Machapisho

RUJAT YATAKA MABADILIKO YA UANDISHI, YAANGAZA ZAIDI VIJIJINI

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Arusha MWENYEKITI  wa Chama cha Waandishi wa Habari za Vijijini Tanzania (RUJAT), Neville Meena, amesema kuwa ni muhimu kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari huku ikiwekewa mkazo sauti ya wananchi wa vijijini ili kuhakikisha hakuna kundi linaloachwa nyuma katika upatikanaji wa taarifa. Akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika jijini Arusha, Meena amesema uhuru wa vyombo vya habari unapaswa kuambatana na uwajibikaji wa kitaaluma kwa wanahabari kuzingatia misingi ya ukweli, usahihi, uwiano na maslahi ya umma. Maadhimisho hayo yaliyowakutanisha wadau wa sekta ya habari kwa siku mbili katika Hoteli ya Mount Meru, yalijadili mustakabali wa tasnia ya habari katika muktadha wa mabadiliko ya kidijitali, yakilenga pia kukuza ubunifu na kuhakikisha uendelevu wa taaluma ya uandishi wa habari. Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa RUJAT, Prosper Kwigize, amesema chama hicho kimejipanga kushirikiana na taasisi mbalimb...

WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUJITEGEMEA KIUCHUMI KUEPUKA USHAWISHI

Picha
  Na Hamida Ramadhan,Arusha.  WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amewataka waandishi wa habari nchini kujenga uwezo wa kujitegemea kiuchumi ili kuepuka kushawishiwa na wanasiasa wasio waadilifu pamoja na wala rushwa. Akizungumza jijini Arusha wakati wa kufunga maadhimisho kuelekea Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, Makonda alisema uhuru wa habari hauwezi kuwa kamili bila uhuru wa kiuchumi kwa wanahabari. Alisema baadhi ya waandishi wamekuwa wakiandika habari kwa maslahi ya wanasiasa, hali ambayo ni hatari kwa mustakabali wa taaluma ya habari na inaweza kupotosha jamii. “Ni muhimu kwa mwandishi wa habari kuwa na uhuru wa kiuchumi ili aweze kufanya kazi yake bila hofu, upendeleo au shinikizo kutoka kwa watu wenye maslahi binafsi,” amesema Makonda. Ameongeza kuwa kuna watu wasiokuwa waaminifu wanaowashawishi waandishi kwa maslahi yao, na kusisitiza umuhimu wa wanahabari kuzingatia maadili ya taaluma yao pamoja na kuandika habari zinazojenga taif...

TAMASHA LA KILIMO LAHITIMISHWA MBEYA

Picha
REA Yapongezwa uhamasishaji matumizi ya nishati safi ya kupikia, Umeme sasa ni kitongoji kwa kitongoji.  Na Mwandishi Wetu, Iwambi - Mbeya.  TAMASHA  la Kilimo lililofanyika mkoani Mbeya limehitimishwa rasmi leo Jumatano, tarehe 29 Aprili 2026, kwa mafanikio makubwa huku likiwa limekusanya wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo, nishati na maendeleo kutoka ndani na nje ya mkoa huo.  Tamasha hilo limekuwa jukwaa muhimu la kubadilishana uzoefu, kuonesha teknolojia mpya na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu njia bora za kuboresha maisha yao kupitia kilimo na matumizi sahihi ya nishati. Akizungumza wakati wa hafla ya kufunga tamasha hilo,mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Rungwe Mhe. Jaffar Haniu ameipongeza REA kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuhakikisha wananchi wanapata elimu ya matumizi ya nishati safi, akisisitiza kuwa hatua hiyo ina mchango mkubwa katika kuboresha afya za wananchi na kulinda mazingira.  Alieleza kuwa matumizi ya nishati safi kama majiko ya umeme, majiko y...

