Machapisho

SHULE ZOTE 18055 ZA MSINGI ZIPO TAYARI KUPOKEA WANAFUNZI- PROF. SHEMDOE

Picha
  Na OWM - TAMISEMI  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe ameridhishwa na maandalizi ya mapokezi ya wanafunzi wa darasa la awali na la kwanza katika Shule ya Msingi Iyumbu jijini Dodoma, na kuuarifu umma kuwa maandalizi katika shule zote za msingi 18055 yamekamilika na zipo tayari kupokea wanafunzi kuanzia Januari 13, 2026. Prof. Shemdoe amesema, ameitembelea shule hiyo ya Msingi Iyumbu leo Januari 12, 2026, ili kujiridhisha na maandalizi ya mapokezi ya wanafunzi wanaotarajiwa kuanza darasa la awali na la kwanza Januari 13, 2026 na amejionea mwenyewe kuwa maandalizi yamekamilika. “Tumeona maandalizi kwenye shule hii yamekamilika, kama ilivyo kwenye shule zote 18055 za msingi, hivyo natoa wito kwa wazazi wenye watoto walio na umri wa kuanza darasa la awali na la kwanza wawapeleke shuleni,” Prof. Shemdoe amesisitiza. Prof. Shemdoe amejionea madarasa ya awali mazuri ambayo yamejengwa kwa fedha za mapa...

SELWA AKAGUA MIRADI 19 YA ELIMU IGUNGA YENYE THAMANI YA BILIONI 3.39.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Igunga. MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Selwa Hamid amefanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi 19 ya Afya na Elimu yenye tahamani ya sh. 3.39 bilioni. Selwa amefanya ziara hiyo ya siku tatu mfululizo katika kata zilizopo kwenye majimbo ya Igunga na Manonga wilayani Igunga. Amesema kukamilika kwa miradi hiyo ni muendelezo wa kuendelea kutoa huduma na furaha kwa wananchi.

SERIKALI YAONYA WATAALAMU WA ARDHI WASIO WAADILIFU

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora SERIKALI imewataka watumishi wa sekta ya ardhi nchini kufanya kazi kwa weledi na uadilifu ili kuhakikisha migogoro ya ardhi iliyopo katika maeneo yao inatatuliwa kwa wakati ili kuepusha malalamiko ya wananchi. Onyo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Kaspar Kaspar Mmuya alipokuwa akiongea na watumishi wa sekta hiyo kutoka taasisi mbalimbali za umma Mkoani hapa. Ameeleza kuwa ni jukumu la wataalamu wa sekta hii kuhakikisha kero na migogoro yoyote inayohusiana na masuala ya ardhi inashughulikiwa ipasavyo na kwa wakati ili wananchi wapate haki zao. ‘Ninyi ni wawakilishi wa Mheshimiwa Rais katika sekta hii, onyesheni weledi wenu, fanyeni kazi kwa uadilifu mkubwa, kuweni na maadili mema, tendeni haki kwa wananchi wote ili wawaamini, wengi wenu mnaitwa wapiga dili’, amesema. Ameonya kuwa serikali haitamvumilia mtumishi yeyote wa sekta hii anayeendekeza vitendo vya upigaji dili badala ya kutekeleza wajibu wake kwa kuzingatia she...

IGEMBENSABO INAWATAKIA WANACHAMA WAKE WOTE HERI YA MIAKA 62 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

Picha
 

WALIMU SIMANJIRO WAJENGEWA UWEZO SIS

Picha
  Na Mwandishi wetu, Simanjiro WAKUU wa shule za sekondari na msingi wilayani Simanjiro mkoani Manyara, wamejengewa uwezo wa kuandaa taarifa za shule kutokana na kasi ya ukuaji na kuongezeka kwa matumizi ya sayansi na teknolojia ulimwenguni. Wakuu wa shule 23 za sekondari, 110 wa msingi wa shule za serikali na binafsi wamejengewa uwezo wa kuandaa taarifa za shule ili kurahisisha utoaji na upatikanaji wa wake kupitia serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kupitia Wizara ya Elimu.  Afisa elimu ya awali na msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro, Darius Daudi Limandola amesema walimu hao wamepata mafunzo hayo ya uandaaji wa taarifa za shule kwenye vituo vitatu vya Orkesumet, Terrat na Mirerani. Limandola ameeleza kwamba mafunzo hayo ya mfumo wa utoaji wa taarifa za kielimu kupitia mfumo wa kidigitali (School Information System) una lengo la kurahisisha utoaji na upatikanaji wa taarifa za shule husika kwa wakati. Ameeleza kwamba mfumo huo unafanyak...

