Machapisho

VIONGOZI WA DINI SINGIDA NA DODOMA WAHIMIZA VIJANA KULINDA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

Picha
Na Hamida Ramadhan, Dodoma. VIONGOZI wa Dini kutoka mikoa ya Singida na Dodoma wamewataka vijana kuepuka vishawishi vya vurugu na mifarakano ya kisiasa, wakisisitiza kuwa kulinda amani ni jukumu la kila Mtanzania kadri Taifa linavyoelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika wiki ijayo. Wito huo umetolewa leo jijini Dodoma katika kongamano la viongozi wa dini mbalimbali kutoka Kanda ya Kati, lililolenga kuliombea Taifa amani na utulivu kuelekea uchaguzi huo. Akizungumza katika kongamano hilo, Askofu Evance Chande wa Kanisa la Carmel Assemblies of God amesema vijana wanapaswa kutumia nguvu zao katika kujenga Taifa badala ya kushiriki katika vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama wa nchi. “Tunapaswa kuikumbatia amani kama tunavyokumbatia imani zetu. Uchaguzi ukipita, Tanzania inabaki kuwa moja. Tusikubali kugawanywa kwa misingi ya kisiasa,” amesema Askofu Chande. Kwa upande wake, Sheikh Mustapha Rajab, Sheikh wa Mkoa wa Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati ...

MUNDE TAMBWE AENDELEA KUHAMASISHA USHINDI WA CCM SKON

Picha
  Na Hamida Ramadhani. MJUMBE wa NEC na aliyekuwa mtia nia wa ubunge Jimbo la Skonge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Munde Tambwe, ameendelea kujikita katika jimbo hilo akihamasisha wananchi kuichagua CCM katika uchaguzi ujao. Amesema sababu kuu ya kuichagua CCM ni mafanikio makubwa yaliyopatikana chini ya uongozi wake, ikiwemo ujenzi wa kituo cha afya, shule, na miundombinu ya barabara, pamoja na uwezeshaji wa wananchi katika sekta ya kilimo. Munde amewataka wananchi waendelee kuiamini CCM kama chama kinachotekeleza ahadi zake na kuboresha maisha ya Watanzania.

POLISI WAANZA UCHUNGUZI KUHUSU KUTEKWA KWA POLEPOLE, WAKISISITIZA KUMUHITAJI KWA DCI

Picha
Na Hamida Ramadhani, Dodoma. JESHI la Polisi nchini Tanzania, kupitia kwa Msemaji wake DCP David Misime, limesisitiza kuwa bado linaendelea kumsubiri Ndugu Humphrey Polepole ili aripoti katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), kwa ajili ya kutoa maelezo kuhusu tuhuma mbalimbali alizozitoa kupitia mitandao yake ya kijamii. Ikumbukwe kuwa mnamo Jumatatu, Septemba 15, 2025, Jeshi la Polisi lilitangaza kuwa limefungua jalada la uchunguzi na linaendelea kuchunguza tuhuma hizo ambazo kada huyo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) amekuwa akizitoa.  "Tuhuma ambazo ametoa na anaendelea kuzitoa, kulingana na jinsi alivyozielezea, zinaashiria uwepo wa makosa ya jinai kwa mujibu wa sheria, makosa haya yanahitaji ushahidi wa kuzithibitisha zitakapowasilishwa mahakamani. Tuhuma hizo amekuwa akizitoa kupitia mitandao ya kijamii. Baada ya kufungua jalada na kuanza uchunguzi, Jeshi la Polisi, mbali na kukusanya ushahidi, limekuwa likifanya jitihada za kumpata ili aweze kutoa mael...

