Machapisho

BABA LEVO KUTUMIA MABANGO YA KAMPENI KUTENGENEZA MEZA ZA WAFANYABIASHARA KIGOMA MJINI

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Dodoma. MBUNGE wa Kigoma Mjini Mheshimiwa Clayton Revocatus Chipando anayejulikana kwa jina la Baba Levo ameonyesha mfano wa ubunifu na uwajibikaji kwa kutumia mabango 80000 ya kampeni yaliyosalia baada ya uchaguzi kutengeneza meza zitakazotolewa bure kwa wafanyabiashara wadogo katika masoko ya Kigoma Mjini. Akizungumza na waandishi wa habari mbunge huyo Baba Levo amesema hatua hiyo inalenga kuboresha mazingira ya wafanyabiashara na kuonyesha kwamba hata vifaa vilivyotumika kisiasa vinaweza kuwa na faida kijamii endapo vitatumiwa kwa ubunifu. Amesema badala ya mabango ya kampeni kubaki yakiharibu mazingira wameamua kuyageuza kuwa meza imara kwa ajili ya wafanyabiashara wa Kigoma ni njia ya kugeuza alama za siasa kuwa alama za maendeleo. Meza hizo zitatolewa rasmi wiki ijayo katika mkutano mkubwa wa shukurani utakaofanyika Kigoma Mjini ambapo Baba Levo atawashukuru wananchi kwa imani waliyoonyesha kwake na kueleza mwelekeo wa uongozi wake mpya. "Mpango wa kutu...

HABARI PICHA KUTOKA BUNGENI

Picha
WAHESHIMIWA wabunge wakijisajili katika viwanja Vya bunge leo Novemba 8 , 2025 kabla ya kuanza kwa mkutano wa kwanza wa bunge la 13 unaotarajiwa kufanyika siku ya Jumanne, Tarehe 11,2025.

UTALII TANZANIA WAZIDI KUNOGA, MAWAKALA 120 WA MAREKANI WAVUTIWA

Picha
Na Lubango Mleka, Serengeti. MAWAKALA wa utalii 120 kutoka nchini Marekani wameonyesha kuvutiwa na vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo nchini Tanzania, hususani mandhari ya kuvutia, wanyamapori, na urithi wa utamaduni wa kipekee. Tukio hilo limejidhihirisha katika usiku wa Novemba 7, 2025 kwenye hafla ya chakula cha usiku iliyofanyika katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mkoani Mara, iliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa ajili ya kuwakaribisha mawakala hao waliowasili nchini kwa ziara ya kutembelea vivutio vya utalii. Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Excellent Guide Tours and Safaris,  Justin Alfred, amesema; "Tumevutiwa sana na mandhari ya Tanzania, hasa wanyamapori kama tembo, twiga, simba na nyati. Nchi hii ni salama, wananchi wake ni wakarimu, watalii wasisite kuja kuitembelea."  Amesema lengo la ziara hiyo ni kuhakikisha Tanzania inatambulika zaidi duniani kama kitovu cha utalii barani Afrika kutokana na urithi wake wa asili, utamaduni na vivutio vya ki...

SALOME MNYAWI MITANO TENA KWAKE MIRERANI

Picha
  Na Mwandishi wetu, Mirerani  MGOMBEA Udiwani wa Kata ya Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Salome Nelson Mnyawi, amewaomba wakazi wa eneo hilo kumpa kura nyingi za ndiyo kwani amefanikisha maendeleo mengi katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. Salome akizungumza kwenye eneo la Maduka Matatu, Mtaa wa Twiga, Kata ya Mirerani, amesema alichaguliwa kwa mara ya kwanza kipindi kilichopita hivyo anaomba kipindi kingine cha miaka mitano ili aweze kushirikiana nao kufanikisha maendeleo ya eneo hilo. Ameeleza baadhi ya mafanikio yaliyofanyika kwenye kipindi chake ni ujenzi wa kituo cha afya Tanzanite ambapo kimekamilika na sasa kinasubiria kufunguliwa na kutoa huduma kwa jamii. "Pia miundombinu ya barabara za lami kutoka soko la getini hadi lango la kuingia na kutoka ndani ya ukuta unaozunguka migodi ya madini ya Tanzanite pamoja na taa na barabara kutoka transifoma hadi kituo cha mafuta cha Kibobo," amesema Salome. Amesema sekta ya elim...

