DKT SEIF- TUREJESHE TABASAMU KWA WANANCHI KWA KUTOA HUDUMA BORA
Na Lubango Mleka, Mwanza. VIONGOZI katika ngazi zote wametakiwa kuhakikisha wanarejesha tabasamu kwa watanzania kwa kuwapeleka huduma bora ikiwa ni sambamba na kusimamia na kutunza miundombinu iliyopo ili iweze kuleta tija na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi. Rai hiyo imetolewa na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Dkt. Jafar Seif (MB) tarehe 16 Desemba, 2025 na) wakati wa ziara yake ya kikazi katika Manispaa ya Ilemela ambapo lengo kuu la ziara ni kutembelea miradi ya afya pamoja na kukutana na watumishi kwa ajili ya kujadili na kubaini changamoto zinazoikablili sekta hiyo katika utoaji wa huduma kwa wananchi. “Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI ni jukumu letu kuhakikisha kwamba tunamsaidia Mhe. Rais kurudisha tabasamu kwa watanzania, ahadi ambayo aliitoa wakati akilihutubia bunge la 13 ambapo aliahidi kwamba ndani ya awamu ya sita kipindi cha pili tuhakikishe tunarejesha tabasamu kwa watanzania kw...