Machapisho

MBUNGE AGNESS AWAFIKIA WANAWAKE WA KIKRISTO KWA KUWASHIKA MKONO

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mara.  MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Agnes Marwa, ameungana na wanawake wa mashirika ya Kikristo katika Musoma kuadhimisha International Women's Day kwa shangwe na mshikamano mkubwa. Katika maadhimisho hayo yaliyowakutanisha wanawake wa Christian Council of Tanzania (CCT) pamoja na WAWATA wa Manispaa ya Musoma, Mheshimiwa Mbunge alitoa pongezi kwa wanawake kwa mchango wao mkubwa katika kuimarisha maadili ya jamii, familia na maendeleo ya Taifa. Akizungumza katika sherehe hizo, Mheshimiwa Agnes Marwa aliwahimiza wanawake kuendelea kushikamana, kujiamini na kutumia fursa mbalimbali za maendeleo ili kujiletea ustawi wao na jamii kwa ujumla. Katika kuonesha dhamira yake ya dhati ya kuunga mkono shughuli za wanawake na taasisi za kijamii, Mheshimiwa Mbunge alitoa mchango wa shilingi milioni 2 na laki 4 (Tsh 2,400,000) kwa ajili ya ununuzi wa tent, hatua itakayosaidia kuimarisha uendeshaji wa shughuli mbalimbali za kijamii na kiroho katika Manis...

MJOMBA MATATANI KWA KUMPIGA NA KUMNING'INIZA MTOTO DIRISHAJI KWA KUUNGUZA MBOGA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  JESHI la Polisi nchini Tanzania linamshikilia Joseph Mbalamwezi Francis Mkazi wa Mtaa wa Imalamakoe B, Wilayani Urambo, Mkoani Tabora kwa tuhuma za kumfanyia mtoto ukatili wa kufungwa kamba miguuni na mikononi na kisha kumning'iniza dirishani. Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania Naibu Kamishna wa Polisi DCP David Misime ameviambia Vyombo vya habari leo Jumatano  Machi 04, 2026 kuwa tukio hilo lilitokea Machi 02, 2026 na mtoto aliyekuwa anafanyiwa ukatili huo ana umri wa miaka 10 na kwamba mtuhumiwa ni Mjomba wake ambaye walikuwa wakiishi pamoja. "Sababu za kumfanyia ukatili huo wa kupigwa na kisha kuning'inizwa inadaiwa ni baada ya mtoto huyo kuunguza mboga (nyama) aliyokuwa anapika." Amesema Kamanda Misime. Jeshi la Polisi pia limewashukuru waliotoa taarifa za tukio hilo na kufanikisha mtoto huyo kuokolewa na kwenda kupatiwa matibabu na mtuhumiwa kukamatwa, Polisi ikisisitiza ushirikiano zaidi katika kuwalinda na kuzuia vitendo vya ukatili...

MHE MBUNGE WA VITI MAALUM MKOA MARA AGNESS MARWA AGAWA VIFAA VYA SALOON.

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mara.  KATIKA kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuwawezesha vijana,Mbunge wa viti maalumu mkoa wa mara Mhe, Agness Marwa amegawa vitendea kazi vya saloon za kike na kiume Kwa vijana zaidi 30 katika manispaa ya Musoma mkoa wa Mara. Dhamira hiyo ni kuwawezesha vijana kujikwamua kiuchumi na kuunga mkono serikali katika kuwawezesha wajasiriamali wadogo. Akizungumza katika kikao cha wajasiliamali  kilichofanyika Manispaa ya Musoma, Mbunge Agnes amesema ataendelea kuyafukia makundi mablimabli wakiwemo wajasiliamali Mali wote katika mkoa wa mara. Mhe. Agnes amesema azma hiyo ni kuunga mkono jitihada za mheshimiwa rais Samia Suluhu Hassan zinazojikita kuwasaidia wajasiliamali wadogo wadogo katika kujikwamua kiuchumi. Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Manispaa ya Musoma Juma Chikoka amempongeza Mbunge huyo ambapo amewataka wajasiliamali hao kuvitumia vifaa hivyo Kwa Lengo lililokusudiwa ili kujiongezea kipato. Nao baadhi ya wajasiliamal...

VIFO VILIVYORIPOTIWA KATIKA VITA KATI YA MAREKANI, ISRAEL NA IRAN.

Picha
SIKU tatu baada ya mzozo unaozidi kuenea uliosababishwa na mashambulizi ya pamoja ya Marekani na Israel dhidi ya Iran, Iran imeongeza kasi ya kampeni yake ya kulipiza kisasi ya makombora na droni dhidi ya Israel na mataifa ya Ghuba ya Kiarabu. Mashambulizi ya Iran yamekumba nchi nyingi katika eneo hilo, na kulazimisha nchi hizo kuzuia makombora hayo na vifusi vya makombora kuziangukia, na kuonesha jinsi vurugu hizo zilivyoenea katika eneo hilo. #vitairan #Israel #Marekani #Masharikiyakati

IRAN YASEMA HAIWEZI KUISHAMBULIA KENYA

Picha
Akizungumza jijini Nairobi, siku ya Jumatatu, Balozi wa Iran nchini Kenya Ali Gholampour, amesema kuwa makombora yatakayorushwa na nchi yake nchi yake, hayatoifikia Kenya. Gholampour anaamini kuwa, serikali ya Kenya haijatoa ngome za kijeshi kwa taifa la Marekani, zenye uwezo wa kuishambulia Iran. Hakikisho hilo linakuja wakati wa mashambulizi mfululizo katika eneo la Mashariki ya Kati, kutoka kwa Marekani na Israel, ambayo pia yalisababisha kifo cha Kiongozi Mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, na maofisa wengine waandamizi.

