Machapisho

WADAAWA WA KIIRAQW WAPATA NAFASI YA KUSIKILIZWA KWA LUGHA YAO, BARAZA LA ARDHI DODOMA LATOA TUMAINI LA HAKI SAWA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  BARAZA la Ardhi na Nyumba la Wilaya, Mkoa wa Dodoma limewasikiliza wananchi wa jamii ya Kiiraqw waliofika katika Baraza hilo kuwasilisha hoja na ushahidi wao katika mgogoro wa ardhi, wakidai kumiliki kihalali shamba lenye ukubwa wa ekari nane lililopo Wilaya ya Chamwino, Mkoa wa Dodoma. Hatua hiyo imekuja kufuatia maombi ya wadaawa hao ambao ni pande mbili zinazohusika katika shauri hilo, kubainisha kuwa wanakabiliwa na changamoto ya lugha, hali iliyokuwa ikiathiri uwezo wao wa kujitetea na kueleza kwa uwazi hoja zao mbele ya Mwenyekiti wa Baraza hilo, Mhe. Omary Mbega. Kutokana na hilo, Baraza lilitoa huduma ya ukalimani kupitia mkalimani, Ndg. Simon Tlatlaa Emmay, ambaye alitafsiri maelezo yao na kuwawezesha wadaawa hao kufafanua kwa kina madai yao, kuwasilisha ushahidi pamoja na vielelezo muhimu bila kikwazo cha lugha. Shauri hilo ni Shauri la Ardhi Na. 92 la mwaka 2025, linalomhusu Ekaristi Ngu’nda kama Mleta Maombi dhidi ya Lolote Nanacha na ...

VIJANA MWANZA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZINAZOTOLEWA NA HALMASHAURI.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Mwanza.  RAI hiyo imetolewa leo Februari 27, 2026 na Mkuu wa Wilaya ya Magu,Jubilate Lawuo wakati akifungua maadhimisho,Elimu na uzinduzi wa mitambo katika teknolojia ya ukandarasi wa madini ambapo madhimisho hayo yamefanyika katika viwanja vya Nyamhongolo jijini mwanza.  Lawuo amesema mikopo ya Halmashauri inasaidia sana vijana katika kujiajiri kwa mtu mmoja , mmoja au vikundi. " Serikali yetu imeweka mazingira mazuri kwa vijana wetu kukopeshwa kupitia vikundi vyao. Pia na Halmashauri zetu zinajitaid sana katika kusaidia vijana wetu" alisema. Vile vile, Lawuo ameagiza  vijana waweze kujitokeza kwa wingi katika maonyesho ya wakandarasi ili waweze kuona mitambo mbalimbali ya uchimbaji na ukandarasi inayopatikana. Ameongeza kuwa mkoa wa Mwanza katika wilaya za Kwimba na Sengerema kuna migodi mbalimbali iliyoajiri vijana wa kitanzania wanaojihusisha na uchimbaji wa madini. Naye Mwenyekiti wa maonyesho ya wakandarasi na wachimbaji, George Mandia alisema mao...

TUITUNZE AMANI KWA UHAKIKA WA KUPATA HAKI MSINGI NA MAHITAJI MUHIMU- BI. MBEGU

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam.  WAKAZI wa Dar Es Salaam wameeleza umuhimu wa amani nchini, Watanzania wakitakiwa kujifunza kutoka kwa mataifa yasiyokuwa na amani namna ambavyo wamekuwa wakipitia changamoto kubwa za kiuchumi na kijamii. Akizungumza na waandishi wa habari, Bi Amina Mbegu Rashid, Mkazi wa Dar Es salaam, ameeleza amani ndio msingi wa uhuru wa wananchi kufanya shughuli zao, akisema amani pia imesababisha Taifa kupiga hatua kubwa za maendeleo ambapo bila amani huenda Taifa lisingeshuhudia maendeleo na ustawi uliopo sasa katika nyanja mbalimbali ikiwemo upatikanaji wa haki za binadamu. "Amani kwenye Taifa letu ni muhimu sana, imetupa nafasi na uhuru wa kufanya mambo yetu bila shuruti. Kwenye nchi za wenzetu kuna shida nyingi sana ambapo hata kutembea tu imekuwa changamoto, hapa kwetu hakuna mwenye viroba 20 ama 30 ndani vya chakula kwahiyo amani ikitoweka unaweza kuona changamoto ambayo tutaipitia hasa katika upatikanaji wa huduma muhimu ikiwemo za matibabu kwah...