MULIRO AONYA WANAOPANGA KUANDAMANA NA KUFANYA VURUGU DSM Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amewaonya wale wote wanaopanga, kuratibu ama kutaka kushiriki kwenye uvunjifu wa amani ikiwemo kufanya vurugu na maandamano Oktoba 29, 2025, akisema Jeshi hilo limekula kiapo kulinda nchi pamoja na raia na mali zao. Kamanda Muliro ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Oktoba 24, 2025 wakati wa kongamano la Vyuo na Vyuo Vikuu kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, Kongamano lililofanyika kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza na kuwashirikisha wanafunzi wa shule za Sekondari, Vyuo na Vyuo Vikuu, akiwataka Vijana pia kuwa waangalifu na kutafakari kuhusu misukumo na mihemko yao kulingana na aina na makundi ama watu wanaoambatana nao. "Tukiwa kama watu tuliokula kiapo tunawaleza kuwa tutatimiza jukumu letu la kuhakikisha kuwa watu wanakuwa salama, watu wajitokeze kwa wingi kupiga kura, wafuate sheria na sisi tutakuwepo barabara kuwalinda wote wanaoenda kutimiza jukumu lao la Kikatiba la kwenda kupigakura. Siku hiyo kutakuwa hakuna maandamano wala hakuna vurugu, siku hiyo ni ya upigaji wa kura bila hofu."Amesema. Kama Muliro pia amesisitiza kuwa Vijana kuwa na fikra chanya ama hasi katika kujadili jambo fulani sio kitu kibaya ila kuipeleka mitazamo hasi kwenye vitendo vya vurugu ndiyo kosa kisheria, akiwataka pia Vijana kulinda hatma zao kwa kuhakikisha nchi inakuwa na amani ili kuwawezesha kutimiza malengo na ndoto zao kiuchumi, kisiasa na Kijamii.

Picha
Na Lubango Mleka, Dar es Salaam. KAMANDA wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amewaonya wale wote wanaopanga, kuratibu ama kutaka kushiriki kwenye uvunjifu wa amani ikiwemo kufanya vurugu na maandamano Oktoba 29, 2025, akisema Jeshi hilo limekula kiapo kulinda nchi pamoja na raia na mali zao. Kamanda Muliro ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Oktoba 24, 2025 wakati wa kongamano la Vyuo na Vyuo Vikuu kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, Kongamano lililofanyika kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza na kuwashirikisha wanafunzi wa shule za Sekondari, Vyuo na Vyuo Vikuu, akiwataka Vijana pia kuwa waangalifu na kutafakari kuhusu misukumo na mihemko yao kulingana na aina na makundi ama watu wanaoambatana nao. "Tukiwa kama watu tuliokula kiapo tunawaleza kuwa tutatimiza jukumu letu la kuhakikisha kuwa watu wanakuwa salama, watu wajitokeze kwa wingi kupiga kura, wafuate sheria na sisi tutakuwepo barabara kuwalinda wote wanaoenda kutimiza jukumu lao la Kikatiba la kwenda ...

VIONGOZI WA DINI WAKEMEA WANAOTAKA KUANDAMANA

Picha
Na Allan Kitwe, Tabora. VIONGOZI wa madhehebu ya dini kutoka Mikoa ya Tabora, Kigoma na Katavi wameiasa jamii kutojihusisha na vitendo vya uvunjifu amani ikiwemo kushiriki maandamano yanayolenga kuvuruga amani na utulivu wa nchi. Wakiongea katika Kongamano Maalumu la Amani lililofanyika leo katika ukumbi wa Panasonic Mjini Tabora wameeleza kuwa maandamano na vurugu hayajengi bali yanabomoa misingi ya amani na kuongeza chuki na uhasama. Akifungua Kongamano hilo Shehe wa Mkoa wa Tabora Ibrahimu Mavumbi ambaye pia ni Mwenyekiti Mwenza wa Kamati ya Maridhiano ya Amani ya Mkoa amesema kuwa amani ni tunu muhimu sana kwa maendeleo ya taifa lolote lile. Amesisistiza kuwa ni muhimu sana jamii ikaelimishwa umuhimu wa kudumisha amani na upendo na kujiepusha na vitendo vyovyote vinavyoashiria uvunjifu wa amani katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu Oktoba 29. ‘Watanzania tusikubali kuliingiza taifa kwenye machafuko, kipindi hiki tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na ...

RC MANYARA AWAPONGEZA FRANONE MINING NA CHUSA MINING KWA CSR

Picha
  Na Mwandishi wetu, Mirerani  MKUU wa Mkoa wa Manyara, Queen Cuthbert Sendiga amezipongeza kampuni mbili za Franone mining LTD na Chusa mining LTD kwa kusaidia miradi ya maendeleo katika utekelezaji wa uwajibikaji kwa jamii (CSR) kwenye sekta ya afya mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro. RC Sendiga akizungumza na wamiliki wa migodi ya madini ya Tanzanite kwenye ukumbi wa Mazubu Grand Hotel mji mdogo wa Mirerani, amesema makampuni hayo yanajitoa katika kufanikisha miradi ya maendeleo kupitia utekelezaji wa uwajibikaji kwa jamii (CSR). Ameeleza kwamba kampuni ya Franone mining LTD, imefanya vyema kwani imetenga shilingi milioni 80 kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ndani ya ukuta unazunguka migodi ya madini ya Tanzanite. "Pia niishukuru kampuni ya Chusa mining LTD, kwa kujenga wodi ya wanawake na watoto na ofisi ya wauguzi katika kituo cha afya Mirerani," amesema RC Sendiga. Hata hivyo, RC Sendiga amewataka wamiliki wa migodi ya madini ya Tanzanite kushiriki kuchangia shughul...

