MANISPAA TABORA YATOA MOTISHA KWA WALIMU
Na Allan Kitwe, Tabora. HALMASHAURI ya manispaa Tabora imetoa motisha kwa walimu na shule za sekondari zilizofanya vizuri zaidi katika masomo mbalimbali kwenye mitihani ya taifa ya kidato cha 4, 6na ule wa kujipima wa kidato cha 2 kwa mwaka 2025. Akitoa taarifa kwenye kikao cha baraza la madiwani, Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Dkt John Pima, ameeleza kuwa wametoa motisha hiyo ili kuwatia moyo walimu na shule zao ili waendelee kufanya vizuri zaidi. Amefafanua kuwa kwa mwaka wa masomo 2025 halmashauri ya manispaa hiyo ilishika nafasi ya kwanza Kimkoa kati ya halmashauri 8 katika mitihani ya taifa ya kidato cha 6, 4 na upimaji wa kidato cha 2. Pima ameongeza kuwa kwa ujumla shule zote katika manispaa hiyo zilifanya vizuri katika mitihani hiyo ikilinganishwa na mwaka uliopita sababu kuu ikitajwa kuwa ni juhudi na weledi wa walimu katika kufundisha watoto hao. Amedokeza kuwa katika mitihani ya kidato cha 4 walimu wa shule za sekondari za kata ambao masomo yao yalipata ...