Machapisho

MADALALI WA MINADA WATAKIWA KUJISAJINI KIELEKTRONIKI.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  WIZARA ya Fedha imeandaa Mfumo wa Kielektroniki wa utoaji Leseni za Udalali na Uendeshaji minada ya hadhara unaowezesha uombaji na upatikanaji wa Leseni kwa njia ya kielektroniki kwa kutumia simu za mkononi au kompyuta mpakato ili kuwaondolea wananchi adha na gharama ya kufuata leseni hizo jijini Dodoma. Akizungumza wakati akitoa elimu kwa wananchi waliotembelea Banda la Wizara ya Fedha kwenye Maonesho ya Nanenane Kitaifa katika Viwanja vya Nanenane, Jijini Dodoma, Msimamizi wa Mali za Serikali wizarani hapo, Bw. George Killo, alisema Mfumo huo utamuwezesha mwananchi kufanya usajili popote alipo hivyo kupata leseni yake kwa wakati. ‘‘Mwombaji wa leseni ya udalali anapaswa kujisajili kupitia Tovuti ya Wizara ya Fedha (www.mof.go.tz) na kisha kubonyeza kipengele cha GAMIS na kujisajili, kujaza taarifa zinazohitajika, kujaza fomu za maombi kikamilifu na kuwasilisha kwa Katibu Tawala wa Wilaya husika kwa ajili ya uhakiki na Saini,’’ alieleza Bw. Killo. Alise...

Total Energies CHAN 2024

Picha
FT’ Madagascar 0️⃣ - 0️⃣ Mauritania

RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA UTEUZI WA VIONGOZI MBALI MBALI.

Picha
 

MAONYESHO YA NANE NANE KANDA YA ZIWA MAGHARIBI 2025 YAFUNGULIWA RASMI

Picha
Na Lubango Mleka, Mwanza. MGENI rasmi Mhe. Hashimu Abdallah Komba, Mkuu wa Wilaya ya Geita akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Geita Ndg. Martin Shigela leo tarehe 03 Agosti 2025, amefungua rasmi maonesho ya Nanenane kanda ya ziwa Magharibi yanayofanyika viwanja vya Nyamhongolo Wilaya ya Ilemela ambapo amesema kila mmoja anao wajibu wa kutembelea maonesho haya ya nane nane kwa ajili ya kujifunza lakini pia kujioatia bidhaa mbalimbali.  “Kama ni mkulima utapata fursa ya kujifunza kilimo cha kisasa na Chenye tija na kama ni mvuvi pia unaweza kujifunza shughuli za uvuvi kwa teknolojia ya kisasa hivyo msiache kutembelea mabanda mbali mbali kujipatia elimu na uzoefu ” Alilisitiza muwakilishi huyo wa mgeni rasmi Mhe Komba.  Akifafanua kauli mbiu ya maonyesho ya Nanenane Mwaka huu “Chagua viongozi bora kwa maendeleo endelevu ya kilimo, mifugo na uvuvi 2025” amewataka wananchi kushiriki uchaguzi mkuu kwa amani na utulivu na kuchagua viongozi bora watakaowaletea maendeleo.

PPAA YASHIRIKI MAONESHO YA NANENANE, KUTOA ELIMU KWA WAZABUNI NA UMMA.

Picha
 Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  MAMLAKA ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) inashiriki Maonesho ya NaneNane Kitaifa yanaendelea katika Viwanja vya Maonesho vya Nzuguni Jijini Dodoma kutoa elimu kuhusu ununuzi wa Umma kwa wazabuni, hususan elimu kuhusu Moduli ya kupokea na kushughulikia Malalamiko na Rufaa katika mfumo wa NeST.  Akiongea kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa PPAA, James Sando, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma, Nelson Kessy amesema PPAA imejipanga kutoa elimu kwa wadau wa ununuzi wa umma na wananchi kwa ujumla ili kutoa wigo mpana zaidi kwa wazabuni na wadau wa sekta hiyo.  Pamoja na mambo mengine, Kessy amewasihi wadau wa ununuzi na wananchi kwa ujumla kutembelea Banda la PPAA linalopatikana ndani ya Banda la Wizara ya Fedha katika viwanja vya Nzuguni, Dodoma. Maonesho haya kwa mwaka 2025 yamebeba kauli mbiu “Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi 2025”. Maonesho ya NaneNane Kitaifa yalifunguliwa rasmi t...

GST YATOA USHAURI NA UPIMAJI SAMPULI ZA MAJI, MIAMBA NA MADINI.

Picha
Wizara ya Madini yaendelea kutoa elimu ya Sheria, Kanuni za Madini.  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  TAASISI ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) imeendelea kutoa ushauri na huduma za upimaji wa sampuli za miamba na madini kwa wananchi mbalimbali wanaofika kutaka kujua aina za miamba na madini waliokuwanayo. Aidha, GST imekuja na vifaa vya utafiti wa miamba na madini iliyo chini ya tabaka ya juu la udongo ambavyo kitaalam vinaitwa vifaa vya jiofizikia. Sambamba na hayo, Wataalamu kutoka GST wamewashauri wananchi kutumia Maabara ya taasisi hiyo kwa uchunguzi wa sampuli zao za miamba na madini ili kubaini wingi na uwepo wa madini ili kuongeza tija na uzalishaji wa madini. Aidha, Wizara ya Madini kwa kushirikiana na taasisi zake imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu masuala mbalimbali ya sekta ya madini kupitia banda lake lililopo katika eneo la mabanda ya Serikali, banda namba 5. Kupitia banda hilo, wananchi wanaelimishwa kuhusu shughuli mbalimbali zinazohusu sekt...

KATIBU MKUU MIFUGO, UVUVI AHIMIZA UTOAJI ELIMU KWA UMMA KUHUSU SHUGHULI ZA OFISI YA WAZIRI MKUU.

Picha
Na Mwandishi Wetu, DODOMA.  KATIBU Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena ametoa rai kwa Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu waendelee kutoa elimu kwa wananchi kuhusu utendaji wa taasisi na programu mbalimbali zinazosimamiwa na Ofisi hiyo. Kauli hiyo ameitoa leo tarehe 02 Agosti, 2025 alipotembelea banda la Ofisi hiyo akiwa ameambatanan na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Dkt. Stephen Nindi na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Jabir Shekimweri katika Maonesho ya Naneane yanayofanyika Viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma. “Wananchi wanauhitaji Mkubwa wa kufahamu shughuli zinazoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, hivyo kuna umuhimu wa kuandaa vipindi vya kuelimisha umma,” ameeleza. Maonesho ya Wakulima maarufu Nanenane yamebebwa na kauli mbiu isemayo: "Chagua Viongozi Bora, kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi 2025"

KARIBU BANDA LA HALMASHURI YA IGUNGA KWENYE MAONESHO YA NANE NANE MKOANI TABORA.

Picha
 

COOP BANK YAJIVUNIA UTOAJI HUDUMA SEKTA YA KILIMO.

Picha
. Coop Bank yatangaza Ushiriki Mkubwa katika Maonesho ya Nanenane, Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  BENKI ya Ushirika Tanzania (Coop Bank) imethibitisha kushiriki kikamilifu katika Maonesho ya Kitaifa na Kimataifa ya Nanenane 2025 yanayofanyika katika viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma, ikiwa ni miongoni mwa wa  dhamini wa maonesho hayo makubwa ya kilimo nchini. Akizungumza na waandishi wa habari katika banda la benki hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Coop Bank, Bw. Godfrey Ng’urah, amesema benki hiyo imejikita katika kutoa huduma za kifedha zenye kuleta mabadiliko chanya katika mnyororo mzima wa thamani wa kilimo-biashara, huku ikitoa kipaumbele kwa wakulima, vijana na wajasiriamali wa vijijini. “Coop Bank ni benki ya ushirika kwa vitendo. Zaidi ya asilimia 51 ya umiliki wake upo mikononi mwa vyama vya ushirika hii ni benki ya wakulima, kwa wakulima,” amesema Bw. Ng’urah. Ameeleza kuwa, Benki hiyo inashirikiana na vyama vya msingi (AMCOS) na vyama vikuu vya ushirika (UNION) nchini kote...

DKT. MPANGO AZINDUA MAONESHO YA 32 NANENANE KITAIFA JIJINI DODOMA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango amezindua rasmi Maonesho ya 32 ya Wakulima (Nanenane) yanayofanyika kitaifa katika Viwanja vya Nanenane, Nzuguni, jijini Dodoma yenye kauli mbiu isemayo "Chagua Viongozi bora kwa Maendeleo Kilimo, Mifugo na Uvuvi 2025". Dkt. Mpango amesema kuwa Tanzania inaadhimisha Maonesho ya 32 ya Nanenane yenye hadhi ya Kitaifa na Kimataifa kwa lengo la kukuza uchumi na kuchochea matumizi ya teknolojia bora na kuimarisha ushirikiano wa kimataifa. Tangu asubuhi ya leo, maelfu ya wananchi kutoka mikoa mbalimbali wamejitokeza kutembelea banda ya Wizara ya Madini na Taasisi zake, wakipata elimu juu ya mchango wa sekta ya madini katika kuimarisha uchumi wa wakulima na taifa kwa ujumla. Banda la wizara hiyo limepambwa na taarifa mbalimbali za kitaalamu kuhusu uongezaji thamani madini, usalama wa wachimbaji wadogo, fursa za uwekezaji, na matumizi ya teknolojia bunifu katika sekta ya madini. Akizungum...

TADB YATOA MIKOPO KWA WAZALISHAJI NA WACHAKATAJI 762,291.

Picha
  IMEELEZWA KUWAMNYORORO WA THAMANI UMEKUWA KWA WAKULIMA NA WACHAKATAJI.  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  BENKI ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kupitia Mfuko wa Dhamana kwa Wakulima Wadogo, imefanikiwa kuwafikia zaidi ya wanufaika 762,291 nchi nzima, kwa kuwasaidia kupata mikopo kupitia taasisi za kifedha bila hitaji la dhamana kubwa. Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dodoma kwenye maonesho ya wakulima na wafugaji Kitaifa  Rosemary  Gordon Afisa Biashara wa TADB anayesimamia mfuko huo, alieleza kuwa mfuko huo unatekelezwa kwa ushirikiano na benki 13 za biashara, benki za ushirika, na taasisi nyingine za kifedha nchini.  “Mfuko huu unahakikisha kuwa wakulima wadogo, hata wale wasio na dhamana ya kutosha, wanapata mikopo ya kuwawezesha kuendesha shughuli zao za kilimo kutoka shambani hadi sokoni,” akisema Gordon. Amesema mikopo inayodhaminiwa na mfuko huo husaidia wakulima kununua pembejeo kama mbegu, viuatilifu na mbolea, pamoja na dhana za kilim...

TAIFA STARS YAPATA MAFUNZO YA UADILIFU MICHEZONI.

Picha
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) leo wamepata mafunzo ya Uadilifu michezoni kuelekea mashindano ya CHAN 2024, yanayotarajiwa kuanza 02 Agosti 2025.