MIRADI 6 YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 2.6 YAZINDULIWA NA MWENGE WA UHURU 2025 WILAYANI IGUNGA.



Na Lubango Mleka, Igunga. 

MWENGE wa Uhuru  zimepokelewa  leo Julai 31,2025 Wilayani Igunga na Mkuu wa Wilaya  hiyo Mhe. Sauda Salum Mtondoo katika Viwanja vya Gulioni kijiji cha Simbo kata ya  Simbo ,Mwenge huo utakimbizwa kwa Umbali wa Kilomita  229.4   utapita katika tarafa tatu na kata tano na kupitia  Miradi  6 ya Maendeleo yenye thamani ya Shilingi Bilioni  2.6 kwa lengo la Kuhimiza maendeleo, Uzalendo na Wanachi Kushiriki Uchaguzi Mkuu utakaofanyika  Oktoba 29 Mwaka huu.

Katika hatua nyingine Mwenge wa Uhuru Wilayani Igunga  utapitia Miradi mbalimbali ya Maendeleo   ikiwemo Kutembelea na kukagua  vikundi vitatu vya  Vijana wanaojihusisha na Usafirishaji  wa abiria na mizigo  vyenye thamani ya Sh. 63 Milioni,Kuzindua mradi wa ujenzi wa  madarasa manne na matundu Sita ya vyoo Shule ya Msingi Igumila  wenye thamani ya 118.2 Milioni,Kufungua Mradi wa Ujenzi wa Majengo manne Hospitali ya Wilaya ya  Igunga wenye thamani ya Sh. 900 Milioni


Vilevile Kufungua  Mradi wa Jengo la Biashara  la Halmashauri  wenye thamani ya Sh.584.2,Kuzindua mradi wa Upanuzi  wa mtandao wa Maji safi  ya Ziwa Victoria (Makomero-Mgongoro) wenye thamani ya Sh. 840.8 Milioni na Kuzindua  Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya RC Church -Barafu kwa kiwango cha Lami mita 245 wenye thamani ya Sh.130 Milioni.
 
Aidha  Mbio za Mwenge zitakagua  masuala ya Lishe,Kudhibiti  UKIMWI,Matumizi nishati safi ,Malaria na Mapambano dhidi ya Rushwa.

Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 zinakwenda na kauli mbiu isemayo:-
"Jitokeze Kushiriki  Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Amani na Utulivu."










Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MWENYEKITI NAMALULU AWEKWA PEMBENI KUPISHA UCHUNGUZI

IGUNGA YAIBUKA MSHINDI WA KWANZA NANENANE TABORA.