuu wa Mkoa, Mwenyekiti wa CCM Mkoa, Said Juma Nkumba amesema kuwa Chama kimeridhishwa na kazi yake, anatekeleza...

REA YAMTAMBULISHA MTOA HUDUMA WA MAJIKO BANIFU KAGERA.

Picha
Wananchi Kunufaika na Ruzuku ya Asilimia 80. Na Mwandishi Wetu, Bukoba-Kagera WAKALA wa Nishati Vijijini (REA) umemtambulisha rasmi mtoa huduma, kampuni ya Burn Manufacturing Company Limited, kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali Yahaya Ramadhani Kido, ikiwa ni hatua muhimu katika utekelezaji wa mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku kwa wananchi wa mkoa huo. Utambulisho huo umefanyika katika kikao kilichowakutanisha viongozi wa mkoa pamoja na wataalamu kutoka REA, ambapo ilielezwa kuwa kampuni hiyo itahusika moja kwa moja na usambazaji wa majiko hayo pamoja na kuhakikisha yanawafikia wananchi kwa bei nafuu kupitia utaratibu wa ruzuku uliowekwa na Serikali.  Mradi huo unalenga kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia na kupunguza utegemezi wa kuni na mkaa, ambavyo vimekuwa na athari kubwa kwa afya za wananchi na mazingira. Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali Yahaya Ramadhani Kido, ameipongeza REA kwa kuendelea kuibua na kusimamia...

SERIKALI YATAKA MATUMIZI SAHIHI YA MITANDAO KUJENGA JAMII NA KULINDA KISWAHILI

Picha
  Na Jasmine Shamwepu, Dodoma.  WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda, Amezindua ofisi mpya za Jumuiya ya Wanahabari ya Mitandao ya kijamii Tanzania (JUMIKITA),Tawi la Dodoma aidha ameitaka JUMIKITA kutumia mitandao ya kijamii kujenga jamii yenye maadili na kuendelea kulinda utamaduni wa Kitanzania kupitia matumizi sahihi ya Kiswahili. Ameyasema hayo Mei 3, 2026 jijini Dodoma wakati akizindua ofisi za JUMIKITA Tawi la Dodoma katika eneo la Ilazo. Aidha, amebainisha kuwa Kiswahili ni sehemu ya utambulisho wa taifa na Afrika kwa ujumla, huku akibainisha kuwa Tanzania kupitia UNESCO imeendelea kupewa heshima kubwa katika kukuza lugha hiyo duniani. Ameeleza kuwa mwaka huu Tanzania inatarajia kushiriki maadhimisho ya Kiswahili duniani yatakayofanyika mjini Paris, Ufaransa.  Aidha, Makonda amebainisha kuwa mitandao ya kijamii inapaswa kutumika kuelimisha na kujenga jamii badala ya kusambaza maudhui yanayoharibu maadili ya taifa. Amesema kuwa wanamitan...

WAFANYABIASHARA SOKO LA REHEMA NCHIMBI WALALAMIKIA KUKWAMA KUFANYA BIASHARA DODOMA

Picha
Na Hamida Ramadhan, Dodoma.  WAFANYABISHARA zaidi ya 300 wa Soko la Rehema Nchimbi jijini Dodoma, waliohamishwa baada ya eneo hilo kuchukuliwa na Bunge Oktoba mwaka jana, wameuomba uongozi wa Jiji la Dodoma kuondoa zuio la kuendesha biashara katika eneo mbadala la Umoga walilopewa na Waziri Mkuu. Wakizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti katika eneo la Umonga, baadhi ya wafanyabiashara hao wamesema ni zaidi ya miezi saba sasa hawajafanya biashara yoyote, hali inayochangia ugumu wa maisha yao. Prisca Chibwaye, mmoja wa wafanyabiashara hao, amesema tangu walipoondolewa kwenye eneo lao la awali wamekuwa wakifuatilia kupata eneo mbadala bila mafanikio. “Mwaka jana tuliondolewa kwenye vibanda vyetu vya biashara bila kupewa taarifa wala fidia baada ya Bunge kuchukua eneo lile lakini tunashukuru serikali kupitia mkuu wa mkoa alisimamia tukaletwa katika eneo hili la Umonga lakini jiji hawataki tufanye biashara hapa,” amesema. Ameongeza kuwa Waziri Mkuu Dk. Mwigulu Nchemba ali...

