Machapisho

ZAIDI YA WATOTO 173,255 IGUNGA KUPATIWA CHANJO YA POLIO BAADA YA KIRUSI KUGUNDULIKA JIJINI MWANZA

Picha
  Na Lubango Mleka, Igunga.  Zaidi ya watoto 173,255 wenye umri chini ya miaka kumi wanatarajiwa kupatiwa chanjo ya ugonjwa wa polio wilayani Igunga mkoani Tabora, kufuatia kugundulika kwa kirusi cha ugonjwa huo mkoani Mwanza. Hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za serikali kuzuia kusambaa kwa ugonjwa huo hatari, hasa kwa watoto wadogo ambao wako kwenye hatari kubwa ya maambukizi. Katika kujiandaa na zoezi hilo, Hospitali ya Wilaya ya Igunga imetoa elimu kwa wadau wa afya kwa lengo la kuwajengea uelewa pamoja na kuongeza nguvu ya uhamasishaji kwa jamii ili kuhakikisha mwitikio unakuwa mkubwa wakati wa utekelezaji wa chanjo hiyo. Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Mratibu wa Chanjo wilayani Igunga, Novat Bijana, pamoja na wataalam wengine wa afya, walisisitiza umuhimu wa jamii kujitokeza kwa wingi kuwapeleka watoto kupata chanjo ili kujikinga na madhara ya ugonjwa wa polio. Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Wilaya ya Igunga, Bi. Elizabeth Rwegasila, aliwataka wadau hao kufikisha ...

TANROADS YAPELEKA TABASAMU MWAMGONGO

Picha
Na Allan Kitwe, Kigoma.  WAKAZI wa Kitongoji cha Mgazo, Mtaa wa Lubona katika Kijiji cha Mwamgongo Kata ya Mwamgongo Wilaya ya Kigoma wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuanza kufungua barabara inayoingia kijijini kwao. Wakizungumza mbele ya waandishi wa habari jana wameeleza kuwa tangu nchi ipate uhuru mwaka 1961 Kijiji hicho hakijui usafiri wa barabara kwa sababu kiko kwenye milima na usafiri pekee wanaotegemea ni wa mitumbwi na boti. Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Lubona, Elias Lutaha ameeleza kufurahishwa na hatua ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuipatia TANROADS Kigoma shilingi bilioni 3 kwa ajili ya kuchonga milima na kuanza kufungua barabara hiyo. ‘Tangu tumepata uhuru barabara hii indo imeanza kufunguliwa, kwa sasa ukitoka Kigoma Mjini kupitia Mkongoro unafika katika Kitongoji hiki kwa usafiri wa barabara lakini haifiki Mwamgongo Kijijini’, ameeleza. ‘Barabara yetu imefunguliwa kutoka Chankere hadi hapa Mganzo lakini haifiki Mwamgongo, chonde chonde, Mheshimiwa R...

SERIKALI YAENDELEA KUTENGA MAENEO NA KUTOA LESENI KWA WACHIMBAJI WADOGO WA MADINI

Picha
Na Hamida Ramadhan,  Dodoma MKURUGENZI wa Ukaguzi wa Migodi na Mazingira kutoka Tume ya Madini, Hamisi Kamando, amesema serikali inaendelea kutenga maeneo maalum kwa ajili ya wachimbaji wadogo wa madini, kuwapatia leseni na kuwaendeleza ili waweze kunufaika na rasilimali za madini. Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dodoma, Mhandisi Kamando amesema kuwa kupitia Wizara ya Madini, serikali imeendelea kutenga maeneo ya uchimbaji wa madini kwa wachimbaji wadogo nchini, ambapo hadi sasa jumla ya maeneo 65 yamependekezwa kutengwa kwa ajili ya kugawiwa kwa wananchi. Amesema maeneo hayo yapo katika mikoa mbalimbali ya kimadini ikiwemo Mtwara, Manyara, Lindi, Morogoro, Dodoma, Tabora, Pwani, Tanga, Geita, Shinyanga, Mwanza, Mara, Mbeya na Ruvuma. Aidha amesema katika kipindi cha Julai hadi Desemba 2025, serikali ilitoa jumla ya leseni 5,983 za uchimbaji mdogo wa madini, sawa na asilimia 71 ya leseni zote zilizotolewa katika kipindi hicho, ambapo leseni hizo hutolewa kwa Watanzani...

REA YAFANYA ZIARA YA UHAMASISHAJI MIRADI YA NISHATI VIJIJINI MKOANI IRINGA.

Picha
  Wananchi wapewa elimu matumizi  bora ya nishati safi, Wananchi wapewa elimu ya  UMETA (READY BOARD), REA yahamasisha wananchi kujiunga na huduma ya umeme. Na Mwandishi Wetu, Iringa.  WAKALA wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuhamasisha matumizi sahihi na endelevu ya umeme kwa Watanzania ikiwa ni pamoja na matumizi ya vifaa vya kisasa vya umeme hususan majiko ya umeme ambayo yanatumia kiasi kidogo cha umeme, salama kwa afya za watumiaji na kwa gharama nafuu. Hayo yamebainishwa na Wataalam wa REA waliofika mkoani Iringa wilaya ya Kilolo kutoa elimu kwa wananchi kuhusu kutumia fursa ya miradi ya REA inayotekelezwa mkoani humo. Akizungumza katika mkutano na wananchi, Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka REA, Abdulrazack Mkomi amesema kuwa, majiko ya umeme yanalinda afya za watumiaji na ni nafuu kulinganisha na matumizi mengine ya nishati ya mkaa na kuni. Ameongeza kuwa, ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, REA itaendelea kusambaza kwa wingi majiko ya gesi...

SINGIDA 0-AZAM 1 MPIRA NI MAPUMZIKO

Picha
NBCPL Ni mapumziko na mbili kibindoni…!!! HT: Dodoma Jiji 0-2 Azam FC  #NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #ImenogaZaidi #DodomaJijiFC #AzamFC #DodomaJijiAzamFC

AFRIKA KUSINI YAONGEZA WANAJESHI KUKABILIANA NA MAGENGE YA DAWA ZA KULEVYA NA MAUAJI YA RAIA.

Picha
WANAJESHI wamepelekwa katika mitaa ya mji mkubwa zaidi nchini Afrika Kusini, Johannesburg, ili kukabiliana na uhalifu unaosababisha idadi kubwa ya watu kuuawa na mapigano kati ya magenge ya dawa za kulevya   Kwa habari zaidi tufuatilie kupitia you tube @habarikamilitv, Facebook habari kamili tv na kwenye blog @habarikamilitv

SERIKALI YAPENDEKEZA KUKUSANYA NA KUTUMIA SH. TRILIONI 62.334 KWA MWAKA WA FEDHA 2026/27

Picha
  Na Mwandishi Wetu.  WAZIRI wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, (Mb), amewasilisha Mapendekezo ya Mfumo na Ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2026/27, ambapo katika kipindi hicho, inatarajia kukusanya nakutumia shilingi trilioni 62.334 kwa ajili ya matumizi ya kawaida, maendeleo na kulipia deni la Taifa. Mhe. Balozi Omar amesema hayo wakati akiwasilisha Mpango huo ambapo amesema kwenye Kamati ya Bunge zima, katika Ukumbi wa Pius Msekwa, ambapo ongezeko hilo ni sawa na asilimia 10.3 ikilinganishwa na Bajeti ya Mwaka wa Fedha, 2025/26. Tukio hilo limeongozwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba na kuhudhuriwa pia na Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azan Zungu, na viongozi waandamizi wa Serikali.