WAPIGA KURA 273,076 WANATARAJIA KUPIGA KURA IFIKIPO OKTOBA 29, 2025 JIMBO LA IGUNGA NA MANONGA

Picha
  Na Lubango Mleka, Igunga. MSIMAMIZI wa Uchaguzi wa Majimbo ya Igunga na Manonga wilayani Igunga mkoani Tabora, Hamisi Hamisi amesema wapiga kura 273,076 wanatarajia kupiga kura ifikapo Oktoba 29, mwaka huu katika majimbo hayo. Hamisi ameeleza hayo katika ofisi ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi iliyopo katika wilaya hiyo mjini Igunga. Kwa mujibu wa kifungu cha 69, (1) cha sheria ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, Hamisi amewaeleza wananchi waliojiandikisha katika Daftari la Kudumu la wapiga kura la Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kuwa uchaguzi utafanyika siku ya Jumatano Oktoba 29 mwaka huu. Amesema vituo vilivyotumika kuandikisha wapiga kura katika Daftari la Kudumu la Wapiga kura ndio vitatumika kupiga kura huku vikifunguliwa saa moja asubuhi na kufungwa saa 10 jioni na kwa upande wa vituo vilivyoko Magereza kufunguliwa saa mbili asubuhi na kufungwa saa tisa alaasiri. "Nitumie fursa hii kuwaomba na9999 kuwakaribisha wananchi wote wa majimbo ya Igunga na Manonga kujitokeza...

VIONGOZI WA DINI SINGIDA NA DODOMA WAHIMIZA VIJANA KULINDA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

Picha
Na Hamida Ramadhan, Dodoma. VIONGOZI wa Dini kutoka mikoa ya Singida na Dodoma wamewataka vijana kuepuka vishawishi vya vurugu na mifarakano ya kisiasa, wakisisitiza kuwa kulinda amani ni jukumu la kila Mtanzania kadri Taifa linavyoelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika wiki ijayo. Wito huo umetolewa leo jijini Dodoma katika kongamano la viongozi wa dini mbalimbali kutoka Kanda ya Kati, lililolenga kuliombea Taifa amani na utulivu kuelekea uchaguzi huo. Akizungumza katika kongamano hilo, Askofu Evance Chande wa Kanisa la Carmel Assemblies of God amesema vijana wanapaswa kutumia nguvu zao katika kujenga Taifa badala ya kushiriki katika vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama wa nchi. “Tunapaswa kuikumbatia amani kama tunavyokumbatia imani zetu. Uchaguzi ukipita, Tanzania inabaki kuwa moja. Tusikubali kugawanywa kwa misingi ya kisiasa,” amesema Askofu Chande. Kwa upande wake, Sheikh Mustapha Rajab, Sheikh wa Mkoa wa Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati ...

MUNDE TAMBWE AENDELEA KUHAMASISHA USHINDI WA CCM SKON

Picha
  Na Hamida Ramadhani. MJUMBE wa NEC na aliyekuwa mtia nia wa ubunge Jimbo la Skonge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Munde Tambwe, ameendelea kujikita katika jimbo hilo akihamasisha wananchi kuichagua CCM katika uchaguzi ujao. Amesema sababu kuu ya kuichagua CCM ni mafanikio makubwa yaliyopatikana chini ya uongozi wake, ikiwemo ujenzi wa kituo cha afya, shule, na miundombinu ya barabara, pamoja na uwezeshaji wa wananchi katika sekta ya kilimo. Munde amewataka wananchi waendelee kuiamini CCM kama chama kinachotekeleza ahadi zake na kuboresha maisha ya Watanzania.

POLISI WAANZA UCHUNGUZI KUHUSU KUTEKWA KWA POLEPOLE, WAKISISITIZA KUMUHITAJI KWA DCI

Picha
Na Hamida Ramadhani, Dodoma. JESHI la Polisi nchini Tanzania, kupitia kwa Msemaji wake DCP David Misime, limesisitiza kuwa bado linaendelea kumsubiri Ndugu Humphrey Polepole ili aripoti katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), kwa ajili ya kutoa maelezo kuhusu tuhuma mbalimbali alizozitoa kupitia mitandao yake ya kijamii. Ikumbukwe kuwa mnamo Jumatatu, Septemba 15, 2025, Jeshi la Polisi lilitangaza kuwa limefungua jalada la uchunguzi na linaendelea kuchunguza tuhuma hizo ambazo kada huyo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) amekuwa akizitoa.  "Tuhuma ambazo ametoa na anaendelea kuzitoa, kulingana na jinsi alivyozielezea, zinaashiria uwepo wa makosa ya jinai kwa mujibu wa sheria, makosa haya yanahitaji ushahidi wa kuzithibitisha zitakapowasilishwa mahakamani. Tuhuma hizo amekuwa akizitoa kupitia mitandao ya kijamii. Baada ya kufungua jalada na kuanza uchunguzi, Jeshi la Polisi, mbali na kukusanya ushahidi, limekuwa likifanya jitihada za kumpata ili aweze kutoa mael...

