Machapisho

WATENDAJI SOKO LA HISA DSE WATAKIWA KUWA WABUNIFU KUVUTIA WAWEKEZAJI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amekutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) Bw. Peter Nalitolela, mazungumzo yaliyofanyika leo tarehe 13 Februari 2026, Dodoma. Katika Mazungumzo hayo, Makamu wa Rais amewahimiza watendaji DSE kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kuwa wabunifu katika masuala ya masoko na kuendelea kuvutia uwekezaji. Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) Bw. Peter Nalitolela, ameahidi kuendelea kushirikiana vema na Serikali katika kutafuta mitaji ili kuweza kusaidia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ya kufikia uchumi wa Dola za Marekani Trilioni Moja ifikapo 2050. Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) ni taasisi ya kimkakati ya Taifa inayowezesha ukusanyaji na usimamizi wa mitaji ya muda mrefu kwa ajili ya kufadhili maendeleo ya uchumi wa Tanzania. DSE ni jukwaa rasmi linalowawezesha wawekezaji wa ndani na ...

DC SENDIGA AWATAKA WACHIMBAJI KUCHANGAMKIA BIMA YA AFYA

Picha
Na Mwandishi wetu, Mirerani.  MKUU wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga amewataka wachimbaji wa madini wa eneo hilo kuchangamkia bima ya afya kwa wote ili waweze kupatiwa huduma za matibabu pindi wakiugua.  RC Sendiga ameyasema hayo wakati akizungumza kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa chama wachimbaji cha wachimbaji madini Mkoa wa Manyara MAREMA uliofanyika kwa muda wa siku mbili Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro.  Ameeleza kwamba wachimbaji madini wa mkoa huo wanatakiwa kuchangamkia fursa hiyo ya bima ya afya kwa wote. Amesema bima ya afya kwa wote unachangia shilingi 150,000 kwa mwaka na unapatiwa huduma za afya kwa kaya ya watu sita wakiwemo baba, mama na watoto wanne.  "Wachimbaji madini mnapaswa kuchangamkia hii fursa kwani unakuwa na uhakika wa kupata matibabu wewe na familia yako pindi mkihitaji huduma na hamtapungukiwa na kitu na kununiana kutaisha," amesema RC Sendiga. Ameeleza kwamba hivi sasa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Ha...

MAREMA WAOMBA GETI LA TANZANITE KUWA WAZI SAA 24

Picha
  Na Mwandishi wetu, Mirerani.  WACHIMBAJI wa madini ya Tanzanite mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara, wameiomba serikali kuruhusu lango la kuingia na kutoka ndani ya ukuta unaozunguka migodi ya madini ya Tanzanite kuwa wazi saa 24 ili shughuli zao zifanyike vyema. Mwenyekiti wa chama cha wachimbaji madini mkoa wa Manyara, (MAREMA) Elisha Nelson Mnyawi ameyasema hayo mbele ya mkuu wa moa huo Queen Sendiga kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa chama hicho uliofanyika mji mdogo wa Mirerani.  Mnyawi ameeleza kwamba changamoto ya lango la kuingia na kutoka ndani ya ukuta kufungwa saa 5 usiku inawakwaza wachimbaji madini ya Tanzanite. Amesema endapo lango hilo likiwa wazi saa 24 kwa siku itakuwa vyema kwani shughuli za kiuchumi zitakuwa zimeboreshwa zaidi. "Tunavipongeza vyombo vya ulinzi na usalama ndani ya ukuta kwani wanafanya kazi nzuri ila wachimbaji wangepewa fursa ya lango hilo kuwa wazi saa 24 itakuwa bora zaidi kwao," amesema Mnyawi. Amesema endapo suala...

UMIKIDO WASHIRIKI MKUTANO MKUU WA MWAKA WA VYOMBO VYA UTANGAZAJI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  UMOJA wa Vyombo vya Habari vya Mitandao ya Kijamii Mkoa wa Dodoma (UMIKIDO) umeshiriki Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Vyombo vya Utangazaji nchini. Mkutano huo wa siku mbili unafanyika katika Ukumbi wa New Generation jijini Dodoma, ukianza leo Februari 12, 2026. Mkutano huo umeandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Katika mkutano huo, mada na mafunzo mbalimbali yanawasilishwa kwa waandishi wa habari pamoja na wadau wa sekta ya utangazaji.  Aidha, kunafanyika mijadala mbalimbali inayolenga kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo na uboreshaji wa vyombo vya utangazaji nchini. Mkutano huo umefunguliwa rasmi na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma.