AAPAM KUKUTANISHA WATAALAM JIJINI ARUSHA ILI KUJADILI NAMNA YA KUIMARISHA UTAWALA BORA NA KUONGEZA UFANISI KATIKA UTOAJI HUDUMA KWA WANANCHI

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Dodoma.  WATAALAMU wa Utawala wa umma na usimamizi wa rasilimaliwatu nchini wanatarajiwa kukutana jijini Arusha kuanzia Mei 5 hadi 8, 2026 katika Mkutano Mkuu wa Pili wa mwaka wa Jumuiya ya Wataalamu wa Utawala wa Umma na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Barani Afrika (AAPAM) Tawi la Tanzania. Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa AAPAM Tanzania Chapter, Leila Mavika, amesema mkutano huo utafanyika jijini Arusha ukiwaleta pamoja wataalamu wa kada hiyo ili kujadili namna ya kuimarisha utawala bora na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi. Kwa mujibu wa  Mavika, mkutano huo unalenga kutoa fursa ya kubadilishana uzoefu, kujadili changamoto zinazowakabili katika utendaji kazi na kubaini fursa za kuboresha usimamizi wa rasilimaliwatu na utawala katika utumishi wa umma. Ameongeza kuwa mkutano huo utaongozwa na wataalamu wabobezi watakaowasilisha mada mbalimbali za kitaaluma zitakazochochea maboresho ya utendaji na kuongeza tija katik...

DC MWEMA AONGOZA ZOEZI LA UTEKETEZAJI BANGI KITETO

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Kiteto - Manyara.  MKUU wa Wilaya ya Kiteto Mheshimiwa Remidius Mwema ameongoza zoezi la uchomaji ekari tano za dawa za kulevya aina ya bangi iliyolimwa ndani ya mashamba ya mahindi katika kitongoji cha Kimaraunga, Kijiji cha Mbigiri Kata ya Partimbo. Mhe DC Mwema amewataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano  kwa Serikali kukabiliana  na ulimaji wa bangi huku akipongeza jitihada za utoaji taarifa zinazosaidia kubaini uwepo wa mashamba hayo.  Amelitaka jeshi la polisi kuhakikisha linawakamata watuhumiwa wote ikiwa ni pamoja na wamiliki wa mashamba hayo huku akisisitiza wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo ili sheria ichukue mkondo wake. “Tumeshirikisha wananchi katika zoezi la kuteketeza dawa za kulevya ili kuonyesha kwa vitendo dhamira njema ya Serikali katika mapambano haya na tunatuma ujumbe kwa wananchi wote kuendelea kukabiliana na hali hii, operesheni hizi zitaendelea wakati wote ndani ya Wilaya yetu ,wananchi waendele...

DOLA BILIONI 1.3 KUJENGA SGR KIPANDE CHA MAKUTUPORA -ISAKA

Picha
  Na Lubango Mleka, Dodoma.  SERIKALI imeandika historia mpya katika sekta ya uchukuzi baada ya kusainiwa  mkataba wa Dola za Marekani Bilioni 1.277 kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa Reli ya Kisasa ya Standard Gauge Railway (SGR) Lot 3 na 4 kutoka Makutupora hadi Isaka kilometa 368 na Tabora mpaka Isaka 165 na kufanya jumla ya kilometa 533, utiaji Saini huo umefenyika leo tarehe 28 Aprili, 2026  katika  Ukumbi wa Treasury Square jijini Dodoma. Zoezi la utiaji Saini huo  lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Taasisi za kifedha, mabalozi pamoja na wadau wa maendeleo, huku Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Dkt. Khamis Mussa Omar, akiwa mgeni rasmi. Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Omar amesema jumla ya mashirika 3 ya fedha kutoka nchi za Italy, Sweden na Poland yamefadhili  jumla ya dola  Bil. 1.277 kwa ajili ya kuendeleza kipande hicho ambacho utekelezaji wake ulishaanza. Amesema huu ni uendelezaji wa ujenzi wa Reli hii ya kisasa kwa ku...