AMANI YATAJWA KAMA FURSA MUHIMU YA WANANCHI KUJIENDELEZA KIUCHUMI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam.  BWANA Rashid Kengwa Rashid Mkazi wa Ilala Mkoani Dar Es Salaam amesema kukosekana kwa amani katika jamii kunakwamisha maendeleo na ustawi wa wananchi pamoja na kutatiza uhuru wa wananchi kufanya shughuli zao za kijamii na kiuchumi, msisitizo akiutoa kwa kila mwananchi kuwajibika kuilinda na kukataa vitendo vyenye kuhatarisha amani na usalama wa Tanzania. "Suala la amani ni jambo la kushukuru kwasababu lipo kwa kiasi kikubwa sana na pasingekuwa na amani hata hapa nisingezungumza nanyi, tungekuwa ni watu wa kujificha tu na tumshukuru Mungu sana kwa amani hii aliyoendelea kutupatia." Amesema Bw. Rashid. Rashid ameeleza pia tofauti ya Tanzania na mataifa mengine yasiyokuwa na utulivu na amani, akisema kukosekana kwa amani kumesababisha madhila makubwa kwa watu wengi ikiwemo vifo, kuongezeka kwa umaskini pamoja na kukosekana kwa uhuru na hivyo kuua fursa za raia kujiendeleza kiuchumi pamoja na kuishi katika wasiwasi na hofu.

NUKUU KUTOKA UN.

Picha
WAKATI dunia inaendelea kutumia fedha nyingi zaidi kwenye silaha na maandalizi ya vita, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anakumbusha kwamba, usalama wa kweli haujengwi kwa silaha, bali kwa imani, mazungumzo na utu wa binadamu. "Kupunguza silaha si jambo la kusubiri hadi amani ipatikane. Ni hatua ya kuzuia vita kabla havijaanza. Ni njia ya kujenga uaminifu kati ya mataifa. Ni kulinda maisha na mustakabali wa dunia yetu."  Sanamu ya Bunduki Iliyofungwa Fundo kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York City inaendelea kuwa ukumbusho kwamba amani huanza pale vurugu zinapokoma. #UN #habarikamilitv #USA #IRAN #URUSI # CHINA

SERIKALI YA RAIS SAMIA YATANGAZA KUNUNUA NDEGE MPYA NANE KWA MWAKA HUU

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam.  MSEMAJI Mkuu wa serikali ya Tanzania Bw. Gerson Msigwa leo Alhamisi Februari 26, 2026 amewaambia waandishi wa habari Mjini Dar Es Salaam kuwa serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan, kwa mwaka huu imepanga kununua ndege mpya nne kati ya nane walizopanga kununua ili kuongeza fursa kwa watanzania katika masoko ya kikanda na Kimataifa pamoja na kusisimua uchumi na Utalii wa Tanzania kama ilivyoahidiwa katika Kampeni za uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025. Akizungumza na waandishi wa habari kwenye Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere Dar Es Salaam, Msigwa amesema  ndege zitakazonunuliwa ni aina ya Bombardier Q400 kama sehemu ya utekelezaji wa mpango wa serikali katika kuimarisha mtandao wa huduma za usafiri wa anga ili kuwa kichocheo muhimu cha Utalii, biashara na usafiri. "Mimi nipo hapa kuwahakikishia kwamba katika lengo hili tumepata mafanikio makubwa, shirika letu sasa hivi tumepata mafanikio makubwa ambapo tumeanza kutajwa kama Shirika...

