Machapisho

DKT. MATARAGIO AAGIZA VIFAA VYOTE VYA UHAKIKI WA JOTOARDHI ZIWA NGOZI KUFIKA KWA WAKATI

Picha
  Ni baada ya kukagua mradi na kukuta baadhi ya vifaa bado havijafika Asisitiza mradi kukamilika kwa wakati ikiwa ni  utekelezaji wa Sera ya Nishati ya mwaka 2015 Kazi ya uhakiki wa Jotoardhi Ziwa Ngozi yafikia asilimia 60. Na Mwandishi Wetu, Mbeya. NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio ameliagiza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Kampuni yake Tanzu ya Uendelezaji Jotoardhi (TGDC)  kuhakikisha kuwa vifaa vyote vya uhakiki wa rasilimali Jotoardhi  katika mradi wa Ziwa Ngozi  vinafika kwa wakati ili kazi za uhakiki  ziweze kumalizika kulingana na muda uliopangwa. Dkt. Mataragio ametoa maagizo hayo leo Oktoba 22, 2025 wakati wa ziara yake ya kukagua kazi zinazoendelea kutekelezwa katika mradi huo wilayani Rungwe mkoani Mbeya. “Huu mradi mnapaswa kuukamilisha kwa wakati kutokana na umuhimu wake nchini, tunapotekeleza miradi hii ya Jotoardhi tukumbuke kuwa tunatekeleza pia Sera ya Taifa ya Nishati ya Mwaka 2015 ambayo inasema Tanzania in...

WANAFUNZI WATAKIWA KUDUMISHA AMANI NA MSHIKAMANO

Picha
Na Mwandishi Wetu, Mara. AFISA Ushirikishwaji Jamii Mkoa wa Mara, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Thomas Mapuli, Oktoba 22,2025 amekutana na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mshikamano iliyopo katika Manispaa ya Musoma, ambapo ametoa elimu juu ya ukatili wa kijinsia na umuhimu wa kutunza amani katika jamii. Akizungumza na wanafunzi hao shuleni hapo ACP Mapuli aliwasisitiza vijana kuwa mabalozi wa amani na kuzingatia maadili mema, huku akiwataka kujiepusha na vitendo vya vurugu, ubaguzi, na ukatili wa aina yoyote, ikiwemo ule wa kijinsia. Aidha, aliwahimiza wanafunzi kuzingatia masomo yao na kuepuka vishawishi vinavyoweza kuhatarisha ndoto zao za baadaye, akibainisha kuwa elimu ndiyo ngao kuu ya kupambana na changamoto mbalimbali za kijamii na kiuchumi. “Jamii yenye amani huanza na mtu mmoja mmoja. Ninyi kama vijana mna wajibu wa kuwa mfano wa kuigwa, kujilinda na kuwalinda wengine dhidi ya ukatili wa kijinsia, na kushirikiana na vyombo vya dola kutoa taarifa za vitendo hivyo pindi vin...

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI

Picha
Na Hamida Ramadhani, Dodoma. SERIKALI kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano, ambapo baadhi ya minara hiyo itajengwa katika maeneo ya mipakani, mbuga za wanyama, na njia kuu za reli za SGR na TAZARA. Hatua hii inalenga kuhakikisha huduma za mawasiliano zinapatikana katika maeneo yote yenye umuhimu wa kimkakati kwa usalama, utalii na maendeleo ya Taifa. Mtendaji Mkuu wa UCSAF, Mhandisi Peter Mwasalyanda, amesema utekelezaji wa awamu hiyo mpya unafuatia mafanikio makubwa ya mradi wa awali wa minara 758, ambao umefikia zaidi ya asilimia 98 ya utekelezaji. Ameeleza kuwa kukamilika kwa mradi huo kumechangia kupunguza kwa kiasi kikubwa pengo la mawasiliano katika maeneo ya vijijini na pembezoni. Jumla ya vijiji 1,407 ambavyo awali havikuwa na mawasiliano, sasa vinafikishiwa huduma hiyo muhimu, hatua inayoboresha maisha ya wananchi na kuongeza fursa za kiuchumi. Aidha, Mhandisi Mwasalyanda ameongeza kuwa...

