Machapisho

MJI ULIOPO CHINI YA ARDHI WAGUNDULIWA SYRIA

Picha
  “Mji uliopo chini ya ardhi” wenye ghorofa tatu uligunduliwa tarehe 27 Januari mwaka 2026 nchini Syria. Mji huo ulijengwa na Jeshi la Kidemokrasia la Syria (SDF) chini ya mlima katika mji wa Sirrin, ambao ni sehemu ya eneo la Ayn al-Arab na unaunganishwa na mahandaki mengi.

DKT. KIJAJI AMWAPISHA CC BADRU NA KUZINDUA BODI YA NGORONGORO

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Arusha KAMISHNA Uhifadhi wa  Mamlaka ya Ngorongoro   Abdul - Razaq  Badru ametakiwa kuhakikisha hifadhi ya Ngorongoro inalindwa na kuhifadhiwa ili ikolojia yake istawi na kuendelea kuvutia watalii,kuhifadhi wanyamapori, misitu na viumbe hai wengine.  Hayo yamesemwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, jijini Arusha baada ya kumwapisha Kamishna huyo na kuizindua Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro. Dkt. Kijaji amesema kuwa, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ameonesha imani kubwa kwa Kamishna huyo, hivyo pamoja na mambo mengine anapaswa kuingoza vyema Mamlaka hiyo ili iweze kufikia matarajio yaliyokusudiwa hususani ya kufikia ya idadi ya watalii Milioni 8 kitaifa.  "Unapaswa uhakikishe huduma za malazi zinaendelea kuboreshwa kwa kuvutia uwekezaji  utakaoongeza vitanda  kutoka  1,555  hadi kufikia vitanda 2,586". Alisema Dkt. Kijaji. Ame...

BUNGE BONANZA: WASHIRIKI WATAJITOELEA KUCHANGIA DAMU SALAMA

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Dodoma. MWENYEKITI  wa Bunge Bonanza, Festo Sanga, amesema washiriki wa Bunge Bonanza wanatarajiwa kujitolea kuchangia damu salama kwa hiari katika tukio litakalofanyika Jumamosi, Januari 31, 2026, kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari John Merlin Miyuji jijini Dodoma. Akiongea na waandishi wa habari  leo Januari 29 ,2026 Bungeni jijini Dodoma Sanga amesema zoezi hilo lina lengo la kuokoa maisha ya wagonjwa, kupunguza dharura za kiafya na kuimarisha mshikamano wa kijamii kati ya washiriki na jamii kwa ujumla. Ameeleza kuwa kuchangia damu ni kitendo cha huruma kinachoongeza uelewa wa jamii kuhusu umuhimu wa afya na mshikamano wa kitaifa. Amesema Bunge Bonanza linahusisha mashindano ya michezo ya burudani ikiwemo mpira wa miguu, kuruka kamba, pete, mashindano ya kula, kufukuza kuku pamoja na michezo mingine yenye lengo la burudani na mshikamano. Ameongeza kuwa tukio hilo litawakutanisha mashabiki wa timu za soka za Simba na Yanga, washiriki kutoka vyuo...

TANZANIA NA BRAZIL ZAAHIDI KUENDELEA KUSHIRIKIANA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma. TANAZANIA na Brazil zimeahidi kuendelea kushirikiana katika sekta za kimkakati zenye maslahi mapana kwa mataifa haya mawili ikiwemo Afya, Kilimo, biashara, uwekezaji, elimu na ulinzi na usalama. Hayo yamebainishwa wakati wa mazungumzo baina ya Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe na Balozi wa Brazil nchini Mhe. Gustavo Martins Nogueira yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara jijini Dodoma Januari 29, 2026.  Viongozi hao wamejadili  masuala kuhusu ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Brazil kwa kipindi cha miongo mitano iliyopita na kukubaliana kuendelea kuuimarisha ushirikiano huo na kuupeleka katika viwango vya juu ili kuwawezesha wananchi kunufaika nao. Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Maghembe aliishukuru Serikali ya Brazil kwa kusaidia utekelezaji wa miradi ya zao la pamba ya Beyond Cotton na Cotton Victoria na kusistiza umuhimu wa kuibua miradi mingine zaidi.  “Miradi hii imejik...

RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI WA VIONGOZI MBALIMBALI

Picha
 

POLISI NJOMBE WAKANUSHA TAARIFA ZA ASKARI KUCHOMWA MOTO NA KUPORWA SILAHA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Njombe. JESHI la Polisi Mkoa wa Njombe katika taarifa yake kwa Vyombo vya habari limekanusha taarifa zilizokuwa zimesambazwa katika Mitandao ya Kijamii nchini zikiambatana na picha mjongeo (Video), zikieleza uwepo wa Askari Polisi wa Mkoa huo aliyechomwa moto na kisha kuporwa silaha Mkoani humo. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Mahamoud Banga, Januari 28, 2026 amesema kuwa katika Mkoa wa Njombe hakuna tukio kama hilo, akionya dhidi ya wanaoandaa na kusambaza taarifa za uongo na upotoshaji. "Jeshi la Polisi linatoa wito kwa baadhi ya wananchi wenye tabia za kuandaa na kusambaza taarifa za uongo na upotoshaji kwa njia mbalimbali kuacha kwani ni kinyume cha sheria za nchi na maadili ya Mtanzania na hakuna faida yoyote kwa wanaofanya hivyo pamoja na familia zao na kwa jamii kwa ujumla." Amesema Kamanda Banga. Polisi pia imesema inaendelea kumfuatilia mtu ama watu waliochukua na kutumia picha mjongeo ya tukio la zamani ambalo as...

MWANACHAMA WA CHADEMA ARUSHA MATATANI KWA KUIBA 'FEDHA ZA LISSU

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Arusha. JESHI la Polisi Mkoa wa Arusha limetangaza kumkamata Bw. Fredrick Mbwambo, Mwanachama wa Chadema na Mkazi wa Arusha kwa tuhuma za wizi wa fedha ambazo alikuwa amezikusanya kutoka kwa wananchi waliokuwa wamechanga kwaajili ya Mwenyekiti wa Chama hicho Bw. Tundu Lissu kupitia Kampeni yao ya "Funga mwaka na Tundu Lissu". Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, SACP Justine Masejo leo Jumatano Januari 28, 2026 Jijini Arusha mbele ya wanahabari, amesema ukamataji wa mtuhumiwa huyo umefanyika baada ya Polisi kupokea malalamiko kutoka kwa Bw. Alute Mughwai, aliyeeleza kubaini wizi wa fedha zilizokuwa zimechangwa. "Ufuatiliaji wa awali umeonesha kuwa ukusanyaji huo wa fedha ulikuwa ukifanywa kupitia namba mbili za simu za makampuni tofauti ya simu na inadaiwa zilihamishwa kwenye namba mbili za simu, moja ikiwa ni ya kampuni ya Tanzania na ya pili ikiwa ni ya kampuni ya simu ya nchi jirani." Amesema Kamanda Masejo...