WASAFIRISHAJI WA KIMATAIFA KUTUMIA AFRIKA KUSAFIRISHA MIZIGO BAHARINI

Picha
Mzozo unaoongezeka unaohusisha Marekani, Israel na Iran umevuruga mojawapo ya njia za baharini yenye shughuli nyingi zaidi duniani, na kulazimisha makampuni makubwa ya meli kuelekeza meli kuzunguka Afrika. Wasafirishaji wa kimataifa, ikiwa ni pamoja na Maersk, Hapag-Lloyd, na CMA CGM, wamesimamisha usafiri kupitia Mfereji wa Suez na Bab el-Mandeb kufuatia mashambulio ya Marekani na Israel dhidi ya Iran na kuzidisha hatari za kiusalama karibu na Mlango-bahari wa Hormuz.

WANANCHI WA MTAA CHINYOYO WACHIMBA MSINGI WA OFISI YA SERIKALI KWA NGUVU ZAO

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Dodoma.  WANANCHI wa Mtaa wa Chinyoyo, Kata ya Kilimani, Jijini Dodoma wameanza rasmi ujenzi wa ofisi ya Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa kwa kuchimba msingi wa jengo hilo leo, hatua inayotajwa kuwa mwanzo wa kutatua changamoto ya muda mrefu ya kukosekana kwa ofisi rasmi ya mtaa. Kwa miaka kadhaa, wananchi wa mtaa huo walilazimika kumfuata Mwenyekiti nyumbani kwake au kwenda katika ofisi ya Mtendaji wa Kata iliyopo mtaa mwingine ili kupata huduma.  Hali hiyo imekuwa ikiwasababishia usumbufu na gharama za ziada za usafiri, hususan kwa kutumia bodaboda au bajaji. Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Chinyoyo, Mhe. Faustina Bendera, amesema kukosekana kwa ofisi kulikuwa kikwazo kikubwa katika utoaji wa huduma. “Wananchi walikuwa wanakuja nyumbani hata wakati wa shughuli binafsi. Ilibidi nisimamishe kazi za nyumbani ili kuwasikiliza na wakati mwingine kuambatana nao kufuatilia changamoto zao,” amesema. Ameongeza kuwa hata watendaji wa mtaa walikuwa wakifanya ...

WAJUMBE WA KAMATI YA JPCDS WAJIONEA MAAJABU YA HIFADHI YA NGORONGORO

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Ngorongoro.  WAJUMBE wa Kamati ya Wataalamu wa Kamisheni ya Kudumu ya Pamoja ya Ulinzi na Usalama (Joint Permanent Commission of Defense and Security – JPCDS) kutoka Tanzania na Zambia, wakiongozwa  na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Patrobas Katambi pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani na Usalama wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Jacob Jack Mwiimbu Februari 26, 2026 walipata fursa ya kutembelea na kujionea maajabu ya Hifadhi ya Ngorongoro wakati wakishiriki kikao cha siku tano Jijini Arusha kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika kukabiliana na uhalifu unaovuka mipaka na matishio yanayoibukia.  Ziara hiyo ilikuwa sehemu ya kuimarisha uelewa wa pamoja kuhusu umuhimu wa kulinda rasilimali za asili kama sehemu ya ajenda ya usalama wa kikanda. Kote duniani inafahamika kuwa, Ngorongoro ni hifadhi ya kipekee duniani, iliyotokana na kaldera bonde kubwa la volkano lililosababishwa na mlipuko na kuporomoka kwa volkano kubwa takribani miaka milioni 2 hadi ...

REA YAENDELEA NA UHAMASISHAJI MIRADI YA NISHATI VIJIJINI MARA.

Picha
  Wananchi wahamasika kujiunga na huduma ya umeme.Wananchi waunga mkono matumizi ya nishati safi ya kupikia. Na Mwandishi Wetu, Mara.  WAKALA wa Nishati Vijijini (REA) unaendelea na ziara ya uhamasishaji wananchi kujiunga na huduma ya umeme pamoja na matumizi ya nishati safi ya kupikia mkoani Mara. Uhamasishaji umehusisha utoaji wa elimu kwa wananachi namna ya kufanya maombi ya kujiunga na huduma ya umeme huku lengo kuu likiwa ni  kuongeza idadi ya watumiaji wa umeme na kuwakumbusha wananchi umuhimu wa nishati ya umeme kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii.  Aidha, Wakala umefanya Kampeni zinahusisha utoaji wa elimu kuhusu umuhimu na faida za matumizi ya nishati safi ya kupikia ikiwemo utunzaji wa afya, mazingira pamoja na usawa wa kijinsia.  Aidha, Wakala umetoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi bora  ya umeme hususani katika shughuli za uzalishaji ikiwemo shughuli za biashara, kilimo, na shughuli za nyumbani. Vile vile, Wakala umetoa elimu kuhusu taratibu...