SIKU 100 ZA RAIS SAMIA ZALETA NEEMA IGUNGA

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora.  SIKU 100 baada ya kuingia madarakani katika awamu ya pili ya uongozi wake,  Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ameleta neema kwa wakazi wa Mji wa Igunga Mkoani hapa kwa kuwawezesha kupata huduma ya maji kwa masaa 24 kila siku. Akizungumza na gazeti hili jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Igunga (IGUWASA) Alex Ntonge ameeleza kuwa kazi nzuri iliyofanywa na Mheshimiwa Rais imemaliza changamoto za huduma ya maji. Amebainisha kuwa maboresho makubwa ya miundombinu na kupanuliwa kwa mradi wa maji ya Ziwa Victoria kumewezesha wakazi wote wa Mji huo na maeneo jirani kupata huduma ya maji safi na salama wakati wote, kwa masaa 24 kila siku. ‘Kazi nzuri iliyofanywa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika siku 100 za kwanza tangu aingie Ofisini, imeleta neema, mabilioni aliyotuletea yameendelea kuboresha huduma ya maji na usafi wa mazingira Mji wote’, amesema. Mkurugenzi amefafanua kuwa zaidi ya asilimia 98 ya wakazi wote wa Mj...

GHAZALY AMPONGEZ WAZIRI MPYA WA VIJANA NA MICHEZO

Picha
Na Mwandishi Wetu, Misri.  MTAFITI wa Anthropolojia Hassan Ghazaly, Mwanzilishi wa Afromedia, mpango wa uandishi wa habari na vyombo vya habari barani Afrika, pamoja na timu ya Afromedia, wanatoa pongezi za dhati kwa Mheshimiwa Waziri Gohar Nabil kwa kuteuliwa kwake kuwa Waziri wa Vijana na Michezo, kufuatia kutolewa kwa amri ya rais na kuapishwa kwake rasmi. Katika taarifa yake, Ghazaly alieleza kuthamini kwa kina imani aliyopewa, akisisitiza kuwa hatua inayofuata inahitaji maono mapya na sera madhubuti za kuwawezesha vijana, kuendeleza vipaji vya michezo, na kuifanya michezo kuwa chombo muhimu cha maendeleo, kwa kuendana na mkakati wa taifa la Misri na dira ya Jamhuri Mpya. Ghazaly pia alibainisha umuhimu wa kuimarisha ushirikiano wa Kiafrika katika nyanja za vyombo vya habari, vijana na michezo, kwa lengo la kujenga madaraja kati ya mataifa, kuimarisha maadili ya pamoja, kugundua na kukuza vipaji vya vijana wa Afrika, kuangazia mifano chanya, kutangaza mipango ya pamoja, na kusu...

.MAIPAC YAWANOA WAANDISHI

Picha
  Na mwandishi wetu. Arusha.  TAAASI ya waandishi wa habari ya kusaidia jamii za pembezoni (MAIPAC) imetoa mafunzo kwa waandishi wa habari nchini, ya uandishi wakati wa migogoro ambao unazingatia usalama.wao na amani. Mafunzo hayo yameshirikisha waandishi wa habari kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Geita, Mara, Manyara, Mbeya na Arusha, yalidhaminiwa na shirika la wanahabari la Press Unlimited. Akifungua mafunzo hayo, Mkurugenzi wa MAIPAC, Mussa Juma aliwataka wanahabari wanaokwenda kuripoti migogoro kuzingatia kuchukuwa tahadhari za kiusalama na.kutopendelea sehemu yoyote.  Juma amesema habari za upande mmoja ambazo hazizingatii maadili na maslahi mapana ya Umma zimekuwa zikisababisha migogoro katika jamii. Hata hivyo, amewataka wanahabari wakati wote wa kazi zao kuzingatia usalama wao,kufanya upembuzi yakinifu wa habari wananayotaka kuandika kabla ya kuandika na baada ya kuandika. "Tujuwe habari ina madhara gani,inafaida gani ,tusiwe na upande katika hiyo habari na...