KUSUASUA KWA UJENZI WA BARABARA MOSHI VIJIJINI: MBUNGE MAKOI AZUNGUMZA NA WAZIRI WA UJENZI

Picha
  Na Hamida Ramadhan,  Dodoma LICHA ya Serikali ya awamu ya sita kuendelea kujenga Miundombinu Mizuri ya Barabara hapa nchini, Mbunge wa Jimbo la Moshi vijiji Mhe. Morris Makoi amekutana na kufanya Mazungumzo na Waziri wa Ujenzi Mhe. Abdallah Ulega kuhusiana na Kusuasua kwa Miradi ya ujenzi katika Jimbo hilo. Mhe. Makoyi ametaja barabara hizo ikiwemo barabara ya Rau Madukani- Mamboleo Materuni yenye urefu wa kilomita 9.99 ambapo urefu uliokamilika ni 2.9. Akizungumza na Waziri wa Ujenzi Mhe. Ulega Mara baada ya kukutana na Kufanya Mazungumzo Mhe. Makoi amesema barabara hizo zimekuwa changamoto hivyo ni vyema serikali ikafanya mchakato kukamilisha ujenzi ili wananchi wapate Kutumia barabaraza hizo. "Barabara ya chekereni-Kahe- Mabogini yenye urefu wa kilomita 31.25, kiboriloni- Mbokomu kilomita 14.34, Moshi International school- kibosho kati-Raphael kilomita 13.9, Samanga Chemchem kilomita 9.91, Mamboleo Shimbwe kilomita 10.3 pamoja na barabara ya Kidia road(usuduni-Kidia) kilo...

DKT.JAFO AIBANA WIZARA YA UJEZNI,BARABARA YA LAMI MLANDIZI-MZENGA-BOGA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma. MBUNGE wa Jimbo la  Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, amehoji mpango wa Serikali wa kutenga bajeti ya kutosha kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya Mlandizi–Mzenga–Maneromango kwa kiwango cha lami, akisisitiza kuwa ni barabara muhimu kwa shughuli za kiuchumi na kijamii. Akiuliza swali la nyongeza Bungeni, Dkt. Jafo amesema barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 70.2 inaanzia Mlandizi kupitia Mzenga hadi Maneromango, na kwamba tayari upembuzi yakinifu umekamilika. Ameeleza kuwa kwa sasa mkandarasi ameanza kazi katika kipande cha Mzenga chenye urefu wa mita 300, hali iliyomfanya kuihoji Serikali kuhusu mpango wake wa kuongeza fedha katika bajeti ya mwaka huu ili kufungua kipande cha Mlandizi hadi Mzenga. “Nini mpango wa Serikali katika bajeti ya mwaka huu kuongeza fedha ili kuhakikisha barabara hii muhimu inaanza kujengwa kuanzia Mlandizi hadi Mzenga?” amehoji Dkt. Jafo. Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, amesema Serikali...

UMIKIDO WAJITAMBULISHA KWA WAZIRI KATAMBI

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Dodoma. MWENYEKITI  wa Umoja wa Vyombo vya Habari vya Mitandao ya Kijamii Mkoa wa Dodoma (UMIKIDO), Benny Majata, amefanya mazungumzo mafupi na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Patrobas Katambi, katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma. Katika mazungumzo hayo, leo Januari 28, 2026 Majata alimweleza Waziri Katambi juu ya malengo ya UMIKIDO katika kusimamia maudhui yenye weledi, kuhamasisha maadili ya habari mtandaoni na kuimarisha ushirikiano kati ya vyombo vya habari na serikali. Waziri Katambi amepongeza hatua ya umoja huo kujitambulisha, na ameuhimiza UMIKIDO kufika ofisini kwake ili kufanya mazungumzo ya kina kuhusu masuala ya kimaadili, matumizi salama ya mitandao, pamoja na namna vyombo vya habari mtandaoni vinavyoweza kushirikiana na serikali katika kulinda usalama na maslahi ya Taifa.

RADA ZA HALI YA HEWA NI MUHIMU KATIKA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA HALI YA HEWA NCHINI.

Picha
  Na Hamida Ramadhani, Dodoma. MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) iliandaa warsha ya mafunzo ya Rada za Hali ya Hewa na matumizi ya taarifa zinazotokana na Rada,  tarehe 26-27 Januari 2026, Dodoma. Lengo kuu la mafunzo haya ni kuimarisha uwezo wa kitaalamu na kiufundi katika matumizi ya teknolojia Rada, hususan katika uchambuzi, tafsiri na matumizi ya taarifa ili kuboresha utoaji wa utabiri zikiwemo tahadhari za  hali mbaya ya hewa kwa wakati na kwa usahihi zaidi.           Mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa warsha hiyo alikuwa ni Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi, Dkt. Ladislaus Chang’a alisema “Kama mnavyofahamu, kwa sasa dunia inashuhudia ongezeko kubwa la matukio ya hali mbaya ya hewa yanayotokana na  kuchagizwa na mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi, ikiwemo mvua kubwa, mafuriko, vipindi virefu vya ukame, pamoja na matukio ya vimbunga na upepo m...

VYANZO VYA MAJI KUENDELEA KUTUNZWA KUONGEZA UHAKIKA WA HUDUMA YA MAJI.

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma. WAZIRI Wa Maji  Mhe.  Jumaa Aweso  (Mb) amewataka wakurugenzi wa bodi za maji za  mabonde nchini kuonyesha umuhimu wa taasisi hizo kwa wananchi kwa vitendo kwa kutoa huduma sahihi.  Waziri Aweso ametoa maelekezo hayo katika kikao cha Bodi za maji za mabonde nchini katika ukumbi wa Jiji la Dodoma.  Aweso ambaye ndiye mgeni rasmi katika kikao hicho amewataka viongozi wa mabonde hayo kutambulika kwa utoaji wa huduma na si kutambulika kwa sifa mbaya kwa wananchi na serikali ikiwemo utozaji wa Kodi zisizi halali.  Aidha Serikali bado inaendelea na mpango mkakati iliyojiwekea katika kujenga mabwawa ya kimkakati kuendelea kupanda miti rafiki wa maji kwa mazingira Ili kuboresha vyanzo vya maji na kutoa huduma ya uhakika kwa wananchi.  Nae Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri amewataka wakurugenzi na wenyeviti wa Bodi za maji za mabonde nchini kuendelea kutunza vyanzo vya maji Ili kuwa na uhakika wa huduma...

VIWANDA NA BIASHARA WAPANDA MITI KUMUUNGA MKONO RAIS, DKT. SAMIA KATIKA SIKU YAKE YA KUZALIWA.

Picha
Na Mwandishi Wetu,  Dodoma. MITI imekuwa muhimili muhimu katika ukuaji wa Sekta ya Viwanda na Biashara kwani kupitia miti, viwanda hupata malighafi, biashara hukua, na uchumi huimarika. Hayo yamesemwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb.), Januari 27, 2026, akiwa ameambatana na Naibu Waziri,Mhe. Dennis Londo pamoja na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Needpeace Wambuya kushiriki zoezi la kupanda miti katika Ofisi za Wizara hiyo zilizopo Mji wa Serikali, Mtumba, jijini Dodoma.  Zoezi hilo ni sehemu ya kusherehekea kumbukizi ya  siku ya kuzaliwa ya  Mwanamazingira namba moja hapa nchini, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye aliazimisha siku yake 27 Januari, 1960 kwa kupanda mti wa Muembe (Mangifera indica) katika eneo la Bungi Kilimo, Mkoa wa Kusini Unguja tarehe 27 Januari, 2026. Aidha, Waziri Kapinga wakati akiongea na Watumishi wa Wizara hiyo baada ya kupanda mti, Altria rai kwa watumishi wa wizara ...

HALMASHAURI YA IGUNGA YAUNGANA NA WATANZANIA KUPANDA MITI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Igunga. MKURUGENZI  Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Selwa Hamid ameiongoza Menejimenti ya Halmashauri hiyo kupanda miti kwa lengo la kuitekeleza 27 ya kijani iliyoasisiwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan. Selwa ameungana na viongozi hao leo,  ikiwa ni ishara ya kuendelea kumuunga mkono Rais Dk. Samia katika kumbukizi ya kazaliwa kwake. "Kipekee ninaishukuru na kuipongeza Menejimenti kujindaa na kushiriki zoezi hili baada ya masaa ya kazi kuungana na 27 ya kijani ikiwemo kumpongeza na kumtakia kila la kheri Mheshimiwa. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan," ameshukuru.  Ameeleza kuwa wamepanda miche 70 ambapo miche 50  yakivuli huku 20 ikiwa ni ya  matunda ambayo yatawafaidisha vizazi na vizazi.