WAFCON QUALIFIERS 2026

Picha
23’ Tanzania 🇹🇿 1️⃣-0️⃣ 🇪🇹 Ethiopia  ⚽️Aisha Mnunka  @twigastars_ @caf_online

WANAWAKE WA TEMEKE WAANZA SHAMRASHAMRA ZA KUMPOKEA MGOMBEA WA URAIS DKT. SAMIA

Picha
Na Hamida Ramadhani, Dar es Salaam. MWENYEKITI wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT) Ndg. Mary Pius Chatanda (MCC) ambaye pia ni Mratibu wa Kampeni za CCM Jijini DSM, Leo tarehe 19 Oktoba, 2025, apokelewa na matembezi ya Wanachama wa UWT Wilaya ya Temeke yaliyoambatana na Ngoma kuelekea kwenye Ukumbi wa Taifa Pub, Kata ya Mibulani, kwa lengo la kufanya Kikao na wajumbe wa Baraza la UWT Wilaya ya Temeke, ili kujiweka sawa na Mapokezi ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mgombe Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), katika kufanya Mikutano ya Kampeni ndani ya Jiji la DSM, na kunadi ilani ya CCM 2025/2030 na kuomba kura za ndiyo kwa Wananchi kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025.   (

CHATANDA AWAHAMASISHA WANAKIGAMBONI OKTOBA 29, 2025 KWENDA KUPIGA KURA NA KUMCHAGUA DKT. SAMIA

Picha
Na Hamida Ramadhani, Dar es Salaam. MENYEKITI wa UWT Taifa, Ndg. Mary Pius Chatanda (MCC) ameambatana na Katibu Mkuu wa UWT Taifa, Ndg. Suzan Peter Kunambi (MNEC). leo tarehe 18 Oktoba, 2025, katika Viwanja vya Tungi Mnadani, Wilaya ya Kigamboni, amewaomba wananchi wa Kigamboni kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi la kupiga kura Oktoba 29, 2025, na kuhakikisha wanapiga kura kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na wagombea wa Ubunge na Udiwani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).  Aidha, Chatanda amewahimiza wananchi, hususani vijana wa Jimbo la Kigamboni, kutobabaishwa na Wagombea Wengine kwasababu Dkt. Samia amejipambanua kwa Kazi zake. Kauli hiyo aliitoa wakati akizungumza na wananchi waliojitokeza kushiriki Bonanza la Mazoezi ya Kutembea (Jogging) na Michezo Mbalimbali lililoandaliwa na Ofisi ya  Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Ndg. Dalmia Mikaya.

VIONGOZI WA VYAMA VYA USHIRIKA IGUNGA WAPATIWA MAFUNZO YA UONGOZI NA USIMAMIZI VYAMA VYA USHIRIKA.

Picha
  Na Lubango Mleka, Igunga - Tabora. KATIKA kuhakikisha kuwa vyama vya ushirika vinaendeshwa kwa weledi na kuzingatia sheria, Chama Kikuu cha Ushirika Mkoa wa Tabora (IGEMBENSABO) kimeandaa mafunzo ya siku nne kwa viongozi wa vyama vya ushirika wilayani Igunga. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Kaimu Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Tabora, Jerude Juma Magubiko, amewataka viongozi hao kufuata sheria, kanuni na misingi ya ushirika katika kuendesha vyama vyao. Kwa upande wao, viongozi wa IGEMBENSABO waliowezesha mafunzo hayo wametoa wito kwa washiriki kuyachukulia kwa uzito mkubwa ili wawe mabalozi wa mabadiliko ndani ya vyama vyao. Washiriki wa mafunzo hayo kutoka vyama mbalimbali vya ushirika (AMCOS) wilayani Igunga wameeleza kufurahishwa na mafunzo hayo, wakisema yatawasaidia kuimarisha utendaji wa kila siku. Huku baadhi yao wakitoa maoni yao ni pamoja na Adelina Blazi (Katibu Meneja Balimi AMCOS), Maria Ramadhani Makamu Mwenyekiti  Mwamapuli AMCOS...