Machapisho

WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI SHULE YA AMALI MKOANI RUKWA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Rukwa.  WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Jumatatu, Machi 9, 2026 ameweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Amali ya Mkoa wa Rukwa iliyopo katika Kata ya Majengo, Namanyere, Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa. Mradi huo unatekelezwa kupitia Programu ya Kuboresha Ubora wa Elimu ya Sekondari (SEQUIP) kwa gharama ya shilingi bilioni 1.6 na unalenga kuboresha elimu ya ufundi stadi kwa kuwaandaa wanafunzi kupata ujuzi utakaowawezesha kujiajiri na kuchangia maendeleo ya kiuchumi ya Taifa. Mradi huo ulianza kutekelezwa Desemba 20, 2024 na ulitarajiwa kukamilika Machi 30 2025, ambapo hadi sasa jumla ya shilingi bilioni 1.5 zimetumika katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za ujenzi wa miundombinu ya shule hiyo. Kwa mujibu wa taarifa ya mradi, hadi sasa ujenzi wa madarasa nane pamoja na jengo la utawala umekamilika na miundombinu hiyo tayari inatumika. Pia ujenzi wa jengo la TEHAMA na maktaba, nyumba ya mtumishi pamoja na vyoo vya wavulana na w...

DKT. MWIGULU: WANAFUNZI WATAKAOFAULU VIZURI KUSOMESHWA NJE YA NCHI KUPITIA SAMIA SCHOLARSHIP

Picha
  Awafikishia wanafunzi salamu za Rais Dkt. Samia; asema Serikali inaendelea kuwekeza katika elimu Na Mwandishi Wetu, Rukwa.  WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema wanafunzi watakaofaulu kwa viwango vya juu watanufaika na ufadhili wa masomo kupitia mpango wa Samia Scholarship unaotolewa na Serikali. Dkt. Mwigulu amesema hayo wakati akizungumza na wanafunzi katika ziara yake mkoani Rukwa, ambapo pia aliwasilisha salamu maalum kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan. “Daktari Samia Suluhu Hassan anasema kwa wale watakaofaulu kwa kiwango cha juu wanapata ufadhili asilimia 100. Na sio ufadhili tu wa asilimia 100 peke yake, asilimia 100 na unaenda kusoma nchi yoyote duniani… hiyo inaitwa Samia Scholarship,” alisema Waziri Mkuu. Aidha, alisema Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kuwekeza kwa kiasi kikubwa katika sekta ya elimu ambapo zaidi ya shule za sekondari 1,300, shule za msingi zaidi ya 2,700 pamoja na maelfu ya madarasa yamejengwa ka...

DKT. MWAMBA: TUMIENI JUKWAA LA WANAWAKE NA KODI KUTOA ELIMU

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam.  KATIBU Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba amewataka Wanawake wa Mamlaka ya Mapato Tanzania kutumia Jukwaa la Wanawake na Kodi lililozinduliwa  hivi karibuni kuelimisha wajasiriamali wanawake kuhusu umuhimu wa kujisajili, kuwasilisha taarifa sahihi na kulipa kodi kwa wakati. Dkt. Mwamba ametoa wito huo wakati akizungumza na wanawake wa TRA,  katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam. Sherehe hizo zilihudhuriwa na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Yusuph Juma Mwenda, Naibu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Bw. Mcha Hassan Mcha, Kaimu Mkurugenzi Usimamizi Rasilimali watu na Utalawa Bw. Nahoda Pandu Nahoda.

PROF. KABUDI AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA 26 WA MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE WA JUMUIYA YA MADOLA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, London.  WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalum), Prof. Palamagamba J. Kabudi, ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 26 wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jumuiya ya Madola (CFAMM) uliofanyika Machi 8, 2026 jijini London, Uingereza akimwakilisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb). Akichangia mjadala, Prof. Kabudi amesema Jumuiya ya Madola inapaswa kubaki kuwa jukwaa muhimu la kushughulikia changamoto za maendeleo na kuimarisha ushirikiano wa kimataifa (multilateralism) katika kipindi cha sasa chenye changamoto za kisiasa, kiuchumi na kimazingira. Katika masuala ya uchumi, Prof. Kabudi amesisitiza umuhimu wa kuimarisha biashara na uwekezaji kati ya nchi wanachama kwa kujifunza kutoka mifano ya ushirikiano wa kikanda kama Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA). Amesema jukwaa la biashara na uwekezaji la Jumuiya ya Madola litasaidia kupunguza vikwazo vya biashara na kuongeza biashara kati ya ...

e-GA YATOA MSAADA KWA WATOTO WENYE UHUTAJI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Pwani.  KATIKA kuadhimisha kilele cha Siku ya Wanawake Duniani, inayoadhimishwa kila mwaka Machi 8, wanawake wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) wametoa msaada wa mifuko 50 ya saruji, matofali 1,000 pamoja na mahitaji mbalimbali ya watoto katika Kituo cha kulea watoto yatima na waliofanyiwa ukatili cha Shalom kilichopo Kidenge B, Kata ya Msangani, Halmashauri ya Mji wa Kibaha, mkoani Pwani Machi 6, 2026. Akizungumza jana wakati wa kukabidhi msaada huo, Meneja wa Udhibiti na Viwango wa Mamlaka hiyo Bi. Sultana Seiff, alisema kuwa wanawake wa e-GA wameamua kusherehekea siku hiyo kwa kuwafikia watoto wanaohitaji msaada katika jamii na kukichagua kituo hicho ikiwa kama sehemu ya kurudisha kwa jamii. Meneja huyo alisema kuwa baada ya kuwasiliana na kituo hicho na kupata changamoto mbalimbali zinazohitaji kutatuliwa katika kituo hicho ikiwemo ujenzi wa uzio ili kuhakikisha Watoto hao wanakua salama waliamua kuchangia vifaa vya ujenzi pamoja na mahitaji mengine muhimu...

