Machapisho

WAZIRI MKUU KUZINDUA MELI YA MV NEW MWANZA KESHO

Picha
Na Mwandishi Wetu, Mwanza. MELI ya MV.New Mwanza yenye uwezo wa kubeba abiria 1200 na tani 400 kwa pamoja katika Ziwa Victoria inatarajiwa kuzinduliwa kesho Januari 23, 2025 mkoani Mwanza huku mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba.  Akizungumza leo na waandishi wa habari mkoani Mwanza, Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa amesema mpaka kukamilika kwa ujenzi wa meli hiyo zaidi ya Bilioni 120 zimetumika huku katika uongozi wa Serikali ya awamu ya sita zaidi ya Bilioni 79 zikitolewa. "Ina uwezo wa kubeba abiria 1,200 na tani 400 za mizigo, pamoja na magari makubwa 3 na magari madogo 20.  Meli hii imeundwa kwa viwango vya kimataifa na ina urefu wa mita 92.6, karibu sawa na uwanja wa mpira wa miguu, na upana wa mita 17, ikiwa na kimo cha ghorofa nne," amesema. Profesa Mbarawa amesema hadi sasa meli ya MV New Mwanza tayari imeshafanya jumla ya safari sita (6) kati ya Mwanza na Bukoba kupitia Kemondo.  "Katika safari hizo, meli imebeba jumla ya abir...

TUNATAKA KAZI ZA SERIKALI ZIFANYIKE MAKAO MAKUU YA NCHI-DKT. MWIGULU.

Picha
  Asisitiza Taasisi za Serikali zinapaswa kufahamu kwamba makao makuu ya nchi ni Dodoma.  Na Lubango Mleka, Dodoma. WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema kuwa Serikali inataka kazi zote zifanyike makao makuu ya nchi ili kusogeza huduma karibu na Wananchi. Amesema hayo leo Alhamisi (Januari 22, 2026) alipotembelea Ofisi za Wizara ya Maji na Wizara ya Madini zilizopo mji wa Serikali, Mtumba jijini Dodoma. “Ninawapongeza sana, mmehamia Makao Makuu, taasisi zote za Serikali zinapaswa kutambua kwamba makao makuu ya nchi ni Dodoma, na huduma zote zinapaswa kutolewa hapa, hii sio kambi na wala hatutakuwa na Makao Makuu mbili zilizo sambamba”. Pia, Mheshimiwa Mwigulu ameziagiza Taasisi zote ambazo zimeshakamilisha ujenzi wa majengo katika makao makuu kuyatoa majengo hayo kwa Taasisi ambazo haziwajibiki kuhamia Dodoma lakini bado zimepanga. “Mheshimiwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu mwelekeze Katibu Mkuu atengeneze timu ifanye tathmini ya majengo yote ya Serikali yaliyoko Dar ...

MWENYEKITI BODI YA NRH AZINDUA RASMI SHUGHULI ZA UJENZI JENGO LA GHOROFA IDARA YA MATERNITY.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Igunga. MWENYEKITI wa bodi ya Hospitali ya Rufaa ya Nkinga (NRH) iliyopo Kata ya Nkinga Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora, Askofu Sixberth Kuzenza wiki hii amezindua rasmi shughuli za ujenzi wa jengo jipya lenye ghorofa katika Idara ya mama na mtoto zinazotazamiwa kuanza mapema mwaka huu 2026. Tukio hilo la kihistoria limefanyika kwa ishara ya kuchimba udongo katika eneo ambalo litajengwa jengo hilo, ambapo hivi karibuni shughuli za ubomoaji wa majengo yanayotumika zitaanza rasmi baada ya huduma zitolewazo mahali hapo kuhamishiwa eneo lingine. Askofu Kuzenza amesema; wanamshukuru Mungu kwakuwa hatua hiyo ni muendelezo wa utekelezaji wa mpango mkakati wa Hospitali wa miaka 5 kuhakikisha huduma na miundombinu ya taasisi inaboreshwa zaidi ili kuwapatia wananchi huduma katika mazingira bora. "Tunamshukuru Mungu sana kwakuwa ni jambo lililokuwa kwenye mpango mkakati wa Hospitali, na sasa tunaanza kuona utekelezaji wake, tunamwamini Mungu litakamilika kwa wakati ili liwe...