SERIKALI YATENGA BILIONI 5 KUFADHILI UZAMIVI DATA SCIENCE NA AI KUPITIA SAMIA SCHOLARSHIP

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  Serikali imetenga Shilingi bilioni 5 kufadhili wanafunzi 20 wa Shahada ya Uzamili katika fani za Sayansi Takwimu (Data Science), Akili Unde (Artificial Intelligence) na Sayansi Shirikishi kupitia mpango wa Samia Scholarship Extended (SSE DS/AI+), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa taifa kuimarisha rasilimali watu katika teknolojia za kisasa. Wanafunzi 10 tayari wameanza masomo yao katika Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST), huku wengine 10 wakitarajiwa kuanza katika Indian Institute of Technology Zanzibar. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, alisema mpango huo maalum wa ufadhili wa uzamili umeanzishwa kwa kuzingatia mahitaji makubwa ya taifa katika maeneo ya teknolojia, ubunifu na uchambuzi wa takwimu. “Vyuo tunavyopeleka wanafunzi wa Samia Scholarship AI/DS+ vinatoa fursa ya mafunzo kwa vitendo katika makampuni makubwa ya teknolojia na vinaendelea kud...

MGODI WA ITRACOM WACHANGIA SHILINGI BILIONI 1.29 MAPATO YA SERIKALI MANYARA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Manyara.  MGODI wa Itracom Fertilizer Limited unaojihusisha na uchimbaji na uchakataji wa madini ya phosphate uliopo  katika eneo la Vilima Vitatu, Wilayani Babati mkoani Manyara, umechangia Shilingi Bilioni 1.29 katika mapato ya Serikali tangu kuanza kwa shughuli zake mwaka 2023. Hayo yamebainishwa na Mjiolojia, Waziri Mkupe, akizungumza kwa niaba ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Manyara, Godfrey Nyanda, ambapo amesema mapato hayo yametokana na mrabaha na ada ya ukaguzi wa madini. Amesema tangu kuanza kwa uzalishaji, mgodi huo umezalisha jumla ya tani 69,929 za madini ya phosphate zenye thamani ya Shilingi Bilioni 36.99, ambazo zimeuzwa katika soko la ndani na nje ya nchi, hususan Nala mkoani Dodoma na nchini Burundi. Kwa mujibu wa Mkupe, mchango huo umeimarisha ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali na kuchochea maendeleo ya jamii inayozunguka mgodi kupitia utekelezaji wa miradi ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR). Ameeleza kuwa tangu kuanza kwa shughuli zak...

MANISPAA TABORA YATOA TUZO KWA WADAU WA MAENDELEO

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora HALMASHAURI ya Manispaa Tabora imetoa tuzo maalumu kwa wadau zaidi ya 10 ambao wamekuwa mstari wa mbele kuunga mkono juhudi za maendeleo zinazofanywa na halmashauri hiyo ikiwemo kuchangia shughuli za kitaifa. Akikabidhi tuzo hizo jana kwenye kikao cha madiwani Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa hiyo Ghullam Hussein Remtullah amempongeza Mkurugenzi Mtendaji Dkt John Pima kwa kuandaa tuzo hizo. Ameeleza kuwa tuzo hizo ni muhimu sana kwa kuwa zinadumisha ushirikiano na mahusiano mazuri na wananchi wanaojitolea kuchangia shughuli za maendeleo ikiwemo matukio makubwa ya kitaifa yanayofanyika katika manispaa hiyo. ‘Hawa tunaowapa tuzo leo ni wakulima, wafanyabiashara na wafugaji ambao wamekuwa wakijitolea kwa hali na mali kuishika mkono halmashauri ili kufanikisha mambo mbalimbali, walitoa chakula, fedha na mifugo’, amesema. Mstahiki Meya amebainisha kuwa manispaa inatambua na kuthamini mchango wao ndiyo maana leo wamekabidhiwa tuzo hizo, aliwaomba kuendele...