WANAWAKE TANTRADE WASHEREKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI SAMBAMBA NA MIAKA 50 YA DHAHABU YA SABASABA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam.  MAMLAKA ya Maendeleo ya Biashara ya Tanzania (TanTrade) imeungana na Wanawake wote Duniani katika kusheherekea Siku ya Wanawake. Akiongea katika maadhimisho hayo Mkurugenzi Mkuu TanTrade Dkt.Latifa Mohamed Khamis amesema "Leo, tunatambua mchango mkubwa wa wanawake katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Tunawapongeza wanawake wote kwa uongozi wao, uvumilivu, na kujitolea katika kuendeleza jamii zetu." TanTrade pia imetumia maadhimisho haya kuwakaribisha Wadau wote wa biashara kushiriki kwenye Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam - Sabasaba ya Jubilei ya Dhahabu ya 50. Ambapo watapata fursa za masoko mapya, teknolojia ya kisasa, na mtandao mpana wa kibiashara. Maadhimisho hayo yamefanyika Mburahati, Wilaya ya Ubungo, jijini Dar es Salaam.

MBUNGE AGNESS AWAFIKIA WANAWAKE WA KIKRISTO KWA KUWASHIKA MKONO

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mara.  MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Agnes Marwa, ameungana na wanawake wa mashirika ya Kikristo katika Musoma kuadhimisha International Women's Day kwa shangwe na mshikamano mkubwa. Katika maadhimisho hayo yaliyowakutanisha wanawake wa Christian Council of Tanzania (CCT) pamoja na WAWATA wa Manispaa ya Musoma, Mheshimiwa Mbunge alitoa pongezi kwa wanawake kwa mchango wao mkubwa katika kuimarisha maadili ya jamii, familia na maendeleo ya Taifa. Akizungumza katika sherehe hizo, Mheshimiwa Agnes Marwa aliwahimiza wanawake kuendelea kushikamana, kujiamini na kutumia fursa mbalimbali za maendeleo ili kujiletea ustawi wao na jamii kwa ujumla. Katika kuonesha dhamira yake ya dhati ya kuunga mkono shughuli za wanawake na taasisi za kijamii, Mheshimiwa Mbunge alitoa mchango wa shilingi milioni 2 na laki 4 (Tsh 2,400,000) kwa ajili ya ununuzi wa tent, hatua itakayosaidia kuimarisha uendeshaji wa shughuli mbalimbali za kijamii na kiroho katika Manis...

MJOMBA MATATANI KWA KUMPIGA NA KUMNING'INIZA MTOTO DIRISHAJI KWA KUUNGUZA MBOGA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  JESHI la Polisi nchini Tanzania linamshikilia Joseph Mbalamwezi Francis Mkazi wa Mtaa wa Imalamakoe B, Wilayani Urambo, Mkoani Tabora kwa tuhuma za kumfanyia mtoto ukatili wa kufungwa kamba miguuni na mikononi na kisha kumning'iniza dirishani. Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania Naibu Kamishna wa Polisi DCP David Misime ameviambia Vyombo vya habari leo Jumatano  Machi 04, 2026 kuwa tukio hilo lilitokea Machi 02, 2026 na mtoto aliyekuwa anafanyiwa ukatili huo ana umri wa miaka 10 na kwamba mtuhumiwa ni Mjomba wake ambaye walikuwa wakiishi pamoja. "Sababu za kumfanyia ukatili huo wa kupigwa na kisha kuning'inizwa inadaiwa ni baada ya mtoto huyo kuunguza mboga (nyama) aliyokuwa anapika." Amesema Kamanda Misime. Jeshi la Polisi pia limewashukuru waliotoa taarifa za tukio hilo na kufanikisha mtoto huyo kuokolewa na kwenda kupatiwa matibabu na mtuhumiwa kukamatwa, Polisi ikisisitiza ushirikiano zaidi katika kuwalinda na kuzuia vitendo vya ukatili...

MHE MBUNGE WA VITI MAALUM MKOA MARA AGNESS MARWA AGAWA VIFAA VYA SALOON.

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mara.  KATIKA kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuwawezesha vijana,Mbunge wa viti maalumu mkoa wa mara Mhe, Agness Marwa amegawa vitendea kazi vya saloon za kike na kiume Kwa vijana zaidi 30 katika manispaa ya Musoma mkoa wa Mara. Dhamira hiyo ni kuwawezesha vijana kujikwamua kiuchumi na kuunga mkono serikali katika kuwawezesha wajasiriamali wadogo. Akizungumza katika kikao cha wajasiliamali  kilichofanyika Manispaa ya Musoma, Mbunge Agnes amesema ataendelea kuyafukia makundi mablimabli wakiwemo wajasiliamali Mali wote katika mkoa wa mara. Mhe. Agnes amesema azma hiyo ni kuunga mkono jitihada za mheshimiwa rais Samia Suluhu Hassan zinazojikita kuwasaidia wajasiliamali wadogo wadogo katika kujikwamua kiuchumi. Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Manispaa ya Musoma Juma Chikoka amempongeza Mbunge huyo ambapo amewataka wajasiliamali hao kuvitumia vifaa hivyo Kwa Lengo lililokusudiwa ili kujiongezea kipato. Nao baadhi ya wajasiliamal...