Machapisho

SERIKALI YAZINDUA MFUMO "ONGEA NA WAZIRI, MWANACHI KUPEWA SAUTI YA MOJA KWA MOJA SEKTA YA AFYA

Picha
  Na WAF, Arusha. SERIKAL imetangaza mwanzo wa enzi mpya ya uwazi, uwajibikaji na ushirikishwaji wa wananchi katika sekta ya afya baada ya kuzindua rasmi kwa mfumo wa kidijitali wa “Ongea na Waziri wa Afya” unaomuwezesha mwananchi kuwasiliana moja kwa moja na Wizara ya Afya saa 24 kwa siku. Hayo yamesemwa na Mhe. Mohamed Mchengerwa wakati wa  hafla ya uzinduzi iliyofanyika leo Januari 26,2026 jijini Arusha. Waziri wa Afya, Mheshimiwa Mohamed Omary Mchengerwa, amesema mfumo huo ni utekelezaji wa vitendo wa dhamira ya Serikali ya kuisogeza huduma ya afya karibu na mwananchi na kuhakikisha sauti ya wananchi inatumika kama dira ya maboresho ya huduma. “Mfumo wa "Ongea na Waziri wa Afya" unatuma ujumbe ulio wazi kuwa sauti ya mwananchi si ya pembeni, bali ndiyo msingi wa maamuzi ya Serikali katika kuboresha huduma za afya,” amesema Waziri Mchengerwa. Amefafanua kuwa uzinduzi wa mfumo huo ni mapinduzi makubwa katika sekta ya afya kwa kuwa unajenga utamaduni mpya wa uongozi unaosiki...

HABARI PICHA

Picha
WAZIRI wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, leo Januari 26, 2026 amefanya kikao kazi na Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) chenye lengo la kujadili mikakati ya kuimarisha na kuendeleza utendaji wa wakala huo. Kikao hicho kimefanyika katika Ofisi za Wizara ya Nishati, Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma, na kuhudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mha. Felchesm Mramba, Mwenyekiti wa Bodi ya PBPA, Dkt. Lutengano Mwakahesya, Mtendaji Mkuu wa PBPA, Bw. Erasto Simon, pamoja na Wajumbe wa Bodi na Wataalamu kutoka Wizara ya Nishati.

WIZARA YA MADINI YAJENGA MAABARA KUBWA YA KISASA DODOMA

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Dodoma. WIZARA  ya Madini imetangaza ujenzi wa Maabara kubwa ya kisasa katika eneo la Nala, mkoani Dodoma, kwa lengo la kusaidia upimaji na utoaji wa taarifa sahihi za sampuli za madini. Maabara hiyo inatarajiwa kuwa kitovu cha utoaji wa huduma za madini kusini mwa Jangwa la Sahara. Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, amesema hayo leo Januari 26,2026 jijini Dodoma wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa Siku 100 za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kipindi cha pili cha Awamu ya Sita ya Serikali. Amesema kuwa ujenzi wa maabara hiyo utaleta mabadiliko makubwa ya kiuchumi kwa Tanzania na nchi jirani, sambamba na kuwajengea uwezo wataalamu wa ndani.  Aidha, Wizara imeingia makubaliano na GST ili taasisi hiyo iwe kitovu cha utoaji huduma za maabara kusini mwa Jangwa la Sahara. Katika kuongeza thamani ya madini, Waziri Mavunde amebainisha kuwa Wizara inaendelea kwa kasi na ujenzi wa viwanda vya kuongeza thamani, ambapo hadi sa...

SERIKALI YASAJILI ZAIDI YA WAFABIASHARA NDOGONDOGO 119,000 NCHINI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma. SERIKALI kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum imesajili jumla ya wafanyabiashara ndogondogo 119,595 katika Mfumo wa Usimamizi na Usajili wa Wafanyabiashara Ndogondogo (WBNMIS), hatua inayolenga kuwawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi na kunufaika na fursa mbalimbali za maendeleo. Akizungumza na waandishi wa habari, Waziri wa wizara hiyo, Mheshimiwa Dorothy Gwajima, amesema mafanikio hayo yamepatikana katika kipindi cha siku 100 za utekelezaji wa ahadi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambapo Serikali imejikita katika urasimishaji wa wafanyabiashara, utoaji wa mikopo nafuu na uwezeshaji wa makundi maalum. "Kati ya waliosajiliwa wanawake ni 73,341 na wanaume 46,254, huku makundi yaliyosajiliwa yakijumuisha machinga 103,102, mama na baba lishe 12,384 pamoja na waendesha bodaboda na bajaji 4,109," Amesema Waziri Gwajima. Ameeleza kuwa katika ...

VIKUNDI 222 UYUI VYAWEZESHWA MIKOPO NAFUU YA BILIONI 1

Picha
   Na Allan Kitwe, Tabora. HALMASHAURI ya Wilaya ya Uyui Mkoani Tabora imetoa mikopo nafuu isiyo na riba ya shilingi bilioni 1 kwa vikundi 222 vya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu wanaojishughulisha na biashara ndogo ndogo ili kuwainua kiuchumi. Akizungumza kwenye hafla fupi ya kukabidhi mfano wa hundi za mikopo hiyo jana, Afisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya hiyo Amoniche Mtweve amesema kuwa mikopo hiyo imetokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri. Ameongeza kuwa jumla ya wanachama 1,121 wanaounda vikundi hivyo wamenufaika na mikopo hiyo na kuwapa nguvu ya kuendeleza miradi yao ya biashara na uzalishaji mali katika maeneo yao. Naye Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Shabani Katalambula, amewataka wanufaika kurejesha mikopo hiyo kwa wakati ili kuwezesha wananchi wengine kunufaika na mikopo hiyo katika awamu zijazo. Amefafanua lengo la mikopo hiyo kuwa ni kusaidia vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kujikwamua kiuchumi kupitia miradi midogo midogo ya ujasiriam...

MADIWANI TABORA WAPEWA MAFUNZO YA UWAJIBIKAJI

Picha
Na Allan Kitwe, Tabora MADIWANI wa halmashauri ya manispaa Tabora na Uyui Mkoani Tabora wamepewa mafunzo maalumu yatakayowawezesha kutekeleza wajibu wao kwa weledi mkubwa kwa kufuata Sheria, Taratibu na Kanuni. Akifungua mafunzo hayo leo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tabora Mohamed Katete amesema kuwa mafunzo hayo yamekuja wakati mwafaka baada ya kumalizika uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani ili kuwajengea uwezo. Amebainisha kuwa mafunzo hayo ni muhimu sana kwa kuwa yatawaongezea weledi katika kusimamia utendaji wa halmashauri zao na kuongeza kasi ya kutumikia wananchi waliowachagua katika kata zao. ‘Tunampongeza sana Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuruhusu mafunzo haya yatolewe kwa madiwani wote nchini ili kuhakikisha miradi yote inatekelezwa kwa weledi mkubwa na kukamilika kwa wakati’, ameeleza. Aidha amewataka kujenga mahusiano mazuri na wataalamu na watendaji wa halmashauri zao na kuhakikisha fedha zinazoletwa na serikali kuu kwa ajili ya miradi ya maendeleo na z...

RAIS SAMIA AMEING'ARISHA SIMANJIRO - DC LULANDALA

Picha
  Na Mwandishi wetu, Simanjiro.  MKUU wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, mwalimu Fakii Raphael Lulandana ameeleza kwamba Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imeing'arisha Simanjiro kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo. DC Lulandala akizungumza mji mdogo wa Orkesumet makao makuu ya Wilaya hiyo amesema Rais Samia katika kipindi kifupi cha utawala wake amefanikisha maendeleo mengi katika eneo hilo. Ameeleza kwamba kwenye sekta ya nishati ya umeme hivi sasa vijijini vyote 56 vya Wilaya ya Simanjiro vina huduma hiyo ikibakia vitongoji vichache ambavyo navyo vitafungiwa umeme. "Wakati Rais Samia anaingia madarakani katika Wilaya ya Simanjiro ni vijiji 21 pekee ambavyo wananchi wake walikuwa wanapata nishati ya umeme," ameeleza DC Lulandala. Amesema hata baadhi ya watu wa Simanjiro waliodanganywa na baadhi ya wanasiasa kuwa maeneo yao yataporwa na kugeuzwa kuwa mapori tengefu na mapori ya akiba niliwaeleza wasiamini hayo. "Rais Samia haw...

FCT YAENDELEA KUWAWEZESHA WADAU ARUSHA KUPITIA MFUMO WA KIELEKTRONIKI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Arusha. BARAZA la Ushindani (FCT) limewahimiza wadau na wafanyabiashara mkoani Arusha kutumia kikamilifu mfumo wa usajili wa mashauri kwa njia ya kielektroniki (e-filing), lengo likiwa ni kuongeza ufanisi na kupunguza gharama katika uwasilishaji wa mashauri. Akizungumza katika mafunzo hayo Msajili wa Baraza hilo, Mhe. Mbegu Kaskasi, alisema mfumo huo wa kisasa umeundwa ili kurahisisha usajili wa mashauri na rufaa bila wadau kulazimika kufika katika ofisi za FCT, hatua ambayo itaokoa muda na kuongeza ufanisi. “Mfumo huu utaimarisha uwazi, kasi ya utoaji haki na kupunguza usumbufu kwa wadau,” alisema Mhe. Kaskasi, akibainisha kuwa hatua hiyo inakwenda sambamba na msukumo wa Serikali ya Awamu ya Sita wa kuimarisha matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa huduma."amesema Mhe.Kaskasi. Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Bw. Moses Pesha, amelipongeza Baraza kwa kuendelea kutoa elimu kwa wanaohusika na wananchi kwa ujumla, akisema hatua hiyo imeongeza ...

MAJI TAKA YAKIDHIBITIWA AFYA BORA KWA KILA MWANANCHI

Picha

MAPATO MANISPAA YA TABORA YAPAA

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora. HALMASHAURI ya manispaa Tabora imeendelea kupiga hatua kubwa kimaendeleo ikiwemo kufanikisha utekelezaji miradi ya maendeleo kutokana na kasi nzuri ya ukusanyaji mapato kutoka katika vyanzo vyake mbalimbali. Hayo yamebainishwa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Dkt John Pima alipokuwa akiwasilisha mapendekezo ya rasimu ya bajeti ya halmashauri hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/2026 katika kikao cha Baraza la madiwani. Amefafanua kuwa kwa mwaka wa fedha 2026/2027 wanatarajia kukusanya zaidi ya sh bilioni 12 kutoka katika vyanzo vyake mbalimbali ikiwa ni sehemu ya rasimu ya mapendekezo ya bajeti yao kwa mwaka huu wa fedha. Amedokeza kuwa mapendekezo hayo ni ishara ya kazi nzuri ambayo imeendelea kufanywa na timu yake ya mapato kwa mwaka wa fedha uliopita ambapo walipanga kukusanya kiasi cha sh bilioni 8.6 na kupata mafanikio makubwa.  Dkt Pima amefafanua kuwa kati ya kiasi hicho sh bilioni 10.57 ni mapato halisi na kiasi cha sh bilioni 1.68 ni m...

JAB YAONYA WAAJIRI KATIKA VYOMBO VYA HABARI KUZINGATIA SHERIA KUEPUKA MIGOGORO YA KISHERIA

Picha
  Na Waandishi Wetu, Dodoma na Iringa. BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imewasisitiza waajiri kwenye vyombo vya habari nchini kuzingatia kikamilifu masharti ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229, hususan wanapoajiri au kuwasainisha mikataba watumishi wa kada ya habari, ili kuepuka migogoro ya kisheria inayoweza kujitokeza baadaye. Wito huo umetolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula tarehe 20-21 Januari, 2026 wakati wa ziara ya kikazi ya Bodi katika mikoa ya Dodoma na Iringa, ilipotembelea vyombo kadhaa vya habari kwa lengo la kukagua kiwango cha uzingatiaji wa Sheria hiyo kwa watumishi wanaojihusisha na shughuli za kihabari, wakiwemo wahariri, waandishi wa habari, watangazaji, wapiga picha waandaaji na waandishi wa kujitegemea. Akizungumza baada ya ziara hiyo, Wakili Kipangula amesema Bodi imebaini uwepo wa waandishi wenye sifa stahiki kwa mujibu wa Sheria kwenye vyombo hivyo, lakini bado hawajajisajili katika Mfumo wa TAI-HABARI ili kuomb...