GST YATOA USHAURI NA UPIMAJI SAMPULI ZA MAJI, MIAMBA NA MADINI.
Wizara ya Madini yaendelea kutoa elimu ya Sheria, Kanuni za Madini. Na Mwandishi Wetu, Dodoma. TAASISI ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) imeendelea kutoa ushauri na huduma za upimaji wa sampuli za miamba na madini kwa wananchi mbalimbali wanaofika kutaka kujua aina za miamba na madini waliokuwanayo. Aidha, GST imekuja na vifaa vya utafiti wa miamba na madini iliyo chini ya tabaka ya juu la udongo ambavyo kitaalam vinaitwa vifaa vya jiofizikia. Sambamba na hayo, Wataalamu kutoka GST wamewashauri wananchi kutumia Maabara ya taasisi hiyo kwa uchunguzi wa sampuli zao za miamba na madini ili kubaini wingi na uwepo wa madini ili kuongeza tija na uzalishaji wa madini. Aidha, Wizara ya Madini kwa kushirikiana na taasisi zake imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu masuala mbalimbali ya sekta ya madini kupitia banda lake lililopo katika eneo la mabanda ya Serikali, banda namba 5. Kupitia banda hilo, wananchi wanaelimishwa kuhusu shughuli mbalimbali zinazohusu sekt...