Machapisho

CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE 2025 BAADHI YA VINARA WA KURA ZA MAONI WAACHWA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) kimetangaza orodha ya makada waliopitishwa kuwania ubunge katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 baada ya mchujo uliofanywa na vikao vya juu  vya chama hicho.  Wakati baadhi ya majina yakiendelea na safari ya kisiasa, waliokuwa vinara kwenye kura za maoni wamejikuta wakiondolewa katika hatua za mwisho. Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa anayeshughulikia Itikadi, Uenezi na Mafunzo Amos Makalla amesema uteuzi huo umefanywa na vikao vya maamuzi vilivyoongozwa na Mwenyekiti wa CCM ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan. Makalla amesema baadhi ya waliokuwa wakiongoza kwenye kura za maoni lakini majina yao hayakurudishwa ni pamoja na aliyekuwa Mbunge wa Tanga Mjini Ummy Mwalimu na Samuel Malecela ambaye aliongoza kura za maoni katika Jimbo la Dodoma Mjini. Katika Jimbo la Kigoma Mjini, chama kimempitisha Clinton Revocutus maarufu kama Baba Leo licha ya kutoshinda katika kura za maoni. Hali ...

CHAMA CHA MAPINDUZI CCM TAIFA CHATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA NAFSI YA UBUNGE 2025 NA WATEULIWA WA NAFASI MBALI MBALI NDANI YA CHAMA HICHO.

Picha
 

BODI YA USHAURI TARURA YAIPA HEKO SERIKALI UJENZI DARAJA LA MOHORO

Picha
Na Mwandishi Wetu, Rufiji.  MWENYEKITI wa Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), Mhandisi Florian Kabaka ameishukuru Serikali kwa kuwezesha Wakala huo kutekeleza ujenzi wa daraja la Mohoro lenye urefu wa Mita 100 wilayani Rufiji. Mhandisi Kabaka ameyasema hayo wakati wa ziara ya kutembelea ujenzi wa daraja hilo pamoja na ujenzi wa barabara za lami zenye urefu wa Km. 4 zinazojengwa katika mji wa Ikwiriri wilayani humo. “Niipongeze serikali kwa uwezeshaji huu kwa TARURA, kwakweli uwepo wake hata wananchi wanaishukuru kwa kufungua miundombinu kila mahali, nitoe heko kwa serikali kwa kuendelea kutoa fedha kwa TARURA pia nitoe heko kwa menejimenti ya TARURA kwa usimamizi”. Aidha, amewataka wananchi wa eneo hilo kulitunza daraja hilo pamoja na vifaa vyote vinavyozunguka, pia kutochezea tuta la daraja hilo kwani linaenda kuleta uhakika wa mawasiliano yao kwa mwaka mzima hususan kipindi cha mvua. “Daraja hili linaenda kuwaondolea shida iliyodumu kwa miaka min...

KESI YA LISSU YAPELEKWA MAHAKAMA KUU.

Picha
Na Lubango Mleka, Dar es Salaam.  KESI ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu, sasa imepelekwa Mahakama Kuu. Hatua hiyo imekuja baada ya Hakimu Franco Kiswaga jana kubaini kuwa Lissu ana kesi ya kujibu, katika shauri lililosomwa kwa takribani saa 8 katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.  Lissu anatuhumiwa kwa kosa la uhaini, kinyume na kifungu cha 39(2)(d) cha Kanuni ya Adhabu, akidaiwa kulitenda Aprili 3 mwaka huu jijini Dar es Salaam.  Katika usikilizwaji wa jana, mashahidi 30 walitoa ushahidi wao. Hata hivyo,mara baada ya mwenendo wa kesi hiyo,  mjadala mkubwa umeibuka kuhusu uamuzi wa mahakama kupiga marufuku urushaji wa moja kwa moja wa kesi hiyo. Endelea kutuatilia habarikamilitv.blogspot.com 

WANANCHI RORYA WAHIMIZWA KUTUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Rorya Mara.  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Ndugu Ismail Ali Ussi amewahimiza wananchi wa Wilaya ya Rorya kutumia nishati safi ya kupikia katika maeneo yao kutokana na faida mbalimbali zinazopatikana kwa kutumia nishati safi.  Akizungumza na wananchi katika Shule ya Sekondari Nyamunga, baada ya kutembelea mradi wa nishati safi wa shule hiyo, Ndugu Ussi amesema kwa kupikia nishati safi wananchi watapika kwa gharama nafuu na pia watakuwa wanatunza mazingira.  “Nishati safi inasaidia sana kwani gharama zake ni nafuu, haiathiri afya ya mtumiaji kama ilivyo katika matumizi ya kuni na mkaa na inasaidia kutunza mazingira yanayotuzunguka, hivyo ni muhimu sisi sote kutumia nishati safi majumbani mwetu” amesema Ndugu Ussi.  Ndugu Ussi ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kwa kuwekeza fedha shilingi milioni 11 kwa ajili ya kutekeleza mradi huo katika Shule ya Sekondari Nyamunga ambao amesema unalinda afya za wapishi na mazingira ya Halmashauri hiyo...

HANDENI MJI YAJA NA MWAROBAINI WA UTORO SHULENI.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Handeni HALMASHAURI ya Mji Handeni, mkoani Tanga kupitia Idara ya Elimu Msingi imepongezwa kwa kubuni mkakati maalum unaoongeza uwajibikaji wa wazazi katika kukabiliana na utoro shuleni. Pongezi hizo zimetolewa Agosti 18, 2025 mjini hapa na Mkuu wa Wilaya ya Handeni, mkoani Tanga, Mhe. Salum Nyamwese katika kikao na Menejimenti ya Halmashauri hiyo (CMT). Amesema mkakati huo unaongeza ushiriki wa wazazi na viongozi wa mtaa na kata katika kufuatilia kwa karibu maendeleo ya wanafunzi ili kudhibiti utoro kwa shule za msingi na kwamba ubunifu huo pia utafanyika kwa shule za sekondari. Amesisitiza watumishi wa halmashauri hiyo kuwa wabunifu katika utendaji kazi wao ili wananchi waendelee kupata huduma bora. Pamoja na hayo, Nyamwese amehimiza uwajibikaji, ushirikiano na kujiepusha kufanya kazi kwa mazoea ili matokeo yaonekane kwa wananchi. “Hakikisheni mnaweka mbele maslahi ya wananchi na taifa kwa kutoa huduma bora kwa wananchi wetu, sisi ni rasilimali ya umma kutokana na ...

TARURA MUSOMA WAPONGEZWA UJENZI WA MIRADI KULINGANA NA THAMANI YA FEDHA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Musaoma.  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa, Ndugu Ismail Ali Ussi amewapongeza wafanyakazi wa TARURA wilaya ya Musoma kwa kufanya kazi kwa weledi na kuhakikisha wanajenga miradi ya miundombinu ya barabara kulingana na thamani halisi ya fedha. Ndugu Ussi ameyasema hayo wakati akiweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa barabara ya Nyabisarye Mahakama kuu Kanda ya Musoma yenye urefu wa Mita 700 kwa kiwango cha lami . Ussi amesema kuwa Serikali  imekuwa ikitumia fedha nyingi katika ujenzi wa miundombinu ya barabara kwa lengo la kuwarahisishia wananchi huduma katika maeneno yao ili waweze kufanya shughuli zao za kiuchumi na kujiingizia kipato. Kwa upande wake  Kaimu Meneja Wilaya ya Musoma Mhandisi Mohamed Etanga amesema jumla ya shilingi Milioni 600.97 zimetengwa  kwaajili ya ujenzi wa barabara ya Nyabisarye- Mahakama Kuu yenye urefu wa Mita 700 kwa kiwango cha lami . Amebainisha kuwa ujenzi wa barabara hiyo ulianza Oktoba mwaka jana na unatarajiwa kuka...

KILIMANJARO YA SWEDEN YATWAA UBINGWA WA BONANZA LA SERENGETI NCHINI UBELGIJI.

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Ubelgiji.  TIMU ya soka ya Watanzania iitwayo Kilimanjaro kutoka Sweden imetwaa tena kwa mara ya nne mfululizo ubingwa wa kombe la Bonanza la Serengeti katika michuano iliyofanyika tarehe 15-16 Agosti, 2025, jijini Antwerp, Ubelgiji. Kilimanjaro ilitetea ubingwa wake baada ya kuifunga timu nyingine ya Watanzania kutoka Uingereza iitwayo Leeds Swahili mabao 2-1 kwenye mchezo mkali wa fainali. Magoli ya Kilimanjaro yalifungwa na Feisal Amir na Fryad Sabri huku la Leeds likifungwa na Murtaza Fuad. Hii ni mara ya tatu kwa timu hizi kukutana fainali. Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Mhe. Jestas Nyamanga, alimkabidhi kombe la ubingwa nahodha wa Kilimanjaro, Abbas Bachu, ambaye naye alimkabidhi Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Mobhare Matinyi, na kuibua shwange za washabiki wao. Kilimanjaro hushiriki ligi ya daraja la sita nchini Sweden katika mfumo wa madaraja saba. Michuano hiyo iliyofanyika kwa mara ya nne tangu mwaka 2021 na kudhaminiwa na Benki ya N...

UMOJA NA MSHIKAMANO VYATAWALA HOTUBA ZA VIONGOZI MKUTANO WA SADC

Picha
Na Mwandishi Wetu, Antananarivo.  MKUTANO wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) umehitimishwa jijini Antananarivo Agosti 17, 2025, huku viongozi hao wakihimizana, umoja, mshikamano na ushirikiano  kama njia ya msingi ya kujikwamua kiuchumi na kukabiliana na changamoto zinazoibuka kila siku ulimwenguni. Katika mkutano huo, Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan aliwakilishwa na Makamu wa Rais, Dkt. Philip Isdor Mpango, na kama ilivyo ada, mwenyeji wa mkutano huo, Madagascar alikabidhiwa uenyekiti wa jumuiya hiyo kutoka Zimbabwe. Mkutano huo ulihudhuriwa na wakuu wa nchi 9 ambapo Mwenyekiti aliyemaliza muda wake, mwenyekiti aliyopekea kijiti, Katibu Mtendaji wa SADC na wakuu wa nchi wanne wa Botswana, Namibia, Msumbiji na Mauritius kutokana na kushiriki kwao kwa mara ya kwanza kama wakuu wa nchi walipata fursa ya kuhutubia mkutano huo. Hotuba za viongozi hao ziligusia maeneo makubwa manne ambayo ni amani na usalama, ujenzi wa miundombinu, uchumi, demokrasia n...