Machapisho

MALALAMIKO YA VIWANJA MBADALA YAPATIWA UFUMBUZI DODOMA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  SERIKALI kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeyapatia ufumbuzi malalamiko ya muda mrefu ya viwanja mbadala kwa wananchi wa jiji la Dodoma. Suluhisho hilo linafuatia malalamiko ya takriban wananchi 4000 wa jiji la Dodoma wanaodai viwanja na halmashauri ya jiji la Dodoma kuwapa ahadi bila kutekeleza mpaka sasa. Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 25 Februari 2026 na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo wakati akizungumza na wananchi wenye migogoro ya ardhi katika eneo la Mahomanyika lilopo kata ya Nzuguni jijini Dodoma. Dkt Akwilapo amesema, eneo la Mahomanyika ni eneo la serikali hivyo lipangwe na kupimwa kwa ajili ya utatuzi wa migogoro ya meneo mbalimbali ya jiji la Dodoma pamoja na matumizi ya serikali. "Eneo hili lenye mgogoro hapa Mahomanyika ni eneo la serikali hivyo lipangwe na kupimwa kwa ajili ya utatuzi wa migogoro na siyo ya hapa tu na mingine ya jiji la Dodoma na matumizi ya serikali...

TAKUKURU MKOA WA MWANZA IMEFANIKIWA KUDHIBITI KIASI CHA TZS MILIONI 85.5

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mwanza.  TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mwanza imefanikiwa kudhibiti kiasi cha Sh milioni 85.5 kupitia uchambuzi wa mfumo wa malipo ya fedha za kujikimu kwa walimu wa shule za sekondari katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza. Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mwanza, Abnery Mganga, amesema kuwa katika utekelezaji wa majukumu ya kuzuia rushwa, taasisi hiyo ilifanikiwa kudhibiti kiasi hicho cha Sh milioni 85.5 na kuhakikisha kinalipwa kwa walimu waajiriwa wapya wa shule za sekondari waliokuwa na madai katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza. Aidha, Mganga amesema mafanikio hayo yametokana na uchambuzi wa mfumo uliofanywa na taasisi hiyo pamoja na halmashauri kutekeleza mapendekezo yaliyotolewa katika kikao kazi kati ya TAKUKURU na wadau wa halmashauri. Hatua hiyo imewawezesha walimu 77 waliokuwa na madai kulipwa stahiki zao.

CCM: MAKAMPUNI YASIYOLIPA WAKULIMA YAPIGWE ‘STOP’

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeitaka Bodi ya Tumbaku (TTB) nchini kuchukua hatua mara moja dhidi ya Makampuni yote yanayonunua zao la tumbaku na kushindwa kulipa wakulima kwa wakati, na kushauri wapigwe stop. Ushauri huo umetolewa jana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tabora Komredi Saidi Nkumba alipokuwa akitoa salamu za chama katika Mkutano Mkuu wa 33 wa Chama Kikuu cha Ushirika wa Wakulima wa Tumbaku (WETCU) Mkoani Tabora. Amesema kuwa haingiii akilini kuona mkulima akihangaika kuandaa shamba lake mwaka mzima tena kwa gharama kubwa ili kuhakikisha anapata tumbaku nzuri inayokidhi viwango vya soko la ndani na nje lakini anapouza halipwi kwa wakati. ‘Chama Cha Mapinduzi hakifurahishwi na hali hii, Wanunuzi wote wanaokuja kununua mazao ya wakulima wanatambulika kisheria na wanapewa leseni, kama hawafanyi kile kinachotakiwa kuna haja gani ya kuwabembeleza’, ameeleza. Komredi Nkumba ameitaka Bodi ya Tumbaku kusimamia ipasavyo zao hilo ili mkulima anufaike na jasho...

SONGORO MARINE UBORA WA KIMATAIFA UJENZI MELI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mwanza.  KAMPUNI ya kizawa ya Songoro Marine iliyojikita katika ujenzi wa meli ndani na nje ya Tanzania inatajwa ni kampuni inayojenga meli kwa viwango vya kimataifa. Kampuni hiyo, imekuwa ikipewa zabuni na serikali za ujenzi wa vivuko, kutokana na kuonyesha uzalendo katika kutekeleza miradi kwa viwango vya kimataifa. Kwa miaka zaidi ya 30 Tangu kuanza kwa kampuni hii ya kizalendo imeonyesha dira kwa kampuni za kizawa baada ya kuaminiwa na serikali katika ujenzi wa vivuko. Kampuni hii iliyoanza kazi mwaka 1993 kwa sasa imeendeleza mizizi ya ujenzi wa meli za kisasa zinazotumiwa ziwani na baharini kwa kufungua matawi nje ya mipaka ya Tanzania. Inaelezwa kuanza kufungua matawi nje ya mipaka ya Tanzania ni hatua iliyotokana na kazi iliyotukuka kwa kujenga meli na vivuko vya umma na binafsi kwa viwango vya kimataifa. Serikali ya Tanzania mara kwa mara imekuwa ikitangaza zabuni za ujenzi wa meli, ambapo kampuni hii ya kizalendo imekuwa ikiibuka kidedea. Songoro...