MALALAMIKO YA VIWANJA MBADALA YAPATIWA UFUMBUZI DODOMA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  SERIKALI kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeyapatia ufumbuzi malalamiko ya muda mrefu ya viwanja mbadala kwa wananchi wa jiji la Dodoma. Suluhisho hilo linafuatia malalamiko ya takriban wananchi 4000 wa jiji la Dodoma wanaodai viwanja na halmashauri ya jiji la Dodoma kuwapa ahadi bila kutekeleza mpaka sasa. Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 25 Februari 2026 na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo wakati akizungumza na wananchi wenye migogoro ya ardhi katika eneo la Mahomanyika lilopo kata ya Nzuguni jijini Dodoma. Dkt Akwilapo amesema, eneo la Mahomanyika ni eneo la serikali hivyo lipangwe na kupimwa kwa ajili ya utatuzi wa migogoro ya meneo mbalimbali ya jiji la Dodoma pamoja na matumizi ya serikali. "Eneo hili lenye mgogoro hapa Mahomanyika ni eneo la serikali hivyo lipangwe na kupimwa kwa ajili ya utatuzi wa migogoro na siyo ya hapa tu na mingine ya jiji la Dodoma na matumizi ya serikali...

TAKUKURU MKOA WA MWANZA IMEFANIKIWA KUDHIBITI KIASI CHA TZS MILIONI 85.5

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mwanza.  TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mwanza imefanikiwa kudhibiti kiasi cha Sh milioni 85.5 kupitia uchambuzi wa mfumo wa malipo ya fedha za kujikimu kwa walimu wa shule za sekondari katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza. Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mwanza, Abnery Mganga, amesema kuwa katika utekelezaji wa majukumu ya kuzuia rushwa, taasisi hiyo ilifanikiwa kudhibiti kiasi hicho cha Sh milioni 85.5 na kuhakikisha kinalipwa kwa walimu waajiriwa wapya wa shule za sekondari waliokuwa na madai katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza. Aidha, Mganga amesema mafanikio hayo yametokana na uchambuzi wa mfumo uliofanywa na taasisi hiyo pamoja na halmashauri kutekeleza mapendekezo yaliyotolewa katika kikao kazi kati ya TAKUKURU na wadau wa halmashauri. Hatua hiyo imewawezesha walimu 77 waliokuwa na madai kulipwa stahiki zao.

CCM: MAKAMPUNI YASIYOLIPA WAKULIMA YAPIGWE ‘STOP’

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeitaka Bodi ya Tumbaku (TTB) nchini kuchukua hatua mara moja dhidi ya Makampuni yote yanayonunua zao la tumbaku na kushindwa kulipa wakulima kwa wakati, na kushauri wapigwe stop. Ushauri huo umetolewa jana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tabora Komredi Saidi Nkumba alipokuwa akitoa salamu za chama katika Mkutano Mkuu wa 33 wa Chama Kikuu cha Ushirika wa Wakulima wa Tumbaku (WETCU) Mkoani Tabora. Amesema kuwa haingiii akilini kuona mkulima akihangaika kuandaa shamba lake mwaka mzima tena kwa gharama kubwa ili kuhakikisha anapata tumbaku nzuri inayokidhi viwango vya soko la ndani na nje lakini anapouza halipwi kwa wakati. ‘Chama Cha Mapinduzi hakifurahishwi na hali hii, Wanunuzi wote wanaokuja kununua mazao ya wakulima wanatambulika kisheria na wanapewa leseni, kama hawafanyi kile kinachotakiwa kuna haja gani ya kuwabembeleza’, ameeleza. Komredi Nkumba ameitaka Bodi ya Tumbaku kusimamia ipasavyo zao hilo ili mkulima anufaike na jasho...