Machapisho

ADAKWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUJITEKA

Picha
Na Allan Kitwe, Tabora JESHI la Polisi Mkoani Tabora linamshikilia Hadija Jimmy Mrijo (39) mpare, kwa tuhuma za kutoa taarifa za uongo kuwa ametekwa na watu wasiojulikana ili ajipatie fedha isivyo halali kutoka kwa mume wake. Kamanda wa Polisi Mkoani hapa SACP Richard Abwao amethibitisha kushikiliwa mwanamke huyo ambaye ni mke wa Emanuel Peter Charles mkazi wa Tabora Mjini. Amesema kuwa mtuhumiwa alikamatwa baada ya kupata taarifa kutoka kwa mumewe kuwa alipigiwa simu na mtu asiyemfahamu akidai kuwa wamemteka hivyo awatumie fedha kiasi cha sh mil 2 ili wamwachie. Amedokeza kuwa mume wa mtuhumiwa baada ya kupokea taarifa hiyo na kusikia mlio wa kuteswa aliingiwa na hofu na kuanza kutafuta kiasi hicho cha fedha ambapo alifanikiwa kutuma kiasi cha sh 1,385,800/-. Kamanda Abwao amefafanua kuwa baada ya kufanya uchunguzi wa kina tumebaini kuwa mtuhumiwa hakuwa ametekwa ila alijiteka mwenyewe ili apate fedha hizo, akishirikiana na wenzake na wote wamekamatwa.  Ametaja watuhumiwa wengine ...

MATUKIO KATIKA PICHA

Picha
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji leo Novemba 18,2025 Ikulu jijini Dodoma.

WADAU WA UTALII NA UHIFADHI NYANDA ZA JUU KUSINI WAHAMASISHWA KUWANIA TUZO ZA SERENGETI

Picha
  Na Mwandishi Wetu - Iringa  WADAU wa uhifadhi na utalii  katika mikoa ya nyanda za juu kusini wamehamasishwa kushiriki katika tuzo za uhifadhi na utalii za Serengeti (Serengeti Awards 2025) zinazotarajiwa kufanyika mwezi Desemba 2025. Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Utalii, Bi. Dainess Kunzugala amesema hayo leo katika kikao na wadau hao wakiwemo makampuni na waendeshaji wa shughuli za utalii , waongoza watalii , watoa huduma za malazi , wahifadhi na mashirika au taasisi zenye mchango katika uhifadhi  kilichofanyika Novemba 17, 2025 Mkoani Iringa. "Natoa hamasa kwa wadau wetu wa utalii kutumia fursa hii muhimu kutuma maombi yao kuwania tuzo hizi muhimu ambapo kuna kategoria zipatazo saba ambazo zimeainisha makundi mbalimbali" amesema Bi. Kunzugala. Amesema lengo ni kutambua mchango wa wadau hao pamoja na kuifanya sekta ya utalii iwe na mwamko katika kuleta maendeleo nchini. Naye, Mwongoza Watalii kutoka kampuni ya Mukuta Travel and Tours, Bw.Fadhili Laizer ameishukur...

ZAIDI YA LESENI 700 ZATOLEWA KWA KIPINDI CHA MIAKA MITATU

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mahenge - Morogoro. KATIKA kipindi cha miaka mitatu kuanzia Mwaka 2022 hadi 2025 zimetolewa  leseni  714 katika Ofisi ya Afisa Madini Mkazi Mahenge zikijumuhisha leseni za  utafiti, uchimbaji na biashara ya madini kwa wadau mbalimbali wanajishughulisha na uwekezaji katika Sekta ya Madini. Hayo yalielezwa Novemba 12, 2025 na Afisa Madini Mkazi , Mkoa wa Kimadini Mahenge Jonas Mwano wakati akielezea kuhusu mafanikio yaliyopo. Mwano alisema kuwa, mafanikio hayo miaka mitatu yamepelekea kufikia lengo la ukusanyaji wa  maduhuli kwa asilimia 78.7 katika wilaya ya Ulanga, Malinyi na Kilombero. Aidha katika kipindi cha mwezi Julai mpaka Oktoba 2025 Ofisi imekusanya asilimia 61 ya lengo katika kipindi  husika. Akielezea kuhusu aina ya leseni zilitolewa Mwano alifafanua kuwa, katika kipindi husika kulitolewa aina mbalimbali za  leseni  kama leseni za utafiti 15, leseni kubwa ya uchimbaji 2, leseni ndogo ya uchimbaji 277, leseni kubwa ya...