NDUGU WASHIKILIWA KWA KUMUUA SHEMEJI YAO 'KISA MGOGORO WA MASHAMBA'

Picha
Na Mwandishi Wetu, Mbeya.  JESHI la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia ndugu wa familia moja ambao ni Solomon Mwambyale (68) na watoto wake wawili, Stephano Mwaisango (32) na Emmanuel Mwaisango (36), kwa tuhuma za mauaji ya Jenti Segelela (87) ambaye alikuwa shemeji yake na mtuhumiwa Solomon, wakidaiwa kumkata na kitu chenye ncha kali kisogoni na kisha kukimbia, chanzo kikiwa ni mgogoro wa mashamba ya ukoo na tamaa ya kujipatia mali kwa njia isiyo halali. Katika tukio la Pili, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Benjamin Kuzaga amesema wanamshikilia Bw. Charles Oden Mwakasege (32) fundi simu Mkazi wa Meta Jijini Mbeya na Bw. Isack Charles 'Bebwa' mkazi wa Shewa, kwa tuhuma za kuingilia mfumo wa kibiashara wa makampuni ya ukopeshaji wa simu. Kulingana na Kamanda Kuzaga katika taarifa yake ya leo Jumanne Februari 10, 2026 kwa Vyombo vya habari, watuhumiwa hao walikamatwa katika msako uliofanyika kuanzia Januari 27, 2026 katika maeneo mba...

WAZIRI WA FEDHA AWAHAKIKISHIA USHIRIANO WAWEKEZAJI NCHINI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  WAZIRI wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amewaahidi wawekezaji kuwa Serikali itaendelea kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya uwekezaji nchini kwa manufaa ya pande zote mbili kutokana na manufaa ya sekta hiyo kwa uchumi wa nchi na wawekezaji. Mhe. Balozi Omar amesema hayo mjini Dodoma, alipokutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Kampuni mpya ya Uchimbaji Dhahabu Nyanzaga (Nyanzaga Mining Company Ltd), unaojengwa katika eneo la Nyanzaga Wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza ambao hadi kukamilika kwake unatarajiwa kugharimu zaidi ya dola za Marekani milioni 523. Alisema kuwa mradi huo ni mkubwa kujengwa Tanzania toka miaka zaidi ya 18 iliyopita ambapo mgodi wa Buzwagi ulijengwa. Na fursa zitaendelea hivyo kwa ukubwa wake. Lakini pia kuchangia uchumi wa nchi Kupitia kodi mbalimbali. “Ni mara yangu ya kwanza kukutana na uongozi wa mgodi wa dhahabu wa Nyanzagi na tumejadili kuhusu changamoto ya msamaha wa kodi na nimewaahidi kuwa hadi mwisho w...

NZUWASA YAONGEZA UZALISHAJI MAJI NZEGA

Picha
  Na Allan Kitwe, Nzega.  MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Nzega (NZUWASA) imeongeza mtandao wa upatikanaji huduma ya maji safi na salama kwa wakazi wa Mji wa Nzega hadi kufikia kilomita 738.3 ambazo ni sawa na asilimia 99.5 ya eneo lote. Akizungumza na gazeti hili jana Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka hiyo Mhandisi Humphrey Mwiyombela amesema kuwa takribani eneo lote la Mji wa wa Nzega kwa sasa limefikiwa na huduma ya maji safi na salama. Amebainisha kuwa mafanikio hayo yametokana na mikakati yao ya kuendelea kuzalisha maji kupitia vyanzo vyake vya ndani kwa lengo la kupanua wigo wa upatikanaji huduma hiyo katika maeneo yote ya Mji huo na maeneo jirani. Ametaja mkakati mwingine uliosaidia kuimarisha upatikanaji huduma hiyo kuwa ni kuendelea kushirikiana na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Kahama na Shinyanga (KASHWASA). Mkurugenzi amedokeza kuwa mahitaji ya maji kwa wakazi wa Mji huo kwa siku ni mita za ujazo 5,600 na kiasi kinachozalishwa kupitia vyanzo vya...