KAMPUNI YA SONGORO MARINE YAKABIDHI KIVUKO UGANDA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Uganda.  KAMPUNI ya kizawa ya Songoro Marine iliyojikita katika ujenzi wa meli ndani na nje ya Tanzania imekamilisha ujenzi wa kivuko kikubwa kitakachokuwa na uwezo wa kubeba abiria 310. Kampuni hiyo imekamilisha ujenzi wa kivuko hicho kitakachokuwa kinafanya safari zake kati ya Bukungu - Kagwara - Kaberamaido nchini Uganda. Songoro marine ambayo imejikita na ujenzi wa vivuko, imeendelea kuaminiwa na serikali ya uganda katika ujenzi wa vivuko kadhaa nchini humo. Mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo, Meja Songoro akizungumza wakati wa kukabidhi kivuko hicho, amesema ujenzi wa kivuko hicho ulianza februari 2020 na kukabidhiwa Februari 20 mwaka huu.  Kampuni ya Songoro Marine, ilisaini  mkataba wa ujenzi wa vivuko viwili pamoja na mashine ya kuondoa uchafu ziwani (dredger) kwa fedha za Uganda shilingi, 41,974,226,085. Baada ya siku ya jana kampuni hiyo kukabidhi kivuko hicho kwa serikali ya Uganda, inaendelea na kivuko kingine kimoja ambacho kitakabi...

BINTI MCHOMA MAHINDI TABORA AWEZESHWA MTAJI WA LAKI 3

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora.  WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, Joel Nanauka ameleta neema kwa kijana muuza mahindi ya kuchoma Hadija Seif (26) mkazi wa Kata ya Ng’ambo, Manispaa ya Tabora baada ya kumwezesha mtaji wa shilingi laki 3. Waziri amemwezesha mtaji huo leo alipokuwa akifungua Jukwaa la Vijana wa Vyuo Vikuu na Vyuo vya Kati vilivyopo Mkoani Tabora, katika ukumbi wa Chuo Cha Utumishi wa Umma Mjini hapa. Ameeleza kuwa jana akiwa katika pita pita yake mitaani baada ya kuwasili Mjini Tabora alimwona dada mmoja akichoma mahindi na alipomuuliza mradi huo unamsaidiaje akasema kuwa unampatia kipato kidogo cha kutunza watoto wake. Na alipomuuliza ndoto yake ni nini, akaeleza kuwa anatamani kuwa na biashara ya kuuza vyombo vya nyumbani na kuuza samaki wa kukaanga, ila mtaji hana na alipoulizwa anatamani kuwa na mtaji wa kiasi gani akasema laki 3. ‘Sikujitambulisha kuwa mimi ni Waziri ila nilimwambia aje ukumbi wa Chuo cha Utumishi wa Umma kuna mkutano wa vijana, ...

KARDINALI POLYCAP PENGO AFARIKI DUNIA

Picha
 

WATUHUMIWA MAUAJI YA BODABODA TABORA WAKAMATWA

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora.  JESHI la Polisi Mkoani Tabora linawashikilia watu wanne kwa tuhuma za ujambazi na mauaji ya waendesha bodaboda yaliyokuwa yakiripotiwa mara kwa mara katika maeneo mbalimbali Mkoani hapa. Hayo yamebainishwa jana na Mkuu wa Mkoa Paul Matiko Chacha alipokuwa akizungumza na Wadau wa Maendelea na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa. Amesema kuwa kukamatwa kwa watuhumiwa hao kumetokana na operesheni maalum iliyofanywa na askari wa Jeshi la Polisi Mkoani hapa kwa kushirikiana na Vyombo Vingine vya Ulinzi na Usalama. Amedokeza kuwa msako huo ulilenga kunasa wahalifu wote waliokuwa wakijihusisha na vitendo hivyo ambavyo vimekuwa vikisababisha taharuki kubwa miongoni mwa jamii na hususan waendesha bodaboda. ‘Kukamatwa watuhumiwa hawa ni hatua moja, uchunguzi bado unaendelea ili kubaini mtandao mzima na kukamata wahusika wote ili kukomesha tabia hii na hatua kali zitachukuliwa dhidi ya wahusika wote’, ameeleza. Aidha ameongeza kuwa watu wengine wawil...