JUKWAA LA NASSER LA KIMATAIFA LA SHEREHEKEA KISWAHILI KUTABULIWA RASMI NA UNESCO.

Picha
  Na Mwandishi Wetu. JUKWAA la Nasser la Kimataifa lisherehekea Kutambulishwa kwa Kiswahili Kama Lugha Rasmi ya UNESCO na Kuimarisha Umaarufu Wake Ulimwenguni. Jukwaa la Nasser limekumbushwa kwa sherehe katika taarifa yake kufuatia tangazo la Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) la kutambulisha Kiswahili rasmi kama mojawapo ya lugha za kazi katika mikutano mikubwa ya shirika hilo, wakati wa Kikao cha 43 cha Bunge Kuu kilichofanyika Samarkand – Uzbekistan kuanzia Oktoba 30 hadi Novemba 13, 2025. Uamuzi huu wa kihistoria ulitokana na ombi lililotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa ushirikiano na Baraza la Kiswahili BAKITA na BAKIZA, ambapo Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa na Mwakilishi wa Kudumu kwa UNESCO, Ali Jaberi Madini, alitoa hotuba ya nchi baada ya uamuzi huo kutambulishwa rasmi. Aidha, Jukwaa hilo limebainisha katika taarifa yake kwamba kwa mafanikio haya, Kiswahili ki...

TAARIFA KWA UMMA

Picha
 

ZAIDI YA WANANCHI 1,500 KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJIKO BANIFU WILAYANI BABATI

Picha
  Majiko banifu 1,582 kusambazwa na kuuzwa kwa bei ya ruzuku, Jiko moja kuuzwa kwa bei ya ruzuku ya TZS 11,200. Na Lubango Mleka, Babati. MKUU wa Wilaya ya wa Babati, Mheshimiwa Emmanuela Kaganda, leo Novemba 12, 2025 kwa niaba ya wakazi wa wilaya ya babati amezindua mradi wa uuzaji na usambazaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku.   Uzinduzi huu ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya mkuu wa mkoa wa Manyara, Mheshimiwa Queen Sendiga akiwataka wakuu wa wilaya wote wa mkoa wa manyara kuzindua na kusimamia kikamilifu utekelezaji wa mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku katika wilaya zao. Uzinduzi umefanyika katika kata ya Magugu wilayani babati, ambapo jumla ya majiko banifu  1,582 yatauzwa na kusambazwa kwa bei ya ruzuku ya TZS 11,200 ambayo ni sawa na aslimia 80 ya ruzuku ya TZS 56,000 ambayo ni bei ya awali ya jiko. Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mheshimiwa Kaganda amesema mpango huo umelenga kuhakikisha wananchi wote, hususani wa kipat...

BALOZI PINDI CHANA AKIPA KATIKA KATIKA KIKAO CHA PILI CHA BUNGE LA TANZANIA

Picha
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Njombe,Mhe. Balozi Dkt.Pindi Chana akiapa rasmi kuwa mbunge katika Mkutano wa Kwanza, Kikao cha Pili cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Novemba 12,2025.

MTINDO BORA WA MAISHA _ LISHE ASILIA.

Picha
  Maelezo ya Kikundi (Group Description): MTINDO BORA WA MAISHA LISHE ASILIA ni jukwaa la kidigitali lililoanzishwa na Mtaala Mr Roghat Falme Robert kwa ushirikiano na wataalamu wa Lishe, afya na kilimo na kwa sasa tunao mabalozi tunaowaandaa.  Kauli Mbiu “Nourish to Flourish Lisha Mwili, Kuza Maisha.” Lengo kuu ni kuhamasisha ulaji wa chakula bora, kuboresha usalama wa chakula majumbani, na kukuza tabia njema za lishe kwa watu binafsi na jamii. Tunalenga kuwawezesha watu kupata maarifa na zana zinazowawezesha kufanya maamuzi sahihi ya lishe ili kuishi maisha yenye afya na ustawi. Malengo (Objectives) Kuelimisha na kuhamasisha kuhusu ulaji bora wa chakula. Kuboresha usalama wa chakula majumbani kwa kutoa rasilimali na msaada. Kukuza tabia njema za lishe kwa watu binafsi na jamii. Kutoa jukwaa la fursa halisi za ajira katika sekta ya kilimo na afya. Kutoa nafasi za matangazo kwa biashara zinazohusiana. Dira (Vision) Dunia ambayo watu na jamii wanapata chakula chenye lishe, elim...

