Machapisho

MSTAHIKI MEYA WA JIJI LA MWANZA ACHAGULIWA KUWA MWENYEKITI WA ALAT TAIFA

Picha
  Na Mwandishi Wetu.  MSTAHIKI Meya wa Jiji la Mwanza amepata ushindi mkubwa katika uchaguzi wa Mwenyekiti wa Association of Local Authorities of Tanzania (ALAT) Taifa, baada ya kujizolea jumla ya kura 273 kati ya kura 339 zilizopigwa. Katika uchaguzi huo uliokuwa na ushindani mkali, jumla ya wagombea wanne walijitokeza kuwania nafasi hiyo muhimu ya uongozi wa mamlaka za serikali za mitaa nchini.  Hata hivyo, Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza aliibuka mshindi kwa kupata kura nyingi zaidi, akionesha imani kubwa waliyonayo wajumbe wa ALAT Taifa kwake. Ushindi huo unaashiria heshima na imani kwa uongozi wa Jiji la Mwanza katika kusimamia na kuendeleza masuala ya maendeleo ya serikali za mitaa nchini.  Aidha, ni hatua muhimu katika kuimarisha ushirikiano kati ya halmashauri mbalimbali na kuendeleza ajenda za maendeleo kwa wananchi. Kupitia nafasi hiyo mpya, Mstahiki Meya anatarajiwa kusimamia na kuratibu shughuli za ALAT Taifa, ikiwa ni pamoja na kutetea maslahi ya mamlaka...

HAWA MWAIFUNGA AAHIDI TABASAMU KWA WAKAZI MANISPAA TABORA

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora.  MBUNGE wa Jimbo la Tabora Mjini Hawa Subira Mwaifunga amefanya mkutano mkubwa wa hadhara Jimboni humo na kupokea kero za wananchi huku akiahidi kuwapa tabasamu kwa mazuri yatakayofanyika. Ametoa kauli hiyo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika juzi katika uwanja wa TBC ulio karibu na Ofisi za CCM Tabora Mjini ambapo alitumia nafasi hiyo kuwashukuru wananchi na wana CCM wote kwa kumchagua kuwa mbunge wao. Mwaifunga amesema kuwa kuanzia sasa ataanza utaratibu wa kupita mtaa kwa mtaa, kata kwa kata ili kupokea mawazo ya nini wananchi wanataka, kusikiliza kero zao na kuzitafutia ufumbuzi wa haraka na wa kudumu. Amefafanua kuwa mbunge ni mtumishi wa wananchi, hivyo ana wajibu wa kutembelea, kusikiliza na kutatua kero na shida za wananchi wake kwa kuwa ndio waliompeleka bungeni. ‘Mbunge na diwani wanawajibika moja kwa moja kwa waliowachagua, kwa kuhakikisha wanajua kero zao na kuzitafutia ufumbuzi, kazi yetu ni kuwapa tabasamu wananchi na si vinginevyo,’ a...

MALIASILI NA UTALII WATATHMINI UTENDAJI WA ROBO TATU MWAKA DODOMA.

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  WATAALAMU wa Ufuatiliaji na Tathimini wa Wizara ya Maliasili na Utalii na taasisi zake wamekutana katika Kikao kazi cha Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini kwa ajili ya Maandalizi ya Taarifa ya Ufuatiliaji na Utendaji Kazi wa Wizara kwa Kipindi cha Robo Tatu Mwaka (Julai, 2025 hadi Machi, 2026) katika Ukumbi wa TANAPA jijini Dodoma. Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Wizara ya Maliasili na Utalii, Bi. Bure Nassibu amesema kuwa lengo la kikao hicho ni Kujadili na Kuandaa Taarifa ya Ufuatiliaji wa Utendaji Kazi wa Wizara kwa kipindi cha Robo Tatu (Julai, 2025 – Machi, 2026) kwa kuzingatia viwango vya ubora na ushahidi wa utekelezaji. Bi Bure aliongeza kuwa kikao hicho kinaongozwa na Kaulimbiu ya Kuimarisha Ufuatiliaji na Tathmini kwa Matokeo Endelevu ya Utekelezaji wa Sera, Mipango na Miradi ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026. Aidha, Wataalamu hao watafanya mapitio ya utekelezaji wa shughuli za Wizara ikiwemo kupima hatua iliyofik...

