NUKUU KUTOKA UN.
WAKATI dunia inaendelea kutumia fedha nyingi zaidi kwenye silaha na maandalizi ya vita, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anakumbusha kwamba, usalama wa kweli haujengwi kwa silaha, bali kwa imani, mazungumzo na utu wa binadamu. "Kupunguza silaha si jambo la kusubiri hadi amani ipatikane. Ni hatua ya kuzuia vita kabla havijaanza. Ni njia ya kujenga uaminifu kati ya mataifa. Ni kulinda maisha na mustakabali wa dunia yetu." Sanamu ya Bunduki Iliyofungwa Fundo kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York City inaendelea kuwa ukumbusho kwamba amani huanza pale vurugu zinapokoma. #UN #habarikamilitv #USA #IRAN #URUSI # CHINA