Machapisho

GST YATOA USHAURI NA UPIMAJI SAMPULI ZA MAJI, MIAMBA NA MADINI.

Picha
Wizara ya Madini yaendelea kutoa elimu ya Sheria, Kanuni za Madini.  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  TAASISI ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) imeendelea kutoa ushauri na huduma za upimaji wa sampuli za miamba na madini kwa wananchi mbalimbali wanaofika kutaka kujua aina za miamba na madini waliokuwanayo. Aidha, GST imekuja na vifaa vya utafiti wa miamba na madini iliyo chini ya tabaka ya juu la udongo ambavyo kitaalam vinaitwa vifaa vya jiofizikia. Sambamba na hayo, Wataalamu kutoka GST wamewashauri wananchi kutumia Maabara ya taasisi hiyo kwa uchunguzi wa sampuli zao za miamba na madini ili kubaini wingi na uwepo wa madini ili kuongeza tija na uzalishaji wa madini. Aidha, Wizara ya Madini kwa kushirikiana na taasisi zake imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu masuala mbalimbali ya sekta ya madini kupitia banda lake lililopo katika eneo la mabanda ya Serikali, banda namba 5. Kupitia banda hilo, wananchi wanaelimishwa kuhusu shughuli mbalimbali zinazohusu sekt...

KATIBU MKUU MIFUGO, UVUVI AHIMIZA UTOAJI ELIMU KWA UMMA KUHUSU SHUGHULI ZA OFISI YA WAZIRI MKUU.

Picha
Na Mwandishi Wetu, DODOMA.  KATIBU Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena ametoa rai kwa Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu waendelee kutoa elimu kwa wananchi kuhusu utendaji wa taasisi na programu mbalimbali zinazosimamiwa na Ofisi hiyo. Kauli hiyo ameitoa leo tarehe 02 Agosti, 2025 alipotembelea banda la Ofisi hiyo akiwa ameambatanan na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Dkt. Stephen Nindi na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Jabir Shekimweri katika Maonesho ya Naneane yanayofanyika Viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma. “Wananchi wanauhitaji Mkubwa wa kufahamu shughuli zinazoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, hivyo kuna umuhimu wa kuandaa vipindi vya kuelimisha umma,” ameeleza. Maonesho ya Wakulima maarufu Nanenane yamebebwa na kauli mbiu isemayo: "Chagua Viongozi Bora, kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi 2025"

KARIBU BANDA LA HALMASHURI YA IGUNGA KWENYE MAONESHO YA NANE NANE MKOANI TABORA.

Picha
 

COOP BANK YAJIVUNIA UTOAJI HUDUMA SEKTA YA KILIMO.

Picha
. Coop Bank yatangaza Ushiriki Mkubwa katika Maonesho ya Nanenane, Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  BENKI ya Ushirika Tanzania (Coop Bank) imethibitisha kushiriki kikamilifu katika Maonesho ya Kitaifa na Kimataifa ya Nanenane 2025 yanayofanyika katika viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma, ikiwa ni miongoni mwa wa  dhamini wa maonesho hayo makubwa ya kilimo nchini. Akizungumza na waandishi wa habari katika banda la benki hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Coop Bank, Bw. Godfrey Ng’urah, amesema benki hiyo imejikita katika kutoa huduma za kifedha zenye kuleta mabadiliko chanya katika mnyororo mzima wa thamani wa kilimo-biashara, huku ikitoa kipaumbele kwa wakulima, vijana na wajasiriamali wa vijijini. “Coop Bank ni benki ya ushirika kwa vitendo. Zaidi ya asilimia 51 ya umiliki wake upo mikononi mwa vyama vya ushirika hii ni benki ya wakulima, kwa wakulima,” amesema Bw. Ng’urah. Ameeleza kuwa, Benki hiyo inashirikiana na vyama vya msingi (AMCOS) na vyama vikuu vya ushirika (UNION) nchini kote...

DKT. MPANGO AZINDUA MAONESHO YA 32 NANENANE KITAIFA JIJINI DODOMA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango amezindua rasmi Maonesho ya 32 ya Wakulima (Nanenane) yanayofanyika kitaifa katika Viwanja vya Nanenane, Nzuguni, jijini Dodoma yenye kauli mbiu isemayo "Chagua Viongozi bora kwa Maendeleo Kilimo, Mifugo na Uvuvi 2025". Dkt. Mpango amesema kuwa Tanzania inaadhimisha Maonesho ya 32 ya Nanenane yenye hadhi ya Kitaifa na Kimataifa kwa lengo la kukuza uchumi na kuchochea matumizi ya teknolojia bora na kuimarisha ushirikiano wa kimataifa. Tangu asubuhi ya leo, maelfu ya wananchi kutoka mikoa mbalimbali wamejitokeza kutembelea banda ya Wizara ya Madini na Taasisi zake, wakipata elimu juu ya mchango wa sekta ya madini katika kuimarisha uchumi wa wakulima na taifa kwa ujumla. Banda la wizara hiyo limepambwa na taarifa mbalimbali za kitaalamu kuhusu uongezaji thamani madini, usalama wa wachimbaji wadogo, fursa za uwekezaji, na matumizi ya teknolojia bunifu katika sekta ya madini. Akizungum...

TADB YATOA MIKOPO KWA WAZALISHAJI NA WACHAKATAJI 762,291.