NYANSAHO FOUNDATION YAZIDI KUHAMASISHA MAENDELEO BILLION 1.4 ZAKUSANYWA KWENYE HARAMBEE KIJIJI CHA MUSATI WILAYANI SERENGETI.

Picha
Na Jovina Massano, Serengeti.  KATIKA kuhakikisha jamii inapata huduma muhimu karibu na maeneo yao Nyansaho Foundation na wadau mbalimbali  wachangia Shillingi Billioni 1.4 zitakazowezesha upatikanaji wa huduma za afya na elimu Kijiji cha Musati. Harambee hiyo imefanyika hivi karibuni katika Kijiji cha Musati wilayani Serengeti mkoani Mara ambapo ilitanguliwa na uzinduzi wa kanisa la Waadventista wa Sabato- Musati Central na nyumba ya mchungaji ambavyo vyote kwa pamoja vimejengwa kwa ufadhili wa taasisi ya Nyansaho  kwa kiasi cha millioni 500. Akiongoza harambee hiyo Waziri wa Ujenzi ,Mh.Abdalah Ulega(MB) ameweza kukusanya jumla ya Shillingi Billioni 1.4 zitakazowezesha kujenga Shule pamoja na Zahanati katika Kijiji hicho. Katika harambee hiyo Waziri Ulega na rafiki zake wamechangia shillingi millioni 100 na kuongoza uchangiaji kutoka kwa wadau mbalimbali wa Maendeleo (wafanyabiashara) zikiwemo taasisi za fedha, wageni waalikwa na wananchi na kuweza kufikisha kiasi hicho ...

TABASAMU LA MATUMAINI: WANAFUNZI 16 KIFUBATA WAPATA NGUVU MPYA YA KUSOMA.

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Igunga.  KUNA nyakati ambapo msaada mdogo hugeuka kuwa mwanga mkubwa wa matumaini. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa wanafunzi 16 wanaoishi katika mazingira magumu wa Shule ya Sekondari Kifubata, Kata ya Nkinga, Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, baada ya kupokea msaada wa vifaa vya shule uliolenga kubadili simulizi ya changamoto zao za kila siku. Msaada huo umejumuisha mahitaji muhimu kama madaftari, kalamu, mabegi ya shule, masweta na sare, vitu ambavyo kwa wengi vinaweza kuonekana vya kawaida, lakini kwa wanafunzi hawa ni daraja muhimu kuelekea ndoto zao za kielimu. Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Mkurugenzi wa taasisi ya Nkinga and Save Care Organisation, Edina Kalibate, alisisitiza umuhimu wa mshikamano wa jamii katika kusaidia makundi yenye uhitaji. "Mbunge wetu amekuwa akishirikiana kwa karibu na taasisi yetu kuwafikia watoto wenye mahitaji maalum pamoja na jamii inayowazunguka. Ushirikiano wa kila mmoja ni muhimu ili kuleta mabadiliko ya kweli,...

LISHE BORA SHULENI YATAJWA KUWA MSINGI WA MAFANIKIO YA ELIMU

Picha
  Na Jasmine Shamwepu, Dodoma KAMISHINA wa Elimu Tanzania, Dk Lyabwene Mtahabwa, amesema mchakato wa ufundishaji na ujifunzaji hauwezi kufanikiwa bila kuwepo kwa huduma bora za chakula na lishe shuleni. Amesisitiza kuwa wadhibiti ubora katika halmashauri zote wanapaswa kuhakikisha chakula kinachotolewa kwa wanafunzi kinazingatia viwango vya ubora ili kuepusha madhara ya kiafya ikiwemo viriba tumbo. Dk Mtahabwa alitoa kauli hiyo jijini Dodoma wakati wa uzinduzi wa mradi wa CRISP unaotekelezwa na SwissAid kwa miaka mitatu katika mikoa ya Lindi, Mtwara na Dar es Salaam. Amesema maboresho ya elimu hayawezi kuleta matokeo chanya kama hayatazingatia lishe ya wanafunzi, akibainisha kuwa serikali imeweka sera na miongozo kuhakikisha shule zinatoa huduma ya chakula. “Mchakato wa ufundishaji na ujifunzaji hatuwezi kufanikiwa bila kuwa na huduma bora za chakula na lishe,” amesema Dk Mtahabwa. Ameeleza kuwa serikali imechukua hatua mbalimbali kuimarisha lishe shuleni, ikiwemo waraka wa mwaka 2...