ZAO LA CHOROKO LALETA NEEMA KWA WAKULIMA TABORA

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora.  CHAMA Kikuu cha Ushirika wa Wakulima (IGEMBEMBENSABO) kimeeleza kufurahishwa na mafanikio makubwa waliyopata wakulima wa zao la choroko na mazao mengine katika msimu uliopita na matarajio yao makubwa msimu huu. Meneja Mkuu wa Chama hicho kinachosimamia wakulima wa Wilaya za Igunga na Nzega, Baraka Samwel Kiboye ameeleza kuwa mafanikio hayo yamechochewa na kazi nzuri inayofanywa na serikali ya Awamu ya Sita kuinua sekta ya kilimo. Ameeleza kuwa katika msimu uliopita wakulima walizalisha jumla ya tani 1,800 za choroko kati ya makisio ya tani 2,000 na kuziuza kwa bei ya sh 1,500 kwa kilo kwa mfumo wa stakabadhi ghalani tofauti na ile ya kawaidia ya sh 800 hadi 1000. "Baada ya mauzo wakulima walilipwa zaidi ya shilingi bilioni 2.7 na zote ziliingia katika mifuko yao, haya ni mafanikio makubwa sana, na mwaka huu tunatarajia kupata kilo nyingi zaidi na zote zitauzwa kwa mfumo huo huo", amesema.  Kiboye ameongeza kuwa pia wameanzisha utaratibu wa wakul...

MATAPELI WATANO WANASWA KWA TUHUMA ZA KUIBA MILIONI 40 TABORA

Picha
Na mwandishi wetu, Tabora. Jeshi la Polisi mkoani Tabora linawashikilia watu watano kwa tuhuma za kuhusika na wizi wa shilingi milioni 40 kutoka kwa mfanyabiashara Fatuma Nasoro, mkazi wa Wilaya ya Kaliua, katika tukio lililotikisa wakazi wa eneo hilo. Kwa mujibu wa taarifa za awali, watuhumiwa hao walinaswa kufuatia msako maalum ulioendeshwa kwa nyakati tofauti ndani ya mkoa huo, baada ya kubainika kuwa walikuwa wakijihusisha na vitendo vya utapeli huku wakiendelea na maisha yao ya kawaida bila wasiwasi wowote. Akizungumzia tukio hilo, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Matiko Chacha, amesema miongoni mwa waliokamatwa, wawili wanaotambulika kwa majina ya Marseli Gwasima na Fred Ricardo walitumia mbinu za udanganyifu kwa kujifanya wahudumu wa kampuni ya mawasiliano ya YAS (zamani Tigo). Ameeleza kuwa kwa kutumia ujanja huo, watuhumiwa walimshawishi mfanyabiashara huyo, anayejihusisha na biashara ya khanga na vitenge wilayani Kaliua, kuwasajili laini yake, hatua iliyowapa mwanya wa kuhamisha ...

REA YATOA ELIMU YA NISHATI SAFI KWA WANANCHI KATIKA TAMASHA LA KILIMO IWAMBI MBEYA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Iwambi-Mbeya.  WAKALA wa Nishati Vijijini (REA) imeendelea kutoa elimu ya matumizi ya nishati safi kwa wananchi katika Tamasha la Kilimo linalofanyika katika viwanja vya Iwambi, mkoani Mbeya. Akizungumza wakati wa tamasha hilo, Mhandisi wa Miradi kutoka REA, Ramadhani Mganga, amesema kuwa lengo la ushiriki wao ni kuwahamasisha wananchi kutumia nishati safi na salama kwa kupikia ili kulinda afya zao na mazingira. Ameeleza kuwa REA inaendelea kusambaza na kuhamasisha matumizi ya teknolojia mbalimbali za nishati safi ikiwemo majiko ya umeme, majiko ya gesi pamoja na majiko banifu, ambayo yanasaidia kupunguza matumizi ya kuni na mkaa. “Ni muhimu kwa wananchi kuelewa faida za nishati safi, si tu katika kulinda mazingira bali pia katika kuboresha afya kwa kupunguza athari za moshi unaotokana na nishati zisizo salama,” amesema Mganga. Aidha, amebainisha kuwa kupitia miradi mbalimbali inayoendelea, upatikanaji wa umeme vijijini umeimarika kwa kiwango kikubwa, hatua inayo...