RC TABORA APIGA MARUFUKU OMBAOMBA

Picha
Na Allan Ntana, Tabora.  SERIKALI Mkoani Tabora imesema kuwa omba omba walio wengi wakiwemo wale wanaosukumwa kwenye vibaiskeli wana uwezo wa kufanya kazi zinazoweza kuwaingizia kipato na sio kukaa au kujipitisha mitaani wakiomba. Akihutubia Watumishi wa Umma na wa Sekta Binafsi kwenye Maadhimisho ya Mei Mosi yaliyofanyika Kimkoa Wilayani Kaliua Mkoani hapa jana, Mkuu wa Mkoa huo Paul Chacha amepiga marufuku ombaomba wanaojipitisha au kukaa mitaani. Ameeleza kuwa serikali ilianzisha Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ili kusaidia kaya zote zisizo na uwezo, hivyo omba omba wote wanapaswa kutambuliwa na kuingizwa katika mfuko huo na sio kuomba omba mitaani. ‘Wengi wao ni watu wazima ambao wana uwezo wa kufanya kazi na hata wale wanaowasukuma kwenye vibaiskeli hawana shida yoyote, hawa hawapaswi kuwa omba omba, wanapaswa kuwepo kwenye mfuko huo’, ameeleza. Chacha amesisitiza kuwa serikali iliweka utaratibu wa kusaidia wale wote wasio na uwezo (kaya maskini) kupitia mfuko huo wa maend...

RUJAT YATAKA MABADILIKO YA UANDISHI, YAANGAZA ZAIDI VIJIJINI

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Arusha MWENYEKITI  wa Chama cha Waandishi wa Habari za Vijijini Tanzania (RUJAT), Neville Meena, amesema kuwa ni muhimu kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari huku ikiwekewa mkazo sauti ya wananchi wa vijijini ili kuhakikisha hakuna kundi linaloachwa nyuma katika upatikanaji wa taarifa. Akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika jijini Arusha, Meena amesema uhuru wa vyombo vya habari unapaswa kuambatana na uwajibikaji wa kitaaluma kwa wanahabari kuzingatia misingi ya ukweli, usahihi, uwiano na maslahi ya umma. Maadhimisho hayo yaliyowakutanisha wadau wa sekta ya habari kwa siku mbili katika Hoteli ya Mount Meru, yalijadili mustakabali wa tasnia ya habari katika muktadha wa mabadiliko ya kidijitali, yakilenga pia kukuza ubunifu na kuhakikisha uendelevu wa taaluma ya uandishi wa habari. Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa RUJAT, Prosper Kwigize, amesema chama hicho kimejipanga kushirikiana na taasisi mbalimb...

WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUJITEGEMEA KIUCHUMI KUEPUKA USHAWISHI

Picha
  Na Hamida Ramadhan,Arusha.  WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amewataka waandishi wa habari nchini kujenga uwezo wa kujitegemea kiuchumi ili kuepuka kushawishiwa na wanasiasa wasio waadilifu pamoja na wala rushwa. Akizungumza jijini Arusha wakati wa kufunga maadhimisho kuelekea Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, Makonda alisema uhuru wa habari hauwezi kuwa kamili bila uhuru wa kiuchumi kwa wanahabari. Alisema baadhi ya waandishi wamekuwa wakiandika habari kwa maslahi ya wanasiasa, hali ambayo ni hatari kwa mustakabali wa taaluma ya habari na inaweza kupotosha jamii. “Ni muhimu kwa mwandishi wa habari kuwa na uhuru wa kiuchumi ili aweze kufanya kazi yake bila hofu, upendeleo au shinikizo kutoka kwa watu wenye maslahi binafsi,” amesema Makonda. Ameongeza kuwa kuna watu wasiokuwa waaminifu wanaowashawishi waandishi kwa maslahi yao, na kusisitiza umuhimu wa wanahabari kuzingatia maadili ya taaluma yao pamoja na kuandika habari zinazojenga taif...

TAMASHA LA KILIMO LAHITIMISHWA MBEYA

Picha
REA Yapongezwa uhamasishaji matumizi ya nishati safi ya kupikia, Umeme sasa ni kitongoji kwa kitongoji.  Na Mwandishi Wetu, Iwambi - Mbeya.  TAMASHA  la Kilimo lililofanyika mkoani Mbeya limehitimishwa rasmi leo Jumatano, tarehe 29 Aprili 2026, kwa mafanikio makubwa huku likiwa limekusanya wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo, nishati na maendeleo kutoka ndani na nje ya mkoa huo.  Tamasha hilo limekuwa jukwaa muhimu la kubadilishana uzoefu, kuonesha teknolojia mpya na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu njia bora za kuboresha maisha yao kupitia kilimo na matumizi sahihi ya nishati. Akizungumza wakati wa hafla ya kufunga tamasha hilo,mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Rungwe Mhe. Jaffar Haniu ameipongeza REA kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuhakikisha wananchi wanapata elimu ya matumizi ya nishati safi, akisisitiza kuwa hatua hiyo ina mchango mkubwa katika kuboresha afya za wananchi na kulinda mazingira.  Alieleza kuwa matumizi ya nishati safi kama majiko ya umeme, majiko y...