WAKULIMA WA MPUNGA WATAKIWA KUPIMA AFYA YA UDONGO IGUNGA

Picha
Na Lubango Mleka - Igunga. WAKULIMA wa skimu ya umwagiliaji wa mpunga Mwamapuli, wilayani Igunga, mkoa wa Tabora, wametakiwa kupima afya ya udongo katika mashamba yao ili kuongeza tija na kuendesha kilimo cha kibiashara. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa mashine za kisasa za kukoboa na kuvuna mpunga, Grace Nyamwanji, Mkuu wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wilayani Igunga, amewahimiza wakulima kuanza maandalizi mapema kwa msimu wa kilimo 2025/2026 na kutumia ushauri wa wataalamu wa kilimo.  "Tukipima afya ya udongo, tutapata mavuno bora na kilimo chetu kitakuwa biashara yenye faida," Grace Nyamwanji. Kwa upande wake, Meneja wa Chama cha Ushirika cha Mwamapuli, Nkwabi Igessa, amesema mashine hizo zitasaidia kuongeza uzalishaji, kuleta ajira kwa wananchi na kuongeza mapato ya ushirika huo. Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Sauda Mtondoo, ambaye alikuwa mgeni rasmi, amewataka wakulima kubadilika na kuwekeza zaidi katika kilimo biashara na teknolojia za kisasa ili kuongeza tha...

USAFIRI WA SGR DAR ES SALAAM- DODOMA WAREJEA, TRC YAOMBA RADHI KWA USUMBUFU

Picha
  Na Hamida Ramadhani, Dodoma. SHIRIKA la reli Tanzania limeufahamisha umma wa Watanzania kuwa huduma za usafiri wa treni za SGR zimerejea na kuendelea kama kawaida, likiomba radhi kwa wateja wake kwa usumbufu uliojitokeza, shirika likiwashukuru pia Wananchi kwa uvumilivu wao katika kipindi ambacho huduma za usafiri huo zilipotatizika kutokana na hitilafu iliyotokea mapema leo Alhamisi Oktoba 23, 2025. Mapema leo Shirika la Reli Tanzania lilitoa taarifa kwa Vyombo vya habari likieleza kuhusu ajali ya Treni ya EMU iliyokuwa ikisafiri kutoka Dar Es Salaam kwenda Dodoma majira ya saa mbili asubuhi kutokana na hitilafu za uendeshaji, tukio ambalo lilitokea Kituo cha Ruvu na kwa taarifa za shirika hilo hakukuwa na athari kubwa za ajali hiyo. Timu ya wataalamu ikiongozwa na Katibu Mkuu wa uchukuzi, Mkurugenzi wa shirika la TRC, Vyombo vya ulinzi na usalama na menejimenti ya TRC ilianza haraka kushughulikia changamoto hiyo na kufanya uchunguzi wa kina wa kuhakikisha kuwa huduma hizo zimer...

DKT.ABBASI, MWAKILISHI MKAZI UNDP WAZINDUA UBORESHAJI MISITU NCHINI.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam. SERIKALI imezindua rasmi utekelezaji wa mradi mkubwa wa kimataifa wa mazingira ujulikanao kama “Mbinu Chanya na Jumuishi za Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi na Kulinda Bayoanuai” (Integrated Net-Zero Nature-Positive Solutions for Climate and Biodiversity Protection), unaolenga kuendeleza sekta ya misitu kwa lengo la kuinua maisha ya watu. Akizungumza leo Oktoba 23,2025 jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa kikao cha kwanza cha Kamati ya Usimamizi wa Mradi huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi, ambaye ni Mwenyekiti alisema mradi huo wenye thamani ya Dola za Marekani milioni 38 ni uthibitisho wa kuaminiwa kwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. “Mradi huu ni ushahidi wa juhudi za Serikali katika kulinda mazingira, kuhifadhi misitu na kuhamasisha nishati safi. Dunia inatambua uongozi wa Tanzania katika masuala ya uchumi wa kijani ndio maana baadhi ya wadau wa Mradi huu pamoja ...