MULIRO AONYA WANAOPANGA KUANDAMANA NA KUFANYA VURUGU DSM Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amewaonya wale wote wanaopanga, kuratibu ama kutaka kushiriki kwenye uvunjifu wa amani ikiwemo kufanya vurugu na maandamano Oktoba 29, 2025, akisema Jeshi hilo limekula kiapo kulinda nchi pamoja na raia na mali zao. Kamanda Muliro ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Oktoba 24, 2025 wakati wa kongamano la Vyuo na Vyuo Vikuu kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, Kongamano lililofanyika kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza na kuwashirikisha wanafunzi wa shule za Sekondari, Vyuo na Vyuo Vikuu, akiwataka Vijana pia kuwa waangalifu na kutafakari kuhusu misukumo na mihemko yao kulingana na aina na makundi ama watu wanaoambatana nao. "Tukiwa kama watu tuliokula kiapo tunawaleza kuwa tutatimiza jukumu letu la kuhakikisha kuwa watu wanakuwa salama, watu wajitokeze kwa wingi kupiga kura, wafuate sheria na sisi tutakuwepo barabara kuwalinda wote wanaoenda kutimiza jukumu lao la Kikatiba la kwenda kupigakura. Siku hiyo kutakuwa hakuna maandamano wala hakuna vurugu, siku hiyo ni ya upigaji wa kura bila hofu."Amesema. Kama Muliro pia amesisitiza kuwa Vijana kuwa na fikra chanya ama hasi katika kujadili jambo fulani sio kitu kibaya ila kuipeleka mitazamo hasi kwenye vitendo vya vurugu ndiyo kosa kisheria, akiwataka pia Vijana kulinda hatma zao kwa kuhakikisha nchi inakuwa na amani ili kuwawezesha kutimiza malengo na ndoto zao kiuchumi, kisiasa na Kijamii.

Picha
Na Lubango Mleka, Dar es Salaam. KAMANDA wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amewaonya wale wote wanaopanga, kuratibu ama kutaka kushiriki kwenye uvunjifu wa amani ikiwemo kufanya vurugu na maandamano Oktoba 29, 2025, akisema Jeshi hilo limekula kiapo kulinda nchi pamoja na raia na mali zao. Kamanda Muliro ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Oktoba 24, 2025 wakati wa kongamano la Vyuo na Vyuo Vikuu kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, Kongamano lililofanyika kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza na kuwashirikisha wanafunzi wa shule za Sekondari, Vyuo na Vyuo Vikuu, akiwataka Vijana pia kuwa waangalifu na kutafakari kuhusu misukumo na mihemko yao kulingana na aina na makundi ama watu wanaoambatana nao. "Tukiwa kama watu tuliokula kiapo tunawaleza kuwa tutatimiza jukumu letu la kuhakikisha kuwa watu wanakuwa salama, watu wajitokeze kwa wingi kupiga kura, wafuate sheria na sisi tutakuwepo barabara kuwalinda wote wanaoenda kutimiza jukumu lao la Kikatiba la kwenda ...

VIONGOZI WA DINI WAKEMEA WANAOTAKA KUANDAMANA

Picha
Na Allan Kitwe, Tabora. VIONGOZI wa madhehebu ya dini kutoka Mikoa ya Tabora, Kigoma na Katavi wameiasa jamii kutojihusisha na vitendo vya uvunjifu amani ikiwemo kushiriki maandamano yanayolenga kuvuruga amani na utulivu wa nchi. Wakiongea katika Kongamano Maalumu la Amani lililofanyika leo katika ukumbi wa Panasonic Mjini Tabora wameeleza kuwa maandamano na vurugu hayajengi bali yanabomoa misingi ya amani na kuongeza chuki na uhasama. Akifungua Kongamano hilo Shehe wa Mkoa wa Tabora Ibrahimu Mavumbi ambaye pia ni Mwenyekiti Mwenza wa Kamati ya Maridhiano ya Amani ya Mkoa amesema kuwa amani ni tunu muhimu sana kwa maendeleo ya taifa lolote lile. Amesisistiza kuwa ni muhimu sana jamii ikaelimishwa umuhimu wa kudumisha amani na upendo na kujiepusha na vitendo vyovyote vinavyoashiria uvunjifu wa amani katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu Oktoba 29. ‘Watanzania tusikubali kuliingiza taifa kwenye machafuko, kipindi hiki tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na ...