IGUWASA YAUNGA MKONO JITIHADA ZA RAIS, DKT. SAMIA KWA KUPANDA MITI.

Picha
  Tabora, Januari 27, 2026. Na Lubango Mleka, Igunga. KAATIKA kuunga mkono tamko la Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuhusu upandaji wa miti kama sehemu ya utunzaji wa mazingira, Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Wilaya ya Igunga (IGUWASA) imefanya zoezi la upandaji wa miti mbalimbali katika eneo la ofisi zake. Zoezi hilo limefanyika ikiwa ni kumbukizi ya siku ya kuzaliwa ya Mheshimiwa Rais, ambapo taasisi hiyo imeeleza kuwa inalenga kuhamasisha jamii kushiriki kikamilifu katika kulinda na kuhifadhi mazingira kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho. Viongozi na watumishi wa IGUWASA wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga, Bi. Selwa  Abdallah Hamid wameshiriki katika zoezi hilo, wakisisitiza kuwa upandaji miti ni hatua muhimu katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na kuhakikisha upatikanaji endelevu wa rasilimali za maji. IGUWASA imewahimiza wananchi kuiga mfano huo kwa kupanda ...

MMOJA AFARIKI KATIKA AJALI YA GARI SHINYANGA 12 WAJERUHIWA

Picha
DEREVA wa Lori lenye namba za usajili RAE 848  Mali ya Kampuni ya Jaja ya nchini Rwanda amepoteza maisha baada ya kugongana uso kwa uso na basi la abiria namba T 229 EEL mali ya kampuni ya Kisire lililokuwa likitokea Kahama kwenda Mwanza na kusababisha Majeruhi 12. Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga, SACP Janeth Magomi amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo iliyotokea Januari 27 katika eneo la Tinde Mnadani na kusema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa Basi la Kisire aliyetaka kupita mkokoteni uliokuwa umebeba matunda na kuhama upande mwingine na kugongana uso kwa uso na lori hilo.

SERIKALI YAZINDUA MFUMO "ONGEA NA WAZIRI, MWANACHI KUPEWA SAUTI YA MOJA KWA MOJA SEKTA YA AFYA

Picha
  Na WAF, Arusha. SERIKAL imetangaza mwanzo wa enzi mpya ya uwazi, uwajibikaji na ushirikishwaji wa wananchi katika sekta ya afya baada ya kuzindua rasmi kwa mfumo wa kidijitali wa “Ongea na Waziri wa Afya” unaomuwezesha mwananchi kuwasiliana moja kwa moja na Wizara ya Afya saa 24 kwa siku. Hayo yamesemwa na Mhe. Mohamed Mchengerwa wakati wa  hafla ya uzinduzi iliyofanyika leo Januari 26,2026 jijini Arusha. Waziri wa Afya, Mheshimiwa Mohamed Omary Mchengerwa, amesema mfumo huo ni utekelezaji wa vitendo wa dhamira ya Serikali ya kuisogeza huduma ya afya karibu na mwananchi na kuhakikisha sauti ya wananchi inatumika kama dira ya maboresho ya huduma. “Mfumo wa "Ongea na Waziri wa Afya" unatuma ujumbe ulio wazi kuwa sauti ya mwananchi si ya pembeni, bali ndiyo msingi wa maamuzi ya Serikali katika kuboresha huduma za afya,” amesema Waziri Mchengerwa. Amefafanua kuwa uzinduzi wa mfumo huo ni mapinduzi makubwa katika sekta ya afya kwa kuwa unajenga utamaduni mpya wa uongozi unaosiki...