TANZANIA YANG'ARA DUNIANI KUNDI LA VINARA WA SERIKALI KIDIGITALI - WORLD BANK 2025.

Picha
Na Hamida Ramadhani. TANZANIA imeendelea kung’ara kimataifa baada ya Benki ya Dunia (World Bank – WB) kuitaja kuwa miongoni mwa nchi zilizo na ukomavu wa juu wa matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika sekta ya umma.  Hatua hii ni uthibitisho wa mafanikio ya mageuzi ya kidijitali yanayoendelea kutekelezwa na Serikali katika kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi. Kwa mujibu wa Ripoti ya GovTech Maturity Index (GTMI) ya mwaka 2025, Tanzania imeorodheshwa katika Kundi A – Ukomavu wa Juu wa Matumizi ya TEHAMA (Extensive GovTech Maturity).  Kundi hili linajumuisha nchi zinazoongoza duniani katika matumizi ya teknolojia katika utoaji wa huduma za serikali na ushirikishwaji wa wananchi kidijitali. GTMI: Kipimo cha Ukomavu wa Serikali Kidijitali. Ripoti ya GTMI hutathmini ukomavu wa matumizi ya TEHAMA serikalini katika takriban nchi zote duniani, ikizingatia maeneo muhimu kama sera, sheria, miongozo, mifumo ya TEHAMA na utekelezaji wake. Toleo la 2025 la ripot...

MIRERANI WALIA NA MAJI YA KUNYWA

Picha
  Na Mwandishi wetu, Mirerani. WAKAZI wa mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara, kwa zaidi ya wiki moja wamelalamikia kutopata huduma ya maji ya kunywa, baada ya malori yanayouza maji hayo kutoka mji mdogo wa Boma ng'ombe wilayani Hai mkoani Kilimanjaro kudaiwa kuzuiwa. Kwa zaidi ya miaka 20 wakazi wa mji mdogo wa Mirerani, wanatumia maji ya kunywa yanayouzwa na malori kutoka mji mdogo wa Boma ng'ombe. Hivi sasa, baadhi ya wakazi wengine wa mji huo wanatumia maji ya visima vifupi na virefu na maji ya mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira jiji la Arusha (AUWSA) Mirerani, kwa ajili ya matumizi mengine ikiwemo kunywa. Baadhi ya wakazi wa mji mdogo wa Mirerani, wakizungumza juu ya changamoto hiyo wameiomba serikali kuingilia kati suala hilo kwani wanatumia gharama kubwa kupata maji ya kunywa. Mmoja kati ya wakazi hao, Andrew John amesema kwa zaidi ya miaka 20 walikuwa wanatumia maji ya kunywa yanayotoka Hai ila wanasikitishwa hivi sasa kupata zuio hilo. "...

JAMII YASWA KUWAPA NAFASI SAWA WATU WENYE ULEMAVU KATIKA ELIMU YA DINI.

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Dodoma. SHEIKH wa Mkoa wa Dodoma, Mustafa Rajab, ameitaka jamii kuacha tabia ya kuwatenga watu wenye Ulemavu na badala yake kuwapa nafasi sawa, hususan katika elimu na masuala ya dini, kwani nao ni sehemu muhimu ya jamii na wana haki sawa ya kujifunza na kutekeleza mafundisho ya dini. Sheikh Rajab ameyasema hayo alipo hutubia katika Mashindano ya Kitaifa ya Kuhifadhi Qur’an Tukufu kwa Watu wenye Ulemavu yaliyoandaliwa na Taasisi ya Riziki Lulida Foundation. Amesema kuwa, mashindano hayo ni ya kipekee kwa kuwa yanawaleta pamoja kundi la watu ambalo kwa muda mrefu limekuwa likisahaulika na kupuuzwa na jamii. " Kwa miaka mingi jamii imekuwa ikiwanyima watu wenye ulemavu fursa mbalimbali bila kutambua kuwa nao ni binadamu kamili wenye haki ya kusoma, kuabudu na kushiriki kikamilifu katika masuala ya dini," amesema Sheikh Rajab. Ameongeza kuwa, kupitia mashindano hayo hatua muhimu imechukuliwa kurejesha heshima, thamani na nafasi yao katika jamii. Aidha, Shei...

SELWA :- ATOA ONYO KALI KWA WASIMAMIZI WA MIRADI IGUNGA.

Picha
  Na Lubango Mleka, Igunga. MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Selwa Hamid amewataka Wasimamizi wa Mafundi na Kamati za ujenzi kusimama  katika nafasi zao kwa lengo la kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa wakati na kuzingatia viwango vya fedha. Selwa ametoa wito huo, wakati wa ziara ya kukagua miradi mbalimbali katika kata za Jimbo la Manonga wilayani Igunga. "Tujirekebishe kwenye miradi yetu na kuongeza usimamizi kwa sababu hali ya  mafundi kuondoka maeneo ya ujenzi wakati unaendelea  hatukubaliani nayo," amesisitiza na kuongeza kuwa, "Ziogopeni fedha hizi za miradi kama ukoma na mambo ya udalali yasiwepo kwenye miradi, wapeni mafundi wanaofanya kazi ipasavyo."

WAKUU WA IDARA NA VITENGO IGUNGA WAGAWIWA VISHIKWAMBI ILI KUACHANA NA MATUMIZI YA KARATASI.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Igunga. WAKUU wa Idara na Vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora,  wamegawiwa Vishikwambi kwa lengo la kuvitumia katika vikao mbalimbali na kuachana na matumizi ya karatasi. Akizungumza baada ya kuwagawia vishikwambi hivyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Selwa Hamid amesema wanaendelea kumuunga mkono Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika matumizi ya kidijitali. Amesema hatua hiyo, inaendelea kuondoa  mnyororo wa matumizi ya karatasi ambazo hutengenezwa kwa miti, hivyo kuendelea kutunza miti kwa mazigira rafiki kwa mwanadamu. Aidha, amewataka wakuu hao wa Idara na Vitengo kuvitumia vishikwambi hivyo kuongeza ufanisi wa kazi huku akiwasihi kutojaza picha na taarifa zisizohusiana na Menejimenti.

TEITI YAIMARISHA ELIMU KWA UMMA KUHUSU MANUFAA YA RASILIMALI ZA MADINI NA GESI

Picha
Na.Mwandishi Wetu. Taasisi ya Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) imesema imeendelea kuhimiza uwazi na uwajibikaji katika usimamizi wa rasilimali za nchi, ili kuhakikisha wananchi wananufaika na shughuli za uchimbaji na utafutaji. Akizungumza  jana katika mahojiano maalum,Katibu Mtendaji wa TEITI, Bi. Mariam Mgaya, amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi 57 zinazotekeleza viwango vya kimataifa vya uwazi na uwajibikaji vinavyosimamiwa na EITI. Amesema Tanzania ilijiunga na EITI mwaka 2009, hatua iliyolenga kuimarisha usimamizi bora wa rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia kwa maslahi ya maendeleo endelevu. “Asasi hii inahamasisha wananchi kuelewa hatua zote za mnyororo wa thamani wa rasilimali hizi, ikiwemo ukusanyaji na ufuatiliaji wa mapato,” amesema Bi.Mgaya Bi. Mgaya amebainisha kuwa utekelezaji wa majukumu ya TEITI unasimamiwa na Sheria ya TEITA ya mwaka 2015 ambayo imeainisha jukumu la kuboresha uwazi na uwajibikaji, hasa katika uvunaj...