Machapisho

VIKUNDI 222 UYUI VYAWEZESHWA MIKOPO NAFUU YA BILIONI 1

Picha
   Na Allan Kitwe, Tabora. HALMASHAURI ya Wilaya ya Uyui Mkoani Tabora imetoa mikopo nafuu isiyo na riba ya shilingi bilioni 1 kwa vikundi 222 vya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu wanaojishughulisha na biashara ndogo ndogo ili kuwainua kiuchumi. Akizungumza kwenye hafla fupi ya kukabidhi mfano wa hundi za mikopo hiyo jana, Afisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya hiyo Amoniche Mtweve amesema kuwa mikopo hiyo imetokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri. Ameongeza kuwa jumla ya wanachama 1,121 wanaounda vikundi hivyo wamenufaika na mikopo hiyo na kuwapa nguvu ya kuendeleza miradi yao ya biashara na uzalishaji mali katika maeneo yao. Naye Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Shabani Katalambula, amewataka wanufaika kurejesha mikopo hiyo kwa wakati ili kuwezesha wananchi wengine kunufaika na mikopo hiyo katika awamu zijazo. Amefafanua lengo la mikopo hiyo kuwa ni kusaidia vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kujikwamua kiuchumi kupitia miradi midogo midogo ya ujasiriam...

MADIWANI TABORA WAPEWA MAFUNZO YA UWAJIBIKAJI

Picha
Na Allan Kitwe, Tabora MADIWANI wa halmashauri ya manispaa Tabora na Uyui Mkoani Tabora wamepewa mafunzo maalumu yatakayowawezesha kutekeleza wajibu wao kwa weledi mkubwa kwa kufuata Sheria, Taratibu na Kanuni. Akifungua mafunzo hayo leo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tabora Mohamed Katete amesema kuwa mafunzo hayo yamekuja wakati mwafaka baada ya kumalizika uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani ili kuwajengea uwezo. Amebainisha kuwa mafunzo hayo ni muhimu sana kwa kuwa yatawaongezea weledi katika kusimamia utendaji wa halmashauri zao na kuongeza kasi ya kutumikia wananchi waliowachagua katika kata zao. ‘Tunampongeza sana Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuruhusu mafunzo haya yatolewe kwa madiwani wote nchini ili kuhakikisha miradi yote inatekelezwa kwa weledi mkubwa na kukamilika kwa wakati’, ameeleza. Aidha amewataka kujenga mahusiano mazuri na wataalamu na watendaji wa halmashauri zao na kuhakikisha fedha zinazoletwa na serikali kuu kwa ajili ya miradi ya maendeleo na z...

RAIS SAMIA AMEING'ARISHA SIMANJIRO - DC LULANDALA

Picha
  Na Mwandishi wetu, Simanjiro.  MKUU wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, mwalimu Fakii Raphael Lulandana ameeleza kwamba Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imeing'arisha Simanjiro kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo. DC Lulandala akizungumza mji mdogo wa Orkesumet makao makuu ya Wilaya hiyo amesema Rais Samia katika kipindi kifupi cha utawala wake amefanikisha maendeleo mengi katika eneo hilo. Ameeleza kwamba kwenye sekta ya nishati ya umeme hivi sasa vijijini vyote 56 vya Wilaya ya Simanjiro vina huduma hiyo ikibakia vitongoji vichache ambavyo navyo vitafungiwa umeme. "Wakati Rais Samia anaingia madarakani katika Wilaya ya Simanjiro ni vijiji 21 pekee ambavyo wananchi wake walikuwa wanapata nishati ya umeme," ameeleza DC Lulandala. Amesema hata baadhi ya watu wa Simanjiro waliodanganywa na baadhi ya wanasiasa kuwa maeneo yao yataporwa na kugeuzwa kuwa mapori tengefu na mapori ya akiba niliwaeleza wasiamini hayo. "Rais Samia haw...

FCT YAENDELEA KUWAWEZESHA WADAU ARUSHA KUPITIA MFUMO WA KIELEKTRONIKI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Arusha. BARAZA la Ushindani (FCT) limewahimiza wadau na wafanyabiashara mkoani Arusha kutumia kikamilifu mfumo wa usajili wa mashauri kwa njia ya kielektroniki (e-filing), lengo likiwa ni kuongeza ufanisi na kupunguza gharama katika uwasilishaji wa mashauri. Akizungumza katika mafunzo hayo Msajili wa Baraza hilo, Mhe. Mbegu Kaskasi, alisema mfumo huo wa kisasa umeundwa ili kurahisisha usajili wa mashauri na rufaa bila wadau kulazimika kufika katika ofisi za FCT, hatua ambayo itaokoa muda na kuongeza ufanisi. “Mfumo huu utaimarisha uwazi, kasi ya utoaji haki na kupunguza usumbufu kwa wadau,” alisema Mhe. Kaskasi, akibainisha kuwa hatua hiyo inakwenda sambamba na msukumo wa Serikali ya Awamu ya Sita wa kuimarisha matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa huduma."amesema Mhe.Kaskasi. Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Bw. Moses Pesha, amelipongeza Baraza kwa kuendelea kutoa elimu kwa wanaohusika na wananchi kwa ujumla, akisema hatua hiyo imeongeza ...

MAJI TAKA YAKIDHIBITIWA AFYA BORA KWA KILA MWANANCHI

Picha

MAPATO MANISPAA YA TABORA YAPAA

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora. HALMASHAURI ya manispaa Tabora imeendelea kupiga hatua kubwa kimaendeleo ikiwemo kufanikisha utekelezaji miradi ya maendeleo kutokana na kasi nzuri ya ukusanyaji mapato kutoka katika vyanzo vyake mbalimbali. Hayo yamebainishwa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Dkt John Pima alipokuwa akiwasilisha mapendekezo ya rasimu ya bajeti ya halmashauri hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/2026 katika kikao cha Baraza la madiwani. Amefafanua kuwa kwa mwaka wa fedha 2026/2027 wanatarajia kukusanya zaidi ya sh bilioni 12 kutoka katika vyanzo vyake mbalimbali ikiwa ni sehemu ya rasimu ya mapendekezo ya bajeti yao kwa mwaka huu wa fedha. Amedokeza kuwa mapendekezo hayo ni ishara ya kazi nzuri ambayo imeendelea kufanywa na timu yake ya mapato kwa mwaka wa fedha uliopita ambapo walipanga kukusanya kiasi cha sh bilioni 8.6 na kupata mafanikio makubwa.  Dkt Pima amefafanua kuwa kati ya kiasi hicho sh bilioni 10.57 ni mapato halisi na kiasi cha sh bilioni 1.68 ni m...

JAB YAONYA WAAJIRI KATIKA VYOMBO VYA HABARI KUZINGATIA SHERIA KUEPUKA MIGOGORO YA KISHERIA

Picha
  Na Waandishi Wetu, Dodoma na Iringa. BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imewasisitiza waajiri kwenye vyombo vya habari nchini kuzingatia kikamilifu masharti ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229, hususan wanapoajiri au kuwasainisha mikataba watumishi wa kada ya habari, ili kuepuka migogoro ya kisheria inayoweza kujitokeza baadaye. Wito huo umetolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula tarehe 20-21 Januari, 2026 wakati wa ziara ya kikazi ya Bodi katika mikoa ya Dodoma na Iringa, ilipotembelea vyombo kadhaa vya habari kwa lengo la kukagua kiwango cha uzingatiaji wa Sheria hiyo kwa watumishi wanaojihusisha na shughuli za kihabari, wakiwemo wahariri, waandishi wa habari, watangazaji, wapiga picha waandaaji na waandishi wa kujitegemea. Akizungumza baada ya ziara hiyo, Wakili Kipangula amesema Bodi imebaini uwepo wa waandishi wenye sifa stahiki kwa mujibu wa Sheria kwenye vyombo hivyo, lakini bado hawajajisajili katika Mfumo wa TAI-HABARI ili kuomb...

WANAFUNZI WA USAGARA WAPATIWA ELIMU YA FEDHA WIKI YA HUDUMA ZA FEDHA TANGA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Tanga. WIZARA ya Fedha kupitia Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha imeendelea kutoa elimu ya fedha kwa makundi mbalimbali ya jamii mkoani Tanga, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha yanayoendelea katika Viwanja vya Usagara, jijini Tanga, kwa lengo la kuwajengea wananchi uelewa wa masuala ya kifedha na kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi. Akizungumza wakati wa utoaji wa elimu katika darasa la Elimu ya Fedha, Afisa Usimamizi wa Fedha kutoka Wizara ya Fedha, Bi. Grace Muiyaza, alisema mafunzo hayo yanawalenga watumishi wa umma, wafanyabiashara wadogo, vikundi vya wajasiriamali, wananchi wa kawaida pamoja na wanafunzi kuanzia ngazi ya shule ya msingi, sekondari hadi vyuoni. “Tuko hapa tunatoa mafunzo kwa makundi yote ya jamii ya Tanga. Lengo letu ni kuwajengea uelewa wa masuala ya kifedha na kuwawezesha kushiriki vizuri katika shughuli za kiuchumi,” amesema Bi. Muiyaza. Ameeleza kuwa katika darasa la siku hiyo, walikutana ...

RAIS DKT.MWINYI AMUAPISHA AMINA MUUMINI KUWA NAIBU MKURUGENZI MKUU WA ZAECA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar. RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amemuapisha Ndg. Amina Muumini kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA), kufuatia uteuzi wake uliofanywa hivi karibuni. Hafla ya uapisho huo imefanyika leo, tarehe 22 Januari 2026, Ikulu Zanzibar, sambamba na kikao cha Baraza la Mapinduzi.

WAZIRI MKUU MWIGULU AIPONGEZA SEKTA YA MADINI KWA KUONGEZA MAKUSANYO YA MAPATO

Picha
  Sekta ya Madini Tanzania imeingia kwenye kumbukumbu za Afrika, Nchi jirani zajifunza uendeshaji wa sekta ya madini Tanzania, Ataka kasi ya utafiti wa kina kuongezwa, Tume ya Madini yatakiwa kukomesha migogoro ya wachimbaji. Na Mwandishi Wetu, Dodoma. WAZIRI  Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameipongeza Sekta ya Madini kwa mafanikio makubwa iliyoyapata katika kuongeza makusanyo ya mapato ya Serikali na hivyo  kuiwezesha Tanzania kuandika historia mpya ya uendeshaji wa sekta hiyo Barani Afrika. Dkt. Mwigulu amesema mafanikio hayo yametokana na mageuzi makubwa ya kisera, kisheria na kiutendaji yaliyofanywa na Serikali kupitia Wizara ya Madini, yaliyoiwezesha sekta hiyo kuwa jumuishi na shirikishi, huku Watanzania hususan vijana, wanawake na watu wenye mahitaji maalum wakishiriki kikamilifu katika mnyororo mzima wa thamani wa madini. Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo Januari 22, 2026, wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo...