Machapisho

COSTECH YAJENGA KITOVU CHA TAASISI ZA UBUNIFU NA UTAFITI DODOMA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma TUME ya Sayansi na Teknolojia Tanzania (COSTECH) inatekeleza kwa kasi mradi wa kimkakati wa ujenzi wa Makao Makuu mapya jijini Dodoma, ikiwa ni hatua ya kuiweka Tanzania kwenye msitari wa mbele katika maendeleo ya maarifa, utafiti na ubunifu wa kisayansi. Ujenzi huo, unaotarajiwa kukamilika Machi 2026, umeelezewa na viongozi wa COSTECH kuwa ni zaidi ya jengo bali ni uwekezaji wa taifa katika mustakabali wa uchumi wa ubunifu na teknolojia ya kisasa. Kwa mujibu wa Dkt. Amos Nungu, Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, jengo hilo litakuwa na uwezo wa kutoa huduma kwa watafiti, wabunifu na wajasiriamali wa teknolojia kwa kutumia miundombinu ya kisasa ikiwemo maabara bunifu, vituo vya Atamizi, kumbi za mikutano ya wataalamu, na ofisi zilizounganishwa na mifumo ya kidigitali.  “Tunajenga jukwaa la kisayansi litakalosaidia taifa kufanya maamuzi yanayotokana na ushahidi, tafiti, na maarifa. Dodoma sasa inapata nafasi ya kuwa moyo wa uvumbuzi nchini,” alisema Dkt. Nungu. Nay...

MAKAMU WA RAIS KUONGOZA KONGAMANO KUBWA LA MASHIRIKA YA KIRAIA DODOMA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Kongamano la Kitaifa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGOs) linalotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 11 hadi 13 Septemba 2025, jijini Dodoma. Kongamano hilo linaandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Tanzania Bara, kwa kushirikiana na mitandao ya NGOs nchini, na litawakutanisha zaidi ya mashirika elfu moja kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania. Akizungumza kuhusu maandalizi ya kongamano hilo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Bi. Felister Mdemu, alisema kongamano hilo ni sehemu ya tathmini ya miaka mitano ya utekelezaji wa kazi za NGOs, ambapo mashirika yatapima mafanikio, changamoto na mchango wao kwa jamii katika maeneo kama afya, elimu, jinsia, na ustawi wa jamii.  “Mashirika haya yamekuwa mstari wa mbele katika kuleta maendeleo ya watu, na serikali ya awamu ya sita inatambua na kuthami...

ISMAIL USSI:- IGUNGA YATIMIZA UJENZI WA MIRADI KWA ASILIMIA 100.

Picha
  Na Lubango Mleka, Igunga. MKIMBIZA Mwenge wa Uhuru kitaifa 2025 Ismail Ali Ussi ameipongeza Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora kwa kusimamia vyema miradi yote iliyozinduliwa na Mwenge wa Uhuru Wilayani hapa kwa asilimia 100. Ussi ametoa pongezi hizo leo tarehe 31.07.2025 alipozungumza na Wananchi na Viongozi mbalimbali waliojitokeza katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru katika uwanja wa Barafu, ambapo amesema kuwa viongozi wa wilaya ya Igunga wakiongozwa na Mkuu wa wilaya ya Igunga Sauda Mtondoo na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga Bi. Selwa Abdalla Hamid wamesimamia maelekezo yote yaliyotolewa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pindi anapotoa fedha za miradi ya maendeleo kwa wananchi. "Nimpongeze Mama yangu Mkuu wa Wilaya na Igunga Sauda Mtondoo na Mkurugenzi Mtendaji kwa kusimamia kwa ukaribu miradi hii yote ambayo tumeizindua leo yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6, kwani katika miradi yote hatujakuta dosari yoyote," Mwenge wa Uhuru unapokimbizwa katika mik...

MIRADI 6 YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 2.6 YAZINDULIWA NA MWENGE WA UHURU 2025 WILAYANI IGUNGA.

Picha
Na Lubango Mleka, Igunga.  MWENGE wa Uhuru  zimepokelewa  leo Julai 31,2025 Wilayani Igunga na Mkuu wa Wilaya  hiyo Mhe. Sauda Salum Mtondoo katika Viwanja vya Gulioni kijiji cha Simbo kata ya  Simbo ,Mwenge huo utakimbizwa kwa Umbali wa Kilomita  229.4   utapita katika tarafa tatu na kata tano na kupitia  Miradi  6 ya Maendeleo yenye thamani ya Shilingi Bilioni  2.6 kwa lengo la Kuhimiza maendeleo, Uzalendo na Wanachi Kushiriki Uchaguzi Mkuu utakaofanyika  Oktoba 29 Mwaka huu. Katika hatua nyingine Mwenge wa Uhuru Wilayani Igunga  utapitia Miradi mbalimbali ya Maendeleo   ikiwemo Kutembelea na kukagua  vikundi vitatu vya  Vijana wanaojihusisha na Usafirishaji  wa abiria na mizigo  vyenye thamani ya Sh. 63 Milioni,Kuzindua mradi wa ujenzi wa  madarasa manne na matundu Sita ya vyoo Shule ya Msingi Igumila  wenye thamani ya 118.2 Milioni,Kufungua Mradi wa Ujenzi wa Majengo manne Hospit...

SDC NA UNFPA WATOA MWELEKEO MPYA KWA WASICHANA WALIOATHIRIWA NA MIMBA ZA UTOTONI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma  ZAIDI ya wasichana 300 waliopata mimba wakiwa na umri mdogo (Young Mothers) wamewezeshwa kupitia mradi wa "Kijana Imara" unaotekelezwa na taasisi ya Restless Development Tanzania kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Uswisi (Swiss Agency for Development and Cooperation – SDC) kupitia Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (United Nations Population Fund – UNFPA). Mradi huu unatekelezwa Tanzania Bara na Visiwani, na kwa sasa unatekelezwa katika mkoa wa Dodoma kwenye wilaya tano ambazo ni Dodoma Mjini, Chamwino, Kongwa, Bahi na Kondoa DC. Wasichana hao walipewa mafunzo ya ujuzi wa maisha, elimu ya afya ya uzazi, na ujasiriamali. Baada ya mafunzo, walipewa vifaa vya kazi ikiwemo mashine za kushona nguo (chelehani), vifaa vya saluni, na mabanda ya kisasa ya kufugia kuku. Akizungumza wakati wa ugawaji wa vifaa hivyo, Afisa Mradi wa Restless Development Tanzania, Ally Saad, alisema taasisi yao inalenga kuwawezesha vijana hasa wasichana waliopata m...

RIPOTI YA FEDHA KUTOKA BENKI KUU YA TANZANIA

Picha
Ripoti ya hivi karibuni kabisa ya Benki Kuu ya Tanzania inaonesha zaidi ya robo ya wale waliochukua mikopo binafsi mwaka 2024 waliitumia kununua magari na kugharamia matibabu.  Katika ripoti hiyo ya Uhimilivu wa Sekta ya Fedha, takwimu zinaonesha asilimia 14.7 ya mikopo ilikwenda kwenye matibabu na 14.2 ilitumika kununua magari. Ujenzi wa nyumba na kulipia masomo ni matumizi mengine makubwa yaliyofanywa na wale waliochukua mikopo binafsi mwaka uliopita. Je, wewe hukopa kufanyia nini?

WAZIRI MKUU MAJALIWA KUWA MGENI RASMI MKUTANO MKUU WA WATUNZA KUMBUKUMBU NA NYARAKA TANZANIA.

Picha
Na. Mwandishi Wetu, Dodoma.  Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa Chama cha Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka Tanzania (TRAMPA) tarehe 27 Agosti, 2025 katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dare s Salaam. Akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya maandalizi ya mkutano huo leo jijini Dodoma, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene amesema pamoja na kufungua rasmi mkutano huo, Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa pia ataendesha zoezi la harambee kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Maarifa kitakachokuwa na masijala ya mfano, kumbi za mikutano pamoja na ofisi za TRAMPA kinachotarajiwa kujengwa jijini Dodoma. Kufuatia mkutano huo wa kitaaluma, Mhe. Simbachawene ametoa wito kwa Waajiri wote kuwaruhusu Watunza kumbukumbu ili waweze kushiriki kwani ni jukwaa muhimu la  kuwajengea uelewa wa majukumu wanayoyatekeleza ukizingatia kwa s...

CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA WA UBUNGE,

Picha
..MAKALLA MCHAKATO UMEVUNJA REKODI Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  BAADA ya kusubiriwa kwa hamu kwa muda mrefu, Chama Cha Mapinduzi (CCM) hatimaye kimetangaza rasmi majina ya wagombea waliopitishwa kuwania nafasi mbalimbali katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025. Tangazo hilo limetolewa leo na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) anayeshughulikia Itikadi, Uenezi na Mafunzo, CPA Amos Makalla, katika Makao Makuu ya chama hicho jijini Dodoma. Makalla amesema kuwa kazi ya kuchambua na kupitisha majina ya wagombea ilikuwa kubwa kutokana na idadi kubwa ya waliojitokeza kuwania nafasi mbalimbali.  Amesema Kamati Kuu ya CCM ilifanya kazi hiyo kwa umakini na weledi ili kuhakikisha kila jina lililopitishwa linaakisi maadili, uwezo na utekelezaji wa sera za chama. “Wagombea walikuwa wengi sana, kazi ya kuandaa orodha haikuwa nyepesi. Tulihakikisha tunamaliza kwa usahihi mkubwa, kwa kuzingatia maoni na mapendekezo ya vikao halali vya chama,” alisema Makalla. Makalla aliwapongeza waombaji wot...

SHULE 6 MPYA ZAJENGWA NA MRADI WA SEQUIP IRAMBA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Iramba, Singida.  SERIKALI kupitia mradi wa Kuboresha Ubora wa Elimu ya Sekondari (SEQUIP) imetumia Bilioni 6.361 kujenga Shule mpya sita za Sekondari, Shule sita zimefanyiwa ujenzi wa upanuzi wa miundombinu ya kidato cha 5 na 6, Ujenzi wa vyoo na nyumba za walimu katika Wilaya ya Iramba Mkoani Singida. Akitoa taarifa ya miradi ya elimu iliyojengwa katika wilaya ya Iramba, Mkuu wa wilaya ya Iramba Mhe. Suleiman Mwenda amesema kuwa ujenzi wa shule hizo utaimarisha sekta ya elimu ikiwemo kuongeza ufaulu wa wanafunzi. Amezitaja shule hizo zilizojengwa wilayani hapo kuwa ni pamoja na ujenzi wa Shule ya Sekondari -MALUGA uliogharimu shilingi milioni 470, ujenzi wa shule ya Sekondari NDULUNGU uliogharimu shilingi milioni 470, ujenzi wa shule ya Sekondari -Mtoa darajani uliogharimu shilingi milioni 544.225. Miradi mingine mipya ni pamoja na ujenzi wa shule ya sekondari -Makunda uliogharimu shilingi milioni 544.225, ujenzi wa shule ya Sekondari-KIZEGA uliogharimu shilin...