SENDIGA AZINDUA MRADI WA USAMBAZAJI NA UUZAJI WA MAJIKO BANIFU KWA BEI YA RUZUKU MANYARA.

Picha
 *Majiko banifu 7,914 kusambazwa na kuuzwa kwa bei ya ruzuku, Jiko moja kuuzwa kwa bei ya ruzuku ya TZS 11,200.  Na Mwandishi Wetu, Manyara. MKUU wa Mkoa wa Manyara, Mheshimiwa Queen Sendiga, leo Novemba 10, 2025 amezindua rasmi mradi wa uuzaji na usambazaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku mkoani Manyara. Uzinduzi huu ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa upatikanaji na uhamasisha wa matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia. Aidha,uzinduzi huu umefanyika katika Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Manyara iliyopo wilaya ya Babati, ambapo jumla ya majiko banifu  7,914 yatauzwa na kusambazwa kwa bei ya ruzuku ya kiasi cha  TZS 11,200 ambayo ni sawa na aslimia 80 ya ruzuku ya TZS 56,000 ambayo ni bei ya awali ya jiko. Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mheshimiwa Sendiga amesema mpango huo umelenga kuhakikisha wananchi wote, hususani wa kipato cha chini, wanapata fursa ya kutumia nishati safi na salama ya kupikia kwa gharama nafuu. Aidha, amewaagiza Wakuu wa Wilaya...

SERENGETI BOYS YAWASILI ADDIS ABABA

Picha
  Timu ya Taifa U17 (Serengeti Boys) imewasili Addis Ababa, Ethiopia kwenye mashindano ya kufuzu AFCON 2026 Kanda ya CECAFA. @serengetiboystz

MWENYEKITI WA KAMATI YA USALAMA BARABARANI MKOA WA TABORA AKABIDHI GARI KWA JESHI LA POLISI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Tabora. Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Barabarani Mkoa wa Tabora, Bw. Hamud Nasor,  leo Novemba 10, 2025 amekabidhi  gari aina ya Toyota Probox kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Richard Abwao kwa ajili ya matumizi ya kikosi cha usalama barabarani.

UTPC YAOMBOLEZA VIFO VYA WANANCHI WALIOPOTEZA MAISHA SIKU YA UCHAGUZI OCTOBA, 29,2025.

Picha
 

BABA LEVO KUTUMIA MABANGO YA KAMPENI KUTENGENEZA MEZA ZA WAFANYABIASHARA KIGOMA MJINI

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Dodoma. MBUNGE wa Kigoma Mjini Mheshimiwa Clayton Revocatus Chipando anayejulikana kwa jina la Baba Levo ameonyesha mfano wa ubunifu na uwajibikaji kwa kutumia mabango 80000 ya kampeni yaliyosalia baada ya uchaguzi kutengeneza meza zitakazotolewa bure kwa wafanyabiashara wadogo katika masoko ya Kigoma Mjini. Akizungumza na waandishi wa habari mbunge huyo Baba Levo amesema hatua hiyo inalenga kuboresha mazingira ya wafanyabiashara na kuonyesha kwamba hata vifaa vilivyotumika kisiasa vinaweza kuwa na faida kijamii endapo vitatumiwa kwa ubunifu. Amesema badala ya mabango ya kampeni kubaki yakiharibu mazingira wameamua kuyageuza kuwa meza imara kwa ajili ya wafanyabiashara wa Kigoma ni njia ya kugeuza alama za siasa kuwa alama za maendeleo. Meza hizo zitatolewa rasmi wiki ijayo katika mkutano mkubwa wa shukurani utakaofanyika Kigoma Mjini ambapo Baba Levo atawashukuru wananchi kwa imani waliyoonyesha kwake na kueleza mwelekeo wa uongozi wake mpya. "Mpango wa kutu...