REA YAHIMIZA WANANCHI KUJIUNGA NA HUDUMA YA UMEME TANGA

Picha
Wananchi wapewa elimu ya kufanya maombi ya umeme, waaswa kutumia umeme kwa tija kujiletea maendeleo. Na Mwandishi Wetu, Tanga.  WAKALA wa nishati vijijini (REA) umepiga kambi Mkoani Tanga kwa ajili ya zoezi la uhamasishaji wananchi kujiunga na huduma ya umeme. Uhamasihaji huo umefanyika katika maeneo ya pembezoni mwa wilaya ya Tanga mjini kwenye maeneo ya sokoni ,vituo vya bodaboda pamoja na mikutano ya hadhara iliyofanyika maeneo ya ofisi za kata na mitaa  lengo kubwa likiwa ni kuwapa uelewa wananchi juu ya umuhimu wa kujiunga na huduma ya umeme. Akizungumza wakati wa uhamasishaji Afisa maendeleo ya jamii kutoka REA , ndugu Abdulrazack Mkomi alisema , Lengo la wakala kufika wilayani humo ni kuwafikia wananchi na kuzungumza nao juu ya umuhimu wa kutumia fursa ya upatikanaji wa huduma ya umeme ambayo ni nafuu sana na kuwahimiza kujiunga mapema na huduma hiyo ya umeme hasa wakati ambapo mkandarasi bado yupo eneo la mradi. Aidha Mkomi amesema, utekelezaji wa miradi hii ya umeme u...

RAIS DKT MWINYI: SMZ KUIMARISHA USAFIRI NA USAFIRISHAJI WA MIZIGO PEMBA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Zanzibar.  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali imejipanga kikamilifu kumaliza tatizo la usafiri na usafirishaji wa mizigo katika Kisiwa cha Pemba. Akizungumza leo tarehe 17 Februari 2026 wakati wa ufunguzi wa Msikiti mpya wa Chachani, uliopo Chake Chake, Mkoa wa Kusini Pemba uliojengwa na mfanyabiashara Ndg. Said Nassor Bopar, Rais Dkt.Mwinyi amesema Serikali imeandaa meli mbili za mwendo kasi na ipo katika hatua za kutafuta meli maalum ya mizigo kwa safari za Unguja na Pemba. Aidha, ameeleza kuwa Serikali imeliagiza Shirika la Meli la Zanzibar kuimarisha huduma zake na kubainisha kuwa meli ya MV Mapinduzi II itaanza kazi hivi karibuni baada ya matengenezo. Ameongeza kuwa uimarishaji wa bandari za Pemba utahamasisha sekta binafsi kuongeza vyombo vya usafiri. Rais Dkt. Mwinyi amewahimiza waumini kuitumia misikiti kujadili changamoto za kijamii, akiwapongeza wafadhili wa msikiti huo kwa mcha...

KIHONGOSI AKAGUA UTEKELEZAJI MIRADI YA BIL 2.5 NZEGA

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora.  KATIBU wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) anayesimamia Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani Kihongosi ameeleza kufurahishwa na kazi nzuri ya utekelezaji miradi ya maendeleo katika Wilaya ya Nzega Mkoani hapa. Akiwa katika siku ya pili ya ziara yake, Kihongosi ametembelea na kukagua utekelezaji miradi yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 2.5 iliyotekelezwa na serikali ya Awamu ya Sita katika Majimbo matatu ya Wilaya ya Nzega. Mradi wa kwanza aliotembelea ni wa ujenzi wa mabweni 2 ya wanafunzi wa kike na kiume katika shule ya sekondari Puge, ujenzi wa vyumba 6 vya madarasa na matundu 10 ya vyoo, vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 450. Amebainisha kuwa ujenzi wa miundombinu hiyo ambayo imefadhiliwa na Kampuni ya Barrick ni kichocheo muhimu sana cha kuinua ya taaluma katika shule hiyo, hivyo akatoa wito kwa walimu na wanafunzi kutumia vizuri miundombinu hiyo. Mradi mwingine ni ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Nzega uliogharimu za...