KAPALATA AIOMBA SERIKALI KUCHUKUA HATUA ZA MAPEMA KUIOKOA MIJI INAYOZUNGUKA MIGODI

Picha
  Aekeza kuwa miji mingi duniani kudorora na kufa kiuchumi baada ya migodi kufungwa, Ataka viwanda, ajira na miundombinu ianzishwe sambamba na uwekezaji wa madini, Waziri Mavunde apongeza ushauri wa kitaalamu na mtazamo wa muda mrefu. Na Hamida Ramadhan, DODOMA MJUMBE wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mheshimiwa Neto Paul Kapalata, ameitaka Serikali kuweka Sera na miongozo madhubuti itakayohakikisha utoaji wa leseni kubwa za uchimbaji madini unaambatana moja kwa moja na wajibu wa kuendeleza miji inayozunguka migodi, ili miji hiyo iendelee kuwa na uhai wa kiuchumi na kijamii hata baada ya rasilimali za madini kuisha. Akizungumza wakati wa kikao cha Kamati hiyo, Mheshimiwa Kapalata amesema uzoefu wa kimataifa unaonesha kuwa utegemezi wa miji mingi kwenye uchumi wa madini pekee umesababisha kudorora kwa shughuli za kijamii na kiuchumi mara tu miradi ya uchimbaji inapofikia tamati, jambo linaloacha athari kubwa kwa wananchi na Serikali. “Miji mingi duniani imekosa uend...

KAPINGA AAGIZA USIMAMIZI MKALI MALIPO YA WAKULIMA WA KAHAWA MBINGA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Ruvuma. WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, amemtaka Afisa Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, mkoani Ruvuma, kuhakikisha anasimamia kwa karibu malipo ya wakulima wa kahawa ili kuwalinda dhidi ya ucheleweshaji wa fedha zao unaofanywa na baadhi ya kampuni zinazonunua zao hilo. Mhe. Kapinga, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini, ametoa maelekezo hayo mapema wiki hii alipokuwa akizungumza katika kikao na viongozi wa Vyama vya Msingi vya Ushirika (AMCOS) kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga. Amesisitiza kuwa zao la kahawa ni uti wa mgongo wa uchumi wa Wilaya ya Mbinga na chanzo kikuu cha maisha ya wananchi wengi, hivyo Serikali haitavumilia kuona watu wachache wanaitia doa kutokana na uzembe au kushindwa kusimamia ipasavyo sheria na kanuni ili wakulima walipwe fedha zao za mauzo ya kahawa kwa wakati. Katika maelekezo yake, Waziri Kapinga amemwagiza Afisa Ushirika wa wilaya hiyo, kufuatilia kwa karibu n...

SERIKALI, WADAU WAWEKA MIKAKATI KUKABILI VIFO VITOKANAVYO NA UZAZI

Picha
  Na WAF, Dodoma. Serikali kupitia Wizara ya Afya, Idara ya Afya ya Uzazi wa Mama na Mtoto, kwa kushirikiana na Shirika la Thamini Uhai wamekutana pamoja na kuweka mikakati utekelezaji wa Mradi wa Ushirikiano wa kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.  Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Idara ya Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto, Dkt. Ahmad Makuwani wakati wa kikao hicho kilichofanyika leo Januari 21, 2026 katika Ofisi za Wizara ya Afya Mtumba jijini Dodoma. "Serikali imeweka nia ya dhati ya kuhakikisha inaendelea kuweka mikakati madhubuti ya kupunguza idadi ya vifo vitokanavyo na uzazi kwa kushirikisha wadau mbalimbali ili kufanikisha utekelezaji wa mradi huo," amesema Dkt. Makuwani. Ameongeza kuwa ni muhimu kwa Wizara ya Afya kupitia Idara ya Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto ikuweka mikakati bora ya namna ya kutekeleza mradi huo ikiwa ni pamoja na kuangalia maeneo yanayopaswa kupewa kipaumbele katika mradi huo ikiwemo ujenzi wa majengo ya uangalizi maalum wa mtoto wenye changamoto mba...

POLISI WAKANUSHA TAARIFA YA CHADEMA "HATUJAKAMATA MTU YEYOTE NKASI"

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Rukwa. JESHI la Polisi Mkoa wa Rukwa leo Jumatano Januari 21, 2026 limekanusha taarifa zisizo sahihi zilizosambazwa mitandaoni zikidai kuwa Wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA wamevamiwa, kukamatwa na kutawanywa kwa nguvu na Jeshi la Polisi wakati wakipanda Miti Wilayani Nkasi, Mkoani Rukwa. Kupitia taarifa yake kwa Vyombo vya habari, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa amesema taarifa hizo za CHADEMA hazina ukweli wowote na zina lengo la kupotosha na kuzua taharuki zisizo na msingi kwani katika Wilaya ya Nkasi na Mkoa wa Rukwa kwa ujumla hakuna tukio la matumizi ya mabavu ama la wafuasi wa Chama hicho kukamatwa na Jeshi la Polisi. "Jeshi la Polisi Mkoa wa Rukwa linaendelea kuimarisha usalama wa raia na mali zao na tunaendelea kusisitiza wananchi kupuuza taarifa zinazoandaliwa na kusambazwa kwa lengo la kupotosha, kuchonganisha, kujenga chuki baina ya wananchi na Taasisi mbalimbali." Imesema taarifa hiyo ya Polisi. Jana kupitia Mitandao...