Picha
  IMEELEZWA KUWAMNYORORO WA THAMANI UMEKUWA KWA WAKULIMA NA WACHAKATAJI.  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  BENKI ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kupitia Mfuko wa Dhamana kwa Wakulima Wadogo, imefanikiwa kuwafikia zaidi ya wanufaika 762,291 nchi nzima, kwa kuwasaidia kupata mikopo kupitia taasisi za kifedha bila hitaji la dhamana kubwa. Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dodoma kwenye maonesho ya wakulima na wafugaji Kitaifa  Rosemary  Gordon Afisa Biashara wa TADB anayesimamia mfuko huo, alieleza kuwa mfuko huo unatekelezwa kwa ushirikiano na benki 13 za biashara, benki za ushirika, na taasisi nyingine za kifedha nchini.  “Mfuko huu unahakikisha kuwa wakulima wadogo, hata wale wasio na dhamana ya kutosha, wanapata mikopo ya kuwawezesha kuendesha shughuli zao za kilimo kutoka shambani hadi sokoni,” akisema Gordon. Amesema mikopo inayodhaminiwa na mfuko huo husaidia wakulima kununua pembejeo kama mbegu, viuatilifu na mbolea, pamoja na dhana za kilim...

TAIFA STARS YAPATA MAFUNZO YA UADILIFU MICHEZONI.

Picha
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) leo wamepata mafunzo ya Uadilifu michezoni kuelekea mashindano ya CHAN 2024, yanayotarajiwa kuanza 02 Agosti 2025.

BEKA FRAVOUR ANOGESHA MKESHA WA MWENGE IGUNGA.

Picha
MSANII wa Mziki wa kizazi Kipya Beka Fravour ni mmoja ya Wasanii waliopanda na kutumbwiza katika jukwaa la Mkesha wa Mwenge wa Uhuru 2025 katika uwanja wa mpira wa miguu wa Barafu ulio katika Kitongoji cha Kati Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora.  Mwenge wa Uhuru 2025 katika uwanja wa mpira wa miguu wa Barafu ulio katika Kitongoji cha Kati Wilaya ya Igunga. 

COSTECH YAJENGA KITOVU CHA TAASISI ZA UBUNIFU NA UTAFITI DODOMA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma TUME ya Sayansi na Teknolojia Tanzania (COSTECH) inatekeleza kwa kasi mradi wa kimkakati wa ujenzi wa Makao Makuu mapya jijini Dodoma, ikiwa ni hatua ya kuiweka Tanzania kwenye msitari wa mbele katika maendeleo ya maarifa, utafiti na ubunifu wa kisayansi. Ujenzi huo, unaotarajiwa kukamilika Machi 2026, umeelezewa na viongozi wa COSTECH kuwa ni zaidi ya jengo bali ni uwekezaji wa taifa katika mustakabali wa uchumi wa ubunifu na teknolojia ya kisasa. Kwa mujibu wa Dkt. Amos Nungu, Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, jengo hilo litakuwa na uwezo wa kutoa huduma kwa watafiti, wabunifu na wajasiriamali wa teknolojia kwa kutumia miundombinu ya kisasa ikiwemo maabara bunifu, vituo vya Atamizi, kumbi za mikutano ya wataalamu, na ofisi zilizounganishwa na mifumo ya kidigitali.  “Tunajenga jukwaa la kisayansi litakalosaidia taifa kufanya maamuzi yanayotokana na ushahidi, tafiti, na maarifa. Dodoma sasa inapata nafasi ya kuwa moyo wa uvumbuzi nchini,” alisema Dkt. Nungu. Nay...

MAKAMU WA RAIS KUONGOZA KONGAMANO KUBWA LA MASHIRIKA YA KIRAIA DODOMA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Kongamano la Kitaifa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGOs) linalotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 11 hadi 13 Septemba 2025, jijini Dodoma. Kongamano hilo linaandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Tanzania Bara, kwa kushirikiana na mitandao ya NGOs nchini, na litawakutanisha zaidi ya mashirika elfu moja kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania. Akizungumza kuhusu maandalizi ya kongamano hilo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Bi. Felister Mdemu, alisema kongamano hilo ni sehemu ya tathmini ya miaka mitano ya utekelezaji wa kazi za NGOs, ambapo mashirika yatapima mafanikio, changamoto na mchango wao kwa jamii katika maeneo kama afya, elimu, jinsia, na ustawi wa jamii.  “Mashirika haya yamekuwa mstari wa mbele katika kuleta maendeleo ya watu, na serikali ya awamu ya sita inatambua na kuthami...

ISMAIL USSI:- IGUNGA YATIMIZA UJENZI WA MIRADI KWA ASILIMIA 100.

Picha
  Na Lubango Mleka, Igunga. MKIMBIZA Mwenge wa Uhuru kitaifa 2025 Ismail Ali Ussi ameipongeza Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora kwa kusimamia vyema miradi yote iliyozinduliwa na Mwenge wa Uhuru Wilayani hapa kwa asilimia 100. Ussi ametoa pongezi hizo leo tarehe 31.07.2025 alipozungumza na Wananchi na Viongozi mbalimbali waliojitokeza katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru katika uwanja wa Barafu, ambapo amesema kuwa viongozi wa wilaya ya Igunga wakiongozwa na Mkuu wa wilaya ya Igunga Sauda Mtondoo na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga Bi. Selwa Abdalla Hamid wamesimamia maelekezo yote yaliyotolewa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pindi anapotoa fedha za miradi ya maendeleo kwa wananchi. "Nimpongeze Mama yangu Mkuu wa Wilaya na Igunga Sauda Mtondoo na Mkurugenzi Mtendaji kwa kusimamia kwa ukaribu miradi hii yote ambayo tumeizindua leo yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6, kwani katika miradi yote hatujakuta dosari yoyote," Mwenge wa Uhuru unapokimbizwa katika mik...