Machapisho

SHULE 6 MPYA ZAJENGWA NA MRADI WA SEQUIP IRAMBA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Iramba, Singida.  SERIKALI kupitia mradi wa Kuboresha Ubora wa Elimu ya Sekondari (SEQUIP) imetumia Bilioni 6.361 kujenga Shule mpya sita za Sekondari, Shule sita zimefanyiwa ujenzi wa upanuzi wa miundombinu ya kidato cha 5 na 6, Ujenzi wa vyoo na nyumba za walimu katika Wilaya ya Iramba Mkoani Singida. Akitoa taarifa ya miradi ya elimu iliyojengwa katika wilaya ya Iramba, Mkuu wa wilaya ya Iramba Mhe. Suleiman Mwenda amesema kuwa ujenzi wa shule hizo utaimarisha sekta ya elimu ikiwemo kuongeza ufaulu wa wanafunzi. Amezitaja shule hizo zilizojengwa wilayani hapo kuwa ni pamoja na ujenzi wa Shule ya Sekondari -MALUGA uliogharimu shilingi milioni 470, ujenzi wa shule ya Sekondari NDULUNGU uliogharimu shilingi milioni 470, ujenzi wa shule ya Sekondari -Mtoa darajani uliogharimu shilingi milioni 544.225. Miradi mingine mipya ni pamoja na ujenzi wa shule ya sekondari -Makunda uliogharimu shilingi milioni 544.225, ujenzi wa shule ya Sekondari-KIZEGA uliogharimu shilin...

HAKI ZA MWANDISHI WA HABARI WAKATI WA UCHAGUZI.

Picha
 

KAMATI YA UKAGUZI TARURA YATEMBELEA MIRADU MINNE YA BARABARA SHINYANGA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Shinyanga.  IKIWA katika muendelezo wa ziara yake ya kutembelea utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa miundombinu ya barabara, Kamati ya Ukaguzi ya TARURA  imetembelea Miradi minne ya ujenzi wa miundombinu ya barabara mkoani Shinyanga.  Katika Manispaa ya Shinyanga Kamati ilitembelea ujenzi wa barabara ya Old Shinyanga-Chibe-Negezi kiwango cha changarawe  na ujenzi wa Kalavati na daraja la Mawe la Nin'ghwa katika barabara hiyo.  Vile vile kamati hiyo ilipata fursa ya kutembelea mradi wa ujenzi wa barabara ya Kinyata-Karena yenye urefu wa Km 0.8 kwa kiwango cha lami inayojengwa Kata ya Kambarage katika Manispaa hiyo.  Pia, Kamati imetembelea Mradi wa uondoaji vikwazo wa ujenzi wa Daraja la seli sita linalojengwa katika barabara ya Magonzo-Shinyanga unaotekelezwa chini Mradi wa  RISE pamoja na mradi wa ujenzi wa barabara ya DED-DC Km 1.0 kwa kiwango cha lami Wilayani Kishapu.  Akielezea manufaa ya Miradi hiyo kiuchumi na kijamii, Men...

MGAWANYO WA MINARA YA MAWASILIANO YA SIMU.

Picha
HADI kufikia Juni 2025, idadi ya minara ya huduma ya mawasiliano ya simu ilikuwa ni 9,448. Mkoa wa Dar es Salaam unaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya minara 1,222. Mikoa mingine ni Morogoro yenye minara 501, Dodoma minara 479, Mwanza yenye minara 453, na Tanga minara 434. Mgawanyo wa idadi ya minara kwa kila mkoa imeoneshwa kwenye ramani 1.6. Tembelea tovuti ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) (www.tcra.go.tz), au kupitia kiunganisho https://bit.ly/44tXbii ilikupitia ripoti kamili ya takwimu ya sekta ya Mawasiliano (Aprili - Juni 2025).  

TAARIFA YA KUKOSEKANA KWA HUDUMA YA UMEME MKOA WA ARUSHA

Picha
 

MBOSO ATOA MSAADA KWA WATOTO YATIMA ILEMELA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Ilemela - Mwanza.  MSANI wa kizazi kipya Mbwana Yusuph Kilungi (Mbosso) amefika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe Amir Mkalipa kwa ajili ya kujitambulisha na pia kufanya tendo la hisani kwa kutoa msaada kwa kituo cha Hisani ambacho kinahudumia watoto yatima na wenye mahitaji maalum kilichopo wilayani hapa Mhe Mkalipa akimkaribisha msanii huyo, alitumia wasaa huo kumueleza fursa mbalimbali zilizopo wilayani hapa lakini pia kumshauri juu ya kuwekeza kwani wakati ni sasa. Mbisso akiwa katika kituo cha hisani ameweza kula chakula cha mchana na watoto hao na ametoa misaada mbalimbali ikiwemo magodoro, chakula, vyandarua n.k, lakini pia ameahidi kuchangia bima ya afya ya watoto hao.

DKT.MWINYI ASHIRIKI MKUTANO MKUU MAALUM WA CCM TAIFA

Picha
   MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar , Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali Mwinyi ameshiriki Mkutano Mkuu Maalum wa CCM ulioongozwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa, na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan kwa njia ya kidijitali ambapo ameongea na Wajumbe wa Mkutano huo Nchi nzima kwa njia ya Mtandao leo tarehe 26, Julai 2025 katika ukumbi wa Mkutano wa NEC(White House) Makao Makuu ya CCM Jijini Dodoma.

RC PAUL CHACHA KUHAMASISHA WANANCHI KUJITOKEZA KATIKA UCHAGUZI MKUU OCTOBA, 2025.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Uyui - Tabora.  MKUU wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha amemuahidi Mkimbiza Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2025, Ismail Ussi kuendelea kuwahamasisha wananchi washiriki uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na  Madiwani unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu. Chacha ametoa wito huo wakati wa mapokezi na makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru 2025 yaliofanyika katika viwanja vya shule ya sekondari Tura wilayani Uyui mkoani hapa. Amedokeza Mwenge wa Uhuru unatembelea, kuzindua na kuweka mawe ya msingi katika miradi mbalimbali ya maendeleo 57 yenye thamani ya sh. 38.8 bilioni. Kwa upande wa Mkimbiza Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2025, Ismail Ussi aliahidi kulinda heshima ya wananchi wa mkoa huo huku akiwashukuru na kuwapongeza wananchi kwa kujitokeza kwa wingi katika mapokezi na makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru.

MRADI WA SEQUIP KUMKOMBOA MTOTO WA KIKE DAR ES SALAAM NA RUVUMA.

Picha
Na Mwandishi Wetu.  SERIKALI inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kupitia Mradi wa kuboresha elimu ya sekondari-SEQUIP imekamilisha ujenzi wa miundombinu mbalimbali katika shule mpya za Sekondari za wasichana Dar es salaam na Ruvuma. Pamoja na dhamira hiyo ya serikali ya kuboresha sekta ya elimu kwa kuwekeza na kufanya ujenzi na ukarabati wa miundombinu kwenye shule na vyuo, pia ikiwajengea Walimu uwezo wa kiutendaji kupitia mafunzo yanayoendelea kutolewa kupitia mradi wa kuimarisha Shule Salama za Sekondari (SEQUIP). Katika kutimiza azma ya kuboresha sekta ya elimu nchini, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia inatekeleza mradi huo wa SEQUIP kwa thamani ya Dola za Kimarekani Milioni 500 ambazo ni sawa na shilingi Bilioni 1.2 kwa kipindi cha miaka mitano. Tangu kuanza kwa mradi huo mwaka wa fedha wa 2021/2022, Serikali imejenga shule mpya za sekondari na kufanya ukarabati mkubwa wa miundombinu pamoja na kutoa mafunzo ya kujenga u...

KIWANGO CHA UFAULU MKOANI SINGIDA KUONGEZWA NA MIRADI YA SEQUIP.

Picha
Na Mwandishi Wetu.  WANANCHI wametakiwa kushirikiana na serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kulimda miundombinu ya shule iliyojengwa ili kuongeza ufaulu wa wanafunzi mkoani Singida. Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Halima Dendego wakati akizungumzia tathmini na hali ya elimu leo tarehe 25 Julai 2025 ambapo amesema kuwa uongozi wa mkoa huo umejipanga kuimarisha sekta ya elimu kufuatia maboresho makubwa yanayofanywa ikiwemo ujenzi wa shule mpya. Rc Dendego amesema kuwa jumla ya shule 30 za kata zimejengwa kupitia Mradi wa kuimarisha Ubora wa Elimu ya Sekondari nchini (SEQUIP) sambamba na ujenzi wa shule mpya 1 ya wasichana ya Solya iliyopo wilayani Manyoni na Ujenzi wa shule 2 mpya za Amali ya Kitukutu iliyojengwa wilayani Iramba pamoja na Unyambwa iliyojengwa katika Manispaa ya Singida. Ameongeza kuwa baada ya ujenzi wa shule hizo mkoa wa Singida umeongeza kiwango cha ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha nne kutoka asilimia 87 mwa...

RAIS MWINYI AWASILI JIJINI DODOMA

Picha
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt.Hussein Ali Mwinyi ameondoka Zanzibar na kuwasili Jijini Dodoma kushiriki kwenye Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa yatakayofanyika katika Uwanja wa Mnara wa Mashujaa uliopo Mji wa Serikali-Mtumba Dodoma, siku ya Ijumaa tarehe 25 Julai , 2025. Katika Uwanja wa ndege wa Dodoma, Rais Dkt.Mwinyi amepokelewa na Viongozi mbalimbali wa Serikali na Vyombo vya Ulinzi na Usalama wa Mkoa huo.

DARAJA LA MSANGI KUFUNGUA MAWASILIANO VIJIJI VYA IRAMBA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, ramba - Singida KUKAMILIKA kwa daraja la Masagi linalojengwa katika barabara ya Kibirigi-Masagi kutasaidia kuunganisha vijiji vya Kibirigi, Masagi na Tyeme katika Kata ya Mtoa, Wilaya ya Iramba mkoani Singida.  Hayo yameelezwa na Meneja wa TARURA Mkoa wa Singida Mhandisi Ibrahim Kibasa wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa Mradi huo mbele ya Kamati ya Ukaguzi ya TARURA inayofanya ziara ya Ukaguzi wa miradi ya ujenzi wa Miundombinu ya barabara mkoani humo. "Vijiji vya Kibirigi, Masagi na Tyeme vinajishughulisha na shughuli za kilimo hususani pamba, alizeti, dengu, mahindi pamoja na ufugaji, hivyo kukosekana kwa daraja katika Mto sekenke linapojengwa daraja hilo ilikuwa ni kikwazo kwao katika kuyafikia masoko ya mazao yao na kurudisha nyuma jitihada za kujiletea maendeleo". amefafanua Mhandisi Kibasa.  Kwa mujibu wa Mhandisi Kibasa kukamilika kwa Mradi huo utachochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika vijiji hivyo na kuchangia ustawi wa maendeleo ya Wi...