SERIKALI KUPANUA UTAFITI WA MADINI YA KINYWE KWA USHIRIKIANO NA MAREKANI

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Dodoma. SERIKALI imetangaza mpango wa kupanua utafiti wa kina wa Madini ya Kinywe kwa kushirikiana na Serikali ya Marekani, hatua inayolenga kuongeza maarifa ya kitaalamu na kubaini fursa mpya za maendeleo katika sekta ya madini. Akizungumza jijini Dodoma, Waziri wa Madini Anthony Mavunde amesema ushirikiano huo ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuhakikisha rasilimali za madini zinatambulika kikamilifu na kutumika kwa manufaa ya Taifa na wananchi. Mavunde amesema maeneo ya awali yaliyofanyiwa utafiti yanaonesha uwepo wa Madini ya Kinywe katika mikoa ya Lindi na Mtwara, na kwamba Serikali itaendelea kupanua wigo wa utafiti ili kupata takwimu kamili za kijiolojia. Ameeleza kuwa Watanzania wanaomiliki leseni za uchimbaji wa madini watapewa kipaumbele katika mpango huo, ambapo Serikali itashirikiana na wataalamu wa Marekani kufanya uchambuzi wa kina wa rasilimali hizo. Kwa mujibu wa Waziri huyo, jitihada hizo zinatarajiwa kuongeza uzalishaji wa madini hayo kwa s...

WAWILI WAFUNGWA MIAKA 30 KWA UBAKAJI

Picha
  Na Mwandishi wetu, Simanjiro. WAKAZI wawili wa mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara, wamehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kumbaka kwa zamu msichana mwenye umri wa miaka 24. Pamoja na kumbaka na kumwingilia kinyume cha maumbile msichana huyo pia walimpora simu aina ya Samsung na kumwibia fedha zake Sh70,000. Hata hivyo, katika hukumu ya kesi hiyo namba 10374/2025 iliyotolewa mji mdogo wa Orkesumet na hakimu wa mahakama ya wilaya hiyo Nicodemo washtakiwa watatu kati ya watano hawakuwepo mahakama hapo.  Hakimu Nicodemo amewataja washtakiwa Meshack Paulo (23) na Ibrahim Ibu (24) ambao ni wachimbaji wa madini ya Tanzanite mji mdogo wa Mirerani walimbaka, kumlawiti  Amesema washtakiwa hao na wenzao watatu Februari 4, 2025 kwa pamoja walimbaka msichana huyo ambaye ni muhudumu wa bar ya Feri mwenye umri wa miaka 24. Ameeleza kwamba wakati msichana huyo usiku huo wa saa 8 akitoka kazini akitembea kwenda nyumbani alimuona mshtakiwa wa kwanza Meshack akiwa...

TARURA YATENGA BIL 7 KUTENGENEZA KM 114 ZA BARABARA TABORA

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora. WAKALA wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoani Tabora wanatarajia kutengeneza barabara zenye urefu wa km 114.05 kwa gharama ya sh bilioni 7.4 katika Wilaya ya Tabora Mjini kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Hayo yamebainishwa jana na Meneja wa Wakala huo Wilaya ya Tabora, Mhandisi Subira Manyama alipokuwa akiwasilishwa rasimu ya mapendekezo ya bajeti ya TARURA kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Ametaja vipaumbele vya rasimu hiyo kuwa ni kukarabati barabara zote ambazo zimekuwa hazipitiki kwa kipindi kirefu ili ziweze kupitika wakati wote, kuzifanyia matengenezo barabara zote za mjini na vijijini ili ziwe imara zaidi. Ameongeza kuwa watafanya matengenezo ya kawaida kwa sehemu korofi zote na ya muda maalumu kwa baadhi ya barabara ili kuwezesha wananchi kusafiri na kusafirisha mazao yao kutoka vijijini kwenda kwenye masoko kwa mwaka mzima. Mhandisi Manyama amefafanua kuwa kwa mwaka wa fedha 2026/2027 wanatarajia kutumia kiasi cha sh bil 7.